QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

Ya kitoto mno mkuu
Hakuna serious man eti yupo bize anayeweza fanya hivi watu hamjang'amua tu
Mi mwenyewe nipo bize kishenzi
Bit not this way kama jamaa anavyojielezeaga
Acha kulalamika mkuu.watu ndio tunafika home ww bahati mbaya usha lala kitambo unajigeuza geuza tuu hapo.ww upo busy na kitanda wengine tupo busy na kulenga madaraja
 
QUEEN MONICA SEASON 3

SEHEMU YA 1


ILIPOISHIA SEASON ILIYOPITA
“He’s
here.Austin
tayari
amekuja.Ngoja nikamchukue yupo
mapokezi “ akasema Linah na kutoka
.Baada ya dakika tano akarejea akiwa
ameongozana na kijana mmoja mtanashati
sana mwenye sura iliyojaa tabasamu
“Wow! What a handsome guy”
akawaza Monica baada ya kumuona
Austin.Alikuwa ni kama mtu aliyepigwa na
butwaa kwa kitu alichokuwa anakitazama
mbele yake.
“Monica “ akaita Linah na kumstua
Monica
“Huyu anaitwa Austin January.Ndiye
mgeni Yule niliyekueleza alikuwa
anakutafuta”
“Austin huyu ndiye Monica Benedict
mwamsole,mkuu wa kampuni hii” LInah
akafanya utambulisho.Monica akasimama
na kumpa Austin mkono.
“Karibu sana Austin.Nimefurahi
kukutana nawe”
“Hata mimi nimefurahi sana kuonana
nawe Monica” akasema Austin na kuketi
katika sofa.Linah akatoka na kuwaacha
Monica na Austin pale ofisini.
ENDELEA..................................
“ Uzuri wa Monica si uzuri wa
kawaida, naweza kumfananisha na viumbe
toka sayari nyingine.Ni uzuri usioweza
kuelezeka kwa maneno.” Akawaza Austin
huku akimtazama Monica kwa jicho la
wizi.
“ Austin karibu sana “ Monica
akaanzisha maongezi
“ Ahsante sana Monica.Pole kwa
safari.Nilifika hapa jana nikataarifiwa
kwamba ulikuwa safarini nje ya nchi.”
“ Ni kweli Austin nilikuwa nje ya nchi
nimerejea jana jioni na nilipofika
nilitaarifiwa kwamba ulifika hapa
kunitafuta”
“Natumai msaidizi wako Linah
amekwisha kueleza kwa ufupi kuhusu
mimi na nini kilichonileta hapa kwako.”
“ Ndiyo alinieleza” akajibu Monica
“ Vizuri.Kwa ufupi naitwa Austin
January,ni mtanzania lakini kwa sasa nina
uraia wa Afrika ya kusini.Kikazi mimi ni
mkurugenzi wa utawala na fedha katika
kampuni ya kitalii ya A.A safari yenye
makao yake makuu nchini Afrika ya
kusini.Tunawapokea watalii toka nchi
mbali mbali duniani na kuwapeleka
sehemu mbali mbali za bara la Afrika.Vile
vile tunazo hoteli zinaitwa AA 5 stars hotel
ambazo zimesambaa katika sehemu mbali
mbali za bara la Afrika.Kwa kifupi naweza
kusema kwamba kampuni yetu ni moja
kati ya kampuni kubwa na bora kabisa za
utalii hapa Afrika” akasema Austin
“Nimefurahi sana kukufahamu
Austin.Mimi ni Monica Benedict ni
mkurugenzi wa kampuni hii
inayojishughulisha na masuala ya ubunifu
na utengenezaji wa mavazi.Tunabuni
mavazi hapa na kupeleka bunifu zetu
katika viwanda vya ndani na nje ya
nchi.Sidhani kama nitakuwa najisifu
nikisema kwamba kampuni yetu ni moja
kati ya kampuni bora kabisa ya mavazi
katika ukanda huu wa Afrika
mashariki.Mbali na mavazi ninayo pia
taasisi yangu inayojisghughulisha na
kusaidia jamii yenye uhitaji na hapa
tumejikita zaidi kusaidia watoto na wazee
wasiojiweza”
“ Hicho ndicho haswa kilichonileta
hapa kwako Monica “ akasema Austin kwa
furaha
“ Kampuni yetu ina kitengo kidogo
cha kusaidia miradi mbali mbali ya kijamii
katika sehemu zile ambazo tuna ofisi zetu.
Tumekuwa tukichangia ujenzi wa
mashule,hospitali n.k.Kwa sasa tuko katika
maandalizi ya kufungua ofisi zetu hapa Dar
es salaam kwa hiyo tunataka kuanza
kushiriki pia katika miradi mbalimbali ya
kijamii lakini kabla ya kufanya hivyo
tumeona tujifunze kwanza toka kwa
wenzetu ili tufahamu ni sehemu gani
tunaweza na sisi kuwekeza nguvu zetu
hapa Tanzania.Kwa hiyo Monica nimekuja
hapa kwako kujifunza kwani wewe na
taasisi yako tayari mnao uzoefu wa
kutosha na mazingira ya huku Tanzania na
kama itawezekana tunaweza kushirikiana
katika baadhi ya miradi ya kijamii” Austin
akanyamaza na kurekebisha tai yake na
kumtazama Monica
“ Austin nimefurahi kusikia kwamba
na ninyi pia mnajishughulisha katika
kusaidia jamii masikini zenye uhitaji
.Hakuna shaka sisi na ninyi tutashirikiana
katika miradi mbali mbali .Jamii masikni
hapa Tanzania zina changamoto nyingi
sana mfano elimu,afya,maji safi na salama
n.k.Haya ni maeneo ambayo sisi tumeyapa
kipaumbele kikubwa kwa kushjirikiana na
wafadhili mbali mbali tumeweza kujenga
vituo zaidi ya kumi na sita vya
afya,madarasa zaidi ya hamshini,visima
vya m,ai zaidi ya sitini katika sehemu
mbalimbali nchini wanakopishi watu
masikini .Tumekuwa tukifadhili matibabu
ya wazee wasiojiweza,kuwasaidia misaada
mingine muhimu kama vile chakula
n.k.Tumekuwa pia tukifadhili pia elimu
kwa watoto toka jamii masikini mfano kwa
sasa tuko katika hatua za mwisho za ujenzi
wa shule kubwa ya watoto wenye ulemavu
wa kutokuona na kusikia.Haya ni baadhi tu
ya mambo ambayo mimi na taasisi yangu
tumekuwa tukiyafanya”akasema Monica
“ Hongereni sana Monica” akasema
Austin.Monica akainuka akaliendea kabati
na kutoa karatasi tatu kubwa akampatia
Austin
“ Hiyo ni shule ambayo tunaanza
kuijenga hivi karibuni.Pesa tayari
tumeipata na kilichobaki ni kumpata
mkandarasi ili ujenzi uanze mara moja”
Uso wa Austin ukapambwa na
tabasamu kubwa
“ Monica unastahili pongezi kubwa
sana kwa hili ulilolifanya.Jamii hii ya
walemavu wana uhitaji mkubwa na
wamesahaulika sana katika jamii
zetu.Shule hii itakuwa ni mkombozi
mkubwa kwao” akasema Austin
“ Ahsante Austin” akasema Monica
na mara mlango ukafunguliwa akingia
Linah.Akamnong’oneza kitu Monica na
kutoka
“Austin nimetaarifiwa kuwa
ninahitajika eneo la ujenzi kuna watu toka
wizarani wamefika na wananisubiri”
akasema Monica
“ Oh ! sawa Monica.Ninashukuru
sana kwa kunipokea vizuri na nina imani
tutapata wasaa mzuri zaidi wa
kulizungumzia suala hili kwa upana
.Nikutakie kila la heri katika kazi zako”
akasema Austin huku akiinuka
“Nashukuru pia kukufahamu
Austin.Nitatafuta nafasi nyingine tukae
tuzungumze kwa kirefu juu ya suala hili”
akasema Monica wakaagana lakini kabla
Austin hajatoka mle ofisini Monica
akasema
“ Austin kama hutojali tunaweza
kuongozana kwenda eneo la ujenzi?
Austin ambaye tayari alikuwa
ameukaribia mlango akageuka haraka
haraka na kusema
“ Hakuna tatizo Monica tunaweza
kwenda
 
SEHEMU YA 2



“ Good” akasema Monica na
kuchukua mkoba wake wakatoka .Kila
mmoja aliingia katika gari lake
wakaondoka
“ Dah ! Monica ni mwanamke
mwenye uzuri wa kipekee mno.Mungu
atanisamehe kwa mawazo haya lakini
amempendelea mno Monica.Licha ya
kumpa uzuri usioelezeka amempa pia
moyo uliojaa huruma na upendo wa
kipekee ndiyo maana amekuwa anajitoa
mno kwa jamii masikini.Nimehisi kuguswa
sana na mambo haya makubwa
anayoyafanya kwa jamii.Huyu ni
mwanamke wa mfano na anastahili kuwa
malkia wa Afrika” akawaza Austin akiwa
njiani wakielekea katika mradi wa shule ya
walemavu
“ Mwanaume atakayepata nafasi ya
kumpata Monica atakuwa na bahati ya
kipekee kabisa,atakuwa amepata kitu cha
thamani kubwa kuliko hata gari lililojaa
madini.Wanawake wa aina hii ni wachache
mno katika dunia ya sasa.Natamani sana
kumjua mpenzi wake ni nani nimpe
hongera yake” akaendelea kuwaza Austin
na kutabasamu baada ya sura ya Monica
kumjia kichwani
“ Nahisi kama vile sura ya Monica
inaingia kwa kasi kubwa katika akili yangu
kiasi cha kumuwaza kila sekunde.Oh no !
sitakiwi kuyaruhusu mawazo haya
yatawale kichwa changu kwa
sasa.Natakiwa kuelekeza akili yangu yote
katika mambo mazito yaliyoko mbele
yangu” akawaza na kumkumbuka mpenzi
wake Maria
“Nina hakika kwa muda huu Maria
tayari atakuwa amerejea au anajiandaa
kurejea afrika kusini.Hawezi kuja Tanzania
bila ya kuwasiliana nami kwanza .Nakubali
sijamtendea vizuri lakini hii ni kwa ajili ya
usalama wake.Siwezi kumruhusu
mwanamke nimpendaye akaingia katika
hatari .Baada ya kazi kumalizika
nitamuomba msamaha na nina imani
atanielewa tu”
Mawazo mengi yalikisonga kichwa
cha Monica wakati akielekea katika eneo la
ujenzi wa shule.Aliwaza kuhusu ndoa yake
na David,akawaza kuhusu maisha mapya
atakayoyaishi ambayo ni maisha ya
kifahari mno,na mara akamkumbuka
Marcelo.Alitaka sana kufahamu mahala
alipo Marcelo.Alihitaji sana kumjulia hali
na kuona namna ya kumsaidia
“ Naamini hadi jioni ya leo,David
atakuwa tayari ameelekezwa mahala aliko
Marcelo ili nimjulie hali na kutafuta namna
ya kumsaidia.Anahitaji sana msaada
wangu na vile vile ninataka niongee naye
kuhusu ugonjwa wa Pauline ,inawezekana
akawa na mchango wowote hata wa
mawazo”
Kwa mbali machozi yakamlenga
alipomkumbuka Pauline.
“Mungu,akuponyePauline.Nakuombe
a sana upasuaji utakaofanyiwa ufanikiwe
na uendelee kuwa mzima.U mwanamke
mwenye upendo wa kipekee kabisa “
akawaza Monica
Waliwasili eneo la ujenzi ,Monica
akakutana na wageni wake waliokuwa
wanamsubiri,wakalizungka eneo lote na
kuelekezana mambo kadhaa wakaondoka
na kuwaacha Monica na Austin
“ Monica narudia tena kusema kuwa
unastahili pongezi za kipekee kwa
mchango wako mkubwa kwa jamii.Jambo
hili unalolifanya ni kubwa sana.Hongera
kwa mara nyingine” akasema Austin
.Monica akatabasamu na kusema
“Ahsante sana Austin.Pamoja na
kwamba mimi ndiye niliyebuni wazo hili la
kujenga shule hii lakini nyuma yangu kuna
kundi la wadau wanaoniunga mkono na
kulifanya jambo hili liwezekane.Wamejitoa
kwa hali na mali na muda wowote toka
sasa mradi utaanza.Ninafurahi sana kwa
mradi huu kufikia hatua hii ya
kuanza.Ilikuwa ni ndoto yangu ya muda
mrefu na sasa inakwenda kuwa kweli”
akasema Monica na ukimya mfupi ukapita
“ Austin mimi ninarejea tena ofisini
kama unavyoelewa sikuwepo kwa siku
kadhaa hivyo nina mzigo wa
kazi.Nitatafuta wasaa na tutakaa tutaongea
.Kuna mambo mengi ambayo tunaweza
tukayafanya kwa ushirikiano.” Akasema
Monica .Austin akaitazama saa yake ya
dhahabu na kusema
“ Sawa Monica nikutakie kazi njema
lakini hata hivyo nina ombi moja kama
hutajali”
“Omba Austin”
“Monica una kazi nyingi
zinazokukabili kwa hiyo kwa sisi kupata
wasaa wa kutosha kuzungumza kwa kina
mambo tunayoweza kushirikiana
itachukua muda kidogo kwa hiyo kama
hutajali naweza kukualika kwa chakula
cha usiku na tukautumia muda huo
kuzungumza?
Monica akatabasamu na kusema
“Usemayo ni ya kweli Austin,nina
kazi nyingi lakini kuhusu ombi lako ngoja
niangalie ratiba yangu endapo itaniruhusu
nitakujulisha.Nipatie namba yako ya simu”
walibadilishana namba za simu wakaagana
kila mmoja akaingia katika gari lake
wakaondoka
“ Imekuwa siku nzuri,nimeanza kazi
yangu vizuri .Monica tayari amenikubali na
hiki
ndicho
nilichokuwa
 
SEHEMU YA 3



nakitafuta.Ninaziona kila dalili za urafiki
mkubwa kati yetu.Ombi langu la kukutana
naye kwa chakula cha usiku amelipokea na
ameahidi kunijibu.Naamini atakubali na
endapo atakubali nitajitahidi kutumia
vyema kila nafasi nitakayoipata ili kuipata
sampuli na hapa ninalenga zaidi nywele.Ili
kuipata nywele yanipasa..oh gosh ! “
akawaza Austin na kujikuta akistuka
“Ili kuipata nywele ya Monica
yanipasa nijenge ukaribu naye mkubwa na
hapa nina maanisha ni lazima kulala naye”
Mwili wote ukamsisimka alipowaza
jambo hili
“Nimesisimkwa mwili wote kwa hiki
ninachokiwaza.Lakini sioni njia nyingine
ya kuweza kuipata nwele ya Monica bila
kufanya hivi ninavyofikiri.Kulala naye
ndiyo njia pekee na rahisi.Halafu ....”
Austin akasita kidogo
“ Baada ya kuonana ana kwa ana na
Monica nahisi kama kuna kitu kimeanza
kujijenga taratibu kichwani kwangu.Sura
ya Monica hainibanduki kichwani.Kila
dakika ninamuwaza yeye.Oh no ! sitaki
kuanzisha mahusiano kwa sasa bali
ninachotakiwa ni kuikamilisha kazi yangu
ya kuipata sampuli na hata kama nikilala
naye lengo litakuwa ni hilo tu na si
vingine.” Akawaza na kutabasamu halafu
akamkumbuka Maria
“ Hiki ninachowaza kukifanya ni
kitendo cha usaliti kwa mpenzi wangu
Maria ambaye ni kwa sababu yake
nimefika hapa nilipo .What am I going to
do ? Austin akajiuliza
“Lakini hii ni sehemu ya kazi.Ili
kuikamilisha kazi niliyopewa lazima
nifanye hivyo.Hata hivyo nitafanya mara
moja tu .Nimekuja Tanzania kufanya kazi
kwa hiyo lazima nikae kikazi.Natakiwa
kumuweka pembeni Maria. Nikiendelea
kumuwaza sana kila dakika nitashindwa
kuifanya kazi yangu.Kwa kuwa tayari nina
uhakika hataweza tena kuja Dar es salaam
ninapaswa kumuweka pembeni muda huu
hadi hapo kazi itakapokuwa
imekamlika.Kazi hii ni muhimu mno
kwangu kuikamilisha”
*******************
Boaz akiwa chumbani kwake katika
hoteli hii kubwa aliyofikia huku
akionekana kuwa na mawazo mengi
akawasha simu yake ambayo huitumia
awapo Tanzania.Akazitafuta namba fulani
akapiga
“ Hallow Boaz.” Ikasema sauti nzito
upande wa pili.
“ Peter Chui.Habari ya Dar es salaam?
Akauliza Boaz.
“ Dar es salaam naweza kusema si
kwema.Bahari imechafuka kuna upepo
mbaya unavuma kwa sasa.Nimekutafuta
sana jana katika simu bila
mafanikio.Nimekufurahi
umenipigia.Welcome home Boaz”
“ Asante sana Peter.Ni upepo huo
mbaya ndio ulionirejesha nyumbani mara
moja.Msijali vijana wangu,baba yenu
nimerudi,mawimbi na dhoruba vyote
vitatulia.Neno langu moja tu linatosha
kabisa kuituliza dhoruba hii.Nataka
umtume kijana aje anichukue nina
maongezi nawe”
“Uko wapi sasa hivi?
Boaz akamuelekeza mtu aliyekuwa
anaongea naye simuni hoteli aliyofikia
akakata simu na kuzitafuta namba
nyingine akapiga
“ Hallow my love.Nimestuka sana
baada ya kuona simu yako.Karibu sana
nyumbani mpenzi” ikasema sauti nzuri ya
kike upande wa pili
“ Hello Julieth.How’re you my queen”
akasema Boaz
“ I’m ok.Mbona umekuja kimya
kimya bila tarifa?
“Imenilazimu kuja kimya kimya
kutokana na huu upepo mbaya unaoanza
kuvuma hapa nchini kwa sasa.Uko wapi
mida hii? Nahitaji tuonane ili unipatie kile
kitabu.Kwa hali ya sasa ilivyo natakiwa
kukihifadhi sehemu salama kwani ndilo
tumaini letu la kutuhakikishia tuko
salama”
“ Kwa sasa niko nyumbani” akajibu
Julieth
“Sawa Julieth,naomba tukutane
Mzizima City.Ninaelekea hapo muda si
mrefu” akasema Boaz na kukata
simu.Hazikupita dakika thelathini kijana
aliyetumwa
kuja
kumchukua
akawasili.Boaz akamuaga Maria na kuingia
katika gari akaondoka.Kituo cha kwanza
ilikuwa ni mzizima city mahala penye
majengo mengi ya biashara ,akachukua
simu na kumpigia Julieth
“Tayari nimefika hapa Mzizima .Uko
sehemu gani? akasema Julieth baada ya
kupokea simu.
“Njoo hapa duka la mavazi
mchanganyiko utaiona gari nyeupe aina ya
Jaguar na bila kuonyesha wasiwasi
wowote fungua mlango wa nyuma na
uingie” akasema Boaz.Baada ya kama
dakika tatu mlango wa gari alimokuwemo
Boaz ukafunguliwa akaingia Julieth kisha
gari ikaondoka.Boaz akamvuta na
kumbusu
“Nafurahi nimekuona Julieth”
“Hata mimi nimefurahi mno kukuona
Boaz.Ila umeniudhi kwa kuja kimya
 
SEHEMU YA 4


kimya.Ungenitaarifu nngekuja kukupokea
uwanja wa ndege” akasema Julieth na
kumbusu tena Boaz
“ Haikuwa katika ratiba zangu kuja
Tanzania kwa sasa lakini imenilazimu
kukatisha baadhi ya shughuli zangu na
kuja kuweka sawa mambo kutokana na
huu upepo mbaya unaoanza kuvuma.Hata
ndugu zangu hapa Dar hawajui kama niko
hapa.By the way kuna taarifa zozote mpya
kuhusiana na Marcelo?
“ Mpaka sasa hakuna taarifa zozote
na bado hatujui aliko.Jeshi la polisi mpaka
sasa bado halijatoa taarifa yoyote
kuhusiana na kupotea kwake.”
“ Damn ! he’s very smart lakini
tutampata tu” akasema Boaz.
“Una uhakika hajahisi chochote
kuhusu wewe kwamba ndiye uliyeingia
chumbani kwake na chukua kitabu ?
Akauliza Boaz
“Sina hakika sana .Nahisi kuna kitu
anakihisi kwani alipokuwa hospitali
alionyesha utofauti .Hakutaka maongezi na
mimi kabisa.Kuna baadhi ya mambo
ambayo hakutaka kabisa sisi ndugu zake
tuyafahamu.Kuna watu wawili ambao
alikuwa nao karibu na kuwasiliana nao
kwa siri.” akasema Julieth
“It’s ok.Where is the book? Akauliza
Boaz.Julieth akafungua mkoba wake
akatoa bahasha kubwa ya khaki na
kumpatia Boaz
“Did you open it? Ulisoma kilichomo
ndani? Akauliza Boaz huku akimtazama
JUlieth kwa macho makali
“Hapana
sijafungua
kama
ulivyoelekeza”
“ Good” akajibu Boaz na kuifungua ile
bahasha akatoa kitabu cheusi
akakitazama,akamvuta Julieth na kumbusu
“ Good Job Julieth” akasema na
kukifungua kile kitabu
********************
Kazi kubwa aliyopanga kuifanya
Austin siku hii ni kuonana na
Monica.Akiwa njiani akirejea nyumbani
baada ya kuachana na Monica Austin
akakumbuka kitu.
“Job Israel..!! akasema kwa suti
ndogo
“ Kwa kuwa ninao muda wa kutosha
kwa nini nisimtafute huyu mtu? Ni mmoja
wa watu ninaofikiria kuwajumuisha
katika
kikosi
cha
kumlinda
rais.Ninafahamu uwezo wake ,nimewahi
kufanya naye kazi kadhaa ni mtu mwenye
uwezo mkubwa.Ni mtu hatari” akawaza
Austin
Alibadili uelekeo na kuelekeo mahala
alikokuwa akiishi Job
“ Miaka kadhaa imepita sasa Dar es
salaam imebadilika mno si ile ya miaka
ile.Wakati naondoka hakukuwa na
majengo mazuri hivi katika mtaa huu.”
Austin alikuwa anaendesha taratibu huku
akitazama nje
“Sijawasiliana na Job muda mrefu na
inawezekana akapatwa na mstuko
mkubwa kwani lazima atakuwa akiamini
nilikufa Somalia.kazi ya mwisho kufanya
naye ilikuwa ni ile tuliyokwenda Malawi
kuwakomboa
majasusi
wawili
waliokamatwa nchini humo.Toka hapo
sikuwahi kuwasiliana naye tena .” akawaza
Austin huku akisimamisha gari pembeni
ya mti wa mkorosho na kutazama nyumba
nzuri ya ghorofa moja
“Job amejenga ghorofa ! Amejitahidi
sana . Lakini ni hapa nyumbani kwa Job au
nimepotea? Akajiuliza Austin.
“ lakini ni hapa kwani
kinachonithibitishia kuwa ni hapa ni lile
duka la Mangi pale pembeni.Duka
lile,lilikuwepo hapa toka wakati ule wakati
ule ninakuja na Job...”
Wakati akiendela kutafakari ghafla
geti la nyumba ile likafunguliwa na gari
zuri la kifahari lenye rangi nyekundu
likatoka likiendeshwa na mwanamke
mrembo .Austin akastuka
“ Yule mwanamke ni nani? Mbona si
mke wa Job?Au nmekosea nyumba? Lakini
hapana sijakosea ngoja nikaulize pale
dukani nipate uhakika zaidi” akawaza
Austin na kuelekea dukani akanunua maji
ya kunywa na kuuliza
“ Samahani ndugu yangu naomba
kuuliza”
“ Bila samahani kaka” akajibu muuza
duka.
“ Natumai wewe ni mwenyeji sana
wa eneo hili”
“ Ndiyo mimi ni mwenyeji sana wa
hapa.Nina miaka zaidi ya ishirini eneo
hili.Baba yangu ndiye mwanzilishi wa
kitongoji hiki cha mafarasi kwani zamani
yeye alihamia huku kukiwa pori ili apate
malisho mazuri ya farasi aliokuwa
anafuga.Baadae
watu
wakaanza
kuongezeka kwa hiyo mimi ni mkongwe
eneo hili ” akajibu muuza duka
“Natumai utakuwa unamfahamu mtu
mmoja anaitwa Job au baba Millen huyu
anaishi hapa jirani yako”
“ Baba Millen ninamfahamu
sana.Alikuwa rafiki yangu”
Akasema muuza duka na kumstua
kidogo Austin.
“Mimi ni rafiki yake nilikuwa nje ya
nchi kwa muda mrefu ,nimerejea na
nikaona nije kumjulia hali rafiki yangu
 
SEHEMU YA 5



lakini nimestuka kidogo kukuta ghorofa
halafu akatoka mwanamke ambaye
simfahamu nikaona ngoja kwanza niulize
wenyeji kama huyu jamaa bado yuko hapa
au kuna mtu mwingine anaishi hapa”
akasema Austin
“Dah ! inaonekana hukuwepo nchini
kwa muda mrefu ndugu yangu.Huyu jamaa
alipatwa
na
matatizo
ya
akili.Alichanganyikiwa
baada
ya
kukimbiwa na mke wake.Inasemekana
mke wake alimpata mwanaume mwingine
halafu akamtupia jini huyu jamaa
akachanganyikiwa.Ndugu zake walikuja
kumchukua na walimpelekea kwa mganga
wa kienyeji kijiji Fulani huko karibu na
Kisarawe kinaitwa Mtoka mbali.Kuna
mganga anaitwa mzee Nyungu ni mganga
maarufu sana kwa magonjwa hayo.Kuna
ndugu yake mmoja niliyekuwa nawasiliana
naye ndiye aliyekuwa akinipa taarifa za
maendeleo ya baba Millen.Eneo hili
wamekwisha liuza na mimi ndiye
niliyewasaidia kutafuta mnunuzi.Labda
nikupe mawasiliano ya huyo ndugu yake
uwasiliane naye anaweza akakupa taarifa
zenye uhakika zaidi kuhusu baba Millen.”
Akasema muuza duka na kumpatia Austin
namba za simu za ndugu yake Job.Austin
akamshukuru Yule jamaa na kumpatia noti
ya shilingi elfu tano akapanda gari na
kuondoka
“Job amekuwa chizi? Ni vigumu
kuamini.Nini kimesababisha akawa chizi?
Ama kweli maisha haya yana maajabu
makubwa lakini sintaamini hadi hapo
nitakapomtia machoni.Kama ni kweli
litakuwa ni pigo kubwa kwangu kwani ni
mtu ambaye nilimuhitaji sana katika
operesheni yangu kutokana na uhodari
wake.Ngoja kwanza niwasiliane na ndugu
yake niliyepewa namba zake”
Austin akasimamisha gari pembeni
ya barabara akapiga zile namba alizopewa
za ndugu yake Job
“Hallow ndugu habari yako.Natumai
naongea na Amani” akasema Austin baada
ya simu yake kupokelewa
“Ndiyo unaongea na Amani.Nani
mwenzangu?
“Naitwa Austin.Mimi ni rafiki wa
ndugu yako Job.Ninaishi nje ya nchi
nimerejea jana na nikataka kumjulia hali
rafiki yangu ,nimefika mahala alikokuwa
akiishi nikapata taarifa kwamba amepatwa
na matatizo ya akili.Ninataka kufahamu
anaendeleaje hivi sasa?
“Ni kweli alipatwa na matatizo ya
akili.Nilimchukua na kumpeleka kwa
wataalamu .Kwa sasa hali yake siwezi
kusema ni nzuri au mbaya ila kidogo ana
unafuu”
“Dah!poleni sana kwa tatizo
hili.Nawezaje kuonana naye?
“Kwa sasa anaishi nyumbani kwangu
mji mpya Tegeta.Unahitaji mtu wa kwenda
naye kwani kwa kukuelekeza katika simu
inaweza kukupa ugumu kidogo kufika.Uko
wapi mida hii?
“Niko hapa karibu na alipokuwa
akiishi Job” akajibu Austin
“Sawa,Mimi niko hapa katika
kiwanda cha viatu cha Ndura.Kama una
usafiri njoo unichukue nikupeleke moja
kwa moja.Ukifika getini uliza Amani
mjeledi utanipata haraka”
“Ahsante sana Amani nitafika hapo
muda si mrefu” akasema Austin
********************
Msafara wa makamu wa rais
uliwasili nyumbani kwa waziri mkuu
aliyevuliwa madaraka na kupokelewa na
mwenyeji wake akakaribishwa sebuleni.
“Habari za maisha mapya? Akauliza
makamu wa rais wakati wakielekea
sebuleni na wote wakaangua kicheko
Sebuleni alikuwepo pia bi Agatha
Mkasa mke wa rais ambaye alisimama na
kusalimiana na makamu wa rais halafu kila
mmoja akaketi.Muhudumu aliyevalia
nadhifu akawahudumia vinywaji kisha
wakaendelea na maongezi.
“Ndugu zangu nimewaitieni hapa
kwa ajili ya kuzungumza kwa kina juu ya
hiki kilichotutokea.Sote tulikuwepo katika
kikao na tuliafikiana mambo ya
 
SEHEMU YA 6

kufanya.Ninayaheshimu maamuzi ya kikao
kile kikubwa lakini ndugu zangu pale
katika kikao hatukupata nafasi ya kutosha
kulijadili suala hili kwa undani wake na
ndiyo maana nimeona ni vyema endapo
tukikutana sisi watatu kulijadili suala hili
kwa kina zaidi.Baada ya kulitafakari kwa
kina nimegundua kwamba hatukuchukua
maamuzi sahihi kuhusiana na suala
hili.Kwa ufupi naweza kusema kwamba
tulikurupuka sana”
“Kwa nini una sehemu hivyo
Jeremiah? Akauliza Makamu wa rais
“Ninasema tulikurupuka kwa sababu
tulikwenda kinyume na katiba ya Alberto’s
ambayo iko wazi kwamba yeyote ambaye
ataisaliti jumuiya na ikathibitika hivyo basi
adhabu yake ni kifo.Ernest Mkasa
amefanya usaliti mkubwa na wa
wazi.Ameisaliti jumuiya kwa kitendo
chake cha kufuta ule muswaada na
kulivunja
baraza
zima
la
mawaziri.Akaenda mbali zaidi na kumvua
wadhifa mkuu wa majeshi.Ni wazi
ameanzisha vita na Alberto’s na tayari
ameanza kuikata mizizi yetu kwa
kasi.Nyote mnafahamu muswada ule
ulikuwa ni kila kitu kwetu.Endapo
tungefanikisha kuupitisha muswada ule
basi matrilioni na matrilioni ya fedha
yangemwagika hapa Tanzania.Tungekuwa
tumefanikiwa kuikomboa nchi hii toka
umasikini mkubwa lakini tumeshindwa
kulifanikisha
hilo.Tumeshindwa
kuikamilisha kazi tuliyopewa na Alberto
mkuu wa tatu .Tumemuangusha sana
kwani Tanzania ni nchi ambayo
anaitegemea mno.Hiki ni kioo cha nchi
nyingi” akanyamaza akavuta pumzi ndefu
na kuendelea
“ Kikao kile cha juzi cha kujadili hili
lililotokea ,kumezidi kutuzamisha na
kutufanya tuonekane hatufai na hatuna
uwezo
wa
kuiongoza
jumuiya.Tumeshindwa kuchukua hatua
zipasazo kulikabili suala hili.Toka
tulipokaa kikao hakuna taarifa yoyote
iliyotolewa na wala hakuna juhudi zozote
zinazoonekana za kutatua jambo
hili.Tumezidi kumpa nguvu Ernest ya
kutudhoofisha na anazidi kufanikiwa na
kama hatutachukua hatua za makusudi za
haraka ndani ya muda mfupi ujao
hakutakuwa na Alberto’s hapa
Tanzania.Atatufagia wote na hiyo ndiyo
dhamira yake.Kwa hiyo ndugu zangu
nimewaiteni hapa tulijadili kwa kina
jambo hili na sisi watatu tunaweza kufanya
jambo la msingi sana la kuinusuru jumuiya
yetu na tuzidi kuaminiwa na baba Alberto
mkuu” akasema Jeremiah
“ Alichokiongea ndugu yangu
Jeremiah ni kitu cha msingi sana na
ninaweza kukubaliana naye.Binafsi
maamuzi yaliyochukuliwa katika kikao kile
sikuyafurahia.Hayakuwa maamuzi sahihi
na muafaka kwa jambo kubwa na zito
kama hili.Naweza sema yalikuwa maamuzi
dhaifu mno.Sifahamu kwa nini mwenyekiti
aliamua kuchukua maamuzi kama yale
wakati anafahamu hali halisi ilivyo.Mimi
pia naungana nawe Jeremiah katika
hili.Japokuwa unaweza ukaonekana kama
ni usaliti ndani ya jumuiya lakini hatuwezi
kukaa kimya wakati tunaona tunakoelekea
si kuzuri hata kidog😵fisi ya rais ilikuwa
ni mhimili wetu mkuu ambao umen’goka
na sasa tunayumba na tusipokuwa makini
sote tutaanguka kwa hiyo ndugu zangu
nakubaliana na wazo la Jeremiah kwamba
tusikae kimya bali tuone namna ya
kufanya .Agatha wewe una lipi la
kuchangia kwa upande wako?
“ Kabla sijasema lolote kuna jambo
nataka kuwashirikisha.Nina chanzo
changu cha taarifa ndani ya makao makuu
na kwa mujibu wa chanzo hicho ni
kwamba toka lilipotokea tukio hili
kumekuwa na mfululizo wa vikao vya siri
kati ya Alberto mkuu wa tatu na watendaji
wa juu wa jumuiya.Hakuna bado taarifa
yoyote iliyopatikana wanajadili jambo
gani” Agatha akastuka baada ya simu yake
kuita
“Samahani naomba niipokee hii
simu” akatoka nje akaongea kwa takribani
dakika tano kisha akarejea sebuleni
“Tunaweza kuendelea” akasema
Agatha
“Nimepata taarifa nyingine toka kwa
chanzo changu kuwa mwenyekiti
ameitwa makao makuu haraka.Kwa mujbu
wa taarifa alizozipata huyo mpasha habari
wangu ni kwamba kuna timu imeundwa
ambayo itatumwa Tanzania kuja kulikabili
suala hili.Endapo timu hiyo itakuja
Tanzania basi sote tutawekwa pembeni
kwani tutakuwa tumeshindwa kuifanya
kazi yetu.Binafsi siko tayari hilo litokee
hasa nikikumbuka namna nilivyojitoa kwa
hali na mali kuipigania na kuipenyeza
jumuiya hapa Tanzania.” Akasema Agatha
“Haya yote yamesababishwa na huyu
mwenyekiti wetu kwa kushindwa
kuchukua maamuzi sahihi kwa wakati
unaostahili” akasema Jeremiah
“Kwa hiyo nini basi tunatakiwa
kufanya kwa sasa? Akauliza makamu wa
rais
“Kuna kitu kimoja tu ambacho
tunapaswa kukifanya .Tunatakiwa tumuue
mwenyekiti”
Ukimya mfupi ukapita halafu
makamu wa rais akauliz
 
SEHEMU YA 7


Una uhakika na hicho unachokisema
Jeremiah? Akauliza makamu wa rais
“ Ndugu zangu tukitaka tulimalize
suala hili lazima tumuue Obi.Baada ya
kumuondoa tutafanya kampeni na
kunichagua mimi niwe mwenyekiti wa
muda na tukifanikiwa katika hilo nitafanya
maamuzi sahihi na kitu cha kwanza
nitakachokifanya ni kutoa Baraka za
kumuua
Ernest
Mkasa.Hakuna
tutakachoweza kukifanya tena bila ya
kumuondoa
Ernest
madarakani.Tukifanikiwa kwa hilo kwa
mujibu wa katiba yetu makamu wa rais
utakaimu nafasi ya rais kwa muda na hapo
utanirejesha katika nafasi ya uwaziri mkuu
ili tuweze kuikamilisha kazi tuliyokwisha
ianza.Hivyo ndivyo ilivyotakiwa kufanywa
lakini tunaambiwa unatakiwa ufanyike
uchunguzi kwanza kabla ya kuchukua
hatua yoyote.Huo ni upuuzi
mkubwa.Hakuna ulazima wowote wa
kufanya uchunguzi.Sulala hapa ni moja tu
,Ernest amefanya usaliti hivyo lazima
auawe.Kitendo cha kumuacha mpaka sasa
ni kosa kubwa kwani anaendelea
kujiimarisha na kutufyeka taratibu.Ernest
is a very smart guy,anajua kuzicheza vizuri
karata zake.Kwa kipindi hiki chote
amekuwa akitusoma na baada ya
kutufahamu vyema ameanza kutufyeka
taratibu na tuspokuwa makini sote
tutakwenda na maji.” Jeremiah
akanyamaza na kuwatazama wenzake
ambao wote walikuwa kimya
“Mnaonaje juu ya wazo langu?
Akauliza Jeremiah
“Wazo lako si baya lakini huu ni
usaliti mwingine ndani ya jumuiya kwa
kwenda kinyume na maazimio ya kikao
kikubwa kama kile.Ni vipi endapo Alberto
mkuu akafahamu kuhusu hiki tunachotaka
kukifanya? Mnadhani akigundua tutakuwa
salama? Akauliza Makamu wa rais
“ Alberto he’s not here,we are.Albeto
is not a Tanzania ,we are.Kwa hiyo basi
haya tunayoyafanya ni kwa ajili ya nchi
yetu.Alberto anatutegemea sisi katika
mabadiliko anayotaka kuyafanya hapa
Tanzania kwa hiyo hatuwezi kukaa kimya
tukishuhudia mambo yakienda ndivyo
sivyo .Ndugu zangu tumejitahid sana
kuifikisha jumuiya hapa ilipofika kwa hiyo
basi tusikubali juhudi zetu zote zikaenda
bure.We must do something and we must
do it fast” akasisitiza Jeremiah
“Binafsi nakubaliana na Jeremiah”
akasema bi Agatha
“Ernest ametufanyia kitu kibaya mno
ambacho sikuwahi kutegemea kama
angekuja kukifanya kwa namna
ninavyomfahamu.Ni mume wangu ambaye
kuna wakati tulipendana sana lakini kwa
hili alilolifanya siwezi kumtetea.Nilikula
kiapo cha kuitetea jumuiya hata kwa damu
yangu kwa hiyo nakubaliana na Jeremiah
kwamba Ernest must die.Ernest si wa
kuonewa huruma hata kidogo.Amebadilika
mno,si mwenzetu tena na tukitaka
mabadiliko haya yafanikiwe basi hatuna
budi tumuondoe haraka sana.Me and him
we’re over” akasema Agatha kwa hasira
“ Ahsante Agatha .Sasa umebaki peke
yako makamu wa rais,tafadhali fanya
maamuzi” akasema Jeremiah.Makamu wa
rais akafikiri kwa muda kisha akasema
“Ok I’m in.Let’s do it”
“Good. Kama sote tunakubaliana
hivyo naomba tuendelee kuwa kitu
kimoja.Asitokee mmoja kati yetu akabadili
mawazo na kutusaliti.Kuhusu namna ya
kuutekeleza mpango huu yote niachieni
mimi.Ndani ya siku mbili zijazo nitakuwa
tayari na mpango wa namna
tutakavyoweza
kumuondoa
mwenyekiti.Nikiwa tayari nitawaiteni na
kuwajulisha lakini wakati mchakato huo
ukiendelea Agatha unatakiwa uwe karibu
sana na chanzo chako cha taarifa ili tujue
nini makao makuu wanafikiria kukifanya”
akasema Jeremiah kisha wakaendelea na
maongezi mengine
******************
Boaz alikifungua kitabu kile na
kuanza kupitia ukurasa mmoja baada ya
mwingne.Kila alipoufungua ukurasa sura
yake ilionyesha mabadiliko.Katikati ya
kitabu kile kulikuwa na karatasi
akaifungua haraka haraka na kuanza
kuisoma.Ilikuwa ni barua.Iliandikwa hivi
Kwako Marcelo
Nimeamua kukuandikia ujumbe
huu na kuuficha humu kwani sikutaka
ujumbe huu uupate angali bado niko
mzima.Nimeandika barua hii nikiwa
katika
siku
za
mwisho
za
uhai
wangu.Naandika huku macho yangu
yakiwa yamejaa machozi.Dhumuni kuu
la kukuandikia barua hii kwanza ni
kutaka ufahamu mimi baba yako ni nani
na maisha ya aina gani ambayo
nimeyaishi.Nimekuchagua wewe kati ya
watoto wangu kwani ndiye ninayeona
unastahili kuyafahamu haya.
Kwa
muda
mrefu
umekuwa
masomoni kwa hiyo hujapata nafasi ya
kukaa nami na kunifahamu vyema.Mimi
baba yako ni mmoja wa madaktari
maarufu
barani
Afrika.Nimekuwa
bingwa wa upasuaji wa moyo na kichwa
,vile vile nimekuwa bingwa wa saratan
 
SEHEMU YA 8


ya damu.Nimekuwa bingwa wa kuokoa
maisha
ya
watu
jambo
lililonipa
umaarufu mkubwa lakini katika siku
hizi
za
mwisho
za
uhai
wangu
nimegundua
kwamba
hakuna
atakayeweza
kuyaokoa
maisha
yangu.Natamani sana kama angetokea
bingwa wa kuyaokoa maisha yangu ili
niendelee kuishi lakini hakuna mwenye
uwezo huo so I must die.Baada ya
kutambua kwamba sintaweza kupona
nimeyatafakari maisha yangu niliyoishi
na kama nilitimiza vyema wajibu wangu
wa kuwapo hapa duniani.Robo tatu ya
maisha yangu nimetumia katika kazi
yangu ya udaktari na nimeokoa maisha
ya watu wengi .Nilijitoa kwa hali na mali
kuhakikisha kila mgonjwa ninayemtibu
anapona.Naweza kusema asilimia tisini
ya wagonjwa niliowatibu walipona na
kuendelea na maisha yao na hii ndiyo
iliyonifanya
kuwa
daktari
maarufu.Nilitimiza
vyema
wajibu
wangu kama daktari.Pamoja na mazuri
hayo yote bado kuna mambo ambayo
wengi hawayafahamu kuhusiana na
maisha yangu.Sehemu ya kwanza ya
maisha yangu ni hiyo niliyokueleza
ambayo niliishi kama daktari,kama
baba,mume,mlezi,mtu mwenye nafasi
katika kanisa
na jamii
na
zaidi
nilijulikana kama tajiri mwenye moyo
wa huruma.Hivi ndivyo wengi na hata
wewe mnavyonifahamu.Lakini maisha
yangu yana upande wa pili pia ambao
wengi wenu hamuufahamu na upande
huu ndio sababu ya kuandika barua hii
Nikisema
nikueleze
kwa
kina
kuhusiana na upande huu nitahitaji
maelezo marefu lakini kwa kifupi tu ni
kwamba mimi ni mfuasi wa kikundi au
imani ya Alberto’s.Sina hakika kama
unakifahamu au umewahi kukisikia
kikundi hiki lakini asili ya kundi hili ni
nchini Italia .Ni kundi linaloongozwa na
mtu
anayeitwa
Alberto
mkuu
.Aliyeanzisha kundi hili ni Alberto mkuu
wa kwanza ambaye aliwahi kuwa
kiongozi katika kanisa .Alivulia daraja
na kufukuzwa katika kanisa baada ya
kutaka kuleta uasi ndani ya kanisa
akidai mabadiliko ambayo hayaendani
na imani ya kanisa hilo.Baada ya
kufukuzwa ndipo alipoanzisha kikundi
chake cha Alberto’s na lengo kubwa la
kuanzisha kikundi hiki ni kuyaendeleza
yale ambayo yalisababisha akafukuzwa
na
kanisa
na
kwa
sasa
alitaka
mabadiliko haya yawe ni ya kidunia
.Alberto mkuu wa kwanza alianza kwa
kuwashawishi viongozi wa mataifa
makubwa
kuwa
wafuasi
wake.Alifanikiwa katika hilo na akaanza
kuyatumia mataifa hayo makubwa
yenye nguvu kuusambaza mtandao
wake sehemu mbali mbali za dunia na
hivyo kupelekea nchi nyingi kuyakubali
mabadiliko yake.Mabadiliko aliyokuwa
anayataka Alberto’s ni kila nchi duniani
kutambua haki za wapenzi wa insia
moja,haki
ya
wanawake
kutoa
mimba,haki za uvutaji wa mihadarati
n.k.Karibu
mambo
hayo
yote
yanapingana na imani ya dini zote na
ndiyo maana Alberto’s anawatumia
wakuu wa nchi ili kutumia nguvu na
madaraka yao kushinikiza kutungwa
kwa sheria katika nchi zao kuyatambua
mambo hayo.Kwa kurahisisha tu kuhusu
Alberto ni kwamba hawa ni waabudu
shetani.Wengi wa wafuasi wake ni
matajiri wakubwa,viongozi wa kisiasa
wenye
nguvu
na
ushawishi
mkubwa,wengine ni watu wenye nafasi
kubwa katika imani zao,lakini ukifika
usiku
huweka
pembeni
imani
na
kumuangukia Mungu wa giza.Mimi pia
ni
mmoja
wao.Nilipewa
nguvu
yaakuweza kutibu magonjwa mbali
mbali na ndiyo maana nimekuwa
daktari wa kusifika sana kwa sababu
wengi niliowatibu wamepona.
Pamoja na nguvu na uwezo huo wa
kuponya,nilikuwa na kazi nyingine
kubwa na ya muhimu sana kwa
Alberto’s.Ili upate picha kamili ngoja
nikupe
maelezo
kidogo.Alberto’s
wameifikia sehemu kubwa ya dunia kwa
sasa na serikali nyingi zinaongozwa na
vongozi
ambao
ni
wafuasi
wao.Wanawatumia wakuu wa nchi
ambao ni wafuasi wao kufanikisha
mambo yao.Moja ya mambo ambayo
mkuu wa nchi aliye chini ya Alberto’s
anapaswa
kufanya
ni
kuhakikisha
katika nchi yake wafanya biashara
wakubwa
wa
dawa
za
kulevya
hawaguswi wala kubughudhiwa na
kwamba ahakikishe wanatengenezewa
miundo
mbinu
mizuri
ya
kuweza
kuifanya kazi yao kwa uhuru.Madawa
ya kulevya ni chanzo kikubwa cha
mapato
kwa
Alberto’s
kwani
wafanyabiashara hawa hutoa kiasi
kikubwa cha pesa kwa jumuiya ambazo
huisaidia
jumuiya
iweze
kujiendesha.Kwa hapa Tanzania mimi
ndiye niliyepewa jukumu la kuhakikisha
ninawasimamia wafanya biashara wote
wa dawa za kulevyua walio chini ya
alberto’s na kuhakikisha biashara zao
zinakwenda
vizuri
na
wanalipa
michango
yao
kwa
jumuiya
kwa
wakati.Hiki ndicho chanzo cha utajiri
wangu mkubwa
 
SEHENU YA 9



Mimi ni mmoja kati ya wale
waliochangia vijana wengi kuharibu
maisha yao kwa kujiingiza katika
matumizi ya dwa za kulevya kwani
ndiye niliyeratibu shughuli zote za
uingizwaji wa dawa za kulevya nchini.
Huo ni upande wangu wa pili
ambao
wewe
na
wengine
wengi
hamuufahamu .Ni kutokana na upande
huu nilipata pesa nyingi zilizoniwezesha
mimi na familia yangu tuishi maisha ya
anasa kubwa lakini kwa siku hizi za
mwisho ninayajutia maisha niliyoishi
.Nimekuwa nikijiwa na picha zile mbaya
za
yale
mabaya
niliyoyafanya
na
nyakati
nyingine
ninaota
malaika
anapambana
na
jitu
la
kutisha
wananipigania mimi.Nilimuasi Mungu
na kuchagua kumuabudu shetani kwa
tamaa ya mali utajiri na umaarufu wa
dunia.Ninachokiona katika dakika hizi
cha
mwisho
ni
kigumu
hata
kusimulia.Nimeamua kuyafichua haya
kwako kwa sababu nataka nikuachie
kazi ambayo si nyepesi.Sina hakika
kama utaiweza lakini lazima ujaribu au
ufe ukijaribu.
Nataka uhakikishe kikundi cha
Alberto’s
kinafutika
nchini
Tanzania.Hiki ni kikundi hatari mno na
madhara
yake
kwa
nchi
ni
makubwa.Alberto’s
wako
hapa
,wameotesha mizizi yao na tayari wana
nguvu kubwa.Viogozi wengi wa juu wa
serikali ni wafuasi wao kwa hiyo yale
yote wanayoyataka Alberto’s tayari
yamefanyika au yanaendelea kufanyika.
Taifa hili linakwenda kubomolewa na
ndani ya miaka michache ijayo ile
misingi yote imara iliyosimamisha taifa
hili itabomolewa na zitaletwa tamaduni
mpya
kabisa
ambazo
hazikuwahi
kuonekana hapa nchini.Vizazi vijavyo
vitarithi taifa ambalo limebomolewa .
Nafahamu
mapambano
na
Alberto’s si kitu chepesi lakini fanya kila
uwezalo kuhakikisha unapambana na
kufanikiwa.Huwezi kupambana peke
yako tafuta mtu au watu ambao
utashirikiana nao na kwa pamoja
mtasaidia kuliondoa kundi hili hapa
nchini.Sikutaka
kukuingiza
katika
mapambano haya na watu hawa lakini
sina
mtu
mwingine
ninayeweza
kumuamini kuifanya kazi hii zaidi yako
Marcelo.Nafahamu unasumbuliwa na
kansa ya damu lakini hiki si kigezo cha
kukufanya ushindwe kupambana.
Kitabu hiki nilichokupa ndani yake
kuna kumbu kumbu zangu za namna
nilivyoweza kutibu magonjwa mbali
mbali ,namna nilivyoweza kuponya
watu mbali mbali ,dawa nilizotumia
n.k.Ni kitabu ambacho kitakuwa na
msaada mkubwa kwako katika kazi
yako ya utabibu.Kama nilivyokueleza
wakati nakukabidhi kitabu hiki kwamba
muda wowote ukipatwa na tatizo lolote
katika kazi zako za kitabibu,kifungue na
ukisome na utapata maelekezo kwani
nimeandika
mambo
mengi
.Silaha
kubwa ambayo nakuachia ambayo
unaweza kuitumia katika kuidhoofisha
na kuifutilia mbali Alberto’s hapa nchini
ni kitabu ambacho ndani yake kina
orodha nzima ya mtandao wa dawa za
kulevya hapa nchini.Utawafahamu ni
akina
nani
,wako
wapi,wanamiliki
biashara zipi hapa nchini,mtiririko wao
mzima wa fedha,akaunti zao katika
mabenki mbalimbali na hadi michango
yao
inavyowafikia
Alberto’s.Kama
nilivyokueleza kuwa hiki ni chanzo
kikubwa cha mapato kwa Alberto’s kwa
hiyo ukifanikiwa kuukata mrija huu wa
mapato kutakuwa na upungufu mkubwa
wa mapato kwani Tanzania ndiyo hasa
njia kuu ya kupitishia madawa hayo
kwa hiyo utakapoiziba njia hiyo mapato
yatapungua
kutoka
Afrika.Kitabu
chenye mambo haya yote nimekihifadhi
kwa katika kasiki lililo nyuma ya picha
ya Swala chumbani kwa Vera.
Namba ya simu niliyokupa upige ili
uwasiliane
na
mtu
atakayekupa
maelekezo ya namna ya kukitumia
kitabu hiki ,ukweli ni kwamba hakuna
maelekezo yoyote kuhusiana na kitabu
hiki
kwani
kila
kitu
kinajieleza
chenyewe bali lengo langu ni kutaka
ufahamiane na mtu huyo ambaye ni
mmoja kati ya wafanya biashara
wakubwa wa dawa kulevya .Ukifanikiwa
kumuangusha
huyo
basi
utakuwa
umefanikiwa
kuiteteresha
biashara
nzima ya dawa za kulevya hapa
nchini.Wafanya biashara wote wa dawa
za kulevya hapa nchini huyo ndiye baba
yao.Unatakiwa uwe makini sana naye
kwani ni mtu hatari sana.Atakufundisha
njia zote za kuhusiana na dawa za
kulevya
yanakotoka
hadi
yanafika
hapa.Usithubutu
kuhusisha
chombo
chochote cha usalama katika suala
hili.Mtandao
huu
ni
mpana
na
umesambaa katika sehemu kubwa na
hadi
katika
vyombo
vya
usalama.Narudia tena kukukumbusha
kwamba watu hawa wanalindwa na
serikali kwa hiyo umakini mkubwa sana
unahitajika viginevyo utapoteza maisha
kabla hujafanya lolote.
Kuna wale rafiki zangu watatu
ambao
niliwahi
kukupa
angalizo
usiwape nafasi wakakuzoea.Ni wat
 
SEHEMU YA 10


hatari .Ni wafanya biashara wa dawa za
kulevya na wanafanya kazi kwa huyu
mtu niliyekupa namba zake.Kaa mbali
nao ni wauaji hatari.Mwisho kabisa
nataka nikuweke wazi kwamba hata
mimi tayari nimewekeza mtaji katika
biashara hiyo kwa hiyo mtu niliyekupa
namba zake ndiye anayefahamu kila
kitu na atakupa maelekezo na hiyo
ndiyo njia rahisi ya kujenga mazoea
naye
kwani
ataamini
kwamba
unaendeleza mradi wa baba yako
kumbe una ajenda nyingine.
Marcelo narudia tena kukusisitiza
kwamba wewe ndiye pekee ambaye
ninaamini
unaweza
kuokoa
nchi
yetu.Wewe ni kijana mwenye akili na
jasiri na ninaamini utafanya kila
unaloweza kulifanya ili kufanikisha
jambo hili.Ukishindwa au kupuuzia
utakuwa umefanya kosa kubwa sana na
taifa letu zuri litabomolewa.
Mwishi kabisa naomba haya mengi
niliyokueleza kuhusu maisha yangu
yabaki kuwa siri yako na asifahamu mtu
mwingine yeyote na hasa uhusika
wagnu katika biashara ya dawa za
kulevya.
Natumai
umenielewa
na
utayatekeleza yale yote niliyokuagiza
.Jambo la mwisho kabisa naomba kila
siku kabla ya kulala usiache kuniombea
kwa
Mungu
ili
anifutie
makosa
yangu.Nimekosa sana na katika saa
zangu za mwisho ninauona ubaya wa
yale yote niliyoyatenda.Niombee bila
kuchoka.Wewe ni kijana mwenye hofu
ya
Mungu
usije
kutenda
yale
niliyoyatenda
mimi
katika
maisha
yangu
Mungu akulinde na akubariki
Dr Richard
Boaz akashusha pumzi .Uso wake
ulionekana kuloa jasho jembamba. Kwa
sekunde kadhaa alionekana kama
amechanganyikiwa
“ Is everything ok Mr Boaz? Akauliza
Julieth
“Your father was a devil !! akasema
Boaz kwa hasira
“Laiti kama ningemfahamu kabla Dr
Richard ni mtu wa aina gani naapa
ningemuua kwa mkono wangu
mwenyewe” akasema Boaz huku akihema
kwa kasi.
“What’s wrong Boaz? Nini
kimetokea? Akauliza Julieth
“Unamfahamu Vera? Boaz akauliza
“Vera?!!..Julieth
akaonekana
kushangaa
“Ndiyo.Unafahamumahala anakoishi?
Huku akionekana kuzidi kushangaa
Julieth
akacheka
kidogo..Boazi
akamtazama kwa macho makali na
kusema
“Julieth this is a very very serious
matter.Tell me where Vera is please!!!
Akasema Boaz
“ Boaz I’m not jocking.I real don’t
know where Vera is.Whos is Vera ?
Boaz akaendelea kumkazia macho
Julieth halafu akampa barua ile aisome.
“Oh my gosh !! akasema Julieth baada
ya kumaliza kuisoma barua ile
“Sasa umefahamu namna baba yako
alivyo shetani.Naapa kama ningemfahamu
yuko hivi kabla hajafariki ningemuua kwa
mikono yangu.How could he do this to me?
Nimestuka sana.Sikutegemea kabisa kama
Dr Richard anaweza akanifanyia hivi”
akasema Boaz
“Hata mimi nimestuka sana .Hili ni
jambo la kushangaza mno” akasema
Julieth.Boaz akakishika kitabu kile na
kumtupia Julieth
“Kitabu hiki sicho kile nilichokuwa
nakitafuta .Hiki kimejaa upuuzi mtupu na
hakina msaada wowote kwangu .Kitabu
ninachokihitaji ni hicho ambacho
amemuelekeza Marcelo kwamba
amekihifadhi kwa Vera na ndiyo maana
nahitaji sana kumfahamu huyo Vera ni
nani? Ninaamini huyo Vera anafahamu
alipo Marcelo na kama tukifanikiwa
kumpata
atatuelekeza
mahala
alipojificha.Kwa sasa tumerudi katika
sifuri.” Akasema Boaz na kuinamisha
kichwa
“I’m so sorry Boaz.Hata mimi
sikujua” akasema Julieth
“Si kosa lako Julie.Hata hivyo
tunatakiwa kuanza upya tena na
tunatakiwa kufanya kila ,liwezekanalo
kuhakikisha kwamba kwa gharama zozote
zile tunampata Marcelo na hicho
kitabu.Bila kumpata Marcelo au hicho
kitabu tumekwisha kwani kitabu hicho
kina maelezo yote kuhusiana na sisi kama
ulivyosoma katika barua .Naamini tayari
Marcelo atakuwa amekwisha anza
kutekeleza maagizo ya baba yake na tayari
anao watu anaoshirikiana nao ambao ni
watu wenye uwezo mkubwa .Namna
alivyoweza kutolewa hospitali ni
kithibitisho tosha kwamba watu anao
shirikiana nao si watu wa mchezo.”
Akasema Boaz huku sura yake ikionyesha
wasi wasi mkubwa.
“Rais Ernest amewasaliti wenzake na
kwa sasa anaendelea kuwaondoa Alberto’s
katika nyadhifa zao ndani ya serikali na hii
 
SEHEMU YA 11


ni hatari kubwa kwetu kwani tulikuwa
tunafanya biashara zetu kwa uhuru kwa
kivuli cha Alberto’s kwa hiyo endapo
hakuna Alberto’s biashara yetu itakuwa
ngumu sana kufanyika.Kama hiyo
haitoshi,Marcelo naye ametoweka na
kitabu chenye kumbu kumbu zetu wote.Hii
ni hatari kubwa sana kwetu .Sina hakika
lakini najaribu kujenga hisia kwamba
inawezekana labda Marcelo akawa katika
mtandao wa rais Ernest na wanafanya kazi
pamoja.Kama ni hivyo basi vita hii itakuwa
na ushindi mkubwa kwao kwani
hawahitaji kutumia nguvu kubwa kila kitu
kinajieleza chenyewe katika hicho
kitabu.Hizo ni hisia zangu tu lakini kubwa
kuliko yote ni kumtafuta Marcelo
apatikane akiwa hai au amekufa.” Akasema
Boaz .Julieth akafikiri kidogo na kusema
“Boaz nadhani ipo njia ambayo
inaweza kutusaidia kujua au kupata
mwanga wa kujua aliko Marcelo”
“Ni njia gani hiyo ulieth?
“Marcelo anao watu wake wa karibu
lakini miongoni mwao kuna watu wawili
ambao ni wa muhimu sana kwake.Kwanza
kuna rafiki yake anaitwa Daniel Swai.Huyu
ni rafiki yake wa muda mrefu sana na
wamekuwa marafiki wa muda mrefu na
ndiye msiri wake mkubwa.Urafiki wao ni
mkubwa kiasi Daniel amekuwa ni kama
ndugu yetu.Mambo mengi ya Marcelo
Daniel anayafahamu na hata akiwa
hospitali walikuwa karibu sana na kuna
mambo walikuwa wakaiongea kwa siri na
hawakutaka mimi niyafahamu.Mtu wa pili
anaitwa Monica Benedict.Kwa siku za hivi
karibuni Marcelo na Monica wamekuwa na
ukaribu mkubwa sana na hata alipolazwa
hospitali Monica hakuwahi kukosa kuja
kumtazama.Monica na Marcelo nahisi
watakuwa na mahusiano ya kimapenzi
japo niliwahi kumuuliza Monica na
akakana lakini ninamini watakuwa katika
mahusiano.Moja ya vitu nilivyovichukua
katika kasiki la Marcelo ni faili la matibabu
yake ya kansa ya damu na nililipeleka kwa
Monica.Lengo la kufanya hivi lilikuwa ni
kumfanya Monica aufahamu ugonjwa wa
Marcelo na lakini wameendelea kuwa na
ukaribu mkubwa.Huyu naye alikuwa
akiwasiliana kwa siri na Marcelo kwa njia
ya maandishi na hata nilipotaka kujua
walichokuwa wakiwasiliana hakuwa
tayari.Kwa
namna
walivyokuwa
wakiwasiliana ninaamini kabisa kwamba
kuna
jambo
walilokuwa
wanalificha.Naamini kabisa mmoja kati ya
watu hawa kama si wote atakuwa
anafahamu alipo Marcelo.Nashauri tuanze
na hawa wawili na tukiwapata tunaweza
kupata mwanga Fulani.”
Boaz akafikiri kidogo na kusema
“That’s a good idea.Kuna mtu mmoja
ambaye ninakwenda kuonana naye jioni ya
leo nitampa hiyo kazi ya kuwapata hawa
watu wawili .Ni mtu mahiri sana katika
shughuli hizo ,atawatafuta kokote
waliko,atawapata na atawafanya waseme
mahala aliko Marcelo kama wanajua”
akasema Boaz huku akiuma meno kwa
hasira.
***********************
Austin aliwasili katika kiwanda cha
viatu cha Ndura kama alivyoelekezwa na
Amani.Alishuka garini akaenda katika geti
waliko walinzi akasalimiana nao na
kumuulizia mtu anayeitwa Amani mjeledi
.Huyu alifahamika sana hapo kiwandani
kwani alimpata kwa haraka
“Habari yako bwana Amani” Austin
akamsalimu
“Nzuri kabisa.Natumai wewe ndiye
bwana Austin”
“Ndiye mimi” akajibu Austin
“Karibu sana .Nadhani tusipoteze
muda twende nikupeleke mara moja
ukaonane na rafiki yako.” Akasema Amani
wakaingia garini na safari ikaanza.
“Habari ya wapi Austin? Akauliza
Amani aliyeonekana muongeaji sana
“Ninaishi Afrika ya kusini
.Nimepotezana na Job kwa miaka zaidi ya
kumi.Nimekuja mara moja kusalimia
ndugu na jamaa nikaona si vibaya
nikimtafuta huyu rafiki yangu nimjulie hali
a.Nimekwenda mahala alikokuwa anaishi
nikapata taarifa za matatizo
yaliyompata.Nimesikitika sana”
“Ni kweli Job alipatwa na matatizo ya
akili.Chanzo ni mke wake ambaye
tumeambiwa na mtaalamu kuwa alimtupia
jini awe kichaa ili yeye aweze kuolewa na
mwanaume mwingine” akasema Amani
“Vipi hali yake kwa sasa? Akauliza
Austin
“Hali yake siwezi kusema ni nzuri
kwani bado hajapona japokuwa kuna
nyakati huwa anatulia na baada ya muda
mfupi uchizi unamjia lakini bado
hatujakata
tamaa,tunaendelea
kumshughulikia.Hivi sasa kuna mtaalamu
mmoja anakuja kutoka mkoani Rukwa
anakuja kumshughulikia” akasema Amani
Hatimaye waliwasili eneo la Tegeta
mji mpya anakoishi Amani.Austin
akakaribishwa ndani.Kulikuwa kimya
kabisa
“Austin karibu ndani jisikie
nyumbani.Mama ametoka amekwenda
mihangaikoni kidogo.Job huwa anabak
 
SEHEMU YA 12


peke yake hapa nyumbani na mara nyingi
huwa anashinda shambani.Nisubiri hapa
nikamlete” akasema Amani
“Unaweza kwenda sote huko
shambani kumuona?
“Hakuna tatizo” akasema amani
wakaongozana kuelekea shambani
kumtafuta Job
Walielekea katika shamba lililokuwa
na minazi mingi .Baada ya kuzunguka
zunguka hatimaye wakamkuta Job akiwa
amekaa chini ya mti wa mkorosho akiwa
na kitabu.Alipowaona akina Austin
akakifunika kitabu alichokuwa nacho na
alionyesha mstuko mkubwa alipomuona
Austin
“Job nimekuletea rafiki yako wa siku
nyingi anaitwa Austin.Unamkumbuka?
akauliza Amani.Job hakujibu kitu
akawatazama halafu akaangua kicheko
kikubwa.
“Job !! akasema Amani kwa ukali
“It’s ok Amani.Wewe nenda niache
nibaki naye hapa nitafute namna ya
kuweza kumfanya anikumbuke.Pengine
anaweza akanikumbuka” akasema Austin
“Sawa nitakuwa kule nyumbani
nashughulikia mifugo.Naona kichaa chake
leo kimepanda ila huwa hana
vurugu.Ukimfokea tu anatulia.Ukishindwa
kuzungumza naye labda ujaribu tena
kesho pengine atakuwa vizuri.” Akasema
Amani na kuondoka akamuacha Austin na
Job .Austin akamsogelea Job akaacha
kucheka na kumtazama kwa mshangao
“Job!!..Job..NimimiAustin.Unanikumb
uka?
Job hakujibu kitu akapanda juu ya
mti wa korosho akakaa huko juu kwa
dakika kama tano halafu akashuka
akamsogelea Austin na kumpa mkono na
kucheka kidogo
“ Austn January !!!
Austin akastuka sana na uso wake
ukajenga tabasamu kubwa
“Job umenikumbuka?
“Ndiyo.Siwezikukusahau
Austin.Karibu sana.Siamini ni wewe kweli
au ni mzimu wako? Akasema Job huku
akimshika mkono Austin na kuubonyeza.
“Kweli ni wewe.Umejuaje kama niko
hapa? Akauliza Job
“oh my God !!!..akasema Austin na
kumkumbatia Job
“What happened to you Job? Akauliza
Austin hukuakifuta machozi yaliyokuwa
yanamtoka
“Usilie Austin wala usiongee kwa
sauti kubwa.I’m not crazy.Sina tatizo lolote
la uchizi.Mimi ni mzima kabisa “ akasema
Job na kumfanya Austin amshangae
“Tafadhali usishangae Austin.Mimi si
kichaa
kama
wote
wanavyodhani.Imenilazimu kuishi katika
hali hii kutokana na masahibu
yaliyonipata”
“Oh Mungu wangu !! Nini kilikupata
Job? Akauliza Austin
“Ni hadithi ndefu Austin ambayo
hatuwezi kuongea hapa.Usiku wa leo
naomba tukutane pale Rozana night
club.Tutaongea zaidi”
“Rozana? Akauliza Austin
“Ndiyo”
“How will you get there?
Hatawagundua hawa ndugu zako kuwa
umeondoka? Utatumia usafiri gani? Do you
have a phone? Austin akauliza maswali
mfululizo na Job akacheka kidogo
“Austin nadhani tayari umenisahau
mimi ni nani” akasema na kucheka tena
“Tukutane kuanzia saa nne usiku wa
leo pale Rozana.Ukifika kaa kaunta ya juu
nitakukuta hapo.”
Austin akataka kusema jambo lakini
Job akamzuia baada ya kusikika sauti ya
mtu akipiga mluzi akielekea pande zile.
“Kuna mtu anakuja pande hizi
,atakuwa ni Amani.Tukutane mida hiyo
,fika bila kukosa” akasema Job na kwenda
kuketi chini ya mkorosho akiwa na kitabu
chake .Ni kweli aliyekuwa akipiga mluzi
alikuwa ni Amani kaka yake Job
“Vipi kuna maendeleo yoyote?
Ameweza kukukumbuka ? akauliza Amani
“ Hapana hajaweza kunitambua.Toka
ulipoondoka hajainuka pale chini ya
mti.Nadhani kama ulivyosema kuwa leo
hajaamka vizuri.”
“Dah! leo una bahati mbaya
sana.Umekuta kimeamka.Kuna baadhi ya
siku huwa anakuwa vizuri kabisa anaoga
na kujiweka safi lakini siku nyingine
unamkuta kama hivi” akasema Amani
“Poleni sana kwa tatizo
hili.Namuombea sana rafiki yangu huyu
aweze kupona na kurejea katika maisha
yake ya kawaida kama awali.Kwa kuwa
bado naendelea na mapumziko nitakuja
tena siku nyingine kumjulia hali” akasema
Austin na kugeuka akaanza kupiga hatua
kuondoka
“Job rafiki yako Austin anaondoka”
akasema Amani lakini Job hakujbu
kitu.Amani na Austin wakaondoka na
kumuacha Job peke yake.Baada ya kufika
katika gari lake Austin akafungua droo ya
gari na kutoa bunda la noti akahesabu
shilingi laki tatu akampatia Amani
“Kiasi hiki kidogo kitakusaidia katika
kuuguza.Nitakuja tena siku nyingine ili
 
SEHEMU YA 13



kushauriana namna ya kufanya “ akasema
Austin na kuagana na Amani akaondoka
“Nahisi kama vile natazama
filamu.Job!! nini kimempata na
kumsababisha aishi katika hali ile?
Akawaza Austin akiwa garini
“Lazima kuna jambo kubwa
lililomtokea hadi akaamua kuishi maisha
yale ya kujifanya kichaa.Huu ndio ubaya
wa hizi kazi zetu.Ukiingia katika kazi hizi
fahamu hadi kufa kwako you’ll never have
a normal life.Hiki ndicho kilichonitokea
mimi na ndicho kinachomtokea
Job.Nitafahamu kila kitu nitakapoonana
naye usiku wa leo.Kama anahitaji msaada
lazima nimsaidie.Yule ni mtu muhimu sana
kwangu.Namuhitaji sana” akawaza Austin
*******************
Boaz na Julieth waliwasili katika
jengo la ghorofa tano linalomilikiwa na
bilionea Peter Chui.Hili ni duka kubwa la
magari ya kifahari.Peter Chui akawapokea
wageni wake na kuwaongoza hadi ghorofa
ya juu kabisa kulikokuwa na ofisi yake
kubwa.Ndani ya ofisi yake ile kubwa na
nzuri walikuwemo watu wengine wawili
,wote wakasimama kumlaki Boaz.
“Karibu tena nyumbani Boaz”
akasema mmoja wa wale watu
waliokuwamo katika ile ofisi
“ Nashukuru sana mzee Chimo.Tayari
nimerejea kwa hiyo msiwe na hofu tena”
“Hiki kilichotokea ni kitu cha
kustusha sana.Sielewi huyu rais amepatwa
na nini hadi akafanya haya
aliyoyafanya.Hatujui nini hasa lengo lake
na hivyo anatuweka katika mashaka
makubwa.Kama ameweza kuwasaliti
wenzake hawezi kushindwa kuanzisha vita
na sisi.Nimefurahi umekuja kwa wakati
muafaka ili uweke sawa jambo hili.Peter
aliponitaarifu kwamba umerudi nilifurahi
sana ikanilazimu nije haraka haraka
kukuona ili nijue mipango yako namna ya
kulikabili jambo hili kwani baada ya Dr
Richard kufariki wewe ndiye uliyebaki
mtu tunayekutegemea katika kuweka
mambo yote sawa” akasema mzee Chimo
“Tuanzie na hapo kwa Dr Richard”
akasema Boaz
“Kama mnavyofahamu Yule ndiye
aliyekuwa kama mlezi wetu na aliwekwa
na mkuu Alberto kutusimamia na
kuhakikisha mambo yetu yote
yanakwenda sawa.Katika siku za mwisho
wa uhai wake Dr Richard alinieleza
kwamba anataka mwanae arithi nafasi
yake pindi atakapofariki.Ombi lake hili
liliwasilishwa kwa Alberto mkuu wa tatu
na akakubali kwamba ikitokea Dr Richard
atafariki dunia basi mwanae afundishwe
kazi kwanza na itakapothibitika kwamba
amefahamu kazi vyema basi anaweza
akakabidhiwa nafasi ya baba yake.Kwa
mujibu wa makubaliano yangu na Dr
Richard,ni kwamba mara tu atakapokuwa
amefariki basi atamuachia maagizo
mwanae Marcelo anitafute ili niweze
kumpa maelekezo na kumfundisha
kazi.Baada ya Dr Richard kufariki muda
ulizidi kusonga bila ya Marcelo kutokea na
nilipoulizwa nikamtetea kwamba bado
yuko masomoni na atakapomaliza
atajiunga nasi hivyo nikaendelea kuyabeba
majukumu yote ya Dr Richard.Hata
alipohitimu masomo yake na kurejea
Tanzania bado Marcelo hakufanya juhudi
zozote za kunitafuta.Nilianza kuingiwa na
shaka kama Marcelo ana nia ya dhati ya
kujiunga nasi hivyo ikanilazmu kuchukua
hatua.Kitu cha kwanza tulichokihitaji toka
kwake ni kitabu alichopewa na baba yake
ambacho kina orodha ya wafanya biashara
wote wa dawa za kulevya ambao Dr
Richard alikuwa anawasimamia. Kitabu
hicho kinaonyesha mahala walipo,biashara
na mali wanazomiliki,akaunti zao za benki
na mtiririko wao mzima wa fedha na
mwisho ni namna wanavyochangia katika
jumuia.Ilinilazmu kumtumia dada yake
Marcelo anaitwa Julieth ambaye ndiye
huyu niko naye hapa kuingia chumbani
kwa Marcelo akafungua kasiki na
kuchukua kitabu nilichomuagiza.Kwa
bahati mbaya baada ya kukiona kitabu
hicho muda mfupi uliopita nimegundua
kwamba kitabu hicho si chenyewe.Si kile
tunachokitafuta chenye taarifa zetu.Ndani
ya kitabu hicho nimekuta barua ambayo
Dr Richard alimuandikia Marcelo.Ni barua
ndefu kidogo“ akaitoa barua ile akampa
mzee Chimo aisome.Ukimya ukatawala
mle ofisini wakati mzee Chimo akiendelea
kuisoma ile barua.Kadiri alivyoendelea
kuisoma ndivyo sura yake ilivyobadilika
na uso ukajikunja kwa hasira na mshangao
“Bastard !!! akagonga meza kwa
hasira baada ya kumaliza kuisoma barua
ile
“I hope he’s now burnng in hell!!
Sikutegemea kabisa kama Rich....” Mzee
Chimo akatulia kidogo baada ya simu ya
Peter Chui kuita,akasogea pembeni
akaipokea.Baada ya maongezi mafupi na
mtu aliyempigia ,Peter akamfuata Boaz
“Waziri mkuu Jeremiah anataka
kuongea nawe”
Boaz akaichukua simu na kusogea
pembeni.
“Hallow mheshimiwa waziri”
akasema Boaz
 
SEHEMU YA 14



“Hallo Boaz.Nimefurahi kusikia uko
Tanzania.Nimekutafuta sana leo.Nimepiga
afrika ya kusini nikaambiwa uko Comoro
nikapiga tena namba niliyopewa ukiwa
Comoro nikataarifiwa kwamba haupo tena
Comoro.Nikaona nimpigie Peter Chui
akaniambia kwamba tayari umerejea
Tanzania.Karibu sana nyumbani japokuwa
mambo si shwari huku.Upepo mbaya
unavuma kwa kasi ya ajabu hivi sasa lakini
naamini kabisa kwamba ujio wako
unaweza ukaimaliza dhoruba hii”
“Ahsante sana mheshimiwa waziri
.Kwanza kabisa pole sana kwa masahibu
yaliyokupata.Nimelazmika kusimamisha
kidogo shughuli zangu nyingine na kuja
haraka Tanzania kutokana na hiki
kilichotokea”
“Imekuwa vizuri sana umekuja
Boaz.Ninahitaji mno kuonana nawe jioni
ya leo kuna mambo ya msingi nahitaji
kuzungumza nawe.Saa ngapi utapata
nafasi ?
“Leo jioni kuna mtu nitaonana naye
na nitakapotoka huko nitakuja kuonana
nawe.Tukutane wapi?
“Karibu katika makazi yangu”
“Sawa waziri mkuu,nitakuja baada ya
kumaliza kikao changu na huyo mtu
ninayekwenda kuonana naye usiku”
akasema Boaz na kukata simu akaenda
kuendelea na maongezi na wenzake
“Nadhani tayari nyote mmekwisha
isoma barua hiyo ambayo Dr Richard
alimuandikia Marcelo na tayari mnalo jibu
ni kwa nini Marcelo hakuweza kujiunga
nasi kama tulivyokubaliana na baba
yake.Nina uhakika kama alivyopewa
maelekezo na baba yake tayari amekwisha
pata watu wa kushirikiana nao na lengo
lao kubwa ni kuhakikisha wanatumaliza
kabisa .Ni hao watu anaoshirikiana nao
ndio waliomtorosha hospitali .Kwa taarifa
nilizopewa namna tukio la kumtorosha
Marcelo hospitali lilivyofanywa,lilikuwa ni
tukio la kitaalamu sana na hiyo ni picha ya
wazi kwamba watu wanaotutafuta bila ya
sisi kufahamu ni watu hatari sana.They are
very professional na wamejipanga
vizuri.Hata hivyo tayari nimeanza
kuchukua hatua na usiku wa leo kuna mtu
ambaye ninakwenda kuonana naye ,kuna
kazi nitampa aifanye na baada ya hapo
nitawataarifu hatua itakayofuata
.Nawahakikishia lazima Marcelo apatikane
pamoja
na
kitabu
tunachokitafuta.Nawaomba msiwe na wasi
wasi kabisa mimi ndiye mtuliza rabsha na
dhoruba” akasema Boaz kwa kujigamba
kisha wakaendelea na maongezi mengine
kuhusu biashara zao
********************
Saa kumi na mbili na dakika
kumi,Austin aliwasili katika makazi yake
akasalimiana na Marcelo na kuelekea
chumbani kwake.Kichwa chake kilijaa
mawazo mengi na kubwa zaidi ,likiwa ni
suala la Job.Alikaa kitandani akaendelea
kutafakari na mara mlango wake
ukagongwa akaichukua bastora yake
iliyokuwa chini ya mto akaenda kuufungua
akakutana na Marcelo ambaye alistuka
kumuona Austin akiwa na bastora
mkononi.
“Karibu ndani Marcelo” akasema
Austin .Kwa wasi wasi Marcelo akaingia
ndani
“Nimestuka baada ya kukuona na
bastora.Toka niliponusurika kuuawa kwa
risasi nimekuwa ninastuka mno kila
nionapo bastora au bunduki.Is everything
ok Austin? Akauliza Dr Marcelo
“Don’t worry.Everything is ok.This is
how I am.I don’t trust people”
Ukimya mfupi ukupita Marcelo
akauliza
“Anyword from David Zumo?
“Mpaka sasa bado sijapata taarifa
yoyote toka kwa rais.Nitawasiliana naye
jioni ya leo kama kuna lolote atanieleza
nitakwambia” akasema Austin.Dr Marcelo
akainama na kushika kichwa baada ya
muda akainua kichwa na kusema
“Austin kichwa changu kinataka
kupasuka kwa mawazo .Kuna mambo
mengi yananitatiza na sijui wapi nitaanzia
kupata majibu.Naomba sana msaada wako
uweze
kunikwamua
hapa
nilipokwama.Bila wewe kunisaidia maisha
yangu
yatakuwa
kama
ya
ndege.Nitaendelea kujificha humu hadi
lini? Lazima nitafute njia ya kujikwamua
hapa nilipokwamba na wewe pekee ndiye
unayeweza kunisaidia nikatoka katika giza
hili.Please help me Austin”
Austin aliyekuwa anamtazama
Marcelo kwa makini akavuta pumzi na
kusema
“Unataka nikusaidiaje Marcelo?
“Kuna mambo mengi yamenizunguka
ambayo
nahitaji
kuyapatia
ufumbuzi.Ninahisi
kuna
jambo
linaloendelea na mimi ni kama mlengwa
mkuu bila kujifahamu.Nataka kujua n.....”
Saa ya mkononi ya Austin ikatoa mlio
na kumfanya Marcelo anyamaze
kwanza.Austin akabonyeza kitufe katika
simu yake na ikatokea picha ya mtu
aliyekuwa getini
 
SEHEMU YA 15


vans.!! Akasema Austin kwa sauti
ndogo
“Who is Evans? Akauliza Marcelo
“Ni mlinzi wa rais.Marcelo nenda
chumbani kwako tutaongea baadae
yawezekana rais amekuja”
“Kama ni rais tafadhali nahitaji
kuzungumza naye”
“Sawa nitamweleza” akasema Austin
na kufutika bastora kiunoni akatoka na
kuelekea getini.Akachungulia katika tundu
dogo la getini na kuliona gari
moja.Taratibu na kwa tahadhari kubwa
akalifungua geti na gari lililokuwa nje
likaingia ndani.Akafunga geti na
kulisogelea gari lile kwa tahadhari.Mlango
wa dereva ukafunguliwa akashuka Evans
mlinzi wa rais
“Hello Austin” Evans akamsalimu
Austin
“Hi Evans.Karibu san.....” Austin
akastushwa na mlango mwingine wa gari
uliofunguliwa na akashuka mtu aliyemstua
“Mr Boaz..?!!!!.. akasema Austin kwa
mshangao
“Hallo son !! akasema Boaz
“Surprised to see me here? Akauliza
Boaz huku akitabasamu
“Umejuaje kama niko hapa mzee?
Akauliza Austin
“Iam Boaz remember,hakuna
ninachokihitaji katika hii dunia
nikakikosa.Nilihitaji kufahamu mahala
ulipo na maendeleo yako and here I am
.I’m happy to see you” akasema Boaz
“Austin
nimeelekezwa
na
mheshimiwa rais niwalete wageni hawa
hapa kwako” akasema Evans
“Wageni? Kuna mgeni mwingine
tena? Akauliza Austin akiendelea
kumkazia macho Boaz
“Yes ! A very big surprise !! akasema
Boaz na kuufungua mlango wa gari
akashuka Maria
“M..ma..ma...Mar...Maria...!!! Austin
akastuka sana.Alihisi kama miguu
inamuisha nguvu
“Hallo my love” akasema Maria
hukuakitabsamau na kwend akumkubatia
nma kumwagia mabusu.
“ Oh my God ! I cant believe this “
akawaza Austin
“How are you my king? Nimefurahi
mno kukuona tena Austin” akasema Maria
lakini Austin hakuongea chochote
aliendelea kumtazama kwa macho
makali.Maria akautambua mstuko
alioupata Austine na kuuliza
“Are you ok my love? Aren’t you
happy to see me? Akauliza Maria .Austin
akastuka kama mtu aliyetoka usingizini
akajilazimisha kutabasamu na kusema
“This is a big surprise na ndiyo
maana nimekosa neno la kusema.Karibuni
sana ndani” akasema Austin na kumshika
mkono
Maria
akawakaribisha
sebuleni,Evans akabaki nje.
“Umekuja lini Tanzania? Austin
akamuuliza Maria
“Nimekuja jana ila utanisamehe
nimekuja bila taarifa.I only wanted to
surprise you.Siwezi kueleza furaha
niliyonayo kukuona tena mfalme wangu”
akasema Maria
“Karibu sana Tanzania.Karibu Dar es
salaam” akasema Austin
“What a beautiful house” akasema
Maria baada ya kuingia sebuleni.Austin
akatabasamu na kuwakirimu wageni wake
vinywaji
“Austin kwanza kabisa nataka
nikuombe radhi kwa kukuvamia bila
taarifa.Nimekuja Dar es salaam kwa
shughuli zangu lakini nikaona si vyema
endapo nitaondoka bila ya kuonana na
mwanangu hivyo nikawasiliana na rais
akanipa mtu wa kunileta hapa.Nilipofika
Dar es salaam nikamkuta Maria tayari
amefika naye alikuwa na lengo moja tu la
kuja kuonana nawe hivyo nikaona si
vibaya endapo nitaongozana naye kuja
kukuona .Vipi maisha ya Dar es salaam?
Akauliza Boaz
“Nashukuru
ninaendelea
vizuri.Maisha hapa ni mazuri kama
mnavyoona.Hata mimi nimefurahi mno
kuwaoneni watu wangu wa muhimu.Kwa
mara nyingine karibuni sana” akasema
Austin
 
SEHEMU YA 16


“Ahsnate Austn.” Wakasema Boaz na
Maria
“Austin naomba unielekeze ulipo
msalani tafadhali” akasema Boaz na Austin
akamuelekeza.Mara tu Boaz alipotoka pale
sebuleni,Austin akamfuata Maria
“I told you not to come to
Tanzania,what are you doing here ???
..akauliza Austin kwa sauti ndogo
“Austin I real don’t understand
you.What’s going on? Kwa nini hutaki nije
Tanzania? Kuna nini hutaki nikijue?
“Sikiliza Maria,kesho natakiwa
uondoke urejee afrika ya kusini.Hutakiwi
kuwepo hapa.This place is dangerous”
“Austin umekuwa ukirudia hilo neno
la kuhusu usalama mara kwa mara.What’s
going on? I’m not going back to South
Africa until you tell me whats going on ?
Are you back on your old job? Akauliza
Maria lakini kabla Austin hajajibu Boaz
akarejea.Austin na Maria wakatabasamu
na kubadili maongezi
“You missed each other huh !!.. Boaz
akasema huku akitabasamu
“Yes father.I missed Austin so
much.Siku moja bila kumtia machoni ni
sawa na mwaka mzima.Nimekaa Dubai
kwa zaidi ya wiki tatu nadhani unaweza
kupata picha how I missed him” akasema
Maria na wote wakacheka
“By the way Austin,safari ya maria
Dubai imekuwa ya mafanikio
makubwa.Amesaini mikataba mitano na
makampuni makubwa.Mikataba hiyo
itatuwezesha kuvuna pesa nyingi
sana.Mnastahili pongezi kubwa kwa
namna mnavyoendesha biashara zetu kwa
mafanikio.” Akasema Boaz na wote
wakapongezana .Boaz akaitazama saa yake
ya mkononi na kusema
“Austin,naweza kupata kama dakika
kumi na tano za mazungumzo nawe? Sitaki
kuchukua muda mwingi hapa.Kuna mtu
ambaye natakiwa kuonana naye usiku huu
wa leo.Nadhani wewe na Maria mtapata
nafasi nzuri ya kuzungumza kesho”
akasema Boaz
“Sure.Let’s go to study room”
akasema Austin
“Maria naomba ubaki hapa kuna
mambo nataka kuzungumza na Austin.It’s
men’s talk.” Boaz akamwambia Maria.
“Feel at home Maria” Austin
akamwambia na kumuongoza Boaz hadi
katika chumba cha kusomea
“Now,let’s have a short and serious
talk” akasema Boaz
“Nakusikiliza mzee” akasema Austin
“Austin you are my son.Ninakupenda
na kukuamini zaidi ya ninavyoweza
kukueleza.Toka wakati ule nilipokutoa
mikononi mwa Alshabaab umekuwa ni
mwanangu.Umefanya mambo mengi ya
mafanikio kwa familia yetu,ahsante sana
kwa hilo” akasema Boaz na kunyamaza
kidogo halafu akaendelea
“Baada ya utangulizi huo,Austin
nimekuja kwako kuna mahali
nimekwamba ahitaji msaada wako”
aaksema Boaz
“Sijapata kukuomba msaada katika
jambo lingine lolote zaidi ya biashara
lakini kwa sasa nimelazimika kukuomba
msaada wako kwani suala hili si langu
binafsi bali ni la familia nzima kwa
ujumla.” Akanyamaza kidogo na kuendelea
“Kuna mtu mmoja aliitwa Dr Richard
ambaye aliwahi kuwa mshirika wangu
mkubwa katika biashara lakini kwa bahati
mbaya alifariki kwa maradhi ya saratani ya
damu.Enzi za uhai wake biashara zetu
yeye ndiye aliyekuwa akizisimamia na
alipofariki mtoto wake ndiye aliyeshika
umiliki wa mali zote zikiwamo zile ambazo
mimi na baba yake tulikuwa na ubia.Mtoto
huyo anaitwa Dr Marcelo”
“Dr.Marcelo? Austin akamkatisha
Boaz
“Ndiyo.Mbonaumestuka.Do
you
know him? Boaz akauliza
“Hapana simfahamu.Endelea”
“Huyo Marcelo anataka kuniondoa
katika ubia ili biashara zote zibaki mali
yake. Kuna kitabu ambacho baba yake
aliweka kumbu kumbu zote kuhusiana na
biashara zetu na Marcelo amekificha
kitabu hicho ili kupoteza ushahidi.Kwa
bahati mbaya ubia wetu hatukuufanya
kisheria na ilikuwa ni kati yetu sisi wawili
kwa kuwa tulikuwa tukiaminiana sana
.Marcelo anaamini kwamba kukificha
kitabu hicho ni kupoteza ushahidi
wote.Nilijaribu kumtumia ujumbe mara
kwa mara ili tuonane tulimalize suala hili
kwa njia ya mazungumzo akapuuzia
ikanilazimu nitumie nguvu kidogo ili
niweze kukipata kitabu hicho chenye
kumbu kumbu zote.Niliwatuma vijana
wangu kukitafuta kitabu hicho lakini
Marcelo akawa jeuri na kuwafyatulia risasi
vijana wangu na wao wakajibu shambulizi
na katika kurushiana risasi Marcelo
akajeruhiwa na kukimbizwa hospitali
ambako baada ya siku mbili akatoroka na
hadi sasa hajulikani alipo.Austin ubia huo
nilioingia na Dr Richard ni mkubwa na
niliwekeza fedha nyingi mno ambazo
siwezi kukubali zipotee kwa hiyo
ninahitaji msaada wako.Nataka unisaidie
kumtafuta huyo Marcelo na kukipata
kitabu hicho chenye kumbu kumbu zote za
biashara kati yangu na baba yake ii niweze
kurejesha fedha zangu.Inawezekana ikawa
ngumu kidogo kumpata Marcelo kwa sasa
 
SEHEMU YA 17



kwani tayari amejificha baada ya
kufahamu kwamba ninamsaka hata hivyo
kuna watu wawili ambao ni watu wake wa
karibu sana na ambao wanaweza
wakatuongoza mahala aliko Marcelo.Wa
kwanza ni mwanamke mmoja anaitwa
Monica Benedict ambaye hivi majuzi
alitangazwa kuwa ni mrembo kuliko wote
Afrika.Huyu ni mtu wa karibu sana na
Marcelo na kuna tetesi kwamba wana
mahusiano ya kimapenzi.Wa pili anaitwa
Daniel Swai.Huyu ni rafiki wa muda mrefu
wa Marcelo na ni mtu wake wa karibu
.Huyu ni mtoto wa mfanya biashara mmoja
tajiri.Watu hawa wawili endapo unaweza
kuwapata
watakuongoza
aliko
Marcelo.Nina uhakika mkubwa lazima
wanafahamu chochote kuhusu mahala
aliko Marcelo.Find them and make them
talk!!! Akasema Boaz
Austin alihisi kama nyundo kubwa
imekipiga kichwa chake baada ya kumsikia
Monica akitajwa na Boaz kama mtu
anayepaswa kutafutwa aeleze aliko
Marcelo.Alistuka vile vile kusikia kwamba
Marcelo na Monica wana mahusiano.
“Austin !! akaita Boaz baada ya kuona
Austin haongei chochote
“Najua ninachokuomba ukifanye si
kitu chepesi na hukuwa umekitarajia lakini
sina namna nyingine zaidi ya kukuomba
msaada.Tafadhali nisaidie katika hilo
kijana wangu” akasema Boaz na Austin
akainamisha kichwa akazama mawazoni
“Please help me son” akasema
Boaz.Austin akainua kichwa na kusema
“Ulilipa kiasi kikubwa cha pesa
kunikomboa kutoka mikono ya
Alshabaab.Wewe ni sababu ya mimi kuwa
hivi nilivyo leo.Umenipokea na
kunijumuisha katika familia yako.Wewe ni
mtu wa thamani sana kwangu na kwa ajili
hiyo basi nitaifanya kazi uliyonipa”
“Ahsante sana Austin.Thank you so
much my son.Sipati neno zuri la
kukushukuru.Ninaamini kwa uwezo ulio
nao unaweza kabisa kulikamilisha suala
hili ndani ya muda mfupi ili niweze kupata
pesa zangu .” Akasema Boaz kwa furaha
“ Mr Boaz uchunguzi wangu utaanzia
kwa hao watu wawili uliowataja ambao
wana ukaribu na Marcelo lakini kabla
sijaifanya kazi yangu nataka uwe na
uhakika.I want you to be 100% sure that
one of them or both knows where Marcelo
is.I dont want 97%,98% or 99% I need
100% .Sitaki kumuumiza mtu asiye na
hatia.So mr Boaz I’m going to ask you
again are you sure these two people knows
where Marcelo is?
Boaz akavuta pumzi ndefu na
kumtazama Austin kisha kwa sauti yenye
kitetemeshi akasema
“ I’m not 100% sure but just do it
son.These two are the only lead to
Marcelo.Take them and use whatever
methods you know to make them talk and
show us where Marcelo is.Nina uhakika
lazima kuna kitu wanakifahamu kuhusiana
na Marcelo.Austin you are my family and
the money I’m talking here belongs to our
family.So do this for our family.What I
have is yours too so do whatever you can
to find this bastard Marcelo.He’s
somewhere hiding here in Dar es salaam.”
Akasema Boaz .Austin akamtazama kwa
makini na kusema
“Ni vipi endapo baada ya kuwahoji
nitajiridhisha kwamba wawili hawa
hawafahamu chochote kuhusu Marcelo?
“Endapo hawafahamu chochote
hakuna haja ya kuwacha kill them all...”
akasema Boaz .Austin akainama akawaza
kidogo halafu akasema
“Mr Boaz,nitaifanya hiyo kazi kama
ulivyoniomba lakini nataka nikuweke wazi
kwamba haitakuwa kazi rahisi kama
unavyodhani.Itachukua muda lakini kuna
kitu kimoja ambacho nataka
nikuombe.Nataka ufanye kila uwezalo
kuhakikisha kwamba Maria anaondoka
hapa
nchini
haraka
iwezekanavyo.Ikiwezekana hadi kufikia
kesho jioni awe amerejea afrika ya
kusini.This place is dangerous for her”
“Kwani rais amekupa kazi gani
Austin? Akauliza Boaz
“Kuna kazi yake binafsi
ninamfanyia.Si kazi kubwa lakini kama
unavyoelewa historia yangu watu
waliotaka kuniua bado wako hapa hivyo
wakifahamu kwamba niko hai na
nimerejea watatafuta kila namna ya
kuniangamiza kwa hiyo hapa nilipo
nimezungukwa na hatari kubwa.Sitaki
Maria adhurike au aingie katika
hatari.Naomba umuondoe haraka sana”
“Ok sawa niachie suala hilo
nitalishughulikia na kesho Maria atarejea
afrika ya kusini.Ahsante sana kwa kumjali
mwanangu.By the way Austin,tumia kiasi
chochote cha fedha unachokihitaji toka
katika akauti ya kampuni na endapo kuna
msaada wowote unahitaji usisite
kunieleza”
“Sawa mzee nitakapohitaji chochote
nitakujulisha”
“Austin ahsante sana .Nitakuwepo
hapa Dar hadi jambo hili litakapokamilika
kwa hiyo nitakuwa nikija hapa mara kwa
mara
kukutazama.Vipi
kuhusu
mawasiliano? Tayari umekwisha pata laini
ya simu ili kurahisisha mawasiliano
 
SEHEMU YA 18


apana bado sijapata laini ya simu
kama unavyofahamu laini zote huwa
zinasajiliwa na mimi si raia wa Tanzania
kwa hiyo kuna ugumu wa mimi kupata
laini hata hivyo nitajitahidi ”Marcelo
akadanganya
“Usijali nitakufanyia mpango wa laini
simu kesho.Nadhani tumeelewana.Twende
sasa sebuleni ili Maria asipate
wasiwasi.Tafadhali naomba usimueleze
chochote kuhusiana na kazi hii.Hatakiwi
kufahamu kama umerudia tena kufanya
kazi hizi” akasema Boaz wakarejea
sebuleni.
“Austin ahsante sana kwa kutupokea
na kutukaribisha japokuwa tumekuja bila
taarifa.Maria amefurahi kukuona na kiu
yote aliyokuwa nayo imekwisha baada ya
kujua uko salama.Hana hofu tena.Si ndiyo
Maria?akasema Boaz na Maria
akatabasamu
“Kwa
hiyo
Austin
sisi
tunaondoka,tutapanga tena siku ya kuja
kukutembelea ila utakapomaliza shughuli
zako urejee mara moja Afrika ya kusini”
“Dady !! .Maria akahamaki kwa kauli
ile ya baba yake na kusimama
“ Tumekuja kumtazama Austin ,kwa
nini tukimbie? Sijaonana na Austin kwa
zaidi ya wiki tatu ,nina mambo mengi ya
kuongea naye kwa hiyo siondoki sasa
hivi.Kama wewe una haraka ya kuondoka
nenda kaendelee na shughuli zako mimi
ninabaki hapa na Austin atanirejesha
hotelini baadae” akasema Maria
“Maria we have to leave
now.Tumekuja bila taarifa na kwa kuwa
tayari tumekwisha onana naye tumuache
aendelee na shughuli zake hadi kesho
tutakuja kumtembelea tena.” Akasema
Boaz
“ No day ! you can go I’m staying here
!! akasisitiza Maria.Austin akainuka na
kumuendea
“It’s ok my love you can go now.Mimi
na wewe tutapanga tena siku nyingine ya
kuonana”
Maria akapatwa na mshangao kwa
kauli ile ya Austin akashindwa aseme
nini.Akawatazama Austin na baba yake
kwa zamu
“Austin what’s going on?Why aren’t
you happy to see me?
“Are you hiding something ? Akauliza
Maria kwa ukali
“I’m not hiding anything from you
my love.Kama alivyosema mzee
tutawasiliana na tutapata nafasi nzuri ya
kuongea yale yanayotuhusu” akasema
Austin.Kwa hasira Maria akachukua pochi
yake ndogo na kutoka kwa kasi kuelekea
garini huku akilia.Boaz na Austin
wakatoka hadi katika gari wakaagana na
Austin akafungua geti gari likaondoka
“Maria tafadhali usilie my
princess.Haikuwa vizuri kwa sisi
kuendelea kukaa pale kwa muda mrefu
wakati Austin ana ratiba zake nyingine
hasa ukichukulia kwamba kilichomleta
huku ni masuala ya kifamilia.” Akasema
Boaz wakiwa garini baada ya kuondoka
nyumbani kwa Austin.Maria aliyekuwa
ameinama akainua kichwa na kumtazama
baba yake kwa hasira na kuuliza
“Whats going on dady? Kitu gani
ulichoongea na Austin na hamkutaka
kunishirikisha? na halafu mlipomaliza
ukanitaka tuondoke mara moja wakati
unafahamu kabisa kwamba nimesafiri toka
Dubai kwa ajili ya jambo moja tu la kuja
kuonana na Austin.Why you didn’t let me
spend time with the man I love? Why
dady? Akauliza Maria.Boaz akakohoa
kidogo na kusema
“Maria there is one more thing you
have to know”
“Whats that? Akauliza Maria
“Kesho utaondoka kurejea Afrika
kusini.Anatakiwa mtu wa kuwepo kule
kusimamia biashara zetu.Kwa hiyo
nitafanya utaratibu wa ndege kesho na
utarejea nyumbani mara moja.Najua
nitakuwa nimekuumiza kwa hili and I’m so
sorry” akasema Boaz
“What?!! Dady that cant
happen.Whats going on? Kuna kitu gani
wewe na Austin mnakificha? Je Austin
ndiye aliyekushauri hivi? Toka awali
nilipomueleza juu ya mimi kuja Dar es
salaam alipinga vikali na hata leo
aliponiona hakuonyesha kufurahi.I need to
know the truth,whats going on? Why
Austin is here? Whats he doing here?
Akaulza Maria
“Haya si mawazo ya Austin bali ni
mimi ndiye niliyeamua hivyo.Kuhusu kazi
anayofanya Austin hapa Dar es salaam ni
mambo yake binafsi ya kifamilia ambayo
hatuwezi kuyaingilia .The guy has done a
lot for us so we have to respect him whe he
needs a privacy” akasema Boaz.Maria
hakuongea tena akaendelea kulia kwa
kwikwi.Boaz aliumia lakini hakuwa na
namna nyingine ya kufanya
“Lazima kuna jambo linaloendelea
hapa kati ya baba na Austin ambalo
hawataki nilifahamu.Toka mwanzo Austin
alipinga vikali nisije Dar na hata leo
aliponiona
alionyesha
wazi
kutokufurahishwa
na
ujio
wangu.Wakaenda kuongea kwa siri bila
kunishirikisha kitu ambacho si cha
kawaida na kama hiyo haitoshi naambiwa
kwamba kesho natakiwa kuondoka
kurejea afrika ya kusini.Kuna nini
kinaendelea hapa ambacho ninafichwa?
Mimi si mtoto mdogo wa kushindwa
kung’amua kwamba kuna kitu kinaendelea
hapa na ndiyo maana ninaondolewa
haraka haraka.Ninaanza kuhisi kama vile
baba ameanza kumtumia Austin katika
kazi zake . I Must find out the truth.Usiku
huu nitarejea tena huku nyumbani kwa
Austin” akawaza Maria
***********************
Baada ya akina Boaz kuondoka
Austin alirejea ndani kama mtu aliyerukwa
na akili .Moja kwa moja akaelekea katika
kabati kulimohifadhiwa chupa za mvinyo
akachukua moja na kumimina katika glasi
akagugumia yote
“ Aaaaggghhhh !!!! akatoa ukelele wa
hasira
“ Hii si ndoto bali ni kitu cha kweli
kabisa.Sikuwahi kufikiri kama siku moja
ningeweza kujikuta nikiwa njia panda
kama sasa.Kumbe ni Boaz anayetaka
kumuua Marcelo? Ni vigumu sana
kuamini.Imekuwa bahati sana Marcelo
hakujitokea kwani endapo angefahamu
yuko hapa hivi sasa tungekuwa tunaongea
mambo mengine ” Akawaza Austin na
kuvuta pumzi ndefu akamininina tena
mvinyo akanywa
“Marcelo anatafutwa kwa udi na
uvumba na Boaz na ninatakiwa
nihakikishe ninawapata Monica na Daniel
ili wanieleze mahala aliko Marcelo.Boaz
anataka nimtese malkia wa Afrika.Anataka
nimuumize mtoto mzuri kama Yule
ambaye hana hata chembe ya
mkwaruzo.Boaz ananiweka katika mtihani
mgumu sana”
Kichwa cha Austin kilijaa mawazo
mengi na mara akakumbuka kwamba
anatakiwa kwenda Rozana night club
kuonana na Job Israel
“Sikutaka kujihusisha katika suala la
Marcelo lakini nimejikuta nimeingia katika
suala hilo bila kutaka.Ninahisi kuja
Tanzania ulikuwa ni mpango wa Mungu ili
 
SEHEMU YA 19


niweze kuwaokoa watu wake wasio na
hatia kama hawa akina Marcelo.Ngoja
kwanza niliweke pembeni suala hili hadi
hapo baadae nitakaporejea na kuongea na
Marcelo ili niupate ukweli.Naamini kuna
sababu kubwa iliyopelekea Boaz anitake
nimsake
kwa
kila
namna
niwezavyo.Lazima nikiri jambo hili
limenitikisa sana ndani ya dakika hizi
chache.Nimewekwa kati kati ya watu
wawili wa muhimu .Rais Ernest amemtoa
mdogo wangu kutoka kifungoni nchini
China kama malipo kwa kazi anayotaka
nimfanyie ambayo ni kuhakikisha ninapata
sampuli toka kwa Monica kwa ajili ya
kufanya kipimo cha vinasaba ili kujua
kama ni mwanae au vipi kwa hiyo
natakiwa kumlinda kwa namna yoyote
ile.Kwa upande wake Boaz ameniokoa
kutoka katika mikono ya Alshabaab kwa
kulipa
kiasi
kikubwa
cha
fedha.Amenikaribisha katika familia yake
na amenitunza kama mwanae wa kumzaa
lakini malipo ya kila alichonifanyia ni
kumuua Monica mwanamke ambaye hana
kosa lolote.Nimesimama kati kati na
itanilazimu
nifanye
maamuzi
magumu.Ngoja kwanza niachane na jambo
hili niende Rozana club kuonana na
Job.Nitatafakari na nitapata ufumbuzi ila
siwezi kuifanya kazi ya Boaz” Austin
akaelekea katika chumba cha Marcelo.
“Rais ameondoka tayari? Akauliza
Marcelo
“Hapana hakuwa rais bali ni mlinzi
wake kuna maagizo alipewa aniletee”
“Still no word from David? Akaulzia
Marcelo
“Hapana
bado”
akasema
Austin.Marcelo akashika kichwa ishara ya
kukata tamaa
“Marcelo ninatoka kidogo kuna
sehemu
ninakwenda.Nitakaporejea
tutakuwa
na
mazungumzo
mazito.Usimfungulie geti mtu yeyote
Yule.Nitakuachia
kifaa
ambacho
kitakuwezesha kuona picha za kamera
zote zilizofungwa hapa .Mimi pia ninacho
kifaa cha kuniwezesha kujua kila
kinachoendelea hapa kwa hiyo endapo
kutakuwa na tatizo lolote hapa nyumbani
nitajua na nitakuachia simu ambayo
tutawasiliana nitakuelekeza nini cha
kufanya.”
Austin akaenda chumbani kwake
kujiandaa na kisha akamuaga Marcelo
akaondoka.
“Bado mwili unanitetemeka kwa
kuwaona Boaz na Maria.Sikuwa
nimetarajia kabisa kuwaona .Nilimkatalia
ombi lake la kuja Dar es salaam na kama
haitoshi nikakata kabisa mawasiliano naye
lakini kwa kumtumia baba yake ameweza
kunipata.Imekuwa rahisi kwa Boaz kujua
mahala nilipo kwani amewasiliana moja
kwa moja na rais akamuelekeza
nilipo.Ninachojiuliza Maria ana fahamu
kinachoendelea? Anafahamu mipango ya
baba yake? Naanza kuhisi kama vile mimi
na Maria tunaelekea katika sintofahamu
kubwa. I love her and I don’t want
anything happen to us.So what am I going
to do? Tell her the truth what I’m doing
here? No I cant do that.Ngoja tu niachane
naye.Siwezi kumweleza ukweli wa
ninachokifanya hapa Tanzania.” Austin
akaendelea kuwaza
*********************
Ni siku iliyokuwa na pilika pilika
nyingi kwa Monica.Alikuwa na mizunguko
kadhaa vile vile alikuwa na vikao mbali
mbali.Hadi giza linaingia tayari Monica
alikuwa amechoka sana.Saa tatu kasoro
dakika nane alitoka ofisini akaenda katika
gari lake na kuondoka kuelekea nyumbani
“Niliwaahidi baba na mama kuwa
ningeenda kuonana nao jioni ya leo lakini
nimechoka sana nitakwenda siku
nyingine.Ninahitaji mapumziko”
Monica akastuliwa mawazoni na
simu yake iliyoita.Akatazama mpigaji
alikuwa ni David Zumo
“Oh ! its David.Siwezi kuzungumza
naye sasa hivi wakati ninaendesha
.Nitampigia nikifika nyumbani.Leo nataka
anieleze mahala aliko Marcelo.Nahitaji
sana kuonana naye kujua hali yake”
akawaza Monica huku simu ikiita na
kukata,akatabasamu baada ya sura ya
David kumjia kichwani.
“Inaonyesha tayari David ameanza
kuzama kichwani kwangu.I feel like I’m
missing him.The way he was holding me
gently,the way he kissed me,oh gosh ! it
was so lovely.Should I say I’m luckt to have
him? Akajiuliza.
“Ndiyo ninaweza kusema ninayo
bahati.Mwanaume kama David ukitoa
utajiri wake ana mambo mengi ambayo
kila mwanamke anayapenda.Kitandani
nampa digrii tano.Ni mjuvi wa
mambo.Mapenzi anayafahamu.Ana pumzi
kama farasi.Alinipeleka hadi nikahisi
kutaka kupoteza fahamu.Au inawezekana
ni kutokana na ugeni wangu katika mambo
haya ya mapenzi? Lakini pamoja na ugeni
wangu katika mapenzi lazima nikiri David
is a real man.Alinifikisha mahala ambako
sikuwahi kufika.Kila mara ninapokumbuka
mambo tuliyoyafanya mwili wote
hunisisimka na kwa uchovu huu nilio nao
natamani kama ningefika nyumbani na
kumkuta David akinisubiri” akatabasamu
“It looks like I’m going crazy.Kumbe
mapenzi matamu kiasi hiki.Naweza sema
bado sijachelewa kwani subira yangu
ndiyo iliyonifanya nikutane na
David.Endapo ningekuwa tayari nina
mpenzi au tayari nimeolewa leo hii
nisingekuwa najianda kuolewa na mtu
mkubwa kama David zumo tajiri namba
moja Afrika”
Safari nzima Monica alikuwa akiwaza
mambo mengi kuhusu maisha yake
yatakavyokuwa.Aliwasili nyumbani kwake
akawajulia hali watumishi wake wote
halafu akaelekea chumbani kwake
akachukua simu na kumpigia David Zumo.
“Hallow mpenzi “ akasema David
Zumo mara tu alipopokea simu
“Hallow mpenzi” akasema Monica na
kumfanya David astuke na kuvuta pumzi
ndefu
“Hatimaye umeniita mpenzi.Mungu
mkubwa .Ahsante sana Monica.Niliisubri
kwa hamu kubwa siku ambayo ungewez
 
Back
Top Bottom