Pwani: Ajali ya Magari imeua Watu 21 na wengine 15 kujeruhiwa. Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi

Pwani: Ajali ya Magari imeua Watu 21 na wengine 15 kujeruhiwa. Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi

Soma post namba 46 hapo juu imeeleza chanzo cha ajali. Coaster mbili zilikuwa zinafukuzana, ndipo tairi ya coaster ikapasuka ghafla na coaster ikayumba ( kuhamaupande wake) na kwenda kugongana uso kwa uso na lori.
Uzembe wa dereva! Ukiwa unaendesha chombo cha moto usijiamini asilimia 100 kuwa upo salama, unapaswa kuchukua tahadhari lolote linaweza tokea hata kama gari yako ni mpya au umepiga service ya maana.
Kama hivi hapa dereva angechukua tahadhari kwa kwenda mwendo wa wastani madhara yangekuwa madogo na angeokoa maisha ya watu.
Pale kilimahewa mbona pako vizuri tu tena Hakuna kona wala mashimo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Coaster ina uwezo wa kubeba abiria 22-25, sasa hiyo number ya majeruhi + marehemu unapata thelathini na ushehe plus ambao hawajajeruhiwa unapata ngapi?
Hio ni Rosa, huwa ina cabin ndefu zaidi na viti vingi zaidi.
 
Hii ajali nimempoteza kaka yangu na binamu wa huyo kaka.

Kaka yangu(best ya kaka wa kuzaliwa tumbo moja) alikua dereva wa hiyo Rosa na binamu yangu kondakta..
Pia tumewapoteza matajiri wa kijiji cha magawa BM na Mfaume binadamu wabaya sana wamechukua pesa zote 1.6 alizokua nazo marehemu Kaka,BM awamemchukulia pesa zote 2.8M na Mfaume 6M walizokua wanafuata bidhaa mjini, watu wameanza kuchukua hela kabla ya kutoa msaada Mungu awalaani wote.

Msiba ulikua mkubwa sana kijiji kilizizima watu ilibidi tujigawe katika kuzika wengine walienda huku wengine kule gari ya maiti ilikua inashusha maiti hapa wengine wanabaki wengine wanaenda hivyo hivyo mpaka mwisho.

Chanzo cha ajali

Kuliko na gari mbili moja Rosa maarufu kwa jina la Mchilu(iliyokua inaendeshwa na marehemu) na nyingine Coaster(box maarufu kwa jina la Mama Peter) hizi gari zilikua zinafukuzana Mama Peter Mbele na Mchilu nyuma.Walipofika kilima hewa Mama Peter alisimama njiani bila kutoka kwenye barabara kuchukua abiria,Mchilu ilipoona hivyo ikabidi itanue lakini alikua spidi hamadi anakutana na Scania iliyokua inafuata tiles Mkiu na pale kulikua na kona pembeni kuna hospital..Rosa ikabidi itoke nje ya barabara kuikwepa ile Scania na ile Scania nae alikua na akili hiyo hiyo hivyo zikakutana uso kwa uso nje ya barabara na kila gari kugeuka kule ilipotokea..wengine walikufa kutokana na uzembe wa watu kujali mali kuliko uhai wa watu.

kuona maiti ya mtu unaemfahamu akiwa imeharibika kiasi kile ni jambo gumu sana sikuwahi kuwaza kama Bro angekufa kifo kile alivunjika kiuno,miguu,mikono,kichwa kimepasuka la haula kifo kibaya sana.Marehemu ameacha wake wawili na watoto watano na gari aliyokua akiendesha ni ya kaka ake ambayo tarehe 18 mwezi huu inatimiza mwezi.


Nimejaribu kueleza tu yale ninayoyafahamu jana tumewazika wote,tunamshukuru mbunge wa mkuranga Mh Abdallah Ulega kutoa sanda na gari ya maiti ,,, Mungu azilaze roho za marehemu panapostahili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ajali nimempoteza kaka yangu na binamu wa huyo kaka.

Kaka yangu(best ya kaka wa kuzaliwa tumbo moja) alikua dereva wa hiyo Rosa na binamu yangu kondakta..
Pia tumewapoteza matajiri wa kijiji cha magawa BM na Mfaume binadamu wabaya sana wamechukua pesa zote 1.6 alizokua nazo marehemu Kaka,BM awamemchukulia pesa zote 2.8M na Mfaume 6M walizokua wanafuata bidhaa mjini, watu wameanza kuchukua hela kabla ya kutoa msaada Mungu awalaani wote.

Msiba ulikua mkubwa sana kijiji kilizizima watu ilibidi tujigawe katika kuzika wengine walienda huku wengine kule gari ya maiti ilikua inashusha maiti hapa wengine wanabaki wengine wanaenda hivyo hivyo mpaka mwisho.

Chanzo cha ajali

Kuliko na gari mbili moja Rosa maarufu kwa jina la Mchilu(iliyokua inaendeshwa na marehemu) na nyingine Coaster(box maarufu kwa jina la Mama Peter) hizi gari zilikua zinafukuzana Mama Peter Mbele na Mchilu nyuma.Walipofika kilima hewa Mama Peter alisimama njiani bila kutoka kwenye barabara kuchukua abiria,Mchilu ilipoona hivyo ikabidi itanue lakini alikua spidi hamadi anakutana na Scania iliyokua inafuata tiles Mkiu na pale kulikua na kona pembeni kuna hospital..Rosa ikabidi itoke nje ya barabara kuikwepa ile Scania na ile Scania nae alikua na akili hiyo hiyo hivyo zikakutana uso kwa uso nje ya barabara na kila gari kugeuka kule ilipotokea..wengine walikufa kutokana na uzembe wa watu kujali mali kuliko uhai wa watu.

kuona maiti ya mtu unaemfahamu akiwa imeharibika kiasi kile ni jambo gumu sana sikuwahi kuwaza kama Bro angekufa kifo kile alivunjika kiuno,miguu,mikono,kichwa kimepasuka la haula kifo kibaya sana.Marehemu ameacha wake wawili na watoto watano na gari aliyokua akiendesha ni ya kaka ake ambayo tarehe 18 mwezi huu inatimiza mwezi.


Nimejaribu kueleza tu yale ninayoyafahamu jana tumewazika wote,tunamshukuru mbunge wa mkuranga Mh Abdallah Ulega kutoa sanda na gari ya maiti ,,, Mungu azilaze roho za marehemu panapostahili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuu!!! Poleni Sana.

Matukio yote hayo siku moja?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Barabara ile ni nyembamba sana. Gari zinapopishana kwa kasi ikitokea moja ikakata wimbi la lami tu mwafwa!
 
Yeah ndo hivyo ndugu niko na huzuni sana dereva alikua mtu poa sana japo kuhusu mwendo kwake ilikua kama chakula...siku moja aliwahi kusema "Mimi sitaki nipate ajali afu niwe kilema niteseke ,nikipata ajali nataka waokote vipande sitaki mambo ya kuuguzwa..kweli kimetokea kile alichoomba japo ajali kwa asilimia 90 ajali imesababishwa na hiyo coaster nyingine maarufu kama Mama Peter kwa kusimama ghafla barabarani ili achukue abiria bila kuingia kituoni"
Ni kweli ilikuwa ni overtaking tu, aliyeniambia alikurupuka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
R.I.P

"Cᵒᵃᶜᵏʳᵒᵃᶜʰ ⁿᵘʰ ᵇᵘˢˢⁱⁿᵉˢˢ ⁱⁿⁿᵃ ᶠᵒʷˡ ᶠⁱᵍʰT"
 
Yeye mwenyewe ndio chanzo,
unataka nini tena

R I P
Yeye ndiye mtu gani huyo mbona mpenda kurahisisha mambo hivyo kama huna data kaa kimya wenye data za uhakika walete sio majungu na umbea tu kila saa.
 
Yeah ndo hivyo ndugu niko na huzuni sana dereva alikua mtu poa sana japo kuhusu mwendo kwake ilikua kama chakula...siku moja aliwahi kusema "Mimi sitaki nipate ajali afu niwe kilema niteseke ,nikipata ajali nataka waokote vipande sitaki mambo ya kuuguzwa..kweli kimetokea kile alichoomba japo ajali kwa asilimia 90 ajali imesababishwa na hiyo coaster nyingine maarufu kama Mama Peter kwa kusimama ghafla barabarani ili achukue abiria bila kuingia kituoni"

Sent using Jamii Forums mobile app

Ni kweli kasimama gafla lakini hao si kama walikuwa wanafukuzana? Maana kama wangementain distance na speed ingekuwa wastani sidhani kama yangekuwa makubwa, unajua hapo ilipotokea ajali ni zebra shule ya msingi kilimahewa kaskazini ndipo niliposoma miaka 7 hapo shule ya msingi. Napajua vizur hilo eneo.
 
Yeye ndiye mtu gani huyo mbona mpenda kurahisisha mambo hivyo kama huna data kaa kimya wenye data za uhakika walete sio majungu na umbea tu kila saa.
Aiseee pole sana mkuu
Nafikiri sikuelewa na sikueleweka pia
Iliulizwa hivi "chanzo?"
Nikafikiri chanzo cha hii taarifa ni kipi? Jibu likaja ni yeye mwenyewe!

Kumbe wengi mmeelewa chanzo cha ajali
 
Back
Top Bottom