Rais gani aliwahi kukubalika akiwa madarakani Tanzania?

Mtanzania huwa hana shukrani hata siku moja. Alimtukana Mwinyi wakati ndiye muanzilishi wa mageuzi aliikuta hii nchi imejaa watu wanaovaa vidabwada wakila ugali wa yanga, na bado wakamuona hafai kwa lolote.

Wakamtukana Mkapa wakati alianzisha TRA inayokusanya mabilioni kwa mabilioni yanayoendesha nchi kila kukicha, pamoja na taasisi nyingine za kiuchumi.

Wakamtukana Kikwete wakati ndugu zao wakivunjwa miguu kwa ajali za bodaboda wanakwenda kuungwa pale MOI.

Wanamtukana JPM wakati kajenga fly overs za kwanza tangu tupate uhuru pamoja na daraja la busisi na mambo mengi ya maana ameyafanya.

Mtanzania msikilize akiongea halafu tikisa kichwa kama ishara ya kukubaliana na anachosema, ukishaachana nae nenda endelea kufanya shughuli zako, kwa kifupi mpuuze.
 
Kila mmoja kati ya marais watano waliopita ametimiza majukumu yake kama ilivyopaswa.
Ingawa kila mmoja alikuwa na mapungufu, maana nao ni binadamu.
Ila ni jambo lisilowezekana, kwamba wananchi wote milioni 60 waridhishwe na utendaji wa rais.

Kuna watakaomuona rais huyo kama malaika, nabii, masihi nk, na wengine watamuona shetani.tena shetani mkuu.

Hiyo ni kawaida tu.
 
Wasifiwe kwa lipi sasa mkuu.... Na wakiondoka sio kwamba wanasifiwa.. Ila wanakuwa bora kuliko anayekuwepo...
 
Hakuna raisi aliyependwa na watu wote, haijawahi kutokea na haitotokea

Jambo lolote utalofanya either liwe zuri au baya lazima watatokea wapi ngaji, assume unakataza ushoga na madawa ya kulevya kuna watu watakuchukia pamoja na Kuwa jambo zuri.

"If you want to make every one happy, don't be a leader, sell ice cream"
 
👏👏👏👏
 
Siku tukapopata viongozi lawama zitapungua ila kiuhalisia Africa hakuna viongozi ila kuna watawala yaan hawana tofauti na utawala wa kifalme kwakuwa utawala wa kifalme hauna demokrasia
Katika umri nimebahatika kuona utawala wa mkapa kikwete na magu na samia
Kwangu mimi kiongozi aliyetumia madaraka vibaya wa kwanza magu nchi ilikuwa imeshajiozea hadi international maana alikuwa muoga sana that's why alikuwa anajihami sana ktk utawala wake tukaona mambo ya kutekana sana na ubabe nje nje na waliobaki mkapa kikwete na samia ufisadi unakithiri chama kinawapa power sera mbovu katiba inawapa uhuru sana wa kuvynja sheria
 
Kwako wote hakuna zuri hata moja?
 
Rais wa hovyo ever ni Magufuli..kaweka visasi hadi leo watu wanauana tu...
Alifelisha mifumo yote ya HAKI ili wamsikilize yeye anataka nini...

Akafa.
5 & 6 ni tawala za hovyo kabisa kuwahi kutokea dunaini
 
Ila kiongoz mbovu kabsa toka tupate uhuru ni POMBE

alijificha kwenye kichaka cha wanyonge na akafanya uchafu wake alioutaka

1.5 T ipo kwenye account za familia saa hii
 
Hakuna raisi anayekubalika akiwa madarakani
 
Watanzania kwa unafiki,shetani akajifunze.
Ahahaha

Uko sahihi.
 
Kwako wote hakuna zuri hata moja?
Binadamu umeumbwa kutenda mema fanya mema 99 ila ukifanya baya 1 watu watalikumbuka hilo baya pia wanalipwa hela nyingi mno wakiwa madarakani mpk kustaafu hivyo wakifanya baya moja tunaanza na mabaya siku zote na mahali popote sisi binadamu huwa hatuesabu mema ila tunahesabu mabaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…