QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

LEGE HEBU FANYA KUWA UNAWEKA # TANG KWENYE PAGE YA KWANZA TU ILI TUJUE KILA NO YA STORY UNAPATIKA KWENYE PAGE IPI?? mfano..sehemu ya kwanza inapatikana ukursa #48...ili mtu asihangaike kuitafuta mana comment ni nyingi mno hope utakuwa umetusaidia cc tunaotumia Simu.
 
WAKUU TUSAMEHEANE AISEE NILIPATWA NA MATATIZO KIDOGO YA KIMAJUKUMU HIVYO NIKASHINDWA KABISA KUINGIA JF JAPO HATA KUSEMA NENO JUU YA MWENDELEZO WA HII STORY KWA MASIKITIKO MAKUBWA NIWAOMBE RADHI KWA KUSHINDWA KUKAMILISHA AHADI NILIYOIWEKA KWENU YA DOZI YA 10 MARA 3. NA MBAYA ZAIDI HATA LEO SITO WEZA KUIWEKA LKN KESHO ASUBUHI NAMAPEMA WEEK END ITAKUWA YA BURUDANI NITAWEKA VIPANDE VYA KUTOSHA.

TUKUTANE KESHO ASUBUHI.

MAISHA NJE YA JF SOMETIMES YANATINGA WAKUU NA KUWA KIKWAZO
Pole sana Lege
 
WAKUU TUSAMEHEANE AISEE NILIPATWA NA MATATIZO KIDOGO YA KIMAJUKUMU HIVYO NIKASHINDWA KABISA KUINGIA JF JAPO HATA KUSEMA NENO JUU YA MWENDELEZO WA HII STORY KWA MASIKITIKO MAKUBWA NIWAOMBE RADHI KWA KUSHINDWA KUKAMILISHA AHADI NILIYOIWEKA KWENU YA DOZI YA 10 MARA 3. NA MBAYA ZAIDI HATA LEO SITO WEZA KUIWEKA LKN KESHO ASUBUHI NAMAPEMA WEEK END ITAKUWA YA BURUDANI NITAWEKA VIPANDE VYA KUTOSHA.

TUKUTANE KESHO ASUBUHI.

MAISHA NJE YA JF SOMETIMES YANATINGA WAKUU NA KUWA KIKWAZO
basi sawa, tutasubiri tu mkuu
 
Ngoja nisafiri nikirudi atakuwa nae karudi maana naona LEGE majukumu yanamuandama
 
nilichoshikilia ni kilevi no 1 [emoji23]
kwapozi hilo matata tafadhali naomba nijumuike nawewe... ili tufanye mambo mubashara tupunguze na arosto mubashara..😀
UNASEMAJE...?
 
SEHEM YA 29


Ni saa tano za usiku sasa Mzee benedict
Mwamsole na mke wake Janet wako
chumbani kwao wakijipumzisha baada ya
shughuli za kutwa nzima.
“ Ben kuna jambo lilitokea jana na
sikutaka kukwambia mapema nilitaka
kwanza nifanye uchunguzi wangu”
akasema Janet
“ Ni jambo gani hilo kwa sababu
nawe huishiwagi mambo” akasema mzee
Ben huku akitoa kicheko kidogo
“ Katika sherehe ya Monica jana
Daniel Yule kijana wa mzee Swai
hakuwepo
inaonekana
hakualikwa.Nadhani Monica aliyafanyia
kazi maneno yangu”
“ Uliongea na Monica kuhusu suala
hilo? Akauliza mzee Ben
“ Ndiyo niliongea naye na
kumtahadharisha kuhusu ukaribu na
Daniel “ akasema bi Janet
“ Hukupaswa kufanya hivyo.Monica
ataona kama vile tunaingilia masuala yake
binafsi” akasema Ben
“ Hapana siwezi kukaa kimya wakati
ninamuona kabisa mwanangu yuko karibu
na chui mwenye ngozi ya
kondoo.Nilimtahadharisha
awe
muangalifu asije akaingia katika mitego ya
Yule kijana.Kutomuona Daniel jana katika
sherehe ni dalili za wazi kwamba tayari
amekwisha anza kumkwepa kijana yule
mchafu wa tabia.” Akasema bi Janet na
baada ya sekunde kadhaa akaendelea
“ Jana wakati sherehe ikiendelea
Monica alikuwa anazunguka zunguka
kusalimia watu mbali mbali walioalikwa
na baadae akapotea ghafla .Nilikuwa
nikimfuatilia na nikamuona akiondoka na
kijana mmoja hivi mtanashati sana
ambaye ni mara ya kwanza kumuona naye
wakaeleka kule kwenye bwawa la
kuogelea ambako kuliandaliwa meza
.Nadhani Monica alipanga kukutana na
kijana Yule kule ili waongee mambo
yao.Niliwafuatilia na kuwakuta wakiwa
wamezama katika maongezi na kwa
namna nilivyowakuta kuna kila dalili
kwamba kuna kitu kinaendelea kati yao.”
Akanyamaza tena na baada ya muda
akaendelea.
“ Kijana huyo anaitwa Dr Marcelo
Richard.Kwa mujibu wa Monica ni
kwamba kijana huyo ni mmoja wa
wafadhili wa mradi wake wa kujenga
shule ya watoto walemavu.Lakini kwa
mtazamo wangu kuna kitu zaidi ya
ufadhili nilichokiona kati yao.Kama
kawaida yangu nilifanya utafiti wangu
nilitaka kumfahamu Dr Marcelo ni kijana
wa namna gani”
“ Umepata majibu gani ? akauliza
mzee Ben
“ Dr Marcelo ni kijana msafi wa
tabia,ni msomi mzuri,anatoka katika
familia tajiri ,hajawahi kuwa na mke na
hana tabia chafu za kubadilisha wanawake
kama alizonazo Daniel.Anaongoza
hospitali inayofadhiliwa na familia yake
inayohudumia wagonjwa wa saratani ya
damu.Kwa ujumla ni kijana mwenye sifa
nzuri na ni kijana anayeweza kumfaa sana
Monica ila kuna tatizo moja.” Akasema Bi
Janet na kunyamaza
“ Tatizo gani hilo? Akauliza Ben.Bi
Janet akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Dr Marcelo ana tatizo la saratani ya
damu”..
Zilipita kama dakika mbili za ukimya
mzee Ben akasema
“ Kwa namna ulivyowaona kuna
dalili zozote za Monica na huyo Dr Marcelo
 
SEHEM YA 30


kuwa katika mahusiano? Akauliza mzee
Benedict
” Mimi ni mtu mzima na nimeyapitia
mambo haya ,ni wazi kuna dalili za
kupendana kati yao” akajibu Bi Janet
“ Kama tayari kuna dalili hizo na
wakati huo huo unadai kwamba kijana
huyo ana saratani ya damu ambayo
kiuhalisia hatakuwa na maisha marefu
,unashauri nini kifanyike?
“ Ben hapa hakuna mjadala kuna
kitu kimoja tu cha kufanya ni
kuwatenganisha Monica na huyo kijana.”
Akasema Bi Janet.Mzee Ben akafikiri
kidogo na ksuema
“ Sikatai wazo lako lakini huoni
kuwa hatutakuwa tunamtendea haki
Monica tukisema aachane na kijana
anayempenda? Mimi kwa matazamo
wangu kama Monica anampenda huyo
kijana basi awe naye ila aelezwe ukweli
kwamba kijana huyo ampendaye ana
maradhi ya saratani ya damu ili afanye
uamuzi yeye mwenyewe kuliko kungilia
masuala yake ya kimahusiano.” Akashauri
Ben
“ Hapana Ben.Sitaki mwanangu awe
mjane katika umri mdogo.Nataka Monica
ampate mwanaume ambaye hana kasoro
hata moja.Huyu Dr Marcelo ni kijana
mwenye sifa zote lakini tatizo lake ni hilo
moja tu la ugonjwa huo unaomsumbua.”
Akasema bi Janet
“ Kumpata mtu asiye na kasoro
yoyote katika ulimwengu huu wa sasa ni
ngumu sana.Nashauri tukae na Monica
tuongee naye na tumueleze ukweli
kwamba kama anampenda Dr Marcelo
basi afahamu kwamba anasumbuliwa na
maradhi ya saratani ili yeye mwenyewe
afanye uamuzi kuliko sisi kumuingilia
katika maisha yake.Monica ni msichana
mkubwa sasa na ana uwezo wa kufanya
maamuzi kuhusu maisha yake kwa hiyo
usimnyime nafasi hiyo mhimu ya kupanga
maisha yake .Kama anampenda Dr
Marcelo kwa dhati ya moyo wake basi
lazima atakubaliana na mapungufu yake
yote ikiwemo na ugonjwa huo
unaomsumbua “ akashauri mzee Ben
“ Haopana siwezi kukubaliana na
hilo Ben.Monica bado ni msichana
mwenye ndoto nyingi za maisha kwa hiyo
anatakiwa ampate mwanaume ambaye
atamsaidia kuzitimiza ndoto hizo na si
ampate mwanume ambaye baada ya
kipindi kifupi atakuwa kitandani na
Monica kuutumia muda wake mwingi
kumuhudumia na kusahau kuhusu ndoto
zake. Siwezi kukubali mwananagu abebe
mzigo wa kuhudumia mtu mgonjwa .Na
vipi iwapo watapata watoto ambao nao
watarithi maradhi hayo ya saratani ya
damu? Maisha ya Monica yatakuwa ni
kuuguza wagonjwa .Sikubaliani na
hilo.Monica ana fursa nyingi sana za
kumfikisha mbali na siko tayari kumuona
akizizima ndoto zake kwa sababu eti ya
mapenzi.Wanaume hawajaisha .Dunia hii
bado ina mamilioni ya wanaume vijana
wazuri na nina hakika Monica atampata
mmoja wa maisha yake.” Akasema Bi Janet
“ Lakini Janet tukifanya hivyo
hatutakuwa
tumemtendea
haki
mtoto.Tumuache Monica mwenyewe
afanye maamuzi kuhusu maisha yake “
akasema mzee Ben
“ Ben tutakuwa wajinga na
tutachekwa na dunia kama ndoto za
Monica zitazimika huku tukiona kwa
 
SEHEM YA 31

kigezo eti cha kumuacha awe huru
kuchagua kuhusu maisha yake.Sisi kama
wazazi lazima tutumie vyema nafasi yetu
kuhakikisha mtoto anakuwa na maisha
mazuri yenye furaha.Kama wewe hauko
tayari kwa hilo niachie mimi.Nitahusika
kwa chochote kitakachotokea .Wewe kaa
pembeni niache mimi nibebe mzigo wote
wa lawama kama zitakuwepo lakini siwezi
kukubali kumuona Monica akijiingiza
katika mahusiano yasiyo na manufaa
kwake” akasema Bi janet.Mzee Ben
hakutaka tena kuendelea na mjadala ule
akageuka upande wa pili
“ Tutafanya kosa kubwa kuingilia
mahusiano ya Monica.Kama anampenda
huyo daktari mimi sina kipingamizi
chochote kama ndiye chaguo lake .Suala la
kumpangia awe na nani ni mambo ya
miaka ya zamani sana.Zama hizi watoto
wako huru kufanya uchaguzi wa watu
wanaowataka wawe nao katika
mahusiano.Hata hivyo siwezi kukaa kimya
na
kumuacha
Janet
afanye
atakavyo.Nitamuita Monica nitaongea
naye na kumuweka wazi kama anampenda
huyo daktari kwa moyo wake wote basi
afumbe macho na aweke pamba masikioni
ili asisikie ya watu bali aendelee naye .”
akawaza mzee Benedict.
“ Benedict bado ana mawazo ya
kizamani sana.Zama hizi tunaangalia
mambo mengi kabla ya kuamua kuwa na
mtu Fulani kimahusiano.Siwezi na sema
siwezi kukubali kumuacha Monica aingie
katika mahusiano na Dr Marcelo wakati
nikifahamu kabisa kuwa Yule kijana hana
kitu chochte atakachomletea Monica zaidi
ya furaha ya muda mfupi na
kitakachofuata hapo ni kilio na
majonzi.Sitaki Monica aachwe mjane
katika umri mdogo.Ni bora hata Daniel
anaweza akabadilika kuliko huyu ambaye
hana maisha marefu .Nitawatenganisha”
akawaza Bi Janet.
 
EHEM YA 32

Kumepambazuka tena ni siku ya
jumamosi na jiji la Dar es salaam likiwa
limeamshwa na tukio moja kubwa ambalo
ni mbio za nusu marathoni zilizoandaliwa
na Monica kwa lengo la kuchangisha fedha
za ujenzi wa shule ya watoto wenye
ulemavu wa kutoona na kusikia. Kuanzia
saa kumi na mbili za asubuhi maelfu ya
wakaazi wa jiji la Dar es salaam tayari
walikuwa wamewasili katika viwanja
ambako mbio hizo zingeanzia.Watu
walihamasika vya kutosha na ndiyo maana
wakajitokeza kwa wingi mno.
Saa mbili za asubuhi mgeni rasmi
akawasili ambaye ni waziri wa habari
sanaa na michezo ambaye naye alikuwa
mshiriki katika mbio hizo.Utepe ukakatwa
na mbio zikaanza rasmi.
Monica
alikuwa
akikimbia
sambamba na mgeni rasmi pamoja nao
walikuwepo pia baba na mama yake
ambao walikuja pia kumuunga
mkono.Alikuwepo pia Dr Marcelo ambaye
timu yake ya madaktari ilikuwapo katika
mbio hizo kwa ajili ya kutoa huduma ya
kitabibu kwa wale wote watakaopatwa na
tatizo lolote .Vile vile wafanyakazi
wengine wa taasisi yake walishiriki pia
katika mbio hizo.Miongoni mwa washiriki
wa mbio hizo alikuwa ni Daniel akiwa na
kundi la marafiki zake.Alitamani sana
kama angeweza kupata nafasi ya
kuzungumza na Monica lakini hakuipata
nafasi hiyo ya kuonana na Monica.Aliumia
sana kumuona Monica akiwa karibu na Dr
Marcelo.
“Mimi ndiye niliyetakiwa niwe pale
karibu na Monica kwani nmemsaidia sana
kuandaa mbio hizi lakini ametokea Yule
mshenzi Marcelo ameniharibia kila
kitu.Naapa
lazima
nimfundishe
adabu.Nimeujenga urafiki na Monica kwa
miaka mingi na kwa gharama kubwa
lakini amekuja na kuuvuruga kwa siku
moja tu.Hapana sikubaliani kabisa na hilo
lazima nimfunze adabu” Akawaza Daniel
huku akiendelea na mbio taratibu.
Hatimaye mbio zikamalizika na
ukafika wasaa wa mgeni rasmi
kuwatunuku zawadi washindi toka
makundi mbali mbali waliofanya vizuri
katika mbio hizo lakini kabla ya kutoa
zawadi mgeni rasmi alikuwa na machache
ya kuongea.Wakati mgeni rasmi akitoa
maneno machache kwa washiriki kabla ya
kukabidhi zawadi,Linah msaidizi wa
Monica akamfuata na kumvuta pembeni.
“ Madam Monny,kuna mtu anahitaji
kukuona anasema ana ujumbe wako toka
kwa rais David Zumo wa jamhuri ya
kidemokrasia ya Kongo” akasema Linah
“ Kutoka kwa rais wa Kongo?
Akauliza Monica
“ Ndiyo” akajibu Linah
“ Unamuamini huyo mtu ni mkweli?
Akauliza Monica
“ Anaonekana ni mkweli” akajibu
Linah.Monica akafikiri kidogo na kusema
“ Kwa sasa mgeni rasmi anatarajia
kukabidhi zawadi kwa washiriki
waliofanya vizuri,mwambie nitaonana
naye baada ya shughuli zote kumalizika”
akasema Monica na kurejea jukwaani.
“ Rais wa Kongo !! akawaza
“ Ana ujumbe gani kwangu?
Akajiuliza
“ Ngoja nitafahamu baada ya
shughuli kumalizka.Halafu nilimuona
Daniel na alionekana kutaka sana kuongea
nami lakini sitaki kumpa nafasi hiyo . Ni
kijana asiye mstaarabu hata
kidogo.Kitendo cha jana kumfuata Dr
Marcelo na kumtolea maneno ya kejeli na
vitisho na kujitangazia kwamba mimi ni
mpenzi wake sijayapenda kabisa.”
Akawaza Monica.
Mgeni rasmi akatunuku zawadi kwa
washiriki waliofanya vizuri na kilichofuata
 
SEHEM YA 33

baada ya hapo ni burudani ya muziki toka
kwa wasanii mbali mbali walioshiriki pia
katika mbio hizo .Monica akaagana na
mgeni rasmi pamoja na baadhi ya watu
wengine walioshiriki mbio hizo na mara
akakutanisha macho na Daniel
“ Monica..Monica..tafadhali naomba
unipe dakika mbili tu” akasema
Daniel.Monica akatabasamu na kumpa
mkono
“ Hallow Daniel.” Akasema na
kumfanya Daniel atoe tabasamu pana
“ Hallow Monica” akasema Daniel
“ Daniel nashukuru sana
umehudhuria .Nilikuwa na wasiwasi
pengine hutaweza kuhudhuria leo”
akasema Monica
“ Kwa nini nisihudhurie jambo
kubwa kama hili Monica? Siwezi katu
kufanya hivyo.Hata hivyo ninaomba
samahani sana kwa yale yaliyotokea..”
akasema Daniel lakini Monica
akamkatisha
“ Daniel hapa si mahali pa kuongelea
masuala yale.Hapa tuko katika masuala
mengine kabisa.Tutatafuta nafasi ya
kuongelea suala hilo siku nyingine na
mahala pengine” Akasema Monica
“ Sawa Monica ila napenda
kukuhakikishia kwamba hakuna mtu au
kitu chochote kinachoweza kuuvunja
urafiki wetu.Mimi na wewe ni marafiki
hadi mwisho wa nyakati” akasema Daniel
“ Sawa Daniel.Nimefurahia uwepo
wako ila kwa sasa utanisamehe nina watu
wengi ninaotakiwa kuonana nao na
kuwashukuru pia kwa kufika
kwao.Tutawasiliana zaidi” akasema
Monica na kuondoka.
“ Daniel amefurahi sana kwa namna
nilivyomuonyesha tabasamu kana
kwamba hakuna kilichotokea lakini hajui
kama moyoni nimetokea kumchukia sana
kwa kitendio alichokifanya” akawaza
Monica na kumfuata Linah
“ Linah yuko wapi huyo mjumbe wa
rais wa Kongo? Akauliza Monica.
“ Yuko pale katika gari anakusubiri”
akasema Linah na kumuongoza Monica
moja kwa moja hadi alipokuwa Jean Pierre
Muyeye.Alikuwa nje ya gari moja la
ubalozi wa Kongo akiwa na taulo begani
na chupa ya maji .Naye alikuwa ni mmoja
wa washiriki wa mbio hizo.Linah
akawakutanisha na kuwaacha waongee
“ Monica naitwa Jean Pierre Muyeye
ni msaidizi wa David Bikumbi Mukaya
Zumo rais wa jamhuri ya kidemokrasia ya
Kongo.” Akajitambulisha Muyeye
“ Nafurahi sana kukufahamu Pierre
Muyeye na nimefurahi sana kwa kushiriki
mbio hizi.” Akasema Monica
“ Ahsante sana Monica.Jambo hili ni
zuri na ndiyo maana nimeshiriki
nikimuwakilisha rais wa Kongo ambaye
ndiye aliyenituma nishiriki”
“ Kweli !! akauliza Monica kwa
furaha
“ Ndiyo.Yeye ndiye aliyenituma nije
nimuwakilishe katika mbio hizi.Yuko hapa
nchini kwa ajili ya mkutano wa marais wa
nchi za maziwa makuu mkutano unaoanza
hii leo na kama angekuwa na nafasi
angeweza kushiriki yeye mwenyewe ila
kwa kuwa hana nafasi amenituma mimi
nimuwakilishe” akasema Muyeye
“ Dah ! nimefurahi kupita maelezo
kwa rais wa Kongo kuamua kushiriki
katika shughuli hii muhimu.Mfikishie
 
SEHEM YA 34

shukrani zangu za dhati kwa jambo hili.”
Akasema Monica
“ Mheshimiwa rais hakunituma nije
kushiriki tu kukimbia bali amenipa pia na
ujumbe mwingine mkubwa na wa muhimu
sana” akasema Muyeye na kutulia kidogo
akamtazama Monica na kusema
“ Mheshimiwa rais ni mtu wa
kusaidia sana taasisi mbali mbali
zinazofanya mambo makubwa kwa jamii
na hata kule Kongo amekuwa akisaidia
sana taasisi mbalimbali .Jana alipofika
hapa Tanzania akapata taarifa za kuwepo
kwa mbio hizi ulizoziandaa zenye lengo la
kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga
shule
ya
watoto
wenye
ulemavu.Ameguswa sana kwa jambo hilo
na kwa hiyo anataka kutoa mchango wake
.Hakutaka kunipa mimi mchango wake
niulete bali anataka akukabidhi ana kwa
ana .Kwa hiyo amenituma nikwambie
kwamba anahitaji kuonana nawe usiku wa
leo kwa ajili ya chakula maalum na
akukabidhi mchango wake.Anaomba
ukutane naye katika hoteli aliyofikia ya
Kobe Village ”
Monica akastuka na kuiweka mikono
yake
kifuani
mahala
uliko
moyo.Akamtazama Muyeye kwa sekunde
kadhaa na kusema
“ Pierre Muyeye ninashindwa nikupe
jibu gani kwa ufupi nimestushwa kidogo
na mwaliko huu wa rais David.Sikuwa
nimetarajia kabisa kama mtu wa kutoka
mbali angeweza kuguswa na juhudi zangu
wakati watu wa hapa hapa nchini
wanashindwa .Hii ni heshima kubwa sana
na niko tayari kuonana na mheshmiwa
rais.” Akasema Monica
“ Ahsante sana Monica.Mheshimiwa
rais atafurahi sana kwa kukubali kuonana
nawe.Nakuahidi hutajutia uamuzi wako
wa kukubali kwenda kuonana naye.Ni mtu
mwenye moyo wa kusaidia na tayari
amekwisha wasaidia watu wengi sana kwa
hiyo hii ni fursa kwako ya kuweza
kufanikisha mipango yako.Ukifika
mueleze mipango yako yote unayokusudia
kuifanya na ninakuhakikishia Monica
lazima David atakusaidia “ akasema
Muyeye.
“ Ahsante sana Muyeye nitafanya
hivyo”
“ Sawa Monica basi kwa kuwa
umekubali mimi nitamjulisha habari hizi
na saa moja na nusu za jioni utakuja
kuchukuliwa na gari la ubalozi kupelekwa
hotelini kuonana na mheshmiwa rais”
akasema Muyeye akaagana na Monica
akaondoka zake.
“ Dah ! ama kweli huu ni mwaka
wangu.Mbona
mambo
mazuri
yanaongozana namna hii? Naamini Mungu
ananitumia ili kuwasaidia watu wake
wenye matatizo na ndiyo maana
anaelekeza mambo mazuri namna hii kuja
kwangu.Rais wa Kongo kuguswa na jambo
ninalolifanya ni mafanikio makubwa sana
kwangu.” Akasimama kidogo akelekeza
macho jukwaani kulikotoka shangwe
kubwa kutokana na mambo makubwa
aliyokuwa anayafanya mmoja wa wasanii
wakubwa aliyekuwa anatumbuiza lakini
akili yake haikuwa jukwaani alikuwa
mbali sana kimawazo
“ Nimewahi kuzisikia taarifa za rais
huyu wa Kongo kuwa ni rais tajiri kuliko
wote afrika.Kama kweli ana nia ya dhati ya
kutaka kunisaidia basi nina hakika
mipango yangu itakwenda kama
 
SEHEM YA 35

nilivyokusudia.Napaswa kumshukuru
sana Mungu kwa jambo hili” akawaza
Monica na kuelekea moja kwa moja
mahala walikokuwa wamekaa wazazi
wake akaomba wasogee pembeni
waongee.
“ Monica hongera sana zimekuwa ni
mbio nzuri sana na zenye
mafanikio.Muitikio umekuwa mkubwa na
watu wamehamasika sana.Hongera kwa
hilo juhudi zako zinaonekana na nina
hakika Mungu ataendelea kukubariki ili
mambo yako yaendelee vizuri uzidi
kuwasaidia watu wengi wenye uwezo”
akasema mzee Benedict
“ Ahsante sana baba.Usemayo ni
sahihi kabisa nina haki ya kumshukuru
Mungu kwani ni kweli jambo hili limefana
kwa kiwango ambacho sikuwa
nimekitarajia.Japokuwa
tumefanya
umasishaji mkubwa lakini sikuwa
nimetegemea kama watu wangehamasika
na kujitokeza kwa maelfu.Ninamshukuru
sana Mungu kwa kunisaidia jambo hili
limekwenda vizuri” akasema Monica
“ Nimemuona Daniel hapa “ akasema
bi Janet.Monica akacheka kidogo na
kusema
“ Mama hapa si mahali pa
kuliongelea
hilo.Tutapata
wasaa
tutaongea ila kuna jambo moja ambalo
nimeona
ni
vyema
endapo
nitawashirikisha ninyi wazazi wangu”
“ Ni jambo gani hilo? Akauliza mzee
Benedict
“ Nimetoka kuongea na mtu moja
anaitwa Jean Pierre Muyeye msaidizi wa
rais wa Kongo” akasema Monica na
kunyamaza kidogo
“ Ameshiriki katika mbio
akimuwakilisha rais wa Kongo lakini
alikuwa na ujumbe pia kutoka kwa rais
ambaye yuko hapa nchini kwa ajili ya
mkutano wa marais wa nchi za maziwa
makuu unaofanyikia hapa Dar es
salaam.David Zumo rais wa Kongo
ameguswa na kile ninachotaka kukifanya
na ameamua atoe mchango wake kwa hiyo
amenikaribisha
hotelini
kwake
nikaonanaye naye jioni ya leo ili aweze
kunikabidhi mchango wake.Kwa mujibu
wa Pierre Muyeye,David amekuwa
akisaidia sana watu wengi na hasa
wanaofanya mambo makubwa kwa
jamii.Nimeona niwashirikishe jambo hili
ili mnishauri japokuwa tayari nimekwisha
mkubalia Muyeye kuwa nitaonana na rais
wa Kongo jioni ya leo.Mnasemaje kuhusu
hilo ? akauliza Monika. Mzee Benedict na
mke wake wakatazamana kisha mzee
Benard akasema
“ Monica milango ya mafanikio
inazidi kufunguka na sasa imekwenda
mbali zaidi .Naweza sema kwamba hii ni
fursa kwako kufanikisha malengo yako
yote kwani kila unachokifanya
kinakwende vizuri na hata watu wakubwa
tayari wameanza kuziona juhudi zako na
wamejitokeza kukuunga mkono.Nenda
kaonane na David Zumo kama
alivyokuomba.Ni tajiri namba moja afrika
na anaweza akakusaidia sana.Nadhani
hakuna haja ya kuongea mambo mengi sisi
tunakubaliana na ulichokifanya na
tunakutakia kila la heri.Utakaporejea
utakuja kutujuza kitakachokuwa kimejiri
huko” akasema mzee Benedict.Monica
akawakumbatia wazazi wake kwa furaha
Shughuli zilizopangwa kufanyika
siku hii ya jumamosi zilikamilika na watu
wakatawanyika.Monica akawaacha
wasaidizi wake wakiendelea na kumalizia
shughuli ndogo zilizobaki akaondoka kwa
ajili ya kwenda kujiandaa kuonana na rais
wa Kongo David Zumo
 
kwapozi hilo matata tafadhali naomba nijumuike nawewe... ili tufanye mambo mubashara tupunguze na arosto mubashara..😀
UNASEMAJE...?
karibu sana wote tuwe mateja
 
Back
Top Bottom