Raila Odinga ana hoja,Tume imeteleza. Fomu 34A na 34B zipo kisheria

Raila Odinga ana hoja,Tume imeteleza. Fomu 34A na 34B zipo kisheria

Raila naye ifike mahali aache kugombea, mara nne zote looh! hana bahati na hiyo kazi ya urais.
 
Mgombea wa Urais wa Kenya kupitia NASA,Raila Odinga amejitokeza na kupinga matokeo ya awali ya Urais ya Kenya yanayotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya yakimweka mbele Rais Uhuru Kenyatta.

Hoja ya Odinga ni kukosekana kwa Fomu 34A na 34B zinazopaswa kujazwa na kusainiwa,ikiwa ni pamoja na mawakala, kisheria kabla ya kutangazwa matokeo. Fomu 34A hujazwa na kusainiwa katika Kituo cha Kupigia kura. Kimsingi,Fomu 34A hubeba taarifa za kura za kituo kimoja.

Fomu 34A huwasilishwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo. Taarifa zote za vituo vya Jimbo husika hujazwa kwenye Fomu 34B. Hatimaye,Fomu 34B huwasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi kwa ajili ya kutangazwa matokeo rasmi.

Kujazwa kwa Fomu nilizozitaja,ni sharti la kisheria. Lazima kuzijaza na kuziwasilisha. Inataarifiwa kuwa Tume ya Uchaguzi ilitangaza matokeo bila Fomu 34A na 34B. Kwasasa,Tume inakusanya Fomu wakati matokeo yameshatangazwa na kubishiwa.

Hivyo,Odinga ana hoja ya kisheria kuyabishia matokeo hayo. Je,atayapinga matokeo ya Urais kisheria au kisiasa? Matokeo yaliyotangazwa bila fomu husika yanabakije kama halali? Raila Odinga ataamua muda ukifika.Kwa mujibu wa Katiba ya Kenya,Tume ya Uchaguzi ina siku 7 kumtangaza mshindi wa Urais.


Mkuu uliambiwa 34A na 34B hazipo???

Mkuu wewe umesoma lakini siamini kwenye hili kama ulijiridhisha kuwa hizo form hazipo kabla ya kuandika.

Hata tume ya Uchaguzi jana imesema itafanya mahesabu kupiti form hizo sasa hii yako kuwa form hazipo umelitoa wapi?
 
Mkuu uliambiwa 34A na 34B hazipo???

Mkuu wewe umesoma lakini siamini kwenye hili kama ulijiridhisha kuwa hizo form hazipo kabla ya kuandika.

Hata tume ya Uchaguzi jana imesema itafanya mahesabu kupiti form hizo sasa hii yako kuwa form hazipo umelitoa wapi?
Mkuu, sikusema fomu hazipo. Nimesema, matokeo yalitangazwa kabla ya fomu kuwasilishwa kwa Tume. Ndiyo hoja ya Raila
 
Ukweli Ambao Upinzani hawataki kuusikia ndio huu.Huwezi kutenganisha tume ya uchaguzi na Uongozi uliopo madarakani kwa nchi zetu hizi.

Raila hawezi kuwa Rais hata kama ameshinda.Ukweli mchungu kwake.
Mbona nchi nyingine za Afrika wameweza? Nchi kama Ghana, Zambia, Nijeria, Malawi n.k.Hiyo conclusion ibaki tu east Afrika siyo Afrika nzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa Fomu No. 34 Raila na NASA wako sahihi. Je suala la Udukuzi wa tume ya IEBC,huu udukuzi kupataje kama nae hajadukua? Kwa nini aseme leo siku ya kutangaza Matokeo wakati Kifo cha Chris Msando kimetokea juma 1 lilipita?
Sasa kama matokeo yanayotangazwa na tume ni tofauti na yaliyopo kwenye form maanake nini si kwamba either servers na iebc zimeingiliwa au iebc wanafanya makusudi. Tatizo tunarukia tu hoja bila kufuatilia mambo yalivyo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, sikusema fomu hazipo. Nimesema, matokeo yalitangazwa kabla ya fomu kuwasilishwa kwa Tume. Ndiyo hoja ya Raila


Sawa mkuu nimekuelewa lakini kwenye huo mstari hapo chini ndiyo uliozua hoja yangu.

"Hoja ya Odinga ni kukosekana kwa Fomu 34A na 34B zinazopaswa kujazwa na kusainiwa......."

Form zipo ila huyu mzee anataka kuingia tena serikalini kupitia mlango wa nyuma kama mwanzo
 
Niliacha kufuatilia haya matokeo baada ya IEBC kusema Hayo matokeo ni "provisional".....
 
Scanned copy ya matokeo ndio inayochakachuliwa wakati wa kutransmit! Hivyo kuhakiki scanned copy sio suluhu! Watumie original forms kutoka kwenye vituo vya kupigia kura! Ikiwa Odinga ni mwongo achukuliwe hatua kali za kisheria kwa uchochezi!

If you know your enemy than yourself you shall never suffer a defeat
 
Mbona Jana walisema zipo na matokeo yanayotangazwa yanatoka kwa hizo fomu
Pia wakawakaribisha wanaotaka kuhakiki waende
Ila wakasisitiza kuwa matokeo ni ya awali yanaweza badilika aliye chini akaja juu maana vituo vyote havijahesabiwa
 
Naomba niende kinyume na wewe tume huru ni dhana, ila uhalisia wake haupo katika maana/dhana/definition ila upo katika utendaji kazi wake kwa maana uhuru/kutoingiliwa, uwazi, effeciecy ya kumudu majukumu ya kichaguzi, usawa/fairness na mwisho kabisa uundwaji wake/upatikanaji wake na udhibiti wake kwa maana ya vyombo kama mahakama huru au kamati zibiti za ambazo zitakuwa shirikishi za wanufaika wa chaguzi. Tume ikitimiziwa haya inaweza kuwa huru.

Tume huru ni kitu cha kufikirika tu.
 
Tatizo nini Mkuu? Punguza jazba na chuki
Tatizo anataka na wewe utumie akili za bendera kufuata upepo bila kutumia akili yako uliyoipata kutoka kwa Mungu. Huyu jamaa akiambiwa na Lissu avue nguo atembee uchi atafanya hivyo maana akili yake imemuambia kila asemacho Lissu ni sawa. Kuna watu humu wanafanya nijitoe tena JF
 
Tatizo anataka na wewe utumie akili za bendera kufuata upepo bila kutumia akili yako uliyoipata kutoka kwa Mungu. Huyu jamaa akiambiwa na Lissu avue nguo atembee uchi atafanya hivyo maana akili yake imemuambia kila asemacho Lissu ni sawa. Kuna watu humu wanafanya nijitoe tena JF
Usitoke mtani,tuwajibu kwa hoja.
 
Mgombea wa Urais wa Kenya kupitia NASA,Raila Odinga amejitokeza na kupinga matokeo ya awali ya Urais ya Kenya yanayotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya yakimweka mbele Rais Uhuru Kenyatta.

Hoja ya Odinga ni kukosekana kwa Fomu 34A na 34B zinazopaswa kujazwa na kusainiwa,ikiwa ni pamoja na mawakala, kisheria kabla ya kutangazwa matokeo. Fomu 34A hujazwa na kusainiwa katika Kituo cha Kupigia kura. Kimsingi,Fomu 34A hubeba taarifa za kura za kituo kimoja.

Fomu 34A huwasilishwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo. Taarifa zote za vituo vya Jimbo husika hujazwa kwenye Fomu 34B. Hatimaye,Fomu 34B huwasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi kwa ajili ya kutangazwa matokeo rasmi.

Kujazwa kwa Fomu nilizozitaja,ni sharti la kisheria. Lazima kuzijaza na kuziwasilisha. Inataarifiwa kuwa Tume ya Uchaguzi ilitangaza matokeo bila Fomu 34A na 34B. Kwasasa,Tume inakusanya Fomu wakati matokeo yameshatangazwa na kubishiwa.

Hivyo,Odinga ana hoja ya kisheria kuyabishia matokeo hayo. Je,atayapinga matokeo ya Urais kisheria au kisiasa? Matokeo yaliyotangazwa bila fomu husika yanabakije kama halali? Raila Odinga ataamua muda ukifika.Kwa mujibu wa Katiba ya Kenya,Tume ya Uchaguzi ina siku 7 kumtangaza mshindi wa Urais.
Nani amekwambia kwamba matokeo ya uchaguzi yaliyo tangazwa hayakuwa kutoka ktk hizo form nchi nzima kama tume inavyotakiwa na katiba ya Kenya? Msilete visingizio vya uwongo vya Raila

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Raila anaonekana hataki kukubali matokeo., ni.wakati sasa Rais Magufuli ambaye ni rafiki yake binafsi ajitenge na kusema hamuungi mkono tusikie

Sisi watanzania hatutaki vurugu zitokee Kenya , Aige mfano wa.Edward lowassa ambaye pamoja na ushahidi wa kuibiwa kura kuwepo na vituo vya Tallying centre vya Chadema kuvamiwa na vijana kama 100 wataalamu wa IT kuwekwa ndani bado alijizuia na..kukaa kimya pamoja na wananchi..kuwa tayari kupigania ushindi na...kuandamana kupinga Magufuli kuiba...kura .

Ni unafiki kama...yeye Lowassa hajamzuia...kutawala asimshauri huyo rafiki yake amuache Uhuru...atawale.
Kwanza Raila pia alishiriki kuibia watanzania kura mwaka 2015,..akimtuma.msaidizi wake mmoja...kuongoza timu.ya IT ILIYOKUWA.DOUBLE TREE HOTEL..na kumeletea rafiki..yake pesa za kampeni

Bora wakenya mmemuadhibu Raila . mnhetawaliwa kwa visasi kama..huko Tanzania
Pia raila ni..project ya muda...mrefu...ya kutawala afrika mashariki ya Kagame na Museveni...tayari wamekamata Congo kupitia Kabila.
TANZANIA tumeshatekwa..kupitia..huyu..ndugu yao mwaka 2015 na walitaka kutumia Raila kuteka Kenya
THE BAHIMA EMPIRE SYNDICATE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom