Pre GE2025 Rais Dkt. Mwinyi achangia milioni 100 ukarabati wa Kanisa Katoliki Zanzibar

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuimarisha Uhuru wa Kuabudu na kuziagiza Taasisi za Kidini kuendelea kuiombea Nchi amani na umoja.

Rais Dk, Mwinyi amefahamisha kuwa Taasisi za kidini zina wajibu mkubwa wa kushirikiana na Serikali na kuunga mkono juhudi za kuleta amani, umoja na mshikamano wa Watanzania.

Rais Dk, Mwinyi ameyasema hayo leo October 27, 2024 alipoongea katika Maombi maalum ya kumpongeza Askofu Agustino Shao kwa utume wake katika Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar na maombi kwa Taifa iliyofanyika Viwanja vya Mao Tse Tung Mkoa wa Mjini Magharibi.

Rais Dk.Mwinyi amechangia Tsh. milioni 100 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk, Samia Suluhu Hassan amechangia Tsh. milioni 50 kwa ajili ya ukarabati wa Kanisa la Mtakatifu Joseph liliopo Shangani Wilaya ya Mjini.
Your browser is not able to display this video.
Soma, Pia
+ Rais Samia Achangia Milioni 100 katika Ujenzi wa Kanisa la AICT
+ Rais Samia achangia shilingi milioni 50, ujenzi wa shule ya Msingi na ujenzi wa majengo ya Zahanati inayomilikiwa na Bakwata Simiyu
 
Wabatizwe hawa watu na kupokea komunio na kipaimara.
 
Katoliki wanapenda chapa sana!
 
Pokeeni tu, ni pesa zetu hizo.

Hashim Rungwe anasema, wakituita wanatugaia pesa, na tunapokea hatukatai, ni pesa zetu hizo.

Huna namna ya kula pesa zao kama hakuna uchaguzi.
 
Bila amejumuika kwenye karamu ya Bwana jioni ..Muda si mrefu atashiriki KITI......MO
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…