Psychic Powers: Ni nguvu za kufanya miujiza. Wengi wanazo bila kujitambua. Je, wewe unazo?

Acheni kudanganya watu nyie viumbe
Ingekuwa hii rubbish iko kweli kwanini serikali ipeleke watu kusomea mambo ya upelelezi miaka 20 na pia wakirudi wanashindwa kuelewa ukweli wa kesi ndogo ndogo tu.? si wangekuita wewe Ukamtazame macho huyo muhalifu kisha uwaambie kafanya nini na mahala gani?

Hivi mnapata faida gani kudanganya watu?
hamuogopi Mungu ?
 
Tafadhali MziziMkavu naomba uweke na nyota ya Samaki
Nyie ndio mnasababisha hawa washirikina wapate viburi na kujiona wanafanya ya maana kumbe ni waongo wakubwa.

hakuna cha nyota wala nini. nenda kapige kazi, Hakuna cha nguo ya bahati wala siku mbaya.
siku zote ni nzuri na nguo rangi zote ni njema tu.
Utaibiwa hizo senti zako ndugu.
 
Wewe Pasco una nguvu gani kati ya ulizozitaja?
Nguvu za kuandika Uongo JF.
Hakuna ziada.
na SIO yeye tu. Hawa washirikina wote hawana nguvu wala uwezo wwt ambao Mimi na wewe hatuna. kazi zao kutafuta umaarufu na kuibia watu tu.

Nilisema huko Juu yyt mwenye uwezo wa kujua kilichojificha aniambie Mimi nina Umri gani tu naahidi kutembea makende nje wiki nzima.
Sijui mshana,Pasco, na mganga wao mzizi mkavu. Hawa wote waongo watupu.
 
Mkuu Shemeji Kahatani, nitakupigia darasa mdogo mdogo hadi tutakwenda pamoja.
Somo la kwanza, Mungu au Allah ni nini, ni nani, yukoje yuko wapi, alianzaje na ana uwezo gani?.

Somo la pili shetani nini, ni nani, yukoje yuko wapi, alianzaje na ana uwezo gani?.

Somo la tatu
Binadamu ni nini, ni nani, yukoje yuko wapi, alianzaje na ana uwezo gani?.
Ukishajibu ndipo nita determine IQ yako na uwezo wako wa kuelewa hivyo nitaamua nikupige darasa au nisijisumbue kumpigia mbuzi gitaa.
P
 
Nguvu za kuandika Uongo JF.
Nilisema huko Juu yyt mwenye uwezo wa kujua kilichojificha aniambie Mimi nina Umri gani tu naahidi kutembea makende nje wiki nzima.
Sijui mshana,Pasco, na mganga wao mzizi mkavu. Hawa wote waongo watupu.
Usichanganye ushirikina, wabashiri, wapiga ramli, ma palmistry, astrology na mambo ya parapsychology.
P
 
Usichanganye wabashiri, wapiga ramli, ma palmistry, astrology na mambo ya parapsychology.
P
Baada ya kudai kuwa wewe umejifunza hizo extra Senses In India and so On. na Baada ya kuanza kulewa ukazipoteza
Nimekuuliza swali hapo juu NANI KTK DUNIA HII Tunayoishi ana UWEZO wa Kunambia yaliojificha? NITAJIE MMOJA TU anaejulikana.
Usinitajie majina ya Vitabu na Philosophers!
or Name of the Movie.

Nipe jina la mtu anaejulikana mwenye hizo so called 8 senses Bull crap!

Watu wanasoma miaka 20 ili waweze kutambua tu namna gani ya kumuhoji mhalifu wewe unatwambia kuna mtu ANA UWEZO WA KUUONA UHALIFU WA MTU hata kabla HAJASEMA?

Pasco kaka hizi habari zako bora upeleke kwenye Jukwaa la Jokes. hapa utasababisha baadhi ya wadau dhaifu wakufuate Inbox uwapatie solution ya Umaskini wao hali ya kuwa wewe mwenyewe Rizki miguuni.

Tazama mzizi mkavu anavyodanganya watu.
matokeo yake anauza dawa za Bahati na zingine za ajabu ajabu kwa bei anazojua yeye wakati yeye mwenyewe anatafuta Bahati mpk leo.
 
MziziMkavu tafadhali pia andika na nyota ya Ng'ombe(Taurus)
 
Ni Ushetani na Ushirikina mtupu.

Hawa wapiga Ramli Wana Laana ya Mungu.
kazi kuibia watu tu. kazi za halali hawawezi kufanya. Yaani ni Mashetani wabaya sana hawa .
Mambo ya nyota, sio ushirikina, ni astrology.
P
 
Mambo ya nyota, sio ushirikina, ni astrology.
P
Don't make me laugh P. I'm not in the mood.
Astrology means the study of the movements and relative positions of celestial bodies interpreted as having an influence on human affairs and the natural world.

These morons Never ever been to any study of celestial bodies rather they learn from JINN. au kwa kiswahili Mashetani to practice their whitch crafts.

watabiri wapiga Ramli Wana shule inayojulikana?
Kuna School of Astrology wanafukiza mavi ya panya na miguu ya chura? na kuvaa hirizi na vitambaa vyeusi?

Pasco unatetea huu Uchafu au na wewe unataka kuwa mwanga?
 
Tafuta vitabu vya Linda Goodman's Sun Signs na Love Signs, ameeleza vizuri, kwenye astrology hakuna uchawi wowote, bali the effects of powers from the movements and relative positions of celestial bodies inavyo influence on human affairs siku unazaliwa depending on exactly time and location and also its influence, effects na impacts on the natural world, inayotokana na nguvu ya uvutano kati ya dunia, mwezi na nyota, ndio zinasababisha maji kujaa na kupwa, ndio ina control siku za wanawake na changing moods zao, ndio ina determine kuanza kwa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadan na kuisha kwa mfungo, ndio determinant ya direction ya Kibla na hata Masiya alipozaliwa, no nyota zilionyesha.

Ukiondoa ma astrologers matapeli, the real astrology is for real na haitumii uchawi wowote!.
P
 
kama ni hivyo basi wengi tuna hizo nguvu zaidi ya mbili.mfsno. kwa uoande wangu huwa naota kila mara nakemea vitu viovu hasa vya kishirikina. na hata kuruka hewami ninapokuwa na pambana na kitu.
 
Nimesema niliishi India kwa mengine ila nikapata wasaa wa kujifunza hayo kwa kujisomea tuu, hivyo sikufundishwa na yeyote na wala sikwenda India kusomea hayo.

Kwa vile mimi source yangu ni kusoma tuu vitabu na wala sijawahi kujifunza rasmi chochote, na popote, then siwezi kukutafutia mtu yoyote zaidi ya kukushauri utafute vitabu vya mtu anaitwa Uri Geller usome.

Wenzetu CIA, FBI, Scotland Yard, wanawatumia watu hawa kusolve mysterious deaths. British Airways wanawatumia kuzuia ajali za ndege. Balozi zote za Israel dunia nzima zinawatumia kulinda usalama wa rais wao. Kuna mamia ya Wa Israel wanafanya kazi Twin Towers, siku ya 9/11, wote walitumiwa warning wasiende kazini, hakuna hata mmoja wao alipoteza maisha.

By now usikute tayari kuna watu, wenye hizi powers wanamuona huyu dogo mahali alipo, fichwa, ila hawaruhusiwi kusema!, At the same time matapeli wa kuchungulia mtungini na kumuona yule yule, wako busy kustrategize jinsi ya kupiga hela.

Ni kweli baada ya kupandisha uzi huu, kiukweli nimefuatwa sana inbox, watu wakitaka msaada wangu kwa kunidhania mimi ni teacher na wako tayari kulipa nifungue darasa, na wenginei ni 'fundi'
Wote ninawaeleza humu knowledge yangu kwenye mambo haya ni kwa kusoma tuu vitabu, na links zote nimempata humu.

Baada ya mimi kugoma kupokea senti tano ya mtu, wenye jicho la kuangazia fursa, wakaona fursa, wakachangamkia, wameunda ma group yao ya WhatsApp, wanajipigia pesa yao na kujilia mpunga wao kwa ulaini na mimi kazi yangu ni kushauri tuu kama hapa kwenye bandiko hili, angalia watu wanafundishwa nini na uangalie mchango wangu nimeshauri nini
Jinsi ya kutoka nje ya mwili (Astral Projection) - JamiiForums
P
 
Now you are talking about something different all together P.

kwanza ulianza kuleta habari za jicho la nne sasa unaongelea habari tofauti kabisa.

Nadhani utakuwa umekubaliana na Mimi kuwa HAKUNA MTU mwenye uwezo wa kuona kesho wala kuona YALIOJIFICHA.

Huu ni uongo na utapeli wa kitoto kabisa.
 
Huku sio kunitendea haki!.
P.
kiongozi unapoandika kuwa ulijifunza elimu ya Yoga huko India na ukathibitisha kuwa kuna watu wana uwezo wa kuona yasio onekana kwenye macho ya watu wengine (So called 8 senses) huo ulikuwa ni Uongo Bro.

tuseme ukweli Pascal.
 
Superpowers sio za kupublicize au kushow off, huwezi mwamini mtu au jua wanataka wakutumieje, maybe wanakutega, as many people don't officially believe in it ndo maana inakuwa ni undercover, na ndo maana people with powers wanajidistance away from people au hawainteract sana na watu.
 
Akikutajia hayo majina unitag na mie niendelee kujifunza zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…