TANZIA Pumzika kwa amani Pudenciana Temba

TANZIA Pumzika kwa amani Pudenciana Temba

Hivi huyu mama sio yule alikua anaishi mbezi beach, alikuwa na mtoto wa kike mrembo hivi.
anyway nitauliza, hizi picha zimenipoteza, lakini maelezo ni kama ninayemfikiria.

poleni sana.
 
Mzee rika lako wanapukutika.

Pole sana .
Dr.
Hapana.
Nimekuwa nikifiwa na wenzangu.
Nikiwa na umri kiasi cha miaka 7 hivi nilifiwa na rafiki yangu Abdul.

Abdul alikuwa umri sawa na mimi alipata kidonda mguuni na ndiyo ikawa sababu ya kifo chake.

Katika kipindi cha maisha yangu hali imekuwa hivi.
Hakuna cha ajabu.
 
TAAZIA: PUDENCIANA TEMBA

Majonzi.
Inachoma sana moyo.

Ikiwa mtakumbuka miezi michache sana hapa hapa niliwekewa kumbukumbu ya kifo cha Dr. Edith Kitambi nami kwa kuwa sikupata taarifa ya kifo chake nikaandika taazia.

Edith katika picha ni huyo dada kulia kwangu.
Nimesoma kifo cha Pudenciana Temba alipata kuwa Editor Daily News.

Pudenciana ni huyo kulia kwangu kwenye picha.

Pudenciana alikuwa mwanafunzi School of Journalism University of Wales Carfiff.

Picha hii imenitia majonzi sana.

Hawa dada zangu niliishinao kwa wema na ni bahati mbaya sana kuwa tulipoachana Uingereza hatukapata kuonana tena hadi napokea taarifa ya vifo vyao.

R.I.P Pudenciana Temba, Mwendo umeumaliza salama katika dunia hii 🤭
 
Mzee ulikuwa una bahati iliyoje kuzungukwa na warembo wakali namna hio?
100...
Nilipokuwa mtoto kiasi miaka 5/6 hivi marehemu mama yangu akiniambia, "Mohamed wewe Mashaallah una maji ya nguo."

"Maji ya nguo," maana yake ni ukivaa nguo zinakupendeza.

Kisha anaongeza anasema kuwa Mashaallah nina, "Sudi."

"Sudi" maana yake ni "Kupendwa."

Basi mama atamalizia kwa kusema, "Hao akina mama ndiyo wa kuangalia vinginevyo watakuangamiza."
 
TAAZIA: PUDENCIANA TEMBA

Majonzi.
Inachoma sana moyo.

Ikiwa mtakumbuka miezi michache sana hapa hapa niliwekewa kumbukumbu ya kifo cha Dr. Edith Kitambi nami kwa kuwa sikupata taarifa ya kifo chake nikaandika taazia.

Edith katika picha ni huyo dada kulia kwangu.
Nimesoma kifo cha Pudenciana Temba alipata kuwa Editor Daily News.

Pudenciana ni huyo kulia kwangu kwenye picha.

Pudenciana alikuwa mwanafunzi School of Journalism University of Wales Carfiff.

Picha hii imenitia majonzi sana.

Hawa dada zangu niliishinao kwa wema na ni bahati mbaya sana kuwa tulipoachana Uingereza hatukapata kuonana tena hadi napokea taarifa ya vifo vyao.

pole sana shekh, uingereza ni nchi ya makafiri, wewe huwa unaita wakristo kuwa ni makafiri, ilikuaje sasa ukaenda kutembelea na kula mema huko uingereza? tupe story kidogo.
 
pole sana shekh, uingereza ni nchi ya makafiri, wewe huwa unaita wakristo kuwa ni makafiri, ilikuaje sasa ukaenda kutembelea na kula mema huko uingereza? tupe story kidogo.
Yes...
Sijapata kutoa maneno hayo.

Isiwe umeyasoma kwa Mohamed Said mwingine.

Hakikisha kabla ya kuandika kuzuia fedheha kwako na kwangu.
 
Yes...
Sijapata kutoa maneno hayo.

Isiwe umeyasoma kwa Mohamed Said mwingine.

Hakikisha kabla ya kuandika kuzuia fedheha kwako na kwangu.
nilishawahi kukusikia, ulikuwa unajadili namna waislam walivyopigwa mwembechai, namna mnavyoenda kuhiji, haya maneno uliyaongea, sema kwasababu kila binadamu ana madhaifu labda useme tu uliteleza, na wewe unapenda watu wote wakristo kwa waislam, na hautaki makafiri wauawe. ukisema hivyo nitakuelewa sana mzee. usijisahaulishe, sijakujua leo.
 
Pole sana Mzee Mohamed Said kwa msiba huu. Mwenyezi Mungu awajalie pumziko la Amani na la Milele. Amina.
 
Back
Top Bottom