R.Mengi for President?

R.Mengi for President?

Status
Not open for further replies.
If Mengi failed to be honest in his marriage, what makes you think he will be honest once he has full control and powers to rule 40 million people?
 
jmushi, i thought wazo lako la mwanzo ilikuwa ni kumweka Mengi ajadiliwe kama anafaa kwa urais ama ala, lakini baadaye nikaja kugundua kumbe ushapiga mahesabu yako na umewapigia tayari wananchi mahesabu ya kumuona kuwa anafaa, na mtu yeyote anayefikiri vinginevyo ana CHUKI, kama hiyo ndo staili yako mzee SLOW DOWN.
 
Honest?uwezo kisiasa?experience?.............

Watanzania lazima tubadilike,tumekuwa tunawabagua sana wachaga kuwapa nafasi za juu ktk siasa(mfano mzuri Mh.Mrema alidondoshwa na hao mnaawaita wana experience,mahonest,wene uwezo kisiasa,n.k).Mengi na wachanga wengine wote wene uwezo amkeni tutawapa kura siye.Mchaga hata akiiba,lakini anajenga kwao,hawa watu hawana tabia ya kuuza nchi kwa wazungu,wahindi,waarabu,n.k.
Wana uzalendo wa kweli.
Kuhusu ukabila wao,mie nawafagilia tuu,kila mtu ni mkabila hapa tz,why not wachaga?

Aboud,RA na wahindi wengine + waarabu walioko ndani ya serikali wanafaa nini hasa kwa mtanzania?kwanini hamuwapigi vita hawa?katolewa Mengi ishaiingiza ukablia,kisa mchaga.Acheni wivu watz,hatutaendelea kamwe,watz wana wivu mkali sana juu ya watz(weusi) wenzao,kuliko mafisadi wageni(wahindi,wazungu,waarabu,n.k) hawa wanaohujumu uchumi wetu.

Mengi chukua fomu,kura utapata,achana na wazushi,wameshanunuliwa na wageni hawa.Hawana lolote la kupima hapa.
 
Na kama Waungwana wengine hapa JF...
Mengi akigombea nje ya siasa zetu chafu za pande mbili hapa nchini zinazosheheneshwa na ukabila, udini, chuki binafsi(upinzani vs ccm) na mambo mengi tusiyoweza kuyasema hapa then si tu ana kura yangu!
BALI ANA KURA ZA WAZALENDO WENYE KUONA OUT OF THIS MESS THAT..THERE'S SOMETHING POSITIVE!
 
If Mengi failed to be honest in his marriage, what makes you think he will be honest once he has full control and powers to rule 40 million people?

Ni mwinyi,Mkapa,Kikwete ama Mwalimu waliokuwa waaminifu kwa wake zao?
Rev naomba tuendelee na yale positive!
Our country is in a defining moment and the citizens are in a critical danger!
Usisahau hayo ukabakia kwenye politics za chuki!
Its time for the politics that makes sense!
 
Na kwa wale mnaojindanganya kuwa R.Mengi hana sappoti ya wananchi wa kawaida naomba mnijibu hili...

Mniletee takwimu ya watu wenye kuweza kupata huduma ya internet hapo Tanzania ama wenye uwezo wa kutembelea hii JF!
Utakuta ni viongozi na watu wenye uwezo!
Hao wengi wao hawampendi R.Mengi!
Mengi ni mtu wa watu na tuko tayari kumpigia kampeni huko vijijini!
NI MTU ANAYESEMA SISI NI MATAJIRI!
TUTAMUULIZA ATUONYESHE NI KIVIPI!
TUSIIPITE HII BAHATI MUNGU ALIYOTUPA!
HATA JESUS CHRIST MWENYEWE HAKUWA PERFECT!
 
Hizi mbwembwe za matusi hapa JF hazina nafasi kwa wale wananchi ambao wameshaona kuwa R.Mengi anaweza kulifanyia nini Taifa lake!
Kwanza tutawabana wale watakaoingia kwenye ushindani kuacha politics za matusi ili wananchi waelezwe na wagombea wao kuwa watawafanyia nini rather than personal vendettas za watu flani flani! Its time to talk issues in our politics! Its time to see what they can do for us!
Kwasababu tukianza huo mnaouita uchafu basi hamjaenda kuangalia definition sahihi ya UFISADI!
Kuna uchafu zaidi ya huo kwa masikini?
Na pia inawezekana hamjatafakari bado kuwa hao nyie mnaosema ni safi..ni wangapi wameshagundulika kuwa sivyo kabisa?
Mmesahau usafi wenu wa kufikirika kuhusu Mkapa aliouweka mawazoni mwenu Mwalimu Nyerere?
HII NCHI NI YA WOTE NA NI WOTE TUTAKAOCHAGUA KIONGOZI WETU THIS TIME AROUND!
 
rev. I disagree Putin amemdivorce mke wake kisirisiri so that he can get with his new girlfriend. He is an adulteror lakini a good President in economic and political terms (although Human rights is an issue, lakini everywea human rights is an issue..lol) sasa hata hivyo nadhani JF panaanza kuishiwa maana Mengi should not even come up for discussion. The man is a con... very shrewed.. and CCM doesnt really like him per se... and he knows ndio maana anaukaribu lakini haji involve directly kiivyo. Zile plot za ITV and other companies zake... aliiba kwakuhonga ardhi ili abadilishiwe na mtu mwengine (jina nnalo) that was in the 70s... Na ndio viwanda na Utajiri wake.. sasa Mkimpa Serengeti mnadhani ataifanyaje...? Acheni vitu visivyokuwa na maana... Naamani tunamatatizo mengi tanzania yanayo hitaji fikira zetu... sio Huyu Mzee
 
Kwa kifupi nyie mnaopinga bado hamjazi compare sifa za raisi tunayemtaka zaidi ya matusi,chuki,kashfa,udini na ukabila!

Sasa na wakristo nao wakisema hawamini in poligamy kama waislam mtasema nini?
Nani siyejua kwenye ukristo kuwa na wake wengi ni dhambi?
Mnataka kuzungumzia uchafu?
Tuanze?
Naamini mada halisi itapotea!

UPINZANI BADO HAWAJA NICONVINCE NA CCM NI MAFISADI!
Nualiza tena...Weka sifa ya kiongozi anayetufaa vs sifa za Mengi
Mazuri ya Mengi VS hayo machafu!
Machafu ya viongozi wote waliopita vs machafu yake!
Kazi zake za kizalendo kwenye kumkomboa mtanzania vs kazi ya ufisadi na muflis wa nchi walizofanya viongozi waliopita na current!
Msipo weka chuki kwenye maoni yenu na fikra zenu basi mtaona mengi nje ya chuki!
Kuna wale wenye kugusia UKABILA!
HAYA MAJINA NA MAKABILA YA VIONGOZI WALIOPITA MAFISADI WALIOTUSABABIBISHIA UMASIKINI NAYO YAWEKWE HAPA ILI TUHAKIKISHE HATUTAYAPIGIA MAKABILA YAO KURA TENA?!
TUWACHUKIE WASUKUMA KWASABABU CHENGE FISADI?

AMA WAMASAI KWASABABU YA LOWASAA?

NA MEMA YA MENGI BADO TUYACHUKIE?

Naona kuna watu bado wanaishi kwa ndoto!
Naomba tusiligawe Taifa letu!
Kila mtu ana hakli ya mjadala based on character na si vinginevyo!
Mzalendo huyu anapigwa vita pande zote kutoka CCM na UPINZANI(baadhi)
Ila COALITION ya watu wema anayo!
HILO NI GUARANTEE!

jmushi1, stop your aimless rambling and preaching bwana! Jibu swali nililouliza hapo juu kuhusu namna Mengi angefanikiwa ku-deal na wadhifa wa Urais versus ule wa Ufanya biashara iwapo angechaguliwa kuwa rais?
 
rev. I disagree Putin amemdivorce mke wake kisirisiri so that he can get with his new girlfriend. He is an adulteror lakini a good President in economic and political terms (although Human rights is an issue, lakini everywea human rights is an issue..lol) sasa hata hivyo nadhani JF panaanza kuishiwa maana Mengi should not even come up for discussion. The man is a con... very shrewed.. and CCM doesnt really like him per se... and he knows ndio maana anaukaribu lakini haji involve directly kiivyo. Zile plot za ITV and other companies zake... aliiba kwakuhonga ardhi ili abadilishiwe na mtu mwengine (jina nnalo) that was in the 70s... Na ndio viwanda na Utajiri wake.. sasa Mkimpa Serengeti mnadhani ataifanyaje...? Acheni vitu visivyokuwa na maana... Naamani tunamatatizo mengi tanzania yanayo hitaji fikira zetu... sio Huyu Mzee

Na Rais wa Ufaransa je?
Ama sasa tuna macho tofauti?
 
jmushi1, stop your aimless rambling and preaching bwana! Jibu swali nililouliza hapo juu kuhusu namna Mengi angefanikiwa ku-deal na wadhifa wa Urais versus ule wa Ufanya biashara iwapo angechaguliwa kuwa rais?

Kama hujui leadership theories pamoja na management skills alizonazo..Ama zinazotakiwa kwa kiongozi wa nchi yetu kwenye kipindi hiki cha mpito then nyie ni wale mnaoishi kwenye dunia yenu ya kufikirika!
Wewe si ndiye wa kwanza kuja na aimfull rambling za ukabila we nyama hatari kwa Taifa?
Kama wewe ni force ya Mkapa najua hauko comfortable!
Otherwise usitake ku diminish yale mema ya watu wengine kwa chuki zako za kutaka kuligawa Taifa!
Hujasema kama Tuwachukie watu wa kabila la Mkapa,Chenge na Lowassa ambao tuna ushaihidi kamili wa uchafu na uoza wa KIFISADI!

NB:Naomba pia utembelee ile thread ya "Mafisadi wakamatwe-Wasiruhusiwe kuligawa Taifa"
 
Kitila,

In private Mkapa created ANBEN and later aqcuired Kiwira.

In politics, there is no privacy. Culture ya Tanzania tunapenda sana kuona mambo mengine kuwa si muhimu. Nitakuuliza tena, kama alivunja kiapo cha uaminifu kwa mkewe alichofanya madhbahuni, na akaapa kukilinda, itakuwa vipi vigumu kwake kuvunja kiapo atakachoapa mbele ya Jaji Mkuu?

We are looking for honest people, who are devoted to our country and not deceitful.

Labda nikuulize tena, kwa nini Mengi alitaka kutununua na kutufumba mdomo Jambo Forums wakati ule wa kelele za Manji na yeye mpaka Wazee wa Kichaga wakamweka chini Mike?

He is simply not honest and he is corrupt!

Niletee Robert Kisanga, Barnabas Samatta au Geoffrey Mmari we will be on same page.

Make sure you are not confusing between "honest" and "saint"! I don't think having an affair outside your relationship is being dishonest. It is only dishonest if you don't acknowledge the affair. He is no different from Obama, whom you hapeen to be his staunch admirer, who acknowledged to have once been engulfed in drug consumption. Obama would have been dishonest if he denied this, but he didn't.

In any case no body here is trying to suggest that Mengi is a purist or an absolute clean man, far from it. All I am saying is that he is among the few Tanzanians who have demonstrated an extraordinary leadership capacity; namely, being able to mobilise members of a group to create and achieve a common goal. We are looking for a national leader rather than a national brother or sister to lead us to heaven.

Again, you have not given us any evidence to substantiate your claim that Mengi is corrupt; unless you are using this word fashionably! Mengi's wealth is clearly traceable and there is no evidence to suggest that he amassed it through corrupt practices. Similarly, tuletee ushahidi kwamba Mengi alijaribu kutuziba mdomo hapa JF. Kwamba hili lilisemwa haina maana basi lilikuwa kweli. Kuna mambo kibao hapa yaliyowahi kusemwa ambayo hayakuwa kweli.

Kuhusu hao waheshimiwa uliowataja, sina comments kwa sasa. Labda tu niseme kwamba wanaweza wakawa miongoni mwa watanzania wanaofaa kutuongoza kama alivyo Mengine na wengine ambao hatujawataja, wanajadilika.
 
Mengi anafaa sana kuongoza hii nchi kwani angalao ni mtu aliyeonyesha kujali maslahi ya Mtanzania.Leo hii kuna watu ambao wanatumia kodi zetu hovyo wakimuacha Mengi akishughulika na wagonjwa wa moyo na wa saratani peke yake.

Kwa kweli mtu anapomuuliza JMUSHI 1 kuja na dataz za kusapoti ambayo Mengi amekua akifanya nakua simuelewi
 
Kuna wale wasiofahamu kuwa hata sisi kuwepo hapa JF na kuwajadili viongozi wetu na yeye amechangia sana sisi kuweza kufanya hivyo!
Umaarufu wa wanasiasa wengi tu wa upinzani umefanikishwa na yeye!
He is the God Father for the patriots!
He definetly can lead us!
We have no doubts that he can...Unless proven adawais by hoja!
 
Yes Ni Mkalimu Lakini Mtu Ambaye Hawezi Kusimamia Nyumba Yake Hatufai,hatutaki Mkapa Wa Pili ,yule Bwana Haeleweki Mke Wake Nani Kwenye Public Bonge La Mtu But In Privet Ni Weekest Creatuere,mwache Afe Taratibu Na Radio One.
 
Nimefuatilia mjadala huu na kusoma kila post moja moja na kuna hoja nyingi na za msingi. Naomba, niseme machache kuhusu mada nzima katika maudhui yake.

a. Uongozi wa Taifa ni jambo nyeti.

Kuongoza Taifa siyo sawa na kuongoza chama, familia, biashara, au klabu fulani ya watu. Si sawa hata kidogo na jambo jingine lolote ambalo mtu hata awe na sifa zipi, elimu ipi, kipaji cha namna gani, anaweza kuandaliwa kwacho. Hivyo, hakuna mtu mwenye qualification rasmi ya kumuwezesha kuwa Rais ambayo ukiingalia unaweza kuhisi kuwa atakuwa Rais mzuri au mbaya. Hakuna.

Kuwa na shahada za udaktari na kuwa mwaminifu katika ndoa siyo guarantee kuwa mtu atakuwa kiongozi mzuri wa Taifa, kuwa tajiri au maskini haiwezi kuhakikisha Rais atakuwaje n.k So, kwa wale wanaojaribu kuangalia mtu sifa zake na kujaribu kuprejudge kuwa atakuwa Rais mzuri au mbaya wana overestatement their own assumptions.

b. Uongozi wa Taifa ni uongozi wa ukingano

Kuongoza Taifa ni kuongoza vitu vinavyokinzana; maslahi yanayogongana, na matamanio yanayogongana. Kuongoza watu wenye maslahi tofauti, hamu tofauti, na mitazamo tofauti ili kuweza kufikia lengo moja si jambo rahisi. Kuna maslahi ya makampuni, maslahi ya taasisi binafsi, maslahi watu binafsi, maslahi ya viumbe vingine nk

Hivyo yeyote mwenye jukumu la kuwa Rais anakabiliwa na mgongano usiokwepeka na kazi yake kubwa ni kuhakikisha kuwa maslahi yote yanapata nafasi kwa kiwango kikubwa bila kugonganisha maslahi ya watu wengine au vyombo vingine. Hivyo, kama nilivyosema kwenye (a) hakuna anayeandaliwa kwa hilo.

Mfanyabiashara kama Mengi, Waziri kama Mkapa, Waziri kama Kikwete, Mwalimu kama Mwinyi, Mwalimu kama Nyerere hakuna aliyeandaliwa kushika nafasi hiyo.

c. Uongozi wa Taifa ni mzigo usiotafutwa

Hakuna mwenye haki ya kuwa kiongozi wa Taifa na tuwaogope sana watu wanaotafuta nafasi ya kwenda Ikulu. Nikiwa mwanafunzi mzuri wa Mwalimu naamini kabisa kuwa Ikulu si mahali pa kutafutwa. Na hasa siyo mahali pa kutafutwa kwa "udi na uvumba". "Kuna nini Ikulu?" ni swali ambalo kila mwenye kutamani nafasi hiyo lazima ajiulize.

Hofu yangu ni kuwa Ikulu pamegeuzwa kuwa kisima cha faida, na chimbuko la Biashara. Nyerere pamoja na mapungufu yake mengi ambayo yamesemwa sana, alijaribu sana kuiheshimu Ikulu. Ni wale waliokuja baada yake ndio wamegeuza nyumba hiyo kuu ya watanzania kuwa genge la biashara na kitovu cha ufisadi.

Hivyo binafsi naogopa kabisa na kutetemeka nikisikia mtu anataka kwenda Ikulu au anataka Urais kwani najiuliza kwanini? Hilo peke yake halinitishi sana lakini inapotokea mtu anatumia mbinde kupata nafasi hiyo basi hofu yangu ya mtu huyo inaongezeka mara 180!

Mtu mwenye akili timamu hatamani kubebesha mzigo huo; mzigo huo atabebeshwa kwa kuombwa na watu wenyewe, hautafuti.

d. Uongozi wa Taifa humbadilisha mtu

Kama kuna kitu cha ajabu kinachotokea kwenye Urais ni kuwa una nguvu ya kumbadilisha mtu kwa uzuri au kwa ubaya. Na hapa si urais wa Tanzania tu bali uongozi wa nchi yoyote ule; unaweza kumfanya mtu awe "mwokozi" au "mwovu".

Kile ambacho kinajulikana sana kama "trappings of power" ni kitu kikubwa sana ambacho kinaweza kumfanya mtu mwadilifu kugeuka na kuwa fisadi numero uno. Mtu anapojua ana nguvu fulani au uwezo fulani kama yeye mwenyewe hana proclivities of humility basi mtu huyo ni rahisi sana kupotea katika saluti, ving'ora, makofi, na shangwe.

Lakini uongozi huo huo unaweza kumgeuza mtu dhaifu na mwoga kuwa shujaa, na asiyeweza kusema kuwa msemaji wa ajabu. Urais haujaribiwi kama kwa mtihani wa Mock na kuona kama mtu atafanya vizuri kwenye mtihani kamili. Mtu ambaye anaweza kufeli Mock ukashangaa ukija mtihani wenyewe akapasua vile vile na yule aliyedhaniwa kuwa "kinara" akaanguka.

Sidhani siko peke yangu katika kumjua mtu ambaye darasani kuanzia form one hadi form four alikuwa kati ya mtu wa kwanza na wa tatu, na hata wakati wa mtihani wa Final alikuwa anawaandaa wanafunzi wenzie kusoma na alikuwa msaada sana.

Matokeo yanapokuja mnaweza kupigwa na mshangao kuwa wale wote aliowasaidia wanatoka na Division 1 na 2 halafu yeye anatoka na division three au hata four na hakuna kiumbe duniani kinachoweza kuelezea hilo. Kwa mtu ambaye anaangalia maisha ya nyuma angeweza kutabiri kuwa mtu huyo angetoka na daraja la kwanza la point 7! Lakini matukio ya mtihani na majaribio ya wakati yalimbadilisha.

Kwa maneno mengine, Rais mzuri hajulikani nje ya Urais na Rais mbaya hajulikani nje ya Urais. Tunaweza kuhisi tu itakuwaje lakini kuhukumu by proxy haiwezekani. Kwa hili niko very pragmatic.

Nitawapa mfano; Rais Luiz lula da Silva wa Brazil si msomi wa aina yoyote na maisha yake yamezungukwa na mambo mengi ikiwemo kuzaa nje ya ndoa. Kati ya kazi alizowahi kufanya ni pamoja na ufundi viatu na umachinga (street vendor). Lakini leo hii kutokana na mang'amuzi yake ya maisha na kujifunza kwa makosa amekuwa Rais wa Brazil na sasa yuko katika kipindi chake cha pili, huku uchumi wa Brazili ukikua kwa kasi, akilipa madeni ya IMF miaka miwili mbele, na akiliongoza Taifa lake kuelekea kwenye anga za juu!

Yote hayo yamefanywa na mtu ambaye kwa kwa kuangalia tu maisha yake ya nyuma tunaweza kusema ni failure, si msomi, si mwaminifu katika ndoa yake, na kwa hakika uongozi wake wa chama cha wafanyakazi si kigezo cha kutosha.

On the other hand however, kuna mfano wa Rais Chiluba wa Zambia. Kwa namna yoyote ile ni mtu ambaye ilikuwa rahisi kuamini kuwa atakuwa Rais. Amejisomesha mwenyewe kwa njia ya correspondence na kushika nafasi mbalimbali , kutiwa kizuizini na Kaunda n.k Na yeye naye akawa na kashfa za ngono vile vile. Kwa wengine alionekana ni Mlokole (Nakumbuka niliwahi kumuona kwenye programu ya TBN some years back). Lakini alipotoka ndiyo siri yake ikajulikana, alikuwa ni fisadi tu kwani madaraka yalimbadilisha au alikubali kubadilishwa na madaraka.

e. Uongozi wa nchi ni utumishi.

Kiini cha Urais ni kuelewa, kukubali, na kupokea pasipo utata kuwa uongozi wa nchi ni utumishi kwa Taifa. Anayetaka kuwa kiongozi wa Taifa au anayedhaniwa kuwa anapaswa kuwa kiongozi wa Taifa ni lazima hili lieleweke kwake. Kama mtu anataka kuwa kiongozi ili amalizie miradi yake na ya rafiki zake, au anataka kuwa kiongozi ili alipize kisasi, au anataka kuwa kiongozi ili apigiwe saluti au kukata tepe za ufunguzi huyo mtu hatufai!

Tunataka mtu ambaye kitu pekee na pekee kinachomsukuma kukubali ombi la wananchi wenzake kuwa kiongozi ni utumishi kwao. Nje ya hapo hakuna kigezo kingine kinachomfaa mtu kuwa kiongozi.

f. Uongozi ni timu

Nimetolea mfano wa Lula hapo juu, ukweli ni kuwa mafanikio yake yanatokana na timu aliyojizungusha nayo. Kiongozi mzuri ni yule anayejua mapungufu yake na akayaziba kwa kuweka watu ambao watafanya kile ambacho hana ujuzi au ufundi nacho. Kiongozi mzuri asingemteua Mramba kuwa waziri wa Viwanda au Msolla kuwa waziri wa Elimu ya Juu! Kiongozi mzuri hawezi kumrudisha Wassira kwenye Kilimo wakati taifa linakabiliwa na njaa, na kwa hakika kiongozi mzuri asingeweza kumuweka Lowassa katika nafasi yake.

Hata hivyo, kiongozi mzuri ni yule anayetambua makosa yake na kuyasahihisha.

g. Uongozi ni uadilifu siyo ukamilifu

Mojawapo ya mitego tunayoingia ni ya kujaribu kumtafuta mtu mkamilifu kuliko wote ndiye atufaye kuwa kiongozi wetu. Tunapoangalia maisha ya watu mbalimbali tunajikuta tunakatishwa tamaa kwani mtu anaweza kuwa msomi lakini mtongozaji mno, anaweza kuwa na kipaji sana cha kuzungumza lakini dhaifu, anaweza kuwa tajiri sana lakini si mwanasiasa, n.k n.k Yaani tunajikuta kila tunayemwangalia kwa ukaribu tunajikuta ana mapungufu kibao.

Mwisho tunaanza kuwa kama watu wanaotaka kumla bata, aidha umnunue na kumshughulikia lakini usiende sana kumtafuta kila anachokula na wapi anakunywa maji, vinginevyo hutamla. Tunapowaangalia wanasiasa wetu kuna mambo hatuna budi kuyaweka mbele na mengine kuyaweka nyuma.

Madai ya mtu kutokuwa mwaminifu kwa ndoa yake ni dogo sana ukilinganisha na mtu ambaye siyo mwaminifu kwa fedha za umma. Hakuna direct relation yoyote ile kati ya nani mtu analala naye kitandani na nini mtu anafanya ofisini. Je wezi wote wa fedha za umma ni malaya? Je wale wote wanaofanya ubadhilifu kwenye mashirika na taasisi zetu wana vimada au wanaenda nje ya ndoa zao? Je wala rushwa wote ndoa zao zimevunjika?

Tunachohitaji ni mtu mwadilifu na si mkamilifu. Mtu mkamilifu hayupo duniani lakini mwadilifu tunaweza kumtafuta na kumpata. Mkamilifu hafanyi makosa, mwadilifu hutambua makosa; mkamilifu hasemi uongo, mwadilifu anagundua uongo wake na kuusahihisha; mkamilifu hatamani utajiri wa bure, mwadilifu anatamani utajiri lakini anataka kuufanyia kazi; mkamilifu hatamani kiwowo cha pembeni mwadilifu anakitamani na anakikwepa; mkamilifu hapotezi hata senti moja ya fedha za serikali, mwadilifu anagundua amepoteza fedha na halali hadi ajue ziko wapi na zinarudi; mkamilifu haogopi kufanya kitu kwani anajua atakachofanya kitakuwa kizuri na kitapendwa, mwadilifu anaogopa kufanya kitu hivyo anapima na kuchagua kilichokizuri na anatumaini kitapendwa. Mkamilifu anapatikana mbinguni, mwadilifu anapatikana duniani.

h. Uongozi ni hulka kama ya simba

Niseme mwisho kwamba, uongozi wa Taifa ni kwa mtu mwenye hulka (instinct) kama za simba. Hauna elimu lakini huna instinct ya mwindaji. Hakuna mtu anayeweza kumfundisha simba kuwinda isipokuwa instinct zake zinaandaliwa pole pole na asili na matukio. Simba hata umtunze peke yake zile instinct zake hazifi.

Kiongozi wa Taifa anatakiwa awe na hizo zinazojulikana kama "killer instinct" asiyekuwa nazo hafai kwani hatojua ni wakati gani wa kuunguruma kwa tishio, ni wakati gani wa kunoa kucha zake na kutuma ujumbe "don't play" na pia ni wakati gani wa kuvamia na kurarua!

Ni kwa sababu hiyo basi walioandika Katiba yetu waliamua kuja na sifa chache tu za mtu anayeweza kuwa Rais. Wao wakasema hivi kuwa mtu hatokuwa na sifa za kugombea Urais isipokuwa kama:

a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa
mujibu wa Sheria ya Uraia.
(b) ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa;
(d) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe
wa Baraza la Wawakilishi,
(e) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya
Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika
Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa
kodi yoyote ya Serikali.

kwa msingi huo basi, tunapomuangalia Mengi au mtanzania mwingine yeyote tujiulize je anatimiza sifa hizo? Nje ya hapo ni kujiumiza kichwa kusiko kwa lazima kwani mengine ni sifa za kututuliza akili tu na kutufanya tuwe na hisia ya kuwa salama kwa vile mgombea wetu "ni msomi, anaenda swala au kusali, ana pesa nyingi, ana mvuto, anapenda kucheka cheka n.k".

Hiyo inatosha kwenye somo la Uongozi wa Taifa.
 
Kuna wale wanaodai kuwa tuzo ya MLK si yakiungozi!
Chini ni listi ya watanzania wengine waliowahi kuipata tuzo hiyo!
Wale critics naomba wanionyeshe utofauti wao na mengi kwenye characteristics zilizotumika kuwapa tuzo and then tuone kama R.Mengi alipewa kama kiongozi ama simply.."BEPARI"

Watanzania wengine waliokwisha kuzawadiwa tuzo hiyo na miaka yao kwenye mabano ni Rashid Kawawa (2007), Salim Ahmed Salim (2006), Gertrude Mongella (2005), Mama Justa Mwaituka (2004), Profesa Geofrey Mmari (2003), Jaji Francis Nyalali (2002), Jaji Joseph Warioba (2001) na Mwalimu Nyerere (2000).
 
Mengi Hawezi Akawa President Nyumba Yake Imemshinda,kamwacha Mzee Mwenzanke Kwa Ajil Ya Kimwana Lita So Aendelee Na Charty Work,hata Ukifuta Reads Zangu Hivi Ndiyo Najua Huwezi Kuvuta Moyoni Mwangu Kwani Yeye Ndiye Anayelipia Host Charge Ya Jf,mbona Mnamlinda Sana.
 
If Mengi failed to be honest in his marriage, what makes you think he will be honest once he has full control and powers to rule 40 million people?

Geeez Rev.!! If that is the standard then we are doomed....
 
Mengi Hawezi Akawa President Nyumba Yake Imemshinda,kamwacha Mzee Mwenzanke Kwa Ajil Ya Kimwana Lita So Aendelee Na Charty Work,hata Ukifuta Reads Zangu Hivi Ndiyo Najua Huwezi Kuvuta Moyoni Mwangu Kwani Yeye Ndiye Anayelipia Host Charge Ya Jf,mbona Mnamlinda Sana.

Ndugu yangu hujui hata Kikwete analindwa hapa sometimes licha ya kupondewa!?
Kuna thread hata moja imeshawahi kuanzishwa ya kumjadili R.Mengi zaidi ya zile za migogoro na kina Manji?
Je umeshakuja na sifa za viongozi tunaowahitaji base on vilio vya wananchi?
Kwanini hatupendi kuwauliza wananchi wanataka nini bali tu kuwashindilia yale tunayotaka sisi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom