Papy ndombe
JF-Expert Member
- Oct 24, 2020
- 3,761
- 4,535
Sema tu kuwa "sijaelewa",infact jamaa anazungumzia tukio moja la ajali ya lori lililotumbukia mto wamiHueleweki. Hizi shule za kata bora zifutwe
lengo lake ilikuwa jamaa aje apige nyuma yake asimame, maana hakukuwa na ujanja wa kumkwepa au kuongeza speed amuache.Kuna dereva mwingine wa lori alivyoona gari limemshinda breki mwenzake wa nyuma mto Ruvu pale akaona ajititie na mibreki ili amtumbukize mwenzie mtoni na akafanikiwa.
Kuna mahali niliona ajali kama hiiPana jamaa walikuwa na v8 wameovertake semitrela wamefika kwenye cabin mbele linakuja semi wangu wangu wakaingia kushoto mbele cabin ya semi wanayoovertake ile wameovertake semi A kuingia kushoto Ile kukwepa semi B ya inayokuja.Semi A ikawapush kwa nyuma semi B ikaja wakandamiza kwa mbele yaani walipigwa nyuma na mbele kwa semi zote mbili jamaa v8 awakuomba maji pale pale wote israel aliondoka nao,akawaacha madereva wa masemi.
Kumbe semi A angepunguza au kuminya brake angewaokoa.
Madereva wa matruck uwa wastaarabu lakini usiombe ukutane na madereva wa fuso na vicanter vya kubeba nyanya na vitungu wakitokea zao iringa na mbeya,jamaa kavu sana wale,mida ya usiku uwa wana mchezo wa kupiga full light gari ndogoPole kwa mkasa ambao hutokea mara nyingu kule mbugani barabarani.
Scenario uliyoelezea inatisha sana.
Kule mbugani si kwa ma learner na wakati mwingine ni umwamba, maana hakuna trafiki kila mahali.
Lakini katika uzoefu wangu, madereva wa malori kwa ujumla ni wastaarabu sana , isipokuwa wachache.
Kama unaendesha gari kwa kusita sita mbugani, hatari ni nyingi sana.
Pple!! Ila hamna sehemu ulojibu kuhusu kutelekeza uzi wa kusaka utajiri! Acha uhuni we jamaaMwaka jana Oktoba ni mwaka ambao kumbukumbu yake inanijia sana. Leo nimekumbuka zaidi baada ya kuonana ma Dereva mmoja anaitwa Richard.
Siku hiyo nilikuwa na gari yangu kubwa ni ya Diesel Manual ina Speed 240. Tumetoka Dar na jamaa yangu tunaelekea Dom. Huku kote nlikuwa naendesha mimi mpaka tumevuka Morogoro tunaelekea Kibaigwa kama sikosei.
Jamaa akaomba naye asukume ile mashine. Muda mrefu alikuwa akitamani sana jinsi navyokanyaga mashine,navyopiga mpini n.k akaona ni kitu chepesi na cha kuenjoy sana.
Mimi ni kweli na enjoy kuendesha gari hasa Manual. Akaomba naye akanyoshe nyoshe miguu. Akachukua mashine. Kiukweli jamaa hakuwa amezoea sana Manual ila alikuwa mbishi. Nlimwona anavyochelewa kuingiza gear, anavyoshindwa kurudi vizuri n.k
Nikamwambia kama inamsumbua anirudishie tu akasema hapana akiendesha kama dk 20 zaidi atakuwa master.
Tabu ilianza tumefika mitaa flani mbele yetu kuna truck yenye Trailer. Jamaa akaomba. Mwenye truck akamruhusu. But my friend akawa anajivuta sana ku overtake. Akiwa anataka kutoka mwenye truck akamkataza jamaa akawasha taa ya kulia.
Jamaa hakuelewa. Nikamwona kashaingia kulia kakanyaga accelerator. But kaingia halafu katika kubadili gear kacheka. So ikabidi atoe macho mbele aangalie anaingiza wapi gear.(asome namba).
Kule mbele tulisikia truck inapiga horn imewasha taa....imetoka speed ile mbaya. Speed hasa.jamaa kitete hatuwezi ingia kushoto sababu kuna truck ya jamaa tupo nayo usawa wa nyuma ya cabin na ina trailers zile zinakuwa iliyounganishwa na cabin na nyingine yake.
Jamaa yetu wa kushoto alishajua huu msalama. Akakamata brake tuliona gari yake tairi zikiburuza na kuchora alama barabarani huku gari ikilalamika sana. Ile ndo ilikuwa nafasi yetu finyu jamaa yangu akaingia kushoto kwa sentimita chache sana tulikoswa na lile gari la mbele yetu.halikuhangaika hata kusimama.
Sisi tuliingua kushoto jamaa akayumba na gari hivyo hivyo mpaka mbele tukasimama. Nikashuka haraka kumsimamisha jamaa wa truck ambaye alikuwa nyuma yetu.
Jamaa akaenda simama. Richard ni mmoja ya madereva wenye upendo sijawahi ona. Alishuka akitupa pole na kutuonea huruma. Mimi nlimwomba msamaha na kumshukuru sana kwa kitendo chake. Haraka nikatoa 70,000 mfukoni kumpa kama asante. Aligoma kuchukua kabisa.
Tukabadilishana namba za simu. Ilibidi gari nichukue kuendesha mimi. Tuliendelea kuwasiliana mpaka leo nmekutana naye Hospital akiwa anahangaika kumtibia mama yake. Hana Bima. Nimemsadia nlichoweza nikawasiliana na yule jamaa yangu naye ajipige pige. Tumeweza mchangia tsh 330,000 aongezee.
Jamaa ameshukuru hadi kutokwa na machozi. The man is very humble. Sijawahi ona madereva wastaarabu kama huyu jamaa.
Ndugu zangu tutendeni tu wema. Malipo tumwachie Mungu. Hulipa kwa wakati wake. Jamaa yangu since then hana hamu tena ya kuendesha manual. Ilikuwa atuue sote. Maana tungegongana uso kwa uso na truck ya mafuta. Uso kwa uso.
Sasa mbona unanifokea mkuu.?Wakishasema hii chai, nini kinabadilika ?
Hahaaa huyu jamaa ni tapeli kiukweli hata huu uzi haumuhusu yeye.Wewe tapeli ulieleta huu uzi hauaminiki unatabia ya kuiba story za wengine halafu unajidai za kwako.
Corona ipo na inaua.Sasa mbona unanifokea mkuu.?
Duuh mkuu mimi nilishawahi kwenda kwa jamaa yangu na chuma ya manual ilikuwa mwaka jana tu hapa.[emoji3][emoji3]nakumbuka kipind najifunza gari muhuni/rafik wangu mmoja alikua anasukuma scania 113 gear 8 Jamaa alikua anapanga gia Kama Hana akili nzuri na vile vinanda vya injin ya scania mzee had unataman ule ugali mkavu alaf mboga iwe ile sauti, nikamwambia Jamaa niachie na mm nimsukume msweeden
Jamaa akaweka chuma pembeni akanikabidhi jiko kundoka nikaondoka frsh shida ikaanza pale nimemaliza gear 4 natakiwa nipandishe button nianze kupeleka Hadi 8 jasho lilinitoka ikawa naacha kuangalia mbele naangalia gear lever nikirudishaa macho mbele naona tu vi ist vikiingia kwenye mashamba ya mahindi ya watu huko maana nlikua nayumba njia nzima inabid wao ndo wanikwepe la sivyo wanaingia kwenye uvungu alaf nipo kibati laana, muhuni mwenyewe ali sanda akaniambia pangua gear weka chuma pembeni[emoji3][emoji3][emoji3]
Sio chai tu...ni chai maharage.Basi kuna watu watakuja watasema hii ni chai!
Kama naviona vile vi ist vikiingia mashambani [emoji23][emoji23] dadeq[emoji3][emoji3]nakumbuka kipind najifunza gari muhuni/rafik wangu mmoja alikua anasukuma scania 113 gear 8 Jamaa alikua anapanga gia Kama Hana akili nzuri na vile vinanda vya injin ya scania mzee had unataman ule ugali mkavu alaf mboga iwe ile sauti, nikamwambia Jamaa niachie na mm nimsukume msweeden
Jamaa akaweka chuma pembeni akanikabidhi jiko kundoka nikaondoka frsh shida ikaanza pale nimemaliza gear 4 natakiwa nipandishe button nianze kupeleka Hadi 8 jasho lilinitoka ikawa naacha kuangalia mbele naangalia gear lever nikirudishaa macho mbele naona tu vi ist vikiingia kwenye mashamba ya mahindi ya watu huko maana nlikua nayumba njia nzima inabid wao ndo wanikwepe la sivyo wanaingia kwenye uvungu alaf nipo kibati laana, muhuni mwenyewe ali sanda akaniambia pangua gear weka chuma pembeni[emoji3][emoji3][emoji3]
Sawa mdogo ake @kidukulilo.Heading yako ni ya kichochezi, unataka Jamii imchukie rafik ako.