QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

now nimefika ngoja nishushe za kutosha za haja kwa wale mlio lalamika kuwa siku za kazi sio rafiki sana itabidi mjikaze sababu week end nilizingua.now nikiweka sehem kumi na 5 au 20 hivi sio mbaya
 
now nimefika ngoja nishushe za kutosha za haja kwa wale mlio lalamika kuwa siku za kazi sio rafiki sana itabidi mjikaze sababu week end nilizingua.now nikiweka sehem kumi na 5 au 20 hivi sio mbaya
ziko wapi....[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] ...?????
 
sEHEMU YA 45

Japokuwa hakuweza kupata usingizi wa
kutosha usiku kutokana na kichwa chake
kujawa na mawazo mengi lakini Monica
aliwahi kudamka asubuhi akajiandaa kwa
ajili ya kuianza siku.Alipata kifungua
kinywa kabla hata ya wazazi wake
hawajaamka kisha akatumia gari la mama
yake akaelekea nyumbani kwake
.Alisalimiana na wafanyakazi wake kama
ilivyo ada halafu akaelekea chumbani
kwake ambako alioga na kubadili mavazi
akajiweka tayari kwa ajili ya kwenda
kazini.Wakati akiendelea kujiandaa simu
yake ikaita.Akaichukua na kutazama
mpigaji zilikuwa ni namba ngeni kabisa
katika simu yake.
“ Hallow “ akasema baada ya
kubonyeza kitufe cha kupokelea
“ Hallow Monica” ikasema sauti ya
upande wa pili ambayo Monica aliweza
kuitambua mara moja ilikuwa ni sauti ya
David Zumo
“ Mheshimiwa rais ..!! akasema
Monica
“ Umeamkaje Monica?
‘ Nmeamka salama Mheshmiwa rais
,sijui wewe”
“ Mimi niko salama.Nimeona
nikupigie asubuhi hii kujua maendeleo
yako”
“ Nashukuru sana mheshimiwa rais
kwa kunijulia hali.Ninaendelea vizuri “
akasema Monica huku sura yake ikiwa na
tabasamu kubwa
“ Nafurahi kusikia hivyo
Monica.Nataka nikushukuru vile vile kwa
kukubali mwaliko wa kuja kuonana nami
jana”
“ Mheshimiwa rais mimi ndiye
ninayepaswa kukushukuru kwa kunialika
jana na kwa mchango mkubwa
ulionichangia.”
“ Usijali Monica huu ni mwanzo tu wa
kukuunga mkono katika juhudi zako za
kusaidia
watu
wenye
uhitaji.Nitashirikiana nawe katika mambo
mengi.” Akasema David Zumo
“ Ahsante sana mheshimiwa rais”
“ Monica leo tunamaliza mkutano
wetu wa wakuu wa nchi za maziwa makuu
lakini sintaondoka kwani nilikuahidi
kwamba ninahitaji kuonana na wazazi
wako jioni ya leo.Nitafurahi zaidi iwapo
utaongozana nao”
“ Usijali mheshimiwa rais nitakuja
nao .Tunashukuru sana kwa heshima hii
kubwa unayotupa familia yetu” akasema
Monica
“ Haya nashukuru sana Monica
.Tutaonana hiyo jioni” akasema David
Zumo na kukata simu.
“ oh my gosh !! He called me ....”
Akasema Monica kwa furaha akiwa
ameiweka mikono yake kifuani
“ Sikutegemea kama David Zmo
anaweza akanipigia simu.Huyu ni mtu
mkubwa sana kunipigia simu mtu kama
mimi ni heshima kubwa.Ninajiona
mwenye bahati kubwa kuwa na ukaribu
na mtu kama huyu.” Akawaza Monica na
kuchukua mkoba wake akatoka kuelekea
ofisini kwake.
Akiwa garini bado kichwa cha
Monica kiliendelea kujawa na mawazo
mengi kuhusiana na David Zumo na hasa
msaada mkubwa aliomsaidia.
“ Its like I’m going crazy.David zumo
amenikaa kichwani kwangu ghafla na kila
dakika namuwaza yeye tu. Nadhani ni
kutokana na ukarimu wake wa ajabu.”
Akawaza Monica akiendelea na safari ya
kuelekea ofisini kwake.
Aliwasili ofisini kwake na
kusalimiana na wafanyakzi wake kama
kawaida yake na kisha akaelekea ofisni
 
SEHEMU YA 46

.Mara tu alipoingia ofisini kwake
akakuta kuna bahasha nyeupe juu ya meza
,akaitazama ilikuwa imeandikwa jina
lake.Akamuita Linah msaidizi wake
akamuuliza kuhusiana na bahasha ile
“ Madam bahasha hii imeletwa na
mtu jana usiku na kwa vile hakukuwa na
mtu yeyote akaiacha getini kwa
walinzi.Nilipofika asubuhi nikakabidhiwa
ili nikupe”
“ Ni nani huyo mtu ? hakutaja jina
lake? Akauliza Monica
“ Kwa mujibu wa walinzi mtu
aliyeleta bahasha hiyo hakutaja jina lake”
akasema Linah.Monica akaishika bahasha
ile akaifungua taratibu akakutana na faili
ambalo llikuwa na jina na picha ya
Marcelo Richard.
“ Dr Marcelo !! Hili mbona
linaonekana ni faili la hospitali ? akajiuliza
Monica na kulifungua akaanza
kulisoma.Faili lile lilikuwa na taarifa za Dr
Marcelo ambazo zilionyesha kwamba
alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya
saratani ya damu.
“ oh my God !! is this true??
Akajiuliza Monica na kuanza kulipitia tena
“ Nani kaleta hili faili hapa na kwa
makusudi gani? akajiuliza Monica na
kuanza tena kulipitia lile faili.Alihisi
kijasho kinamtoka.
“ Yeyote aliyelileta faili hili hapa
lazima lengo lake lilikuwa ni ili nifahamu
kuhusu ugonjwa huu wa Dr Marcelo.Nani
basi anayeweza kufanya kitu kama hiki?
Kama lengo lake ni mimi kufahamu
kuhusu ugonjwa wa Dr Marcelo anataka
nini kitokee? Akaendelea kujiuliza.
“ Kwa nini Dr Marcelo hajanieleza
kuhusu maradhi yanayomsumbua?
Aliogopa nini kunieleza? Au inawezekana
kwa sababu tumefahamiana hivi karibuni
ndiyo maana hakuwa tayari kunieleza
.Ngoja nimpigie simu nimuulize kuhusiana
na faili hili na namna lilivyofika hapa”
akawaza Monica na kuchukua simu zake
akatafuta namba za Dr Marcelo
akapigia.Simu ikaita mara ya kwanza na
kukatika bila kupokelewa,akapiga tena
mara
ya
pili
lakini
haikupokelewa.Akaingiwa na wasi wasi
“ Kwa nini hapokei simu?
Inawezekana labda anatazama wagonjwa?
Akajiuliza Monica na kujaribu kupiga
tena.Safari hii ikapokelewa lakini Dr
Marcelo aliongea kwa sauti ya chini kidogo
na Monica akagundua utofauti katika sauti
yake
“ Hallow Monica” akasema Dr
Marcelo.
“ Dr Marcelo uko wapi?
“ Monica nilipatwa na matatizo
kidogo niko hapa kituo cha polisi”
“ Nini kimetokea Dr Marcelo?
Akauliza Monica
“ Jana usiku nikiwa katika zamu ya
kuwatazama wagonjwa kuna watu
walivamia nyumbani kwangu na kuchukua
baadhi ya vitu vyangu vya kwa hiyo
nimekuja hapa polisi” akasema Dr Marcelo
na Monica akabaki kimya.
‘ Monica “ akaita Dr Marcelo
“ Dr Marcelo I need to see you now”
akasema Monica
“ Monica kuna nini ?
“ Dr Marcelo naomba tuonane sasa
hivi kuna suala la muhimu sana nataka
tuongee” akasema Monica.Dr Marcelo
akafikiri kidogo na kusema
“ Sawa Monica uko wapi sasa hivi?
“ Niko hapa ofisini kwangu”
 
SEHEMU YA 47

Nisubiri ninakuja hapo sasa hivi”
akasema Dr Marcelo
“ Hapana usije hapa naomba
tukutane Savana Garden” akasema Monica
na kukata simu akavuta pumzi ndefu
“ Faili hili ninahisi linaweza kuwa ni
moja ya vitu vilivyoibwa toka nyumbani
kwa Dr Marcelo jana usiku na likaletwa
hapa.Laiti kama tungeweza kumpata mtu
aliyelileta hapa ingekuwa rahisi sana
kumfahamu aliyevunja nyumbani kwa Dr
Marcelo.Lakini nini hasa lengo la huyu
mtu kunionyesha faili hili? Akaendelea
kujiuliza bila kupata majibu akalichukua
faili lile na kuondoka kuelekea mahala
alikopanga akutane na Dr Marcelo.Njiani
alijaribu sana kuwaza kuhusiana na mtu
aliyelileta faili lile ofisini kwake na
kusudio lake lakini hakuweza kupata jibu.
“ Najaribu sana kuwaza bila kupata
jibu nini hasa lengo la huyu mtu kuniletea
faili hili? Lakini kuna mtu mmoja tu
ambaye akili yangu inanituma kwamba
ndiye anaweza kuwa amefanya jambo hili
.Ni Daniel.Hakupenda kabisa ukaribu
wangu na Dr Marcelo na alidiriki hata
kumfuata na kumtolea vitisho akimtaka
aachane kabisa na mimi akidai kwamba
mimi ni mpenzi wake.Ni yeye tu
anayeweza akafanya jambo kama hili na
lengo lake kubwa ni kunitenganisha mimi
na Dr Marcelo.Alitaka nifahamu kuhusiana
na ugonjwa wa Dr Marcelo “ akawaza
Monica.
“ NI wazi lengo lake ni hilo kwamba
nifahamu Dr Marcelo ni mgonjwa wa
saratani ya damu na kwamba hana maisha
marefu sana .Ouh poor Daniel kwa nini
amefanya hivi? Nina hakika ni yeye tu
hakuna mwingine anayeweza akafanya
jambo la kijinga kama hili” akawaza
Monica akachukua simu na kuzitafuta
namba za simu za Daniela akampigia
“ Monica” akasema Daniel kwa
mshangao kidogo baada ya kupokea simu
“ Daniel uko wapi? Akauliza Monica
“ Bado niko nyumbani najiandaa
kuelekea katika shughuli zangu.Wewe uko
wapi?
“ Naomba usitoke ninakuja hapo
hapo nyumbani kwako sasa hivi”
“ Kuna nini Mon....” akasema Daniel
lakini kabla hajamaliza Monica akakata
simu
“ Kwa hiki Daniel alichokifanya
ananifanya nimchukie zaidi na
zaidi.Hakuna analoweza kulifanya
kunitenganisha na Dr Marce....” Akawaza
Monica na kustuka
“ Masikini Marcelo.Kwa nini
hakutaka kunieleza mapema kuhusiaana
na kile kinachomsumbua? Aliogopa nini
kunieleza kama ana maradhi ya saratani ?
Japo ameniudhi kwa kunificha kuhusu hali
yake ya kiafya lakini nimeumia sana kwa
kuufahamu ugonjwa alionao.Nina wasi
wasi sana pengine hatakuwa na maisha
marefu.It hurt so much.Nimefahamiana
naye hivi karibuni na tayari moyo wangu
ulikwisha anza kumpenda kwa sababu ana
sifa zote za mwanaume wa ndoto zangu
lakini baada ya kuyafahamu maradhi
yake yanayomsumbua kumeniweka njia
panda.Nashindwa kufanya maamuzi.”
Akawaza Monica na kwa mbali macho
yake yakaonekana kuwa na michirizi ya
machozi
“ Nina mafanikio makubwa katika
kila ninachokifanya lakini sijawahi kupata
mafanikio katika masuala ya
mapenzi.Mpaka leo bado sijabahatika
 
now nimefika ngoja nishushe za kutosha za haja kwa wale mlio lalamika kuwa siku za kazi sio rafiki sana itabidi mjikaze sababu week end nilizingua.now nikiweka sehem kumi na 5 au 20 hivi sio mbaya
We shusha zigo mkuuu tutakua tunafaidi sie wengine, jafu ikizangatiwa hazifutiki
 
SEHEMU YA 48

kumpata mwanaume ambaye ataufanya
moyo wangu usimame.Kidogo Dr Marcelo
alikuwa anakaribia kufikia vigezo vyangu
na niliamini ni mwanaume pekee
anayeweza kunifaa lakini suala hili la
ugonjwa tayari limeweka doa mipango
yangu.It’s obvious siwezi kuwa na
mahusiano ya kimapenzi na Dr Marcelo
tena badala yake ataendelea kuwa rafiki
yangu wa karibu sana.Inaniuma lakini
sina
namna
nyingine
ya
kufanya.Yawezekana labda Marcelo
hakuwa fungu langu ,sintokata tamaa
nitaendelea kumlilia Mungu ili siku moja
aniletee mwanaume ambaye amemuandaa
kwa ajili yangu.” Akaendelea kuwaza
Monica
Aliwasili katika makazi ya
Daniel,akafunguliwa geti akaingia ndani
,akashuka garini na moja kwa moja
akaelekea sebuleni.Daniel akataarifiwa
kuwa Monica tayari amekwisha wasili
akashuka haraka kwenda kuonana naye.
“ Monica ..’ akasema Daniel kwa
furaha huku uso wake ukiwa katika
tabasamu ,akamsogelea Monica na kutaka
kumkumbatia ,akamzuia
“ Monica kuna tatizo gani? Mbona
unaonekana hauko sawa? Akauliza
Daniel.Monica akamtazama kwa macho
makali na kulitupa lile faili mezani
“ Daniel mimi na wewe tumekuwa
watu wa karibu sana na sikutegemea
kabisa kama ungeweza ukafanya kitu cha
kijinga kama hiki ulichokifanya.” Akasema
Monica kwa ukali Daniel akabaki na
mshangao
“ Monica kuna nini? Akauliza Daniel
“Unajifanya hujui ulichokifanya?
Ninashukuru ulichotaka nikifahamu
nimekifahamu lakini nakuhakikishia
kwamba
hautakipata
kamwe
ulichokikusudia.” Akasema Monica.Daniel
akalichukua lile faili na kulifungua,sura
yake ikaonyesha mstuko mkubwa
“ Monica what is this? Akauliza
Daniel
“ Unajifanya hujui kilichomo humo?
Akauliza Monica
“ Monica hili ni faili linalomuhusu Dr
Marcelo !!
“ Ulitaka nifahamu kuhusu ugonjwa
wa Dr Marcelo ? Nashukuru umenisaidia
nimeufahamu lakini nakuhakikishia
kwamba jambo unaloliota katu
halitakuwa.Ulitaka niufahamu ugonjwa
wake ili nisiwe karibu naye kwani lengo
lako ni kuwa na mimi lakini
nakuhakikishia kwamba kwa hilo
umekosea sana.Mimi nitaendelea kuwa na
Dr Marcelo kwani ni mtu ambaye
nimemchagua kuwa rafiki yangu wa
karibu na hata kama nikiamua kuingia
katika mahusiano naye ya kimapenzi
hakuna wa kunizuia kwa hilo na sintojali
ugonjwa wake kwani ndiye mwanaume
anayenifaa . “ akasema Monica kwa hasira
“ Monica naomba unisikilize kwa
makini.Mimi sijafanya jambo kama hili na
katu siwezi kufanya kitu kama hiki za
zaidi ya yote nimekuwa karibu na Dr
Marcelo na sikuwahi kulifahamu jambo
hili.Hajawahi
kunieleza
kama
anasumbuliwa na maradhi ya saratani ya
damu.Kingine ni kwamba ni kweli mimi na
Dr Marcelo tulipishana kauli lakini sina
sababu yoyote ya kufanya hivi hata kama
ningekuwa nafahamu kuhusu ugonjwa
wake.Nimekuwa nawe karibu kwa muda
mrefu unanifahamu vizuri sina tabia kama
hivi.
 
SEHEMU YA 49

.Kwanza jana usiku nilikuwa
nyumbani toka saa moja za jioni tulikuwa
na kikao cha familia sasa ningewezaje
kufanya kitu kama hicho? Believe me
Monica..” akasema Daniel
Monica akamtazama kwa makini na
kuichukua bahasha ile
“ Daniel tafadhali naomba ukae
mbali kabisa nami.I don’t want you near
me anymore.Tabia zako ni chafu na siwezi
kuwa na ukaribu na mtu mwenye tabia
chafu kama zako.” Akasema Monica kwa
hasira akaanza kupiga hatua kutoka mle
ndani
“ Monica please..!! akasema Daniel
na kumkimbilia Monica akamshika mkono
“ Daniel please don’t ever touch me
!!! akasema kwa ukali na mara toka ndani
akatoka mwanamke mmoja akiwa amevaa
nguo za ndani pekee..
“ Daniel whats going here?? And who
is she??Akauliza Yule mwanadada
mweupe mwenye nywele ndefu
“ Margreth please go inside..!!
akasema Daniel kwa ukali lakini yule
mwanadada akazidi kumsogelea Daniel na
Monica ambaye alisimama kwa hasira
“ Daniel kuna tatizo lolote na huyu
kahaba? Akauliza Margreth .Kwa hasira
Monica akamnasa kibao kikali na
kuondoka akaelekea katika gari
lake,Daniel akamfuata na kumtaka
waongee lakini Monica hakuwa tayari
akawasha gari na kuondoka kwa hasira.
“ Kwa mara ya kwanza leo katika
maisha yangu nimeitwa kahaba.Sijawahi
kukosewa heshima kiasi hiki.Lakini kwa
kofi lile nililomnasa Yule kahaba nadhani
nimemtendea haki.Tabia ya Daniel ni
chafu sana na sitaki kabisa kuwa karibu
naye.Nina hakika baada ya maneno yale
niliyomweleza hatathubutu kunikaribia
tena.Lakini..” Akawaza Monica na kusita
kidogo
“ Nimemtazama Daniel machoni he’s
not the one who did this.Ukilichukulia kwa
haraka haraka suala hili unaweza
ukadhani labda Daniel ndiye muhusika
mkuu na usipokuwa makini unaweza hata
kumchukulia hatua lakini Daniel hahusiki
kabisa na hiki kilichotokea.Ni nani basi
aliyefanya hivi? Akaendelea kujiuliza
Monica
“ Nina hakika kabisa aliyefanya
jambo hili lengo lake kubwa ni kutuvuruga
mimi na Dr Marcelo tusiwe na mahusiano
lakini ni nani huyu na kwa nini anataka
mimi na Dr Marcelo tusiwe karibu?? Swali
hili likamuumiza sana kichwa.
Aliwasilli Savana Garden moja kati
ya sehemu nzuri na tulivu,watu wengi
hupenda kuja kupumzika hapa,kuna
bustani nzuri ya majani na miti.Aliegesha
gari na kufungua mlango na kabla
hajashuka akatokea Dr Marcelo
“ Monica” akasema Dr Marcelo
“ Dr Marcelo umeshafika”
“ Nimefika kitambo sana.Habari
yako?
“ Habari yangu nzuri.Habari yako
nawe? Akauliza Monica huku akiufunga
mlango wa gari wakaongozana kutafuta
sehemu ya kukaa.
“ Pole sana Dr Marcelo kwa mkasa
uliokukuta.” Akaanzisha maongezi Monica

Ahsante
Monica.Kama
nilivyokueleza simuni, jana nilikuwa
katika zamu ya usiku nikiwatazama
wagonjwa na nilipofika nyumbani
nikakuta kasiki langu ambalo huhifadi
vitu vyangu vya muhimu liko wazi na
baadhi ya vitu vyangu havipo.
 
SEHEMU YA 50

Hakuna
mlango au sehemu yoyote iliyovunjwa ila
kasiki langu nimelikuta wazi na vitu
vyangu vy amuhimu havipo.Mtu aliyefanya
uhalifu huo lazima atakuwa ni mtu
anayenifahamu vyema hadi akazifahamu
namba za siri za kufungulia kasiki langu”
“ Pole sana .Ni vitu gani
walivyovichukua ? akauliza Monica na Dr
Marcelo akasita kidogo
“ Uhhm wamechukua vitu vyangu
vya muhimu .Kuna faili langu lenye
nyaraka muhimu sana pamoja na baadhi
ya vitu vingine.”
“ Unaishi na nani? Nyumbani kwako
hakuna ulinzi? Akauliza Monica
“ Hapana sijaweka mlinzi.Ni sehemu
salama sana na ndiyo maana sina haja ya
kuweka mlinzi.Hakuna ninayeishi naye ila
kuna mtmishi wa ndani huja kial siku
asubuhi akafanya kazi na kuondoka saa
kumi lakini huyu hawezikufanya hivi na
isitoshe hata funguo za chumba change
hana” akasema Dr Marcelo
“ Hujafunga kamera za ulinzi?
Akauliza Monica
“ Hapana sijafunga”
“ Unatakiwa uimarishe ulinzi
nyumbani kwako ikiwa ni pamoja na
kufunga kamera za ulinzi.Vipi polisi wana
taarifa zozote za mtu aliyefanya uhalifu
huu?
“ hapana bado hawana taarifa zozote
na wanaendelea kuchunguza “ akasema Dr
Marcelo.Ukimya mfupi ukapita Monica
akauliza
“ Dr Marcelo samahani kwa maswali
yangu kama polisi lakini ni kutokana na
kuguswa na jambo hili “
“Usijali Monica uliza chochote
unachotaka”
“ Kuna mtu yeyote unayemuhisi
kufanya uhalifu huu? Kuna yeyote
unayedhani
anapafahamu
vizuri
nyumbani kwako hadi akaweza kulifungua
kasiki unalohifadhi nyaraka zako
muhimu? Lakini kabla hujanijibu swali
langu kuna kitu nataka nikukabidhi”
akasema Monica na kulitoa faili lile la Dr
Marcelo
na
kumpatia.Mikono
ikamtetemeka.
 
SEHEMU YA 51

“ Umelitoa wapi faili hili? Akauliza Dr
Marcelo
“ Nimelikuta ofisini kwangu
asubuhi.Kuna mtu amelipeleka jana usiku
akawaachia walinzi ili wanipatie leo
asubuhi.” Akasema Monica na kuliona
jasho usoni kwa Dr Marcelo
“ Walinzi wanaweza kumfahamu mtu
huyo?

Hapana
nimewadadisi
hawamkumbuki”
“ Umesoma kilichomo ndani ?
akauliza Dr Marcelo
“ Ndiyo Dr Marcelo nimelisoma na
ninafahamu kila kitu kilichomo humo
ndani”
Ukimya wa sekunde kadhaa ukapita
Dr Marcelo akiendelea kulikodolea macho
faili lile.
“ Daniel..!! akasema Dr Marcelo kwa
sauti ndogo
“ Unasema nini Dr Marcelo? Akauliza
Monica
“ Daniel.!!Nimetafakari sana toka
jana usiku kuhusu ni nani anayeweza
kunifanyia hivi lakini baada ya kunieleza
kuhusu faili hili tayari nimepata picha ni
mtu mmoja tu ambaye amelifanya jambo
hili.Ni Daniel. Aliapa kufanya chochote ili
kuuvuruga urafiki wetu na ndiyo maana
akasuka mipango ya kulipata faili hili ili
uweze kuliona.Damn you Daniel..I’m going
to teach you a lesson !!! akasema Dr
Marcelo kwa hasira
“ It’s not him” akasema Monica
“ What ??? akauliza Dr Marcelo
ambaye alikuwa amepandwa na hasira
kali
“ Its not him.It’s not Daniel “ akasema
Monica
Dr Marcelo akamtazama Monica kwa
hasira na kusema
“ It’s him.Hakuna mwingine ambaye
anaweza akafanya jambo hili zaidi yake”
akasema Dr Marcelo
“ Hapana Dr Marcelo Daniel hahusiki
kabisa na suala hili.”
“ Are you sure Monica? Akauliza Dr
Marcelo
“ Yes I’m sure” akajibu Monica.
“ Kabla sijafika hapa nimetoka
kuonana na Daniel na amekana kuhusika
katika jambo hili.”
“ Do you believe him?? Akauliza Dr
Marcelo
“ Yes I do believe him” akajibu
Monica na ukapita ukimya
“ Dr Marcelo kuna mtu aliyefanya
jambo hili na si Daniel.You have to find the
right person who did this but not
Daniel.By the way kwa nini hukunieleza
ukweli kuhusiana na wewe kusumbuliwa
na maradhi ya saratani ya damu? Akauliza
Monica.Dr Marcelo akashindwa ajibu nini
midomo ikabaki inamcheza.
“ Uliogopa nini Dr Marcvelo
kunieleza ukweli? Akauliza tena Monica
“ Monica listen to me please.”
Akasema Dr Marcelo
“ Kwanza samahani sana kuhusu
suala hili lakini kama unavyofahamu
hatuna hata wiki moja toka
tulipofahamiana kwa hiyo nisingeweza
kukimbilia haraka haraka kuanza
kukueleza mambo makubwa kama
haya.Hili si jambo dogo lakini hata hivyo
nisingeweza
kukuficha
lazima
ningekueleza.”
“ Dr Marcelo muda mfupi wa
kufahamiana si kigezo.Ni kweli
tumefahamiana katika muda usiozidi wiki
moja lakini where are we now?.Ni marafiki
 
SEHEMU YA 52

.Ni marafiki
wakubwa kuliko hata wale ambao
nimekuwa nao toka utotoni.Urafiki wetu
una nguvu kubwa na ndiyo maana
nikashangaa sana kwa nini usinieleze
kuhusiana na suala hili toka siku
tulipokutana.? I’m so dissaponed with
that” akasema Monica
“ Monica I’m sorry.Im real very sorry
lakini kama nilivyokueleza awali kwamba
nisingeweza kukurupuka tu na kuanza
kukueleza kuhusu suala hili.Ni jam.....”
Akataka kuendelea Monica akamkatisha
“ Uliogopa nini kunieleza Marcelo?
You don’t trust me? Akauliza Monica
“ I was scared..” akajibu
“ Scared?? Scared for what??
Akauliza Monica .Dr Marcelo hakujibu
akabaki kimya.
“ Answer me Dr Marcelo” akasema
Monica
“ I was scared to loose you..”
“ Loose me!! Monica akashangaa
“ Ndiyo Monica” akajibu Dr Marcelo
“ ungenieleza ukweli kuhusu hali
yako ya kiafya ungenipoteza vipi?
Akauliza Monica
“ Monica let me be honest
.Nilipokuona kwa mara ya kwanza
nilishindwa kujizuia kukupenda na ndiyo
maana nikaogopa endapo ungefahamu
kuhusu hali yangu hii usingeweza
kukubali kuwa na mtu kama mimi.I love
you Monica more than I can explain lakini
ugonjwa wangu huu kwa sasa umefikia
katika hatua mbaya na sintakuwa na muda
mrefi wa kuishi ndiyo maana ninafanya
siri.Sijawahi
kujihusisha
katika
mahusiano yoyote toka nilipofahamu
kuwa nina maradhi haya .Kwa ufupi I’ve
never
been
happy.Nilipokuona
nilikupenda ghafla na nilitaka walau
katiak siku zangu chache zilizobaki niwe
na furaha na ndiyo maana sikukueleza
jambo ” akasema Dr Marcelo na kukawa
kimya.Baada ya kama dakika mbili Monica
akainua kichwa macho yake yalikuwa na
machozi akasema
“ Sikiliza Dr Marcelo.Ikitokea kama
umempenda mtu kwa moyo wako wote
kama unavyosema unanipenda basi
unapaswa kumueleza ukweli mtu huyo
toka siku mnapoonana.Kama kuna jambo
ambalo unadhani anapaswa kulifahamu
basi mueleze kutokea siku hiyo na
usisubiri
hadi
atakapolifahamu
mwenyewe .Ulipaswa kunieleza kuhusu
suala hili mapema kabisa bila kusubiri
.Kwa sasa unadhani nitakuamini tena?
Akauliza Monica
“ Tafadhali naomba uniamini
Monica” akasema Dr Marcelo
“ How can I trust you Marcelo wakati
umenificha jambo hili kubwa? Nilikuweka
karibu yangu sana kwa sababu nilikuona
ni mtu ninayeweza kumuamini .Naomba
nikueleze kuwa hata mimi tayari nilianza
kuhisi kitu kwako lakini ni vipi kama
ningeingia katika mahusiano nawe wakati
sijui kama una maradhi haya japokuwa
haayaambukizi lakini tukafurahi kwa siku
chache tu halafu ukaondoka na kuniachia
majonzi ? Marcelo umeniumiza sana and I
cant trust you anymore” akasema Monica
“ Monica please trust me.I love you.I
real do..” akasema Dr Marcelo
“ Dr Marcelo naomba tafadhali
tuachane na masuala hayo na tuongelee
kuhusu suala la kumtafuta nani aliyefanya
jambo hili.Aliyefanya hivi ni wazi alikuwa
na makusudi yake na ninaamini lengo lake
 
SEHEMU YA 53

Dr Marcelo naomba tafadhali
tuachane na masuala hayo na tuongelee
kuhusu suala la kumtafuta nani aliyefanya
jambo hili.Aliyefanya hivi ni wazi alikuwa
na makusudi yake na ninaamini lengo lake
ni mimi kuliona faili hili na kufahamu
kuhusu hali yako ya kiafya.Nini
anakusudia nikifahamu kuhusu hali ya
afya yako?? Hapo ndipo mahala pa
kujiuliza”
“ Aliyefanya hivi alikuwa na lengo
moja tu la kuharibu mahusiano kati yangu
nawe.Lazima aliyefanya hivi atakuwa
akifahamu kuwa toka tumefahamiana
mahusiano yetu yamekuwa mazuri sana
na hilo halimpendezi ndiyo maana
nikasema kuwa lazima atakuwa ni Daniel
kwani ni yeye ambaye anafahamu kuhusu
ukaribu wangu mimi na wewe” akasema
Dr Marcelo
“ Trust me Marcelo,Daniel is not the
one who did this.Kuna mtu mwingine
aliyefanya hivi.Unatakiwa kushirikiana
sana na vyombo vya dola ilikuweza
kumbaini mtu huyu ni nani..” akasema
Monica.Daniel akainam akafikiri kwa
dakika kama tatu halafu akainua kichwa
na kusema
“ Kwa upande Fulani naweza
kukubaliana nawe Monica .Mtu aliyefanya
hivi lazima ni mtu anayenifahamu na
ndiyo maana akweza kujua muda
ninaorudi nyumbani na hivyo akaweza
kuingia ndani mwangu bila hata ya
kuvunja mlango na kufungua
kasiki.Lazima ni mtu ambaye ananifahamu
vyema kiasi kwamba akaweza kuzifahamu
namba za siri za kufungulia kasiki.Monica
ninaanza kupata picha hili si suala dogo
kama ninavyodhani.” Akasema Dr Marcelo
na kuzama katika mawazo halafu akasema
“ Naweza kukubaliana nawe kwamba
Danel hahusiki katika jambo hili.Hajawahi
kuingia chumbani kwangu na wala hajui
namba za kufungulia kasiki langu.”
Akasema Dr Marcelo
“ Do you believe me now? Akauliza
Monica
“ Yes I do.Nimejaribu kutafakari kwa
haraka haraka na nimeona Daniel hawezi
kuhusika katika suala hili.”
“ Kama si Daniel,nani basi aliyefanya
jambo hili? Akauliza Monica .Dr Marcelo
akabaki kimya akitafakari.Baada ya
tafakari ya muda Dr Marcelo akainuka
ghafla kana kwamba amekumbuka kitu
akasema
“ Monica I need to go,nitawasiliana
nawe baadae.” Akasema na kuinuka
akaanza kupiga hatua za haraka kuelekea
mahala lilipo gari lake,Monica akabaki
anashangaa.
“ What happened? Mbona Marcelo
ameondoka kwa haraka namna hii ? Kuna
kitu amekikumbuka? Akajiuliza Monica
huku naye akiinuka na kuelekea katika
gari lake.
“ Lazima mtu aliyefanya jambo hili
anamfahamu vyema Dr Marcelo.Ni nani
huyo na lengo lake ni nini? Akajiuliza
Monica akiwa garini
“ Ngoja niachane na suala hili la Dr
Marcelo nielekeze akili katika masuala
yangu ya msingi.Kwa sasa ngoja
nikaonane na wataalamu wangu juu ya
suala la kuanza ujenzi wa shule .Sitaki
kupoteza muda , wakati tayari pesa
imepatikana.Ujenzi lazima uanze mara
moja.Sijui nitatumia neno gani
kumshukuru David Zumo kwa msaada
wake huu mkubwa alionisaidia.” Akawaza
Monica.
 
Back
Top Bottom