SEHEMU YA 63
liliingia katika ubalozi wa Chia lakini
ililikuwa ni gari la mizigo na inaonekana
kuna mzigo uliwasilishwa pale
ubalozini.MUkasha naye aliwasili hapo
ubalozini lakini alikuwa peke yake na
baada ya muda akatoka akiwa peke yake ”
“ Are you sure Muhsin? Akauliza
Agatha
“ Ndiyo Agatha.Ninawamini vijana
niliowatuma katika kazi hiyo”
Agatha akafikiri kidogo kisha
akasema
“ Ok Muhsin una taarifa ya
kinachokwenda kujadiliwa katika kikao
cha dharura cha baraza la mawaziri
alichokiitisha rais leo?
“ hapana Agatha,sina taarifa zozote
kuhusu yanayokwedna kujadiliwa katika
kiako hicho.” Akasema Muhsin na ukimya
mfupi ukapita,Agatha akasema
“ Muhsin lakini jitahidi uwe
mchunguzi wa kila jambo Kwa sasa tuko
katika hatua muhimu sana ya kufanikisha
mambo makubwa kwa hiyo hatupaswi
kulala.Kila mtu acheze nafasi yake
vizuri.Utanieleza kitakachojadiliwa katika
hicho kikao kwani Ernest amegoma kabisa
kunieleza chochote”
“ sawa madam nitakujulisha usihofu
“ akasema muhsin,Agatha akakata simu.
“Ninamfahamu vizuri Ernest
kuliko mtu yeyote ,kuna jambo zito
linalomsumbua na analifanya siri.Nitajua
tu kinachoendelea “akasema Agatha.
Ernest mkasa aliingia ofisini kwake
lakini alihisi kichwa chake kizito kufanya
kazi yoyote.
“ What I’m going to do today,i
s
very dangerous but I have to do it because
it’s the right thing .Nimechoshwa na
kupelekwa pelekwa kama gari
bovu.Maneno aliyoyaongea Austin jana
yalinichoma sana na siwezi tena
kuendelea kuwa daraja la watu wachache
kufanikisha mipango yao haramu.Lazima
nisimame kama rais niwapiganie
wananchi
wangu
wanyonge
walionichagua.Kwa kuanzia muswada wa
haki za binadamu ninaufuta kuanzia
leo.Nafahamu kitendo cha kuufuta
muswada huo kutawastua sana hawa watu
na wataanzisha mapambano na mimi na
kwa namna walivyo na nguvu ninaweza
kuuawa kama alivyouawa rais
aliyenitangulia .Alikataa kushiriki katika
mipango yao na kilichofuata
wakamuua.I’m so scared.These people are
monsters”akawaza Ernest na kufungua
kompyuta yake akafungua sehemu
alikohifadhi picha za Monica alizozitoa
mtandaoni akaanza kuzitazama moja
baada ya nyingine akajikuta akitabasamu.
“Ninaomba majibu yatoke na
kunihakikishia kuwa Monica ni
mwanangu kwa sababu kile
ninachokifanya sasa hivi ni kwa ajili
yake.Kama atakuwa kweli ni mwanangu
nitamlinda kwa kila namna
nitakavyoweza kwani wabaya wangu
wakifahamu kuwa ni mwanangu basi
watamtumia kama fimbo ya
kunipigia.Lakini sina wasiwasi kwani
Austine yupo na atakubali kubaki
Tanzania kwani yale yote aliyoyataka
nimeyatekeleza.Nimetokea kumuamini
sana Austine ni kijana mwenye akili nyingi
na mwenye ujuzi wa hali ya juu.Alitaka
kuuliwa kwa sababu tayari alikwisha
kuwa kikwazo kwa watu na hasa
Alberto’s.Sifahamu aligundua nini hadi
wakataka kumuua lakini naamini ni jambo
zito.Austin amenikosha sana kwa namna
anavyojiamini”