Putin asema operesheni ya Urusi nchini Ukraine imefanikiwa

Putin asema operesheni ya Urusi nchini Ukraine imefanikiwa

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Rais wa Urusi, Vladmir Putin amesema kuwa operesheni yake ya kijeshi nchini Ukraine imefanikiwa na kuwa hatoiruhusu nchi hiyo kutumika kama uwanja wa kuitishia Urusi.

Akizungumza katika mkutano wa serikali uliorushwa moja kwa moja kwenye televisheni, Putin amesema operesheni yake inaendelea vizuri kwa kufuata kikamilifu mipango waliyoiweka.

Rais huyo ameongeza kuwa Benki Kuu ya Urusi haina haja ya kuchapisha pesa kwa kuwa nchi hiyo ina rasilimali za kutosha za kifedha za kukabiliana na changamoto za sasa za vikwazo.

Mazungumzo kati ya pande hizo mbili za kivita yanaendelea kwa sasa huku kila mmoja akielezea matumaini ya kupatikana suluhu.

Source: DW
 
Screenshot_20220317-065610_RT News.jpg
Screenshot_20220317-065626_RT News.jpg
Screenshot_20220317-065724_RT News.jpg
 
Back
Top Bottom