Rais huwa hatangazi Utalii

Rais huwa hatangazi Utalii

Kagame hajawahi kuingia field na kuanza kutangaza utalii kwa mtindo huu.

Hakuna mtalii atakayekuja kutalii bila kumwona yule aliyetangaza kwa mantiki hiyo mheshimiwa rais yuko tayari kuacha majukumu yake awe anaambatana na watalii kuthibitisha kilichomo kwenye fkamu badala ya wasaidizi wake walioteuliwa na kulipwa kwa kazi hiyo?

*Msiwe mnapuuza maoni ya wananchi wanapowapa changamoto kutokana na uamuzi mnaofanya bila taathimini ya uhalisia kwa kupima matokeo CHANYA dhidi matokeo HASI.


Kwahiyo ulitaka afanye kama alivyofanya Kagame? Acheni ujinga alichofanya Mama kina impact sana
 
We badala ya kumponheza rais unamshushua. Rais anafufua taifa ambalo jpm aliliua ndani ya miaka mitano. Ndani ya miaka mitano mzunguko wa pesa ulikata kwa sababu uwekezaji ulikata pia na mishara ya wafanyakazi kutoongezwa. Ndani ya miaka mitano alizima kabisa ajira kwa vijana kiasi ambacho walikuwa wanalandalanda mtaani bila kujua wafanye nini mana hata private sector ilikufa ambayo ilikuwa inaajiri pale ambapo serikali imeahindwa kuwaajiri. Ndani ya miaka mitano wakulima wa mbaazi, korosho nk walilia na kusaga meno kwa sababu ya udictor wake. Sasa samia anapambana kuleta ahueni na sasa wakulima wanachekelea. Sasa hivi kuna freedom of speech kiasi ambacho mpaka tbc sasa hivi wanatangaza habari za upinzani japo bado kwa kuibia ibia lakini mwelekeo ni mzuri.

Mama is doing better na sasa hivi kila mwenye uwezo wa kufanya kazi yupo kazini mpaka wale walioonewa eti vyeti feki wamerudishwa japo wengi walikuwa kwa stress. Ndani ya miaka mitano ya jpm aliua na kupoga risasi watu kama lisu.

Jpm hakuwa mru bali sheitwani
 
Kwa mara ya kwanza Dunia inaenda kushuhudia mkuu wa nchi, Rais akitangaza utalii. Rais anapoamua kutangaza utalii maana yake ni kwamba hilo Taifa analoongoza ni Taifa mfu, ni Taifa lililokufa, ni taifa jipya kabisa chini ya jua na halina raslimali zozote na wala kitu chochote, sasa inabidi atoke mkuu wa nchi aifahamishe Dunia kuwa taifa analoongoza lina sehemu za utalii.

Na Kwanza hata kama taifa halina chochote, siyo kazi ya Rais kutangaza utalii. Zipo strategies za kutangaza utalii, Samatta ni maarufu Duniani kuliko Rais Samia.

Rais anapoenda Location kama msanii wa Bongo movie kutangaza utalii,huo mkosi mzito mno kwa taifa, watalii hawaji Tanzania eti kwa sababu Rais aliwatangazia.

Wanakuja kwa sababu usalama wao utakuwa mkubwa zaidi, huwezi kwenda kutalii kwenye Taifa ambalo kiongozi mkuu wa Chama kikubwa Cha Upinzani ni Gaidi, maana yake ni kwamba hata mawaziri nao ni magaidi.

Kenya inapokea maelfu ya watalii kwa mwaka kuliko Tanzania nani alimwona Rais wa Kenya akienda location kutangaza utalii?
Yaani Serikali nzima yenye wasomi wa kada zote haina strategies za kutangaza utalii hadi Rais aende location?

Mbona ni rahisi mno kutangaza utalii kuliko ilivyo rahisi kunywa maji? Tanzania hii yenye vivutio vyote leo hata Rwanda wameanza kuwazidi kupokea watalii wengi kwa sababu ya strategies.

Rais ataenda Location zote na mtatengeneza filamu zote na watalii hamtawaona kwa sababu hamna strategies.

Nyie strategies zenu ni kuua Upinzani tu haya mengine zero kabisa.
Mkuu hata mimi nimejiuliza sana hili suala!!!! Hivi ni kazi ya raisi kutangaza utalii? Mbona ana vitu vikubwa vingi vya kufanya? Au haoni kama anatakiwa alipeleke taifa mbele kwa kuwa na mikakati mizuri? Bodi ya utalii imelala? Yaani raisi wetu hana kazi mpaka atangaze utalii wakati wapo wenye hiyo kazi? Sipati jibu!!!!
 
Mpelekeni na Mbudya akaitangaze pia tunaweza kupata Boti nzuri za kuwa zinatupeleka huko
 
Mabepari wanunuzi Tanzanite ambao wengi wao watakufa bila kukanyaga Tanzani hawajali Tanzanite inatoka wapi, wanachojali ni bei tu.

Kwa nini mnafikiri Rwanda ni taifa la maana saana kuigwa katika kitu chochote cha kimaendeleo? Hamuoni aibu taifa kubwa na la heshima kama hili kuiga jambo lolote kutoka kwa taifa dogo, maskini na linaloendeshwa kidhalimu ?
Hii vita tutaishinda tu sisi ni Taifa huru hivyo ushindi ni lazima. Labda wewe mwenzetu umeamua kukaa pamoja na upande wa hawa wapigaji wakubwa.
 
Wewe utapiga kelele hapo kwa maandishi lakini matokeo yakijidhihiri utatokomea kusikojulikana........akukosooaye ndiye anayekutakiwa mema sio anayekusifia bila kukoonesha upande wa pili wa shilingi athari zikoje
Angalau Mama kaonyesha ushujaa wa kuikubali dunia na kwenda kadri ya matakwa ya ushindani wa kimataifa. Wapo wengine walijawa na ujasiri wa ndani hawakuwa na utayari wa kupambania nafasi yao kimataifa.
 
Kuna Uzi wangu mrefu kuhusu hiki ulichokiandika hapa nilikuja nao mapema tu Wiki hii na Kuhoji hadi Kushangaa pia, ila kwa Masikitiko makubwa Moderators Wakauunganisha kwasababu wanazozijua Wao ambazo naziheshimu.

Ninakubaliana 100% kwa hizi Hoja zako.
Hahahah.acha uoga wew..ukitoa povu unapigilia msumari kabisa.hahahaha
 
Ni vizuri amefanya hiyo Royal Tour ili huko nje wajue kuwa ndiye anayechukia democrasia!!!
 
Nashauri acha kukariri Bandugu. Marais wengine tayari wameshafanya. Na pia sio mbaya hata kama angekuwa wa kwanza kama kuna tija. Naelewa tatizo baadhi yetu Watanzania, ujuaji uliopitiliza kwenye kila kitu.
 
Hili atajilaumu sana baadae maana waliomshaur wamempoteza.ila kwa vile ye mwenyewe hana vision wala mission twendeni tutakapoporomokea hukohuko
 
Kwa mara ya kwanza Dunia inaenda kushuhudia mkuu wa nchi, Rais akitangaza utalii. Rais anapoamua kutangaza utalii maana yake ni kwamba hilo Taifa analoongoza ni Taifa mfu, ni Taifa lililokufa, ni taifa jipya kabisa chini ya jua na halina raslimali zozote na wala kitu chochote, sasa inabidi atoke mkuu wa nchi aifahamishe Dunia kuwa taifa analoongoza lina sehemu za utalii.

Na Kwanza hata kama taifa halina chochote, siyo kazi ya Rais kutangaza utalii. Zipo strategies za kutangaza utalii, Samatta ni maarufu Duniani kuliko Rais Samia.

Rais anapoenda Location kama msanii wa Bongo movie kutangaza utalii,huo mkosi mzito mno kwa taifa, watalii hawaji Tanzania eti kwa sababu Rais aliwatangazia.

Wanakuja kwa sababu usalama wao utakuwa mkubwa zaidi, huwezi kwenda kutalii kwenye Taifa ambalo kiongozi mkuu wa Chama kikubwa Cha Upinzani ni Gaidi, maana yake ni kwamba hata mawaziri nao ni magaidi.

Kenya inapokea maelfu ya watalii kwa mwaka kuliko Tanzania nani alimwona Rais wa Kenya akienda location kutangaza utalii?
Yaani Serikali nzima yenye wasomi wa kada zote haina strategies za kutangaza utalii hadi Rais aende location?

Mbona ni rahisi mno kutangaza utalii kuliko ilivyo rahisi kunywa maji? Tanzania hii yenye vivutio vyote leo hata Rwanda wameanza kuwazidi kupokea watalii wengi kwa sababu ya strategies.

Rais ataenda Location zote na mtatengeneza filamu zote na watalii hamtawaona kwa sababu hamna strategies.

Nyie strategies zenu ni kuua Upinzani tu haya mengine zero kabisa.
Uongo mtupu! Kama hujui mambo si vizuri kuja na uongo humu JF. Marais wengi wametangaza sana vivutio vya nchi zao nchi za nje kwa nia na lengo la kuvutia watalii. Kila mmoja na njia na mbinu zake za kulifanya hili. Muulize Rais Kagame na ile timu ya EPL. Huko siyo kutangaza utalii!? Muulize Rais Narendra wa India, alipokuwa Bollyhood mwaka juzi, alikuwa anafanya nini, kama siyo kutangaza vivutio vya utalii walivyo navyo India!? Kama hujui mambo ya kileo duniani NYAMAZA sisi na SSH wetu tujenge nchi yetu!
 
Uongo mtupu! Kama hujui mambo si vizuri kuja na uongo humu JF. Marais wengi wametangaza sana vivutio vya nchi zao nchi za nje kwa nia na lengo la kuvutia watalii. Kila mmoja na njia na mbinu zake za kulifanya hili. Muulize Rais Kagame na ile timu ya EPL. Huko siyo kutangaza utalii!? Muulize Rais Narendra wa India, alipokuwa Bollyhood mwaka juzi, alikuwa anafanya nini, kama siyo kutangaza vivutio vya utalii walivyo navyo India!? Kama hujui mambo ya kileo duniani NYAMAZA sisi na SSH wetu tujenge nchi yetu!

Hana hoja huyu mpuuzi ni wivu tu umemjaa na kukosa patriotism.
Yani President ana promote sector inayochangia gdp kwa 16% ili iwe na tija zaidi yeye anaona haina maana. Jitu hovyo hili
 
Back
Top Bottom