Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza ofa ya kipekee kwa watanzania kuiona mechi ya timu ya taifa, Taifa Stars, bila malipo. Ofa hii inalenga kuongeza hamasa kwa wapenzi wa soka nchini katika kipindi hiki kigumu baada ya tukio la kusikitisha la kuporomoka kwa jengo katika eneo la Kariakoo.
Soma: Mwana FA: Ushindi wa Taifa Stars ni maalum kwa Rais Dkt. Samia Suluhu
Kwa upande wake, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeungana na Rais kutoa pole kwa waathirika wa tukio hilo pamoja na familia za waliopoteza maisha. Taarifa hiyo imetolewa na Afisa Habari wa TFF, Cliford Marion Dimbo, akibainisha kuwa Shirikisho limeguswa sana na tukio hilo na linaendelea kusimama pamoja na watanzania wote wakati huu wa majonzi.
Wakati taifa likiendelea kuomboleza, hatua hizi zimeonekana kuwa faraja kwa wapenzi wa soka na wananchi kwa ujumla.
Soma: Mwana FA: Ushindi wa Taifa Stars ni maalum kwa Rais Dkt. Samia Suluhu
Kwa upande wake, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeungana na Rais kutoa pole kwa waathirika wa tukio hilo pamoja na familia za waliopoteza maisha. Taarifa hiyo imetolewa na Afisa Habari wa TFF, Cliford Marion Dimbo, akibainisha kuwa Shirikisho limeguswa sana na tukio hilo na linaendelea kusimama pamoja na watanzania wote wakati huu wa majonzi.
Wakati taifa likiendelea kuomboleza, hatua hizi zimeonekana kuwa faraja kwa wapenzi wa soka na wananchi kwa ujumla.