Rais akikosea aambiwe ukweli hadi aelewe

Rais akikosea aambiwe ukweli hadi aelewe

Nchi yetu inaribiwa na ushabiki wa kisiasa, Kwenye maswala muhimu kama haya hatuna umoja, Upinzani ukipinga hili vijana na wanachama wa chama tawala wataingia kati kulisapoti hata kama lina madhara
 
Kuna vitu hamuelewani na huyo
Unaposema mwaka Jana madini yaliingiza $3 billion, unamaanisha nn? Hii ni trllion 8.4
Na hiyo utalii ni trillion 9, jumla trillion 18. Kwa mwaka makusanyo yetu ni trllion 26, hapo si ingekua maji bure, umeme bure, matibabu bure😂😂😂

Huyo anazungumzja government revenues, mapato serikali inayopata kutoka kwenye madini. Mapato ya serikali kwa mwaka kutoka kwenye madini kwa sasa ni around bilioni 700
Kwahiyo fedha za kigeni sio mapato.....

Ni kama market cap flani hivi
 
Lakini kwani huwezi chimba Madini katika namna ya kudhibiti uharibifu wa mazingira na baadae mbuga kurejesha uoto?
Uchimbaji madini unaambatana na matumizi ya kemikali, makundi makubwa ya watu, ukataji miti ovyo, jambo hilo litaleta usumbufu mkubwa kwa viumbe wanaoishi hifadhini na wengi wataangamia.
Hifadhi zetu ziachwe na jukumu lake moja tu.
Mwambieni mama aachane na shuguli za kibinadamu hifadhini.
 
Uchimbaji madini unaambatana na matumizi ya kemikali, makundi makubwa ya watu, ukataji miti ovyo, jambo hilo litaleta usumbufu mkubwa kwa viumbe wanaoishi hifadhini na wengi wataangamia.
Hifadhi zetu ziachwe na jukumu lake moja tu.
Mwambieni mama aachane na shuguli za kibinadamu hifadhini.
Ndio maana ya EIA ,kabla ya kufanya hivyo lazima hiyo kitunifanyike kuonesha namna ikolojia italindwa.

Kwani ni Tanzania pekee ndio wa kwanza kuchimba Madini hitadhini? Huko Amazon inafanyika hivyo na kwingine.

Sijaona hoja ya msingi yaani Kila kitu ni kupinga tuu.

Bwawa la Nyerere limefanyika hitadhini na hakuna kilichoharibika.
 
Huko nyuma baadhi ya watu walisema hiyo wizara kupewa Mavunde sio bure kuna kitu wanatengeneza.

Huyu mama ni predictable ukiona mtu anapewa majukumu ambayo kama vile makubwa kwake, basi ana mikakati yake huko.

Ghafla Kijaji nae mazingira wawekezaji wasisumbuliwe huko na process ndefu za environmental impact assessment.
 
Ndio maana ya EIA ,kabla ya kufanya hivyo lazima hiyo kitunifanyike kuonesha namna ikolojia italindwa.

Kwani ni Tanzania pekee ndio wa kwanza kuchimba Madini hitadhini? Huko Amazon inafanyika hivyo na kwingine.

Sijaona hoja ya msingi yaani Kila kitu ni kupinga tuu.

Bwawa la Nyerere limefanyika hitadhini na hakuna kilichoharibika.
We chawa, huwezi linganisha bwawa la umeme na mgodi wa madini...kimadhara, ni vitu viwili tofauti kabisa.
Jielimishe!.
 
Wakati wa Magufuli niliwahi andika hapa kama Magufuli anao watu wa kumwambia ukweli na akawasikiliza, nilitoa mfano wa Fidel Castro alivyokuwa anaogopwa na watu wengi sana lakini walikuwepo watu wawili walikuwa wana uwezo wa kumwambia ukweli Raul Castro mdogo wake na Comrade Che Guevara. Hawa wawili walikuwa na uwezo wa kumwambia ukweli na makosa yake bila kupepesa macho na akawasikiliza.

Juzi Rais Samia kasema madini yachimbwe kwenye mbuga, cha muhimu hela. Hii kauli si sahihi kabisa tena sio sahihi kutoka kwa Rais wa nchi.

Rais alipaswa kwanza kupata elimu ya kutosha kuhusu uchimbaji wa madini na athari za mazingira, lakini la muhimu zaidi alipaswa kuniuliza kwanini Viongozi kabla yake wote walisita au kukataa kutoa vibali vya kuchimba Mbugani?

Je hata kama tukikubaliana na Rais cha muhimu hela, kwani Rais hajui utalii ndo unaingiza hela Tanzania kupita madini?

Rais hajui au hana ushauri wa kumwambia kuwa athari za kimazingira huko Mbugani zinaweza moja Kwa moja kuathiri utalii na kupunguza mapato kuliko hata kuongeza hayo mapato?

Rais hajui kuwa hayo makampuni ya madini huwa yanaahidi sana mambo mengi mazuri lakini mwisho hushindwa kutekeleza kuanzia Kodi hadi taratibu za kulinda hayo mazingira? Kampuni ya madini inaweza sababisha sumu kwenye vyanzo vya maji ya wanyama hadi binadamu, na hili sio nadharia imewahi tokea na ushahidi upo.

Madini yanaweza chimbwa yakaisha na mapato ya maana yasipatikane, imeshatokea..na haitakuwa la ajabu ikitokea tena.

Mbuga za Wanyama zilzopo Tanzania haipatikani tena kwingine duniani, ni urithi wa dunia. Mbuga kama Serengeti ina Wanyama Wengi kupitia Mbuga yeyote duniani, hii Peke yake ni dhahabu kuliko dhahabu yenyewe.

Mbuga kama Selous ukubwa wa Ardhi tu ni zaidi ya nchi ya Belgium, halafu leo tunaanza tena kuruhusu uharibifu wa mazingira Mbugani mradi ipatikane hela? tuharibu kuku anaetotoa mayai ya dhahabu ili tukatafute mayai mengine tumboni?

Rais akikosea aambiwe hadi aelewe.
Nasikia wamebadilisha pori sasa hivi wanakuepeleka makaburini moja kwa moja
 
Katiba, kumpa Raisi maamuzi makubwa kama nchi ni yake binafsi, ndiyo haya. Mimi naona kwa vyote alivyofanya. Na aina ya wananchi wa Tanzania, ambao wanaendekeza ushabiki wa kisiasa kwa tujipesa.

Ni bora tukae kimya tu, akimaliza kwenye mbuga, amalizie na sehemu ya misitu iliyobaki, akimaliza Rasilimali zote. Ahamie na makazi ya watu, abomoe nyumba zote awape wawekezaji. Watanzania si wanaona sasa hayawahusu. Naomba ifike huko, sijawahi ona watu aina ya watanzania. 🤬
 
We chawa, huwezi linganisha bwawa la umeme na mgodi wa madini...kimadhara, ni vitu viwili tofauti kabisa.
Jielimishe!.
Una uhakika? Kwamba Kuna mgodi ambao utawekezwa Kwa Trilioni 7 hapo Serengeti? Acha upuuzi.

Harafu kazi za uchenjuajinhiwa zinafanyika Nje ya Hifadhi sio ndani,vitu hamjui ila mnapayuka tuu.

Nimewauliza na Tzn tuu ndio Madini yanachombwa hifadhini?
 
Wakati wa Magufuli niliwahi andika hapa kama Magufuli anao watu wa kumwambia ukweli na akawasikiliza, nilitoa mfano wa Fidel Castro alivyokuwa anaogopwa na watu wengi sana lakini walikuwepo watu wawili walikuwa wana uwezo wa kumwambia ukweli Raul Castro mdogo wake na Comrade Che Guevara. Hawa wawili walikuwa na uwezo wa kumwambia ukweli na makosa yake bila kupepesa macho na akawasikiliza.

Juzi Rais Samia kasema madini yachimbwe kwenye mbuga, cha muhimu hela. Hii kauli si sahihi kabisa tena sio sahihi kutoka kwa Rais wa nchi.

Rais alipaswa kwanza kupata elimu ya kutosha kuhusu uchimbaji wa madini na athari za mazingira, lakini la muhimu zaidi alipaswa kuniuliza kwanini Viongozi kabla yake wote walisita au kukataa kutoa vibali vya kuchimba Mbugani?

Je hata kama tukikubaliana na Rais cha muhimu hela, kwani Rais hajui utalii ndo unaingiza hela Tanzania kupita madini?

Rais hajui au hana ushauri wa kumwambia kuwa athari za kimazingira huko Mbugani zinaweza moja Kwa moja kuathiri utalii na kupunguza mapato kuliko hata kuongeza hayo mapato?

Rais hajui kuwa hayo makampuni ya madini huwa yanaahidi sana mambo mengi mazuri lakini mwisho hushindwa kutekeleza kuanzia Kodi hadi taratibu za kulinda hayo mazingira? Kampuni ya madini inaweza sababisha sumu kwenye vyanzo vya maji ya wanyama hadi binadamu, na hili sio nadharia imewahi tokea na ushahidi upo.

Madini yanaweza chimbwa yakaisha na mapato ya maana yasipatikane, imeshatokea..na haitakuwa la ajabu ikitokea tena.

Mbuga za Wanyama zilzopo Tanzania haipatikani tena kwingine duniani, ni urithi wa dunia. Mbuga kama Serengeti ina Wanyama Wengi kupitia Mbuga yeyote duniani, hii Peke yake ni dhahabu kuliko dhahabu yenyewe.

Mbuga kama Selous ukubwa wa Ardhi tu ni zaidi ya nchi ya Belgium, halafu leo tunaanza tena kuruhusu uharibifu wa mazingira Mbugani mradi ipatikane hela? tuharibu kuku anaetotoa mayai ya dhahabu ili tukatafute mayai mengine tumboni?

Rais akikosea aambiwe hadi aelewe.
Huyu akichimba madini Serengeti halafu dunia nzima ikasusa kuja Tanzania ndiyo atajua hajui.
 
labda hata hakumbuki na wala hajui kama alisema hivyo, mambo ya kuandikiwa hotuba kusoma tu kukamilisha ratiba, ndo maana namkubali D.Trump yeye anakwenda offscript hivyo anasema kile anachokiamini na kilicho moyoni mwake …
 
Back
Top Bottom