Putin atoa masharti yake ya kumaliza vita yake na Ukraine, na hivyo kuondoa majeshi yake kwenye nchi hiyo

Putin atoa masharti yake ya kumaliza vita yake na Ukraine, na hivyo kuondoa majeshi yake kwenye nchi hiyo

Urusi imetia aibu kubwa sana, kwa jeshi hili ni vizuri vile Putin hataki NATO wamsogelee zaidi kwani siku wakimwamkia ndani ya wiki wanakamata nchi yote. Anapigana bega kwa bega na Belarus ila output kubwa mpaka sasa ni kuvunja majengo. Zaidi ya nuclear warheads alizonazo hana maajabu yoyote.
Hivi unadhani Ukraine ni kama rwanda?? Ukraine ni kubwa mara tatu ya Tanzania huoni hata mafanikio ya Urusi au unadhani vita ni kama kukimbia mbio tu?
 
Kama ulikua hujui kuwa URUSI ni Nchi nzuri sana na viongozi wake ni wastaarabu sana wacha nikufahamishe;-
Huo Ndio ukweli URUSI Ndio Nchi Kubwa Kuliko zote duniani,
Urusi ni nchi namba mbili kwa ukubwa wa Jeshi duniani,
Ni Nchi ya kwanza Kwa kuzalisha gesi Duniani,
Na ni Nchi ya pili Kwa kuzalisha mafuta Duniani,
URUSI ndio nchi pekee Duniani inayopakana na mabara mawili yaani upande mmoja wa nchi ipo Barani ASIA na upande mwengine wa nchi ipo Barani ULAYA,
Lakini pia Watu wake wengi wamesoma na wanauwezo Mkubwa kiuchumi, kiteknolojia, na kijeshi,
Lakini Pamoja na sifa zote hizo hawajawahi kuwafanyia ubaya wowote wa AFRIKA,
Sasa wewe muafrika unaanzaje kuichukia URUSI na kuwapenda NATO wakati wao wamefanya mambo ya hovyo mengi AFRIKA,
Waafrika inabidi tuamke na kuipenda URUSI kwasababu zifuatazo;-

1) URUSI Hajawahi kuchukua watumwa Afrika

2)Urusi haijawahi kuitawala Afrika kiukoloni.

3) URUSI haijawahi kushiriki Berlin conference, mkutano wa kuigawa Afrika.

4) URUSI hawajahi kupora rasilimali za Afrika.

5) URUSI haijawahi kuweka mikataba ya kilaghai na Machifu wa Afrika.

6) URUSI haijawahi Kupora Ardhi ya Afrika au kuwa mlowezi wa Afrika Kama wale waliopo south Afrika, Kenya na wale walionyang'anywa ardhi na Mugabe kule Zimbabwe.

7) URUSI haijawahi kuivamia kijeshi Afrika Kama Yale majeshi ya NATO inchini Libya.

Makala hii imeletka kwenu na Dhulkad Madara Kutoka Morogoro
Hizi ni sababu mfu kabisa.
 
Mmh..sema putin ametreand sana kpnd hiki..but hope izo no propaganda,kama aeamia kukiwasha akiwashe mazima.
 
Aisee mkuu yawezekana wewe ukawa na intelijensia na ufahamu mkubwa zaidi juu ya jeshi la Russia kuliko hata Defense Secretary wa Marekani General Lloyd Austin anayesema kuwa Russia bado wana uwezo na nguvu kubwa mno ya kuishambulia Ukraine ambayo bado hawajaamua kuitumia.

Itakusaidia zaidi siku ukiamua kuacha ubishi na kutaka kujifunza zaidi. Tunazungumzia nguvu aliyoitumia Urusi mpaka sasa na alichokipata kulinganisha na matarajio ya awali. Ana nukes ambazo hajatumia.
 
Itakusaidia zaidi siku ukiamua kuacha ubishi na kutaka kujifunza zaidi. Tunazungumzia nguvu aliyoitumia Urusi mpaka sasa na alichokipata kulinganisha na matarajio ya awali. Ana nukes ambazo hajatumia.
Generali Lloyd Austin hajaongelea stori za silaha za nyuklia, wala haamini kuwa Putin anaweza au ahitajia kutumia silaha hizo Ukraine. Yeye ana ujuzi na taarifa zaidi za jeshi la Russia kuliko wewe. Sasa tuchukue stori zako wewe ambaye hata pengine hujawahi kushuhudia kwa macho yako tu vita ilivyo, au tuchukue kauli ya General Austin ambaye amewahi kuongoza vikosi vya Marakani ktk vita ya Iraq?

BTW, huyu hapa chini anakujibu zaidi ujue nguvu za Russia
SmartSelect_20220302-120342_Chrome.jpg
 
Punguza munkari, uongozi wa NATO ni rotational na sasa uongozi upo kwa Ufaransa, ndio maana unaona Macron anafanya mawasiliano kwa niaba ya NATO.
Hapo sawa nimekuelewa Boss!! lkn bado la pili hili kiherehere cha wao kutoka mbaali vile kuja kutaka kusaidia huku ni uchokozi wa wazi!!
 
Japo msimamo wangu ni kila nchi iwe huru kujiamulia mambo yake na Urusi hana haki ya kuamua maslahi ya Ukraine lakini sioni ulazima wa Ukraine kujiunga NATO kwa gharama ya kuhatarisha amani ya dunia, na pia sioni ulazima wa USA/NATO kuweka silaha zake Ukraine kwa gharama hiyo hiyo ya kuhatarisha amani ya dunia.
Mkuu ni sawa na kumlazimisha binti aolewe na akikataa atauawa
Binti akikataa na process za kumuua zikianza uanze tena kusema unaunga mkono uhuru wa kuamua lakini huoni ulazima wa binti kukataa kwa gharama ya kunyongwa

Uhuru wa masharti sio uhuru tena
 
Hapo sawa nimekuelewa Boss!! lkn bado la pili hili kiherehere cha wao kutoka mbaali vile kuja kutaka kusaidia huku ni uchokozi wa wazi!!
Anachofanya Urusi ni sawa na mtu atoke anakotoka aje kwako kukupangia watu gani wawe rafiki zako. Ikifika hatua ambapo taifa moja linaweza kujiamulia kupiga taifa lingine kwa sababu zake, bila mataifa mengine kuweza kumsaidia anayeonewa, basi hii dunia itakuwa imekaribia mwisho.
 
Generali Lloyd Austin hajaongelea stori za silaha za nyuklia, wala haamini kuwa Putin anaweza au ahitajia kutumia silaha hizo Ukraine. Yeye ana ujuzi na taarifa zaidi za jeshi la Russia kuliko wewe. Sasa tuchukue stori zako wewe ambaye hata pengine hujawahi kushuhudia kwa macho yako tu vita ilivyo, au tuchukue kauli ya General Austin ambaye amewahi kuongoza vikosi vya Marakani ktk vita ya Iraq?

BTW, huyu hapa chini anakujibu zaidi ujue nguvu za Russia
View attachment 2137128
Wewe ni mtu wa kupuuzia.
 
Anachofanya Urusi ni sawa na mtu atoke anakotoka aje kwako kukupangia watu gani wawe rafiki zako. Ikifika hatua ambapo taifa moja linaweza kujiamulia kupiga taifa lingine kwa sababu zake, bila mataifa mengine kuweza kumsaidia anayeonewa, basi hii dunia itakuwa imekaribia mwisho.
Mbona hayo ndo anafanya M marekani kila siku. Au mkuki kwa nguruwe
 
Tufanye Russia arudi she makombora yake ya nukes pale Cuba kama alivyo fanya 1963. Je USA atakubali ingali Cuba ni nchi huru inayoweza kujiamulia chochote
 
Urusi imetia aibu kubwa sana, kwa jeshi hili ni vizuri vile Putin hataki NATO wamsogelee zaidi kwani siku wakimwamkia ndani ya wiki wanakamata nchi yote. Anapigana bega kwa bega na Belarus ila output kubwa mpaka sasa ni kuvunja majengo. Zaidi ya nuclear warheads alizonazo hana maajabu yoyote.

Sawa msemaji wa NATO,,,Eti nchi yote 😁😁😁😁 huwa mnawaza nini kabla hamjaongea!!😁😁

Wakazi wa tandale bwana
 
Urusi imetia aibu kubwa sana, kwa jeshi hili ni vizuri vile Putin hataki NATO wamsogelee zaidi kwani siku wakimwamkia ndani ya wiki wanakamata nchi yote. Anapigana bega kwa bega na Belarus ila output kubwa mpaka sasa ni kuvunja majengo. Zaidi ya nuclear warheads alizonazo hana maajabu yoyote.

Sawa msemaji wa NATO,,,Eti nchi yote 😁😁😁😁 huwa mnawaza nini kabla hamjaongea!!😁😁

Wakazi wa tandale bwana
 
Sawa msemaji wa NATO,,,Eti nchi yote [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] huwa mnawaza nini kabla hamjaongea!![emoji16][emoji16]

Wakazi wa tandale bwana
Nimeona umenukuu mara mbilimbili nikadhani una hoja,wewe tokea kwenye mada zako za udini nilishakupotezea siku nyingi.
 
Back
Top Bottom