Pugu Boys Secondary School a.k.a Pond boys

Pugu Boys Secondary School a.k.a Pond boys

Mambo ya Mzee wa Shamba na mapande ya mihogo kwa uji yalikuwa ni maisha ambayo hayawezi kusahaulika. Nakumbuka mpambano uliokuwa unatokea siku ya kishoka pamoja na uhaba wa maji duh!!!.

Maisha Pugu kwa ujumla yalikuwa ni zaidi ya jeshini.
 
Nitakuwa sijaitendea haki hii thread kama sitachangia,

Mimi pia nilipita hapa na ni mmoja wa wana-POND, Pugu ilikuwa hata aliyepata Zero amejifunza maisha.

Kulikuwa na walimu kama Swai, Charo, Msungu etc.

Kuna mwalimu mmoja kwa jina la Mabagala, duuu huyo teacher noma kishenzi, mambo ya bed check, kuamsha watu asubuhi asubuhi na mboko kama kawa. Daa noma kishenzi.
 
Nitakuwa sijaitendea haki hii thread kama sitachangia,

Mimi pia nilipita hapa na ni mmoja wa wana-POND, Pugu ilikuwa hata aliyepata Zero amejifunza maisha.

Kulikuwa na walimu kama Swai, Charo, Msungu etc.

Kuna mwalimu mmoja kwa jina la Mabagala, duuu huyo teacher noma kishenzi, mambo ya bed check, kuamsha watu asubuhi asubuhi na mboko kama kawa. Daa noma kishenzi.

Ha!ha!ha!ha!haaaaaa! Kumbe MC nawe ni walewale wa DOCEBIT VOS OMNIA heeee!

Mkuu Mwal. Msungu alishatangulia mbele za haki.......! Kamanda Mabagala aka Mabags aliendaga UDSM......sijui yupo wapi now! Ila huyu jamaa alikuwa noma.....bed check, akikuta mmelala wawili anauliza cheti cha ndoa kipo wapi....h!ha!ha!haaaaa! Aliwatukimbisa hadi Pond ya kule Mapinduzi.......!tukala forest, noma sana yule jamaaa!
 
Ninajua kunawadau wengi sana ambao katika maisha yao watakuwa wamepitia pale Pugu Secondary School kama wanafunzi, wafanyakazi, wakazi etc. Wadau hawa sasahivi wametawanyika sehemu mbalimbali ya nchi yetu na duniani kote.

Mimi binafsi ni mojawapo ya watu waliopitia pale kama dent wa high school...(form 5 to 6), ningependa tujikumbushe mambo mbalimbali kuhusu shule ile ambayo ina historia ndefu sana kwa Taifa letu. Ni shule ambayo viongozi wetu mbalimbali walishapitia pale kama wanafunzi au walimu kama vile Mwal. Nyerere, Mkapa (kama sikosei) na wengine wengi tu.

Kwa kuanza kabisa mimi nakumbuka wakati tukisoma pale, maji yalikuwa upatikanaji wake wa shida sana, kulikuwa na wadudu wa malaria na tryphoid sana, kulikuwa na Fungus acha kabisa....yaani tulikuwa tunakamatwa na fungus kiasi cha kushindwa kutembea au kutembea as if one has STDs.....jamaa mtaani mpaka wakawa wanatuita FUNGUS BOYS Mabafu halikuwa haba sana na machafu...so option ilikuwa kwenda kuogea kule mtoni tulikuwa tunakuita POND....hence tukawa tunaitwa POND BOYS.....!

Anything you remember here?


Pugu boys oyeeee!hahahahaha
fungus boys wale...Na mimi ni mdau mkuu.Nilisoma Pugu form 5&6.Kwa kweli nimejifunza mengi sana na sitajasahau maisha ya Pugu.
 
nimefurahi sana kusikia baghdad!!!!! niliacha kiatu pale masela waliomba hela ya ndumu na mimi nikawa hata 100 ya kupanda gari za chanika sina, pia kwa wale waliokuwepo till 2000 wanakumbuka jamaa mmoja alikua anaitwa Mabagala? anakukimbiza hata ukiwa uchi.

Mazee huyo mukulu tulikuwa tunamwita Mwabagala aka Mwabaks.Jamaa ni noma.Kuna story nilisikia alimfumania mshkaji pond wakati wa assemble asubuhi.Basi akaanza kumfukuza jamaa kuelekea Kisarawe.Basi mshkaji kila akigeuka nyuma Mwabaks yuko mgongoni.Ni parefu na kabla hata hawajafika nusu ya mwendo jamaa alikuwa amechoka kishenzi na Mwabaks akawa anakaribia kumkamata.Mshkaji akadhani nishatiwa mikononi mwa Mwabaks na cha moto nitakiona.
Basi Mwabaks alipomkaribia na kuona jamaa kachoka hawezi tena kukimbia,akaanza kumwambia 'mtoto mimi nakwenda kisarawe mtoto sina shida na wewe rudi shule mtoto'
Mwaba mibange ilikuwa inampeleka pabaya!
 
Last edited:
Unawakumbuka walimu wafuatao?Mabagara,Wajimira,Nzoi,Msungu(marehemu),Secondmaster Swai(marehemu),Headmaster Mtera,Mama Mukuru,Mzee Mukuru,Makono(marehemu),Teti,Mkwiche,Grace Chuma,Mamiro,Mama Mtera,Mbulanya,Godfrey Wasiwasi,Kaunda(mwalimu wa michezo 1984-1988),Mzava,Chamuriro,Mugyabuso(marehemu),Bakari Mbonde(Ex-Rufiji Mp)n.k Orodha yao ni wengi sana,waliotangulia mbele ya haki Mungu awaweke mahari panapostaili, aaaammmmmmiiiiiiiiiinnnn.

Nawakumbuka hao kwenye bold mazee.Nzoi mtaalam wa physics practicals...ukiingia darasa lake umepaka lotion utamskia na lafudhi yake ya kisukuma 'baba unapaka lotion,unataka tukuutaamani'..hahaha
Mwabagala kama kawa mzee wa ndumu.Msungu alikuwa mzee mmoja safi sana,kukiwa na hitilafu kwenye tank la maji basi mara moja ataanza kushughulika(RIP).Mama Mbulanya mtaalam wa Biology sema kwenye vipindi humuoni,mara chache sana nilikula shule yake
Huyo Godfrey Wasiwasi nadhani atakuwa Juma Wasiwasi huyo.
Kuna Ogesa na yule jamaa tolu wa kihaya Songombingo mnawakumbuka?
 
Juma Wasiwasi vipi yupo? mara ya mwisho nilisikia alikuwa anasoma Open University or UDSM. Jamaa alikuwa na misemo ya kutukana, aliniboa pale alipochukua TV ya shule akaweka nyumbani kwake.....watu walipiga kelele lakini jamaa wapi harudishi.....kelele zilipofika mbinguni akaona noma akairudisha


Hahahahaha!
Nakumbuka kipindi kile mchezo wa tausi wa kina mjuba na siti ulikuwa unapendwa kishenzi bongo na tulikuwa tunaangalia kila jumapili usiku pale mbele na dining hall karibu na bweni la ujamaa.
Jamaa alikera kichizi!
 
Umesahau na wale kina mama wauza maji,mbogamboga na samaki,bweni la mapinduzi.Mbu kibao vijana wanapiga msuli wamevaa soksi na wamejifunika neti noma sana.Mabagala noma ana speed tofauti na umbo lake jamaa anakula ndumu yule,wakati anakukimbiza utasia akisema "Kijana ongeza speed na kuovateki".Pugu boy ukimuona ameingiza mkono katika mfuko wa suruali usifikiri anakupa pesa anajikuna fangasi.Nzoi mzee wa Physics jaribu kumwita teacher class ukitaka kumuliza swali utasikia "nani Teacher hivi ndivyo mnavyowanyea wazazi wenu?" "baba unafikiri hapa mnazi mmoja" akiwa anamana umesoma tution mnazi mmoja then unataka kum challenge.Currently Pugu Kuna geti na kaukuta ka kiushikaji.



Oyaa unamkumbuka mama dagaa??Bili za maandazi kwa mama Pendo??
 
Mkandawire ni DADA? Mi namkumbuka yule Mkandawire majasiriamali......mzee wa machemistry......, alikuwa maarufu sana miaka ya 97 hadi 2003 hivi......?


Nani aliwahi kwenda tution za Mkandawile pale Buguruni na watoto wa Jangwani?Jamaa alikuwa anawapigia debe kichizi mapugu boys kwa majangwani boys!!
Kuna mtu anajua huyu mjasiliamali yuko wapi na anafanya nini sasa?Manake alikuwa anaipenda pugu na mapugu boys utafikiri wanae!
Anyway namshukuru sana Mkandawile manake bila yeye nisingefaulu chemistry pugu.
 
Nani aliwahi kwenda tution za Mkandawile pale Buguruni na watoto wa Jangwani?Jamaa alikuwa anawapigia debe kichizi mapugu boys kwa majangwani boys!!
Kuna mtu anajua huyu mjasiliamali yuko wapi na anafanya nini sasa?Manake alikuwa anaipenda pugu na mapugu boys utafikiri wanae!
Anyway namshukuru sana Mkandawile manake bila yeye nisingefaulu chemistry pugu.

MImi nilimuacha mkandawire dada pale miaka ya mwanzo ya tisini, alikuwa anajitahidi aisee!!

I wish tungekuwa na alumni ya Pugu kwenye yahoo groups na vilevile tungefanya bash moja la karne hasa katika kipindi cha kumuenzi nyerere

Hivi yule ticha nyoka yuko wapi?
 
Nani aliwahi kwenda tution za Mkandawile pale Buguruni na watoto wa Jangwani?Jamaa alikuwa anawapigia debe kichizi mapugu boys kwa majangwani boys!!
Kuna mtu anajua huyu mjasiliamali yuko wapi na anafanya nini sasa?Manake alikuwa anaipenda pugu na mapugu boys utafikiri wanae!
Anyway namshukuru sana Mkandawile manake bila yeye nisingefaulu chemistry pugu.
Sikusoma pugu najua ni boys skul, ila nilisoma tution za Mkandawile alipokuwa anafundisha mtendeni primary school na mchikichini, alinipatia elimu nzuri sana kwenye organic chemistry. Ila Siku hizi ana shule yake binafsi ipo mitaa ya Pugu. Inaitwa jina lake Mkandawile high school. Mambo yake siku hizi yapo swafiii.
 
Mimi nilihamia pale mwaka 1993 nikiwa form 4, nilisoma mwaka mmoja lakini ilikuwa kama miaka 10. Nakumbuka siku ya kwanza nilipofika pale baada ya chakula niliona kila mmoja anatoa dumu la maji ya kunywa kutoka katika locker lake, kwa siku hii nilipewa maji na rafiki yangu tuliyesoma nae primary school. Then after ilibidi kila jioni baada ya chakula kwenda kunywa maji mwisho wa lami (imagine that distance), jumamosi yake nami nilitoka nyumbani Dar na dumu langu la maji. Yaani ilikuwa ukipanda basi siku ya jumapili kutoka Dar kila mwanafunzi na galon ya maji ya kunywa. IT WAS TERRIBLE!!!!....!!

Nawakumbuka baadhi tuliokaa nao pale Ujamaa 5 or 3 kama sikosei, bweni lililokuwa linakaa wajanja ambao walikuwa na special attention, nawakumbuka jamaa wawili walikuwa wanaitwa WACHINA nimesahau majina yao. Nawakumbuka Peter Shija, Michael Nandonde, David Mahalu.......,

Kama hapa jamvin yupo aliyemaliza f4 mwaka 1993 naomba tukumbushane majina.
Wale Wachina walihamia Pugu toka china.Nafikiri baba yao alikuwa ofisa kwenye ubarozi wa Tanzania nchini China,nakumbuka walipohamia pale walilala njaa sana kwa kukosa chakula,kwenye kundi la akina peter kulikuwa na kijana mmoja anaitwa Mboka.Nilisikia huyo Peter Shija alikuwa anakaa kigamboni,na mwingine kwenye kampani hiyohiyo alikuwa anakaa Ukonga,namkumbuka Mkandaliwe na Chemisty yake,those time alikuwa bint mdogo nafikiri ndio alikuwa katoka chuo
 
Last edited:
Duh kweli Pugu tulikua na experience za kila namna! Miaka ya karibuni waliintroduce elimu ya watu "wazima" ambayo ilikua ni shule ndani ya shule. Yaani baada ya masomo wao wanaingia mchana. Kasheshe ilikua hao watu "wazima" walikua ni same age na ma-pugu boys alafu ilikua mchanganyiko. Basi ma-pugu boys walikua wanapenda sana kuwasindikiza hao wasichana mpaka mwisho wa lami na kuwanunulia chips!

Namkumbuka sana Mama Pendo na Mama Khalidi, walitusaidia sana na misosi yao. Nakumbuka siku moja dogo mmoja wa O-level alienda pondi akaja na upupu akaweka bweni zima kisa kuna mtu alikua anamdai alafu hataki kumlipa!

Pugu ilikua na sifa sana siku izo hasa kwa A-level kwani walikua wanajua wanachofanya...kwa O-level wengi hawakua siriaz sana na kitabu. Halafu Mabagala was the perfect ticha for such a school sababu hakukua na sheria wala fensi.Mtu ukitaka 'kudrop' town unadrop tu anytime....

Sitasahau my two years of A level at Pugu....the best part is ..kila unapokua town unakutana na Pugu boys wanakukumbusha mlikua darasa moja au uliwatangulia darasa inatia furaha sana!!! Long live Pugu...Docebit Vos Omnia... ("He-The Holy Spirit, will teach you all")

So many memories za Pugu...ngoja niishie hapa....
 
Mimi nilihamia pale mwaka 1993 nikiwa form 4, nilisoma mwaka mmoja lakini ilikuwa kama miaka 10. Nakumbuka siku ya kwanza nilipofika pale baada ya chakula niliona kila mmoja anatoa dumu la maji ya kunywa kutoka katika locker lake, kwa siku hii nilipewa maji na rafiki yangu tuliyesoma nae primary school. Then after ilibidi kila jioni baada ya chakula kwenda kunywa maji mwisho wa lami (imagine that distance), jumamosi yake nami nilitoka nyumbani Dar na dumu langu la maji. Yaani ilikuwa ukipanda basi siku ya jumapili kutoka Dar kila mwanafunzi na galon ya maji ya kunywa. IT WAS TERRIBLE!!!!....!!

Nawakumbuka baadhi tuliokaa nao pale Ujamaa 5 or 3 kama sikosei, bweni lililokuwa linakaa wajanja ambao walikuwa na special attention, nawakumbuka jamaa wawili walikuwa wanaitwa WACHINA nimesahau majina yao. Nawakumbuka Peter Shija, Michael Nandonde, David Mahalu.......,

Kama hapa jamvin yupo aliyemaliza f4 mwaka 1993 naomba tukumbushane majina.

Stan, kweli wewe ulikuwa mtoto wa mama!!!

Mimi nimesoma Pugu A-Level miaka hiyohiyo kwa raha sana na zile adventure za kwenda mwisho wa lami au Gombs kwenye mnanda na watoto wa gombs ilikuwa tamu tupu. nakumbuka tulikuwa tunakutana na wale wanajeshi pale mwisho wa lami, na kutimua mbio maana jamaa walikuwa wana njaa ya kufa mtu.

Shija nadhani yuko Uk, walikuwa wadogo zetu wa O-level by then...

Unakumbuka tulikuwa na timu nzuri sana ya footbal miaka hiyo?
 
Stan, kweli wewe ulikuwa mtoto wa mama!!!

Mimi nimesoma Pugu A-Level miaka hiyohiyo kwa raha sana na zile adventure za kwenda mwisho wa lami au Gombs kwenye mnanda na watoto wa gombs ilikuwa tamu tupu. nakumbuka tulikuwa tunakutana na wale wanajeshi pale mwisho wa lami, na kutimua mbio maana jamaa walikuwa wana njaa ya kufa mtu.

Shija nadhani yuko Uk, walikuwa wadogo zetu wa O-level by then...

Unakumbuka tulikuwa na timu nzuri sana ya footbal miaka hiyo?

Kaka unanikumbusha timu ya kina Juma Ally!
 
Wazee wa Docebit, naskia pugu imeshapata maji, ni kweli??
 
Wazee wa Docebit, naskia pugu imeshapata maji, ni kweli??

Kaka mara ya mwisho kufika Pugu Semi University ni mwaka 1995 that time Head Master alikuwa anakaimu, lakini maji yalikuwa bado!
 
Wazee wa Docebit, naskia pugu imeshapata maji, ni kweli??

Mkuu hizo ni ndoto, nimepita pale last year hakuna kitu hicho, ila wapewa maji ya kisima kipo karibu na bwalo au kiduka cha shule or kibaa cha maticha ile njia ya kwenda masjid........!
 
Mazee huyo mukulu tulikuwa tunamwita Mwabagala aka Mwabaks.Jamaa ni noma.Kuna story nilisikia alimfumania mshkaji pond wakati wa assemble asubuhi.Basi akaanza kumfukuza jamaa kuelekea Kisarawe.Basi mshkaji kila akigeuka nyuma Mwabaks yuko mgongoni.Ni parefu na kabla hata hawajafika nusu ya mwendo jamaa alikuwa amechoka kishenzi na Mwabaks akawa anakaribia kumkamata.Mshkaji akadhani nishatiwa mikononi mwa Mwabaks na cha moto nitakiona.
Basi Mwabaks alipomkaribia na kuona jamaa kachoka hawezi tena kukimbia,akaanza kumwambia 'mtoto mimi nakwenda kisarawe mtoto sina shida na wewe rudi shule mtoto'
Mwaba mibange ilikuwa inampeleka pabaya!

Mkuu P53 Respect! Hapo kwenye bold nimecheka sana mzee......lile lijamaa lilikuwa noma sana!

Oyaa unamkumbuka mama dagaa??Bili za maandazi kwa mama Pendo??

Ha!ha!ha!haaaaa.....Mama Pendo + Pendo mwenyewe we acha tu....ile miandaazi yake ilikuwa poa kweli si tulikuwa tunampiga bao kweli.....ila kale ka Pendo.....mzee kalikuwa kametulia........! mzee unawakumbuka wale chokoraa...watoto wama ex Pugu boys.....hawana baba now? ...wakuu yeyote aliyegonga demu pale, si tulikuta vitoto vingi sana vya ma ex Pugu boys so please rudini mkacheki kuna damu zenu pale!

Mkuu ulikuwa unasoma kombi gani?Nilikuwa PCB na niligudua 2000.

Mzee nilikuwa next to your class....EGM na mzee Msungu, Shire na yule teacher Mhaya wa Hesabu! Mkuu utakuwa ulikuwa na kina Mwatebele, Matobogolo Masalu etc sio?
 
Back
Top Bottom