Rais Kagame ataka M23 watambuliwe na Serikali ya DR Congo

Rais Kagame ataka M23 watambuliwe na Serikali ya DR Congo

Wananchi wenyewe naskia wanaikubali m23
 
PK yupo sahihi
Hakuna namna ya kuwakwepa M23 kwenye hoja ya kuleta amani

Ni kweli wanaweza kuwa na mapungufu yao lakini pia wana haki zao za msingi ziheshimiwe
 
Serikali ya Dr congo lazima ikiri hadharani kuwa banyamulenge ni raia wa nchi hiyo na siyo wahamiaji
adi wanafikia maazimio kuwa T'kedi akutane na m23 maana yake drc imeshawatambua ao wanyamulenge kama ni wananchi halali wa drc. nje ya apo maazimio yangekuwa m23 kuondoshwa apo drc.
 
Kagame apuuzwe
Kagame ameleta msimamo wa M 23 kuwa watambulike na congo DR, sijui ni kivipi serikali ya Congo haiwatambui Wanyamulenge?

RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amesema nchi yake haiwezi kukaa kimya wakati usalama wake unahatarishwa na DRC na kubainisha kuwa Rwanda imejaribu mara nyingi kuzungumza na Congo bila mafanikio huku akisisitiza kuwa suluhisho la kudumu linahitajika badala ya lawama zinazoelekezwa kwa Rwanda kila tatizo linapotokea DRC.

"Congo hawawezi kutuambia tukae kimya wakati wanasababisha matatizo makubwa ya kiusalama dhidi yetu, hakuna wa kutuambia tukae kimya, tumeongea na Congo mara nyingi tumewaita tukae tuongee hawataki, Mimi naomba tusiwe na vikao vingi sana kama ambavyo tayari tumeshakuwa navyo.” — amesema Kagame akizungumza kwenye mkutano wa EAC-SADC.

“Hatuwezi kila siku kukaa kujadili matatizo maana kinachoendelea pale ni vita ya Kikabila ni suala la kutambuana, kujadiliana na kuwapa haki yao, tutumie kikao hiki kupata suluhu ya kudumu na sio matatizo yatokee Congo kisha ubaya anapewa Rwanda" — amesema Kagame.
 
Hili ndio tatizo la kupokea wakimbizi
Mwisho wa siku wanadai haki yao na kuona kama mali yao
Hawa wakimbizi wanaopigana Kagame awachukue maana wao ndio walipigana na kusababisha mauwaji ya Kimbari na watu kuikimbia nchi

Alikosekana wa kumjibu na kumwambia achukue wakimbizi wake?
 
PK yupo sahihi
Hakuna namna ya kuwakwepa M23 kwenye hoja ya kuleta amani

Ni kweli wanaweza kuwa na mapungufu yao lakini pia wana haki zao za msingi ziheshimiwe
Walishaambiwa siku nyingi,wafanye kazi za kiraia, ujasiriamali, kilimo,madini,wao wanang'ang'ania kwenye vyombo vya ulinzi na usalama,Wana agenda gani!?
 
Rais wa Congo sidhani kama atakubali. Tatizo Kongo hawana umoja, suluhisho la hii vita au mgogoro ni mmoja ashindwe, ni aidha congo wakubali kuwatambua m23 na Rwanda waichukue east congo Kwa mgongo wa m23 au congo akubali kuivamia Rwanda au kutangaza rasmi wanaingia vitani na nchi ya Rwanda (hapa gharama kubwa italipwa)....Sioni mazungumzo yakisaidia hapo.

Kuruhusu m23 kukubaliwa ni sawa na kuruhusu jeshi la Rwanda liingie Kongo kitu ambacho mtu mwenye akili timamu hawezi kukubali, kukubaliana na waasi waache silaha zao ni haiwezekani.

Dili na kiini cha tatizo, then m23 watapukutika wenyewe, kudili na kiini cha tatizo Kuna gharama kubwa mnooo za kulipa na congo haitaki kulipa hizo gharama, kwanini maliasili zote hizo mshindwe kununua vyuma vya kijeshi vya maana kabisa, tia pesa watu wakapate mafunzo ya kutosha ya kijeshi, jipe muda then Fanya kweli.
 
Rais wa Congo sidhani kama atakubali. Tatizo Kongo hawana umoja, suluhisho la hii vita au mgogoro ni mmoja ashindwe, ni aidha congo wakubali kuwatambua m23 na Rwanda waichukue east congo Kwa mgongo wa m23 au congo akubali kuivamia Rwanda au kutangaza rasmi wanaingia vitani na nchi ya Rwanda (hapa gharama kubwa italipwa)....Sioni mazungumzo yakisaidia hapo.

Kuruhusu m23 kukubaliwa ni sawa na kuruhusu jeshi la Rwanda liingie Kongo kitu ambacho mtu mwenye akili timamu hawezi kukubali, kukubaliana na waasi waache silaha zao ni haiwezekani.

Dili na kiini cha tatizo, then m23 watapukutika wenyewe, kudili na kiini cha tatizo Kuna gharama kubwa mnooo za kulipa na congo haitaki kulipa hizo gharama, kwanini maliasili zote hizo mshindwe kununua vyuma vya kijeshi vya maana kabisa, tia pesa watu wakapate mafunzo ya kutosha ya kijeshi, jipe muda then Fanya kweli.
Una hoja nzuri
 
Back
Top Bottom