Rais, Idara ya Afya OR-TAMISEMI ihamishie Wizara ya Afya chini ya Mganga Mkuu wa Serikali ili kuongeza Uwajibikaji, utakuja nishukuru baadae

Rais, Idara ya Afya OR-TAMISEMI ihamishie Wizara ya Afya chini ya Mganga Mkuu wa Serikali ili kuongeza Uwajibikaji, utakuja nishukuru baadae

COARTEM

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2013
Posts
3,603
Reaction score
3,658
Lengo la Serikali kufanya ugatuaji wa Madaraka lilikuwa bora sana na kila mtu analipongeza. Kwa sasa mambo yanavyokwenda SEKTA ya Afya ni kama kuna Wizara Mbili tofauti za Afya, yaani WIZARA MAMA YA AFYA (MOH) na WIZARA NDOGO YA AFYA (Idara ya Afya OR-TAMISEMI).

Ukienda Halmashauri na Mikoani, Waganga wakuu wa Wilaya (DMOs) na Waganga wakuu wa Mikoa (RMOs) wanasikiliza maelekezo ya Viongozi wa OR-TAMISEMI zaidi kuliko maelekezo ya Viongozi wa Wizara ya Afya (MOH).

Mambo yakienda mrama sekta ya Afya huko Halmashauri na Mikoani, wizara inayolalamikiwa ni WIZARA YA AFYA na siyo OR-TAMISEMI. Utendaji wa Watumishi wengi wa OR-TAMISEMI kwakweli una mashaka sana, wengi wao wakienda Mikoani na Halmashauri kazi yao ni kuzurura tu.

Viongozi wa Wizara ya Afya wakipita Halmashauri na Mikoani ambako tayari watendaji wa OR-TAMISEMI walipita kufanya usimamizi shirikishi wanayakuta madudu mpaka mtu unajiuliza, hivi hata jambo dogo kama hili OR-TAMISEMI-Afya hawakuliona?

Mhe. Rais Hospitali za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati vikiwa na huduma Mbovu, lawama zote zinapelekwa WIZARA YA AFYA. Hapo OR-TAMISEMI haiwezi laumiwa na Wananchi kwani Mwananchi yeye anaijua Wizara ya Afya.

Kwahiyo ili kuipa nguvu Wizara ya Afya, inatakiwa utendaji wa kila siku wa Hospitali za Wilaya, Vituo vya Afya, Zahanati usimamiwe na Wizara ya Afya.

Kwahiyo RMO na DMO wanapaswa wawajibike moja kwa moja kwa CMO ili mambo yaweze kwenda vile unavyotamani kuiboresha sekta ya Afya.

Mbaya zaidi kumezuka kiburi kwa hawa DMOs na RMOs kutotii ziara za Viongozi wa MOH wakidai wao wanawajibika moja kwa moja OR-TAMISEMI. Mheshimiwa Rais Maboresho sekta ya Afya hayatafanikiwa kama kutaendelea kuwepo kwa Idara ya Afya-OR TAMISEMI. "Hata Biblia inasema huwezi tumikia mabwana wawili maana utampenda huyu na kumchukia yule."

Ushauri:

Irudishe Idara ya Afya -OR TAMISEMI iende kuwa chini ya Mganga Mkuu wa Serikali (CMO) ili uwajibikaji wao usimamiwe na Wizara Mama ya Kisekta. Kwa kufanya hivyo utakuwa umesaidia sana kuimarisha utendaji kazi wa SEKTA YA AFYA Halmashauri na Mikoani.

Naomba kuwasilisha Ushauri wangu huu.
 
TAMISEMI inamfaa Rukuvi, Ole sabaya au makonda huyo mnyambo hmna kitu pale

USSR
 
Lengo la serikali kufanya ugatuaji wa Madaraka lilikuwa bora sana na kila mtu analipongeza. Kwa sasa mambo yanavyokwenda SEKTA ya Afya,ni kama kuna wizara Mbili tofauti za Afya, yaani WIZARA MAMA YA AFYA (MOH) na WIZARA NDOGO YA AFYA (Idara ya Afya OR-TAMISEMI).
Ukienda Halmashauri na Mikoani, Wagagnga wakuu wa Wilaya (DMOs) na Waganga wakuu wa Mikoa (RMOs) wanasikiliza maelekezo ya Viongozi wa OR-TAMISEMI zaidi kuliko maelekezo ya Viongozi wa Wizara ya Afya (MOH).
Mambo yakienda mrama sekta ya Afya huko Halmashauri na Mikoani, wizara inayolalamikiwa ni WIZARA YA AFYA na siyo OR-TAMISEMI. Utendaji wa Watumishi wengi wa OR-TAMISEMI kwakweli una mashaka sana,wengi wao wakienda Mikoani na Halmashauri kazi yao ni Kuzurula tu.
Viongozi wa Wizara ya Afya wakipita Halmashauri na Mikoani ambako tayari watendaji wa OR-TAMISEMI walipita kufanya usimamizi shirikishi,wanayakuta madudu mpaka mtu unajiuliza , hivi hata jambo dogo kama hili OR-TAMISEMI-Afya hawakuliona?
Mbaya zaidi kumezuka kiburi kwa hawa DMOs na RMOs kutotii ziara za Viongozi wa MOH wakidai wao wanawajibika moja kwa moja OR-TAMISEMI. Mheshimiwa Rais Maoberesho sekta ya Afya hayatafanikiwa kama kutaendelea kuwepo kwa Idara ya Afya-OR TAMISEMI.
Ushauri:
Irudishe Idara ya Afya -OR TAMISEMI iende kuwa chini ya Mganga Mkuu wa Serikali (CMO) ili uwajibikaji wao usimamiwe na Wizara Mama ya Kisekta. Kwa kufanya hivyo utakuwa umesaidia sana kuimarisha utendaji kazi wa SEKTA YA AFYA Halmashauri na Mikoani.
Naomba kuwasilisha Ushauri wangu huu.
Nakubaliana na wewe.
 
Lengo la serikali kufanya ugatuaji wa Madaraka lilikuwa bora sana na kila mtu analipongeza. Kwa sasa mambo yanavyokwenda SEKTA ya Afya,ni kama kuna wizara Mbili tofauti za Afya, yaani WIZARA MAMA YA AFYA (MOH) na WIZARA NDOGO YA AFYA (Idara ya Afya OR-TAMISEMI).
Ukienda Halmashauri na Mikoani, Wagagnga wakuu wa Wilaya (DMOs) na Waganga wakuu wa Mikoa (RMOs) wanasikiliza maelekezo ya Viongozi wa OR-TAMISEMI zaidi kuliko maelekezo ya Viongozi wa Wizara ya Afya (MOH).
Mambo yakienda mrama sekta ya Afya huko Halmashauri na Mikoani, wizara inayolalamikiwa ni WIZARA YA AFYA na siyo OR-TAMISEMI. Utendaji wa Watumishi wengi wa OR-TAMISEMI kwakweli una mashaka sana,wengi wao wakienda Mikoani na Halmashauri kazi yao ni Kuzurula tu.
Viongozi wa Wizara ya Afya wakipita Halmashauri na Mikoani ambako tayari watendaji wa OR-TAMISEMI walipita kufanya usimamizi shirikishi,wanayakuta madudu mpaka mtu unajiuliza , hivi hata jambo dogo kama hili OR-TAMISEMI-Afya hawakuliona?
Mbaya zaidi kumezuka kiburi kwa hawa DMOs na RMOs kutotii ziara za Viongozi wa MOH wakidai wao wanawajibika moja kwa moja OR-TAMISEMI. Mheshimiwa Rais Maoberesho sekta ya Afya hayatafanikiwa kama kutaendelea kuwepo kwa Idara ya Afya-OR TAMISEMI.
Ushauri:
Irudishe Idara ya Afya -OR TAMISEMI iende kuwa chini ya Mganga Mkuu wa Serikali (CMO) ili uwajibikaji wao usimamiwe na Wizara Mama ya Kisekta. Kwa kufanya hivyo utakuwa umesaidia sana kuimarisha utendaji kazi wa SEKTA YA AFYA Halmashauri na Mikoani.
Naomba kuwasilisha Ushauri wangu huu.
Sheria inayounda mamlaka ya serikali za Mitaa inaweka mamlaka ya nidhamu ya Mtumishi chini ya baraza la madiwani.

Ingawa hata DMO ( Mkuu wa Idara ) anateuliwa na Katibu Mkuu Utumishi lakini bado anawajibika kwa baraza la madiwani.

Kuna hospitali ziko chini ya Wizara ya Afya na nyingine chini ya TAMISEMI.

Na hata Watumishi ndani ya Wizara ya Afya Kuna walioajiriwa na TAMISEMI ( Hawa wako chini ya DEDs ) na Kuna walioko chini ya Wizara ya Afya.
 
TAMISEMI inamfaa Rukuvi, Ole sabaya au makonda huyo mnyambo hmna kitu pale

USSR
Yaan kwa kuwa mmezoea, watu wa kufoka, teka, UA, fukuza, weka ndani,Basi mkiona mtu Kama Bashungwa mnaona hafai
 
Wazo hili ni jema sana. Wataalam wote warejeshwe kwenye wizara zao mama kama ilivyofanyika kwenye wizara za maji na ujenzi, huko Tamisemi ni kuongeza urasimu na kupotezeana muda.
Utaalamu Urudi wizarani na kujenga vituo vya afya ibaki tamisemi.
 
Wazo hili ni jema sana. Wataalam wote warejeshwe kwenye wizara zao mama kama ilivyofanyika kwenye wizara za maji na ujenzi, huko Tamisemi ni kuongeza urasimu na kupotezeana muda.
Kwahiyo kazi ya TAMISEMI itakuwa Nini?
 
Sheria inayounda mamlaka ya serikali za Mitaa inaweka mamlaka ya nidhamu ya Mtumishi chini ya baraza la madiwani.

Ingawa hata DMO ( Mkuu wa Idara ) anateuliwa na Katibu Mkuu Utumishi lakini bado anawajibika kwa baraza la madiwani.

Kuna hospitali ziko chini ya Wizara ya Afya na nyingine chini ya TAMISEMI.

Na hata Watumishi ndani ya Wizara ya Afya Kuna walioajiriwa na TAMISEMI ( Hawa wako chini ya DEDs ) na Kuna walioko chini ya Wizara ya Afya.
Full mvurugano
 
Wazo hili ni jema sana. Wataalam wote warejeshwe kwenye wizara zao mama kama ilivyofanyika kwenye wizara za maji na ujenzi, huko Tamisemi ni kuongeza urasimu na kupotezeana muda.
Kabisa ndugu yaani Afya kumevurugika kabisa.IDARA YA AFYA TAMISEMI irudishwe Wizara mama (WIZARA YA AFYA)
 
Sheria inayounda mamlaka ya serikali za Mitaa inaweka mamlaka ya nidhamu ya Mtumishi chini ya baraza la madiwani.

Ingawa hata DMO ( Mkuu wa Idara ) anateuliwa na Katibu Mkuu Utumishi lakini bado anawajibika kwa baraza la madiwani.

Kuna hospitali ziko chini ya Wizara ya Afya na nyingine chini ya TAMISEMI.

Na hata Watumishi ndani ya Wizara ya Afya Kuna walioajiriwa na TAMISEMI ( Hawa wako chini ya DEDs ) na Kuna walioko chini ya Wizara ya Afya.
Diwani darasa la 7 anamwajibisha MD??? Hiyo ni akili???
Kibaya zaidi hao Madiwani wengi wao wana njaa sana.. wanatishia kuwaazimia Watumushi huko Halmashauri/ manispaa ili wapate kitu... kiufupi Manispaa zinahitaji overhaul...
1. Mhe Hayati Magufuli almliona ili kwa kuziondoa baadhi ya idara chini ya madiwani mfano idara za
1. maji
2. Ujenzi ( TARURA)
Mhe. Ummy Mwalimu alipendekeza Secretarieti za Miko kuwa ni chombo chenye nguvu ili ku- review maamuzi ya madiwani
 
Diwani darasa la 7 anamwajibisha MD??? Hiyo ni akili???
Kibaya zaidi hao Madiwani wengi wao wana njaa sana.. wanatishia kuwaazimia Watumushi huko Halmashauri/ manispaa ili wapate kitu... kiufupi Manispaa zinahitaji overhaul...
1. Mhe Hayati Magufuli almliona ili kwa kuziondoa baadhi ya idara chini ya madiwani mfano idara za
1. maji
2. Ujenzi ( TARURA)
Mhe. Ummy Mwalimu alipendekeza Secretarieti za Miko kuwa ni chombo chenye nguvu ili ku- review maamuzi ya madiwani
Hiyo ndio demokrasia. Unless hutaki tena demokrasia.

Hao Madiwani ndio reflection ya Jamii wanaoongoza.

Kina Joyce Mukya, Msigwa ,Lema, Sugu, Mbowe, Wana Elimu gani?
 
Mfumo wa uongozi na utawala nchi hii bado unashida sana..kuna gaps nyingi sana moja wapo ikiwa hiyo ya wataalamu kutokuwa chini ya wizara mama.

Suala la waganga wakuu kuongoza idara ya afya hili nalo ni tatizo kubwa sana..wengi hawana skills za uongozi na management..pia hukuiona miungu watu ndani ya idara..ifike mahali sasa kila mtaalamu wa afya mwenye sifa na uwezo awe na nafasi ya kushika idara ya afya haijarishi ni kada ipi.

Suala lingine ni health financing..bado mifumo haijawa rafiki tunahitaji marekebisho makubwa hapa pia.

#MaendeleoHayanaChama
 
Lengo la Serikali kufanya ugatuaji wa Madaraka lilikuwa bora sana na kila mtu analipongeza. Kwa sasa mambo yanavyokwenda SEKTA ya Afya ni kama kuna Wizara Mbili tofauti za Afya, yaani WIZARA MAMA YA AFYA (MOH) na WIZARA NDOGO YA AFYA (Idara ya Afya OR-TAMISEMI).

Ukienda Halmashauri na Mikoani, Waganga wakuu wa Wilaya (DMOs) na Waganga wakuu wa Mikoa (RMOs) wanasikiliza maelekezo ya Viongozi wa OR-TAMISEMI zaidi kuliko maelekezo ya Viongozi wa Wizara ya Afya (MOH).

Mambo yakienda mrama sekta ya Afya huko Halmashauri na Mikoani, wizara inayolalamikiwa ni WIZARA YA AFYA na siyo OR-TAMISEMI. Utendaji wa Watumishi wengi wa OR-TAMISEMI kwakweli una mashaka sana, wengi wao wakienda Mikoani na Halmashauri kazi yao ni kuzurura tu.

Viongozi wa Wizara ya Afya wakipita Halmashauri na Mikoani ambako tayari watendaji wa OR-TAMISEMI walipita kufanya usimamizi shirikishi wanayakuta madudu mpaka mtu unajiuliza, hivi hata jambo dogo kama hili OR-TAMISEMI-Afya hawakuliona?
Mhe. Rais Hospitali za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati vikiwa na huduma Mbovu, lawama zote zinapelekwa WIZARA YA AFYA. Hapo OR-TAMISEMI haiwezi laumiwa na Wananchi kwani Mwananchi yeye anaijua Wizara ya Afya. Kwahiyo ili kuipa nguvu Wizara ya Afya, inatakiwa utendaji wa kila siku wa Hospitali za Wilaya, Vituo vya Afya, Zahanati usimamiwe na Wizara ya Afya. Kwahiyo RMO na DMO wanapaswa wawajibike moja kwa moja kwa CMO ili mambo yaweze kwenda vile unavyotamani kuiboresha sekta ya Afya.

Mbaya zaidi kumezuka kiburi kwa hawa DMOs na RMOs kutotii ziara za Viongozi wa MOH wakidai wao wanawajibika moja kwa moja OR-TAMISEMI. Mheshimiwa Rais Maboresho sekta ya Afya hayatafanikiwa kama kutaendelea kuwepo kwa Idara ya Afya-OR TAMISEMI. "Hata Biblia inasema huwezi tumikia mabwana wawili maana utampenda huyu na kumchukia yule."

Ushauri:
Irudishe Idara ya Afya -OR TAMISEMI iende kuwa chini ya Mganga Mkuu wa Serikali (CMO) ili uwajibikaji wao usimamiwe na Wizara Mama ya Kisekta. Kwa kufanya hivyo utakuwa umesaidia sana kuimarisha utendaji kazi wa SEKTA YA AFYA Halmashauri na Mikoani.

Naomba kuwasilisha Ushauri wangu huu.
Hata idara ya elimu bora irudishwe Wizara ya Elimu
 
Mfumo wa uongozi na utawala nchi hii bado unashida sana..kuna gaps nyingi sana moja wapo ikiwa hiyo ya wataalamu kutokuwa chini ya wizara mama.

Suala la waganga wakuu kuongoza idara ya afya hili nalo ni tatizo kubwa sana..wengi hawana skills za uongozi na management..pia hukuiona miungu watu ndani ya idara..ifike mahali sasa kila mtaalamu wa afya mwenye sifa na uwezo awe na nafasi ya kushika idara ya afya haijarishi ni kada ipi.

Suala lingine ni health financing..bado mifumo haijawa rafiki tunahitaji marekebisho makubwa hapa pia.

#MaendeleoHayanaChama
Upo sahihi mfumo umeoza Tanzania ndiyo maana hatuendelei hata kidogo
 
Back
Top Bottom