Rafiki yangu wa ukubwani kafariki kisa ndoa

Rafiki yangu wa ukubwani kafariki kisa ndoa

Wajumbeeeeeee...

SIKIA hiiii......

Mwaka 2012 nilikutana na Dav (sio jina lake halisi) akiwa mkuu wa kitengo fulani ofisi kubwaa Morogoro.

Kipindi hicho mi nilienda ofisini kwao kufanya field.
Kwasababu yeye alikua mkuu wa kitengo nilichopangiwa field then nilimkubali sanaa mwana.

Alikua mchapa kazi balaaa na mtafuta hela hasaaa.

Kitengo kiling'ara kwasababu yake.

Maisha yake binafsi yalikua mazuri huku akimiliki nyumba na gari (simply kijana mwenye chenji zake).

Field ikaisha na Mimi nikasepa.

Ila urafiki uliendeleaa then ukapotea ghafla.

Baada ya muda bila kuwasiliana siku moja (mwaka jana) ghafla nikamkuta njiani.

Alikua kachoka balaaa, halafu ANATAFUTA KAZI..!!!

Dah ikabidi nisimamishe tukituki yangu ya miguu 4 apande kwenda sehemu kuongea.

Alikua kama kachanganyikiwa.

Nikampa lunch then nikampeleka gheto.

Alikaa gheto kama wiki hivi, then akasepa Dar.

Alichonihadithia....
1. Mwaka ule wa field yangu (2012) alioa.
2. Mkewe alimkuta Dav ana nyumba, gari, mashamba na Mali kibaoo.
3. Baada ya ndoa, miaka iliyofata maisha nyumbani yalianza kuwa magumu, kampuni ilikua ya wazungu. Then mkataba uliisha, wazungu wakarudi kwao, Dav akakosa permanent income.
4. Mkewe akachepuka na kuhamia kwa jamaa mpya mazima.
5. Mkewe alipeleka kesi mahakamani kuomba talaka.
6. Huko nako Dav alichosikia, mkewe alitembeza mbunye na pesa mpaka talaka ikatolewa.
7. Ilibidi gari na mashamba yauzwe iliwagawane na ndoa ivunjwe..!!!

Nikashangaa....

""Mbona hizi Mali ulizipata kabla ya ndoa??""

Alinijibu "hata sijui nini kilifanyika, na vile kuokoa watoto wangu (wawili) ilibidi nikubali liuzwe gari na mashamba ndio tugawane halafu nyumba abaki nayo akae na watoto"

Mwana alikua kama kachanganyikiwa.

Tuliongee akasema anaenda Dar kutafuta ajira na anashukia kwa Steve (sio jina lake halisi).

By accident Steve namjua sanaa (classmate).

Then siku ilivyofika nikampeleka stend akapanda ndinga huyoo Dar.

Yote haya yalitokea February/2021.

Leo yaani alifajiri hii napata taarifa kuwa "Davi kafariki kwasababu ya ugonjwa wa akili"

Steve anasema......
1. Dav alikuwa mwana Sana, tulicheza na kukua wotee kitaa
2. Kwasababu tupo field moja ya Kazi then tuliunda kama team ya kusaidiana kimawazo ya fani yenu.
3. Kila jambo, liwe jipya au gumu tunashirikishana.
4. Ila tokea aoe na kuanza matatizo ya ndoa performance ilishuka.
5. Kazi zikaisha
6. Mali zake zikauzwa
7. Alivyofika Dar alikua kama chizi, kutwa kuwataja wanae, mara aropoke majina ya mkewe kwa hasira na vitu kama hivyo.
8. Tarehe 01/08 hali ilikua mbaya hasa, akakimbizwa hospital.
9. Na leo 07/08/2021 Dav KAFARIKI kwasababu ya matatizo ya akili.

Dah....
1. Watoto wawili hawana baba Tena.
2. Kuna wazazi wamepoteza mpendwa wao mtoto wa kiume PEKEE.
3. Kuna sisi tumepoteza role model wa Kazi na rafiki.
4. Tasinia yetu ya science imepoteza MTALAAMU.
5. Tanzania imepungukiwa na GDP

Yoteee haya eti kisa mbunye..!!!
1. We unadhani angeamua kuwa single kama Mimi ANGEKUFA na NDOA?
2. We unadhani angeamua kum-HIT AND RUN huyo mkewe YANGETOKEA HAYA?
3. We unadhani ...........

Alidhani kuoa ni kuzuri KUMBE KUMEMTAFUTIA KIFO MAPEMA AKIWA NA MIAKA 39 tuuu.

Tafuta hela kijana kuoa ni upuuzi kwa dunia ya sasa.

Hawataki penzi lako ila WANATAKA HIZO MALI ZAKO.

They are GOLD DIGGERS, they need kuchimba dhahabu yotee kutoka kwenye huo mgodi wako then wauache empty.

Leo nipo gheto kusikiliza nyimbo alizozipenda Dav tuu...

RIP BROTHER.

""If you think money can't buy happiness, nenda kaulize ajira mpya walimu wiki hii walivyolipwa HELA ZAO KUJIKIMU na Halmashauri zao WALIJISIKIAJE""

View attachment 1883485

View attachment 1883489

Tafuta HELA kijana.

#YNWA
Ndoa yahitaji mwanaume UWE JAMBAZI kabisa, uamuzi wowote ndani uwe wako na siyo ndugu, mke wala majamaa
 
Mimi naombeni mnisaidie kujua hili swala

Hivi mimi nikioa saiv na huyo mwanamke akanikuta nimali zangu za kutosha ambazo nimezipat kabla yakuwa nae
Je tukiachana hizo mali tutazigawana wote japo nilitafut pekee yangu.
Pre-Marital contract...msainishe ili asiwe na chakuongea akienda mahakamani

Sent from my Infinix X5515 using JamiiForums mobile app
 
Kesi? Kuna koo flani wapo tauari wauze ng'ombe zote za ukoo mzima ndugu yao ashinde kesi..
Kuna Shida mahari.

Muwinda huwindwa

Wakati wewe unawinda mwanamke wa maisha yako atokee.- kuna mwanamke anakuwinda mwanaume aidha wa maisha ama wa kumvusha pale alipo kimaisha.

Kuna wanawake wanahitaji mbegu yako tu, yaan anakuja kwako kwa nia ya kuchukua mbegu tu. ( Anaweza kukushirikisha ama akafanya mission hii kimya na kwa usiri zaidi ya mossad ( hawa ni wengi na ikiwa mwema kwao watakuambia, ishanikuta kwa wanawake zaidi ya 7, wa nne walinichana na nashukuru kwa hilo, yaani yeye anataka mimba tu alafu basi, ila ni mtego huu. Na anaweza kuwa yupo ndani ya mahusiano na mtu ambaye anamtunza ama ndani ya ndoa na akaja kukuomba umtie mimba hata kwa malipo maalumu, naam anakununua umtie mimba na ni mke wa mtu.

Yupo yule anayekupenda kweli, wewe himpendi

Yupo yupo anayekutamani kimapenzi tu, lakini hastail kuwa mke na anajijua ila ukimletea habari za kumuoa hato kataa, ila sasa kwa kuwa ndoa kwake ni option C Huyu lazima atakusumbua na huyu mara nyingi ndio huwa anaondoa wanaume wengi duniani, ( Serial killer ) ukimkosea huyu, malipizi yake huwa mara tatu ya ulivyomfanyia.

Kuna wale waliotoa mimba zaid ya nne kabla ya kuwa na wewe, huyu sina hata muda wa kuelezea atakuzawadia nini siku ukimzingua, hawez kukuacha hiv hivi

Kuna wale wapenda tamaduni, wanawake wa mila na desturi, unakuwa nae kwa sababu kishakupumbaza na dawa za kutosha.

Kuna wale wanafki, mtu wa dini sanaa, kanisani sanaa, ushungi mkubwaa, ila hana huruma na wanawake wenzake ama watoto, yaan akiona mwanamke mwenzie anapitia magumu hashtuki apo ujue unaishi na Covid ndani.

Alaf wapo wanawake wanaofaa kuwa wanawake wa kuishi nao mpaka mwisho wa maisha yenu, hao sidhani kama wamefika hata million moja duniani kote na kama uko nae mwanamke wa hivi una bahati,

Niko na mmoja, uninizingua umemzingua yeye, ukinikosea basi umemkosea yeye na hakuna wa kumtuliza isipokuwa mimi, ana monitor matumizi yangu mpaka nakubali, japo kuna zile backup hazikosekani. Mwanamke anayekustua kuwa ukifanya jambo flani utakosea, hasubiri ukosee akukosoe bali anakuelekeza mashaka yake na mwenendo wako mapema iwezekanavyo, mwanamke ambaye huwezi ficha jambo maana akikuangalia tu anajua unajambo na hujaliweka wazi, anatafta namna ya kukufanya uliseme kwa kujiamini na akushauri kama inawezekana...

Pamoja na yoote binaadam hakuna mkamilifu, yeye anaweza kuwa muaminifu kwa kila kitu, mm nikawa mshenzi vile vile au kinyume chake..

HAPO KWENYE KUGAWANA MALI HAPO, HAPO KWENYE MALI ALIZOZIKUTA HAPO...WENGI WANATUTOA ROHO.

KISA WATOTO ALAFU UNAWEZA KUKUTA HUNA MTOTO HATA MMOJA KATIKA HAO WATOTO WAKO.. WAMEZALIWA NDANI YA NYUMBA YAKO, WAPO WANNE PENGINE WAKO NI MMOJA AMA HATA HUYO MMOJA SI WAKO LABDA WA NDUGU YAKO.
 
Na wangu alitaka kujiua kwa bahati nzuri maziwa na majirani walikuwa karibu.Nilimchana live,usilete nuksi mjini,ufe kwa ajili yangu,mimi nisiyenduguyo,huwez fikiria tabu alizopata mother wako mpaka umefika hapa?

Huwez waza maumivu atakayopata mama ako ukifa? Embu itazame sura yangu vizuri je hujutii kutaka kujiua sababu yangu ambaye siingii hata mara moja kwa warembo utakaowaacha duniani na wenye kiu kweli ya ndoa?

NAONA ALINIELEWA MAANA NAONA HATA KUPIGAPIGA SIMU KUWAJULIA HALI WATOTO KAPUNGUZA.Ndo nitajua sijui safari hii,sijui nilianzajeanzaje kumsanua...nadhani kabla ya kumchana alikuwa ananiona mimi tu dunian sasa sijui huko anafanyaje eti?
Duu! Kwahiyo ulimfiligisa mwenzio mpaka akaona bora ajitoe uhai? Ina maaana ile ndoa yako ya mbwembwe nyingi imeshavunjika mara hi?

Binafsi bado naamini watu wema wapo wengi tu tena sana kushinda hao wabaya cha muhimu ni kufanya tafiti za kutosha kabla ya kuamua.
 
Utawapataje bila kusex?
Kwahyo utasex kavu na kila mwanamke unayemuona ili upate watoto?

Na nyumbani nani atakuwa msaidizi wako ktk hali na Mali

Ndugu yangu usijidanganye ukajiona ni mzima wa afya.
Unaweza ukabanwa usiku ukakosa hata mtu wa kuomba maji.

Ukajifia week nzima ndani ,,
watu wanapata taarifa kwa harufu unayotoa chumbani kwako.
Usidhani watu wanaoa kwa lengo la kusex pekee.
Mke ni zaidi ya sex .

Kuna tatizo,,linaweza kukukuta ghafla ukakosa hata wa kutoa taarifa haraka usaidiwe.

Mtu akishakuwa over 50 bila mke au kuishi na family ni tatizo kubwa sn.
Na hili limemtokea ndugu wa jamaa yangu,yeye huyo mwamba alikua anaishi na mke lakini mkorofi balaa na ni mgonjwa wa kifafa,yule mkewe alikua mvumilivu kweli kweli na ndio alikua msaada mkubwa kila alipokua ana anguka kwa kumgeuza ili asipate madhara.
Lakini stori za vijiweni mwamba akaanza kumfanyia vituko mkewe kwa kumtembezea kichapo cha nguvu bila ya sababu za msingi kwa mujibu wa majirani waliokua wanaishi nao. Basi mwisho mwamba akalazimisha akampa talaka ili apate kuingiza migoma,na kweli alifanikiwa hilo akawa anabadilisha tu.
Baada ya mda kama wa siku nne hivi mwamba akawa haonekani,kwenye mishe wanasema yupo home,ndugu wanasema yupo kazini na majirani nao wanasema mwamba anapambana hivyo kila mtu akawa na jibu lake mpaka pale harufu ya mzoga ilipoanza kusikika wakaja kuvunja mlango wakamkuta mwamba amelala kifudifudi ameng'ata godoro,kwa mujibu wa madaktari alikutwa na kifafa hivyo akashindwa kujigeuza na ndizo nyakati kama hizo mkewe alikua anamgeuza.
 
Inasikitisha sana.

Ila naamini Dav alikosa ushauri mzuri. Pengine angeweza bakiza sehemu kubwa sana ya mali zake upande wake na kiasi kidogo kwenda kwa mtalaka wake. Sababu kama ulivyoeleza sehemu kubwa ya mali zake alizipata kabla ya kuoana na huyo mwanamke.

Pia, hatuwezi jua Mapenzi yalimchota Dav kiasi gani, usikute aliharibu kwenye madocuments huko kuweka majina ya mkewe kisa mapenzi.

Nakumbuka Mimi kabla sijaoa watu wazima niliowashirikisha walinisisitiza sana nisije kujiona nimepata dhahabu au malaika hadi ikapelekea kufanya maamuzi ya kunigharimu hapo baadae. Wala huyo mke asije kuwa sababu ya kukaa mbali na ndugu zako. Mke anaweza kukutema muda wowote lakini ndugu zako wa damu na wazazi sio rahisi. Hivyo nisije ruhusu mke akaniweka mbali na wazazi na ndugu zangu wa karibu.

Mwingine alienda mbali zaidi akasema kwani unajua kabla yako wewe huyo mkeo ameshagongwa na wanaume wangapi?? Na una uhakika gani kwamba wewe ndio unamkaza vizuuuri kuliko hao wote waliokutangulia?? So usijione umepata dhahabu sana hadi ukajitenga na watu wako wa siku zote. Yeye ana sababu zake za kukubali kuolewa na wewe ambazo unaweza usizijue. Mwisho akasema nenda ujenge ndoa yako na jitahidi usiwe chanzo cha mgogoro kati yako na mkeo lakini usisahau kudumisha mahusioano na ndugu zako. Mwanamke anabadirika muda wowote, biblia yenyewe imeseza ishi nao kwa akili.

Mwingine mdada aliniambia, ni ngumu sana mdada kugomea ndoa kama anaona maisha unayo. So wewe mwanaume unayechagua ndio unatakiwa utulize sana akili.

Hivyo napata shida kutokuona role ya ndugu zake Dav katika story yako. Je alikaa mbali nao?
Kwani kitu gani kinaweza kuwa ushahidi pale mnapotalakiana kitakachoonesha kuwa Mali hizi na hizi mwanaume alizipata Kabla ya kuoana na Mali hizi zilipatikana mkiwa mmesha oana?
 
,"nliongeza nyumba za kupangisha tu nkiwa nae"
Unaijua the so called the law of marriage Act? Nenda ukasome s. 160
Inshort chochote ulichokifanya ukiwa nae haijarishi alichangia au lah lazima mgawane.

Afu usiwe na kinyongo na mali zako oa mwanamke anaejitambua na anajua sheria inasemaje, mambo ya mali ukishakufa wanakula watakao baki.

Omba uwe na mke anaejielewa hizo mali hata uandike majina ya wazazi wako haina mantiki

Think about living a happy life thats all.
Hilo najua ila wanaojielewa ni wachache sana wengi wako aftermoney....nimeona wengi wamefariki wajane wanafuja mali kwa kulea wanaume...mimi naona kipimo kizuri cha ndoa ni mda mrefu mtakao ishi
 
Mimi nasemaga siku nafukuzwa kazi au biashara yangu kwenda mrama na kazni namefukuzwa aisee mwanamke wangu hataniona kamwe Bora unyanyaswe na mhindi kwenye kazi zake kuliko mwanamke unayelala naye kitanda kimoja hutakaa Kwa Amani maisha yako yote na itakuumiza siku zotee
 
Haawa viumbe bwana ...wakikupanda lazma utakuwa chizi ...
Mimi it was half way nilipandwa walionizunguka wakijua Hilo ..Mimi pekee yangu ndo nilijiona najua kubembeleza ndoa...

Siku Moja niliwaza siku nzima mpaka saa Kuni usiku nimekaa bar napiga via mdo mdo .huyu mwanamke hata kuniuliza uko wapi hakuna Ila yupo online nk...na hapo kulikuwa na ma skendo mengi niliyapuuzia ... Nikaamua siku hiyo hiyo navunja ndoa TU kiroho safi nimuombe tuachane maisha yasonge

Akaelewa kwel kiroho safi

ASE long story short week baada ya hii transition nikawa natafuta sehem ya kupanga Ila nalala chumba Cha wagen ..hata watoto wahaelewi mchezo...bwana bwana jioni asimlete uyo jamaa niliesikia ana chepuka nae..kaja kusalimia..
Mimi huwa kikaz nipo mkoa jirani..Kwa mwez unakuta nashinda kama week TU...
Aseee nikaliita jembe langu first born kumuuliza vyema..uyu anko mnamfaham..akasema anakujaga kusalimia..afu alituletea tv baada ya Ile kuvunjika(Kuna tv Walivunja madogo..nilimuagiza mama Yao atafute nyingine nitume Hela akapata nikalipia direct Sasa uyu mwanamke alimshtua mwamba apitie apeleke home )

Aahhh niliagiza watoto waende Kwa shangazi na dada wa kazi...
Yule jamaa nikamwambia ntakuua sepa..kwakuwa sikuwahi kupiga yule mwanamke..alijiamini kabisa hatoguswa...
Mtume walaiii hatokuja sahau...nilimtwanga yule mwanamke siku Ile...aliuguzwa mwezi mzima..nilitoka nikaenda polis nikakaa kama siku tatu...mpaka msala umeisha talaka juu ...

Nikasepa nikaanza upya..marafiki na ndugu walinitia moyo Sana ..niliacha Kila kitu ..

Miaka mitano baadae nimebarikiwa mtoto mwingine kakiwanja na gari Yan maisha matam Nina ka mwanamke kabich mno Hela hizi ..yule chizi nae kazaa uko na yule mpuuz wake..wanangu mmoja nakaa nae mmoja anakaa nae .Ila naona nae anamshinda ntamchukua tu
Hao viumbe ukiwa dhaifu unaweza kuharibu maisha yako kabisa,kumpa ukilema,kuua ...mtu umemkuta n papa lake hana undgu nawe eti unaogopa kumuacha watoto watateseka,fukuza songa mbele
 
Hili jambo hata wewe ukioa itakuwa hivyo hivyo unajua kwa nini?

Ukiwa na mke unamchoka hutombi kila siku wakati wao huwa hawana kukinai kwa hiyo hapo snaziba gap.

Pili kadiri mwanaume unavyokua kiumri na kimajukumu uwezo wa kutiana unapungua wakati mwanamke wala sasa hapo ni kuziba gap tuu.

Binafsi sina shida na hilo jambo ila tuu nisijue afu siku zote vya kuiba vitamu hata wanaume wanachepuka vya pembeni.
Mkuu kwa ke unayempenda kiukweli unaweza kumuacha baada ya kumfumania Mara ngapi ?.
 
Na hili limemtokea ndugu wa jamaa yangu,yeye huyo mwamba alikua anaishi na mke lakini mkorofi balaa na ni mgonjwa wa kifafa,yule mkewe alikua mvumilivu kweli kweli na ndio alikua msaada mkubwa kila alipokua ana anguka kwa kumgeuza ili asipate madhara.
Lakini stori za vijiweni mwamba akaanza kumfanyia vituko mkewe kwa kumtembezea kichapo cha nguvu bila ya sababu za msingi kwa mujibu wa majirani waliokua wanaishi nao. Basi mwisho mwamba akalazimisha akampa talaka ili apate kuingiza migoma,na kweli alifanikiwa hilo akawa anabadilisha tu.
Baada ya mda kama wa siku nne hivi mwamba akawa haonekani,kwenye mishe wanasema yupo home,ndugu wanasema yupo kazini na majirani nao wanasema mwamba anapambana hivyo kila mtu akawa na jibu lake mpaka pale harufu ya mzoga ilipoanza kusikika wakaja kuvunja mlango wakamkuta mwamba amelala kifudifudi ameng'ata godoro,kwa mujibu wa madaktari alikutwa na kifafa hivyo akashindwa kujigeuza na ndizo nyakati kama hizo mkewe alikua anamgeuza.
Hayo ndy madhara ya kuishi peke yako bila mke.
Ahsante mkuu kwa ushuhuda.
 
Wajumbeeeeeee...

SIKIA hiiii......

Mwaka 2012 nilikutana na Dav (sio jina lake halisi) akiwa mkuu wa kitengo fulani ofisi kubwaa Morogoro.
Karibia initokee na mimi ila EMAUS ikaniokoa ilifikia stage father toka Ghana akaniambia sio kwamba watumishi ni waganga wa kienyeji wa kupiga ramri na kukutatulia matatizo yako Faith and time heal
 
Duu! Kwahiyo ulimfiligisa mwenzio mpaka akaona bora ajitoe uhai? Ina maaana ile ndoa yako ya mbwembwe nyingi imeshavunjika mara hi?

Binafsi bado naamini watu wema wapo wengi tu tena sana kushinda hao wabaya cha muhimu ni kufanya tafiti za kutosha kabla ya kuamua.
Bado niko nae, namwogopajee
 
Back
Top Bottom