Rafiki yangu anasumbuliwa na jini mahaba. Je, ni namna gani ya kumtoa?

Rafiki yangu anasumbuliwa na jini mahaba. Je, ni namna gani ya kumtoa?

Nje ya mada kuu. Kipindi nabalehe na sina uwezo wa kukamata mademu nilikuwa naombea sana nopate huu ugonjwa wa kuwa na jini mahaba ila mikawa hata siyapati
Hauwezi kuyapata kwanza sio kitu cha kuombea na isije kuthubutu ya kukute ni hatari kubwa

Mara nyingi haya mambo huwa kuta watu wanaotokea ktk familia zenye mzizi wa mambo hayo wengi wa watu wanao patwa na hayo matatizo mababu na mabibi zao walikuwa na Hiyo asili
 
Kukosa elimu ndogo ndogo ni mbaya Sana, yaani vijini vijini vinawasumbua, sisi human wenye kila intelegency, shame!,
-Nunua indi kavu, lichome liive, kila jioni tafuna ukiwa chooni, kwa siku tatu, atakimbia na nyuma asigeuke, endapo atakuwa sugu, changanya indi lako na ulevi mweusi, tafuna.
Kama jini huyo ana power kubwa na ni inborn character yako hauwezi kumuondoa Kwa style na anaweza kumuua
 
Kuna rafiki yangu amekutwa au naweza kusema anasumbuliwa na jambo ambalo dalili zake zinaonyesha kua huenda akawa na jini mahaba ndani yake. Kwaio ameniombea kupitia jukwaa hili la ma great thinkers niweze kumuulizia jambo hili.

Dalili zenyewe ambazo kwa maelezo yake ameziona ni kama zinaendana na mtu mwenye jini mahaba ni pamoja na KUOTA AKIFANYA MAPENZI na kubwa zaidi KUPOTEZA HAMU YA KUFANYA MAPENZI katika maisha yake ya kawaida. Na hili la pili sasa ndo limepelekea hali kua ya wasiwasi mpaka kufikia kuniomba kuja kwenu wajuzi wa mambo kuulizia swala hili.

Jamaa stori yake huko nyuma ni kua amewai kua kwenye mahusiano na wanawake watatu nyakati tofauti tofauti, na wote sababu za kuachana nao ni kuwachoka na kutowahitaji tena muda mchache tu baada ya kukutana nao kimwili kwa mara mbili au tatu tu.

Nyakati hizo za nyuma alikua akihisi huenda alikua hajatokea kuwapenda ndomana pengine alikua akiwachoka haraka na kutowahitaji tena ila ni mpaka sasa ambapo yupo kwenye mahusiano na mwanamke mwingine ambae yeye anadai anampenda lakini katika hali ya ghafla amekua hana tena hamu ya kufanya nae mapenzi hata akiwa nae utupu chumbani, hali ambayo sio ya kawaida kabisa kwa sababu hana tatizo lolote la kiafya na ni mtu wa mazoezi.

Kwa dalili hizi moja kwa moja tumeona inawezekana ikawa huenda ana kitu tofauti kinachomsababishia hali hiyo. Na katika kujaribu kuuliza kwa mtu mmoja mwenye kufahamu mambo mengi kidogo, aliweka tiki pia kua dalili hizo zinakuaga ni za mtu mwenye jini mahaba.

Sasa lengo la uzi huu ni kutaka kufahamu zaidi kuhusu jini huyu mahaba, yani namna ya kumtoa na kuweza kujikinga nae wakati mwingine. NATANGULIZA SHUKRANI
NIpe mawasiliano yake, anilink na huyo jini, binafsi nasumbuliwa na mahaba,tubadilishane uzoefu!
 
Kuna rafiki yangu amekutwa au naweza kusema anasumbuliwa na jambo ambalo dalili zake zinaonyesha kua huenda akawa na jini mahaba ndani yake. Kwaio ameniombea kupitia jukwaa hili la ma great thinkers niweze kumuulizia jambo hili.

Dalili zenyewe ambazo kwa maelezo yake ameziona ni kama zinaendana na mtu mwenye jini mahaba ni pamoja na KUOTA AKIFANYA MAPENZI na kubwa zaidi KUPOTEZA HAMU YA KUFANYA MAPENZI katika maisha yake ya kawaida. Na hili la pili sasa ndo limepelekea hali kua ya wasiwasi mpaka kufikia kuniomba kuja kwenu wajuzi wa mambo kuulizia swala hili.

Jamaa stori yake huko nyuma ni kua amewai kua kwenye mahusiano na wanawake watatu nyakati tofauti tofauti, na wote sababu za kuachana nao ni kuwachoka na kutowahitaji tena muda mchache tu baada ya kukutana nao kimwili kwa mara mbili au tatu tu.

Nyakati hizo za nyuma alikua akihisi huenda alikua hajatokea kuwapenda ndomana pengine alikua akiwachoka haraka na kutowahitaji tena ila ni mpaka sasa ambapo yupo kwenye mahusiano na mwanamke mwingine ambae yeye anadai anampenda lakini katika hali ya ghafla amekua hana tena hamu ya kufanya nae mapenzi hata akiwa nae utupu chumbani, hali ambayo sio ya kawaida kabisa kwa sababu hana tatizo lolote la kiafya na ni mtu wa mazoezi.

Kwa dalili hizi moja kwa moja tumeona inawezekana ikawa huenda ana kitu tofauti kinachomsababishia hali hiyo. Na katika kujaribu kuuliza kwa mtu mmoja mwenye kufahamu mambo mengi kidogo, aliweka tiki pia kua dalili hizo zinakuaga ni za mtu mwenye jini mahaba.

Sasa lengo la uzi huu ni kutaka kufahamu zaidi kuhusu jini huyu mahaba, yani namna ya kumtoa na kuweza kujikinga nae wakati mwingine. NATANGULIZA SHUKRANI.
Mpeleke kwa ositazi amfanyie kisomo
 
Hakunaga vitu kama hivi sijui jini mahaba sijui popobawa. Ni story tu za vijiweni na mabarazani kupoteza muda na kusogeza siku watu wakishashiba kande na kuvimbiwa.

Msingi wa maisha ni kufanya kazi.
Mkuu kistaarabu iko hivi, hoja ama jambo lolote hukanushwa ama kubishaniwa kwa vielelezo vyenye mshiko.

Kuibuka tu na kusema: 'jambo hilo halipo' ni dalili za ubishi wa kiha.

Unakuta hata jambo lipo sahihi, ye'ababishana tu.

Kumbe nia ya ubishi huo lengo lake ni kutengeneza ligi ya kutafuta mshindi katika hoja inayoongelewa, yaani yeye mbishi hutafuta ubingwa kwa kubishana!

Mpaka leo hujiuliza, enhe ushindi anaoupata mbishi hulenga manufaa gani, maana hakuna mfadhili anayedhamini na kulipia ushindi wa ubishi huo!
 
Back
Top Bottom