Hii Story niliisoma jana kwenye hilo gazeti la Raia Mwema nikabaki najiuliza hivi ni nani hasa huwa mshauri wa Rais, au labda tusimlaumu mshauri tumlaumu JK mwenyewe.........Kiukweli arais wetu, haeleweki wala kutabirika anabadilika kila sekunde utadhani mshale wa saa, kama kuna sehemu ambayo niliona JK angetengeneza jina pengine kupita waliomtangulia ukimuacha Nyerere ni kwenye hili suala la Katiba, lakini matokeo yake ndio kavurunda na kusiriba jina lake na lami ili lisisomeke kabisa siku zijazo.
Hapa ndio najiuliza huwa anashauriwa au ndio anachanganya na zake mpk zinapitiliza? sipati picha Jaji Warioba yupo katika hali gani kwa sasa, yeye na Tume yake.