Rais Kamuzu Banda alizitaka Mbeya, Njombe na Songea kuwa sehemu ya Malawi

Rais Kamuzu Banda alizitaka Mbeya, Njombe na Songea kuwa sehemu ya Malawi

Mkuu ukiangalia kwa jicho la Tatu utagundua mipaka iko wazi kabisa kwa sababu dunia ya leo watu wanaiba kwa kutumia kalamu , watu wanatumia akili, sisi tunapumbazwa na maneno ya kitapeli tu utasikia mara Diplomasia Mara uwekezaji, hiyo yote ni wizi tu.

Wenzetu siasa zao wanafanya kisayansi na kutumia hesabu kali ila sisi tumekalia porojo tu. Hivi unajua kuna ndege binafsi zinatua direct huko migodini na mbugani? Unajua zinabeba mali kiasi gani? Unajua mwelekeo wa dunia kwenye matumizi ya Nishati ya Gesi? Unajua sisi tuna huge deposit ya Gesi ila hatuwezi kunufaika ipasavyo? Jeshi badala ya kulinda rasilimali za nchi linatumika kulinda maslahi ya watu wachache na kuizanisha nchi.

Shtuka mkuu dunia ya sasa haipigani vita kwa mitutu na mabomu bali kwa maneno, kalamu, akili kubwa na mahesabu makali.

Malawi, tunayoipa msaada, inafanya nini kati ya hayo?
 
Sisi ambao tuko mipakani karibu na Malawi ikitokea tukapiga kura ya kuwa sehemu ya Malawi hatukatai.Malawi kunamifumo mizuri ya kielimu,kiuchumi , kibiashara na,kijamii kuliko Tanzania.

Uchumi gani? Mabeki tatu wote siku hizi kusini wanatoka Malawi. Shortage ya mafuta, chakula, umeme nk. Hamia Malawi usisubiri boarder dispute.
 
Tungekomaa na kwenye Dhahabu na Gesi yetu ingependeza sana !

Alisikika Mwamba mmoja akisema
“Tumepigwa “ 😳😱
Rest in peace JPM 🙏🙏

Dhahabu na gesi vimefanya nini? Kuna tatizo gani? Mnaibiwa? How? Wapi? Breakdown bila vague statements za vijiweni.
 
Ile vita hata haukuchukua muda mrefu ikawa imeisha wanajeshi wa Nyerere walitoboa meli za adui zikazama adui akaona huu mziki siuwezi akakimbia na alikuwa akisaidiwa na makaburu.
Hata mtaa wa Rufiji jijini Mwanza ulikuwa ukiitwa Banda street baada ya vita hilo jina Banda liliondolewa ukaitwa Rufiji street
Hizii stori za kijiweni
 
Sehemu pekee ambako unakutana na watanzania ambao unahisi hawa hawakupaswa kuwa watanzania ila kuwa wamalawi nafikri ni vijiji vyote vulivyo karibu na Nang'ombo mwaziwa nyasa nyumbani kwao Judge Samatha na maeneo fulani ya Ileje. Kule lugha wanayozungumza ni ya Malawi kabisa. Yote kwa yote mipaka iheshimiwe maana ikisemwa maeneo yote yachukuliwe itakuwa shida. Kuna maeneo fulani ya Mhukuru Ruvuma kule ndani kabisa mambo mengi yanafanyika ni ya nchi ya msumbiji. Bidhaa zinatoka msumbiji hadi Kanga za kina Frelimo na Fanta ni za huko..

Fikiria Wazambia pia wakiamua kuchukua eneo la Wamambwe kule mambwe Kenya Rukwa pia linaweza enda Zambia maana wakina Sinkala ndio watawala wa eneo la Tanzania na Zambia kule mpakani.

Maeneo yote ya mipakani yapo hivyo dunia nzima. Unaweza sema hayo maeneo yaende Malawi na TZ inaweza sema maeneo ya Malawi yawe Tanzania sababu ya muingiliano. Mipaka ni imaginary lines, natural landmarks zilitumika kutengenesha nchi au mikoa au majimbo kwa nchi zingine ndo maana unaona mara nyingi mipaka ni mito, milima, maziwa na landmarks zingine. Watu wa mipakani wataendana tu duniani kote.
 
Mipaka ya ukoloni haikuangaliq setup ya makabila ya eneo husika. Ukienda kaskazini kuna masai wa Kenya na Tanzania, jaluo hivyo hivyo. Kusini utakuta Makonde wa Msumbiji na Tanzania. Yaani hivyo

Kwa kawaida mipaka haiangalii makabila bali landmarks hii ni duniani kote sio Africa tu. Ni kawaida watu wa mipakani kuendana sababu mipaka ni imaginary lines tu. Sehemu nyingi mipakani utakuta mito, milima, ziwa au any other natural landmark regardless ya watu wa upande mmoja na mwingine kuwa wamoja.
 
Kama Tanzania inaweza kutikiswa hata na Malawi basi sitakuwa tena na sababu ya kunivunia kuwa Mtanzania.Suala la kutamani sehemu ya nchi nyingine limekuwepo tangu kitambo na Mwalimu alionesha mfano wakati Mzee Idd alipoitamani sehemu ya Kagera, na Kamuzu alijionea mwenyewe kilichotokea wala hakuhadithiwa.Na kama kuna wa kuogopwa iwapo ataitamani sehemu ya jirani yake basi ni sisi Tanzania, na si Tanzania kumuogopa Malawi,Uganda,Zambia,Kenya,Uganda n.k.
 
They are stupid najua hata wakati wa uongozi wa yule mama ndio alianzisha hii chokochoko, aisee pale panalindwa kuliko wanavyodhani na hatutaachia hata hatua moja mipaka ilishakuwa settled zamani so wasitutafute ubaya sababu wanajua vema uwezo tulionao.

Africa iligawanywa na wazungu ikawekwa mipaka kila nchi ikapigania uhuru wake na kulinda mipaka yake. Haya yanayokuja kuibuka baada ya miaka zaidi ya 60 ya uhuru ni uhuni tu na hakika hakuna ardhi wataipata kama ni ziwa Nyasa tulishakubaliana miaka kibao ligawanywe katikati na hiyo imekuwa hivyo miaka yote sasa haya wanayoleta kuna kitu wanakitafuta na watakipata watanzania sio wapole kiasi hicho mbona tunawaacha tunwanakaa kwetu hatuwapi shida hata kuwasumbua kuhusu permits zao? Si tunaishi nao tu ? Hakika kwa hili diplomasia ikishindwa naamini kila mtanzania atakuwa tayari kuvaa konbati na kuingia front uzuri watanzania halisi tunajijua when it comes to national interests.
Kuingia frontline kupigania mpaka ? 😅🤣 Mimi nitakua wa mwisho kuvaa hizo kombati. Nitavaa kombati kupigania amani na utulivu na sio mipaka. Mipaka ni mamno ya kipuuzi tu haya. Watu wanaoishi pande zote ni wale wale tu na tena wengine wana ndgu upande huu na ule.
 
Ngoja waje...Tanzania tumekuwa shamba la bibi, ziwa nyasa hilo linakwenda, ziwa victoria tayari tumepigwa pini, Bagamoyo nayo Zanzibar wanaivutia pumzi waibebe...Bandari,mito na maziwa makuu tumekabizi Dipiiweldi, Mbuga zote na Misitu , tumekabizi kwa waarabu, Madini na Gesi tumekabizi kwa Mchina na Mzungu wanajichotea wanavyotaka...Mwisho wa siku tumebaki na Pumbu tu Mazafanta, #Tusi
Ziwa Victoria tumepigwa pini gani.
 
Hata huyo Kenya ukija kwenye ubora wa raia mmoja mmoja mKenya hamkuti mTanzania.

Mfano Ardhi tu, imeshikwa na wachache huku kwetu hata mpare aliyetoka kijijini mbaga akishauza tangawizi zake anaweza miliki kiwanja akajenga karibu na bahari sababu vinanunulika. Ukija kwenye msosi ndo usiseme.
Eti Mpare wa Mbaga anunue kiwanja ufukweni?Wapare hawahawa ninaowajua?labda ufukwe wa ziwa Jipe.
 
Eti Mpare wa Mbaga anunue kiwanja ufukweni?Wapare hawahawa ninaowajua?labda ufukwe wa ziwa Jipe.
Mkuu, hujakutana na wapare wenye ukwasi? Kuna wapare kina mchome, mndeme, wagonja, msuya wapare wa ugweno wana ukwasi sana tu, sema tofauti yao na makabila kama watani zao kina mushi, kimaro, shao, temu wao hawajui kunyanyuana. Mchaga akifika sehemu akafanikiwa ni suala la muda tu atavuta wachaga wenzie ila wapare siwaoni wakifanya haya ndo maana wengi wanabaki choka mbaya.
 
Mkuu, hujakutana na wapare wenye ukwasi? Kuna wapare kina mchome, mndeme, wagonja, msuya wapare wa ugweno wana ukwasi sana tu, sema tofauti yao na makabila kama watani zao kina mushi, kimaro, shao, temu wao hawajui kunyanyuana. Mchaga akifika sehemu akafanikiwa ni suala la muda tu atavuta wachaga wenzie ila wapare siwaoni wakifanya haya ndo maana wengi wanabaki choka mbaya.
Ni Watani zangu hao nawajua mimi nje ndani.Any way niko kiutani zaidi.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Unapuga kura ili iwe nini kama unataka kuhamia malawi si unaenda tu au mpaka uvunje international borders ? Kama unaona kuna maisha mazuri huko we vuka hamia huko tuone kama watakupikea kirahisi kama unavyodhani.

Sisi hatutoi ardhi yetu anayetaka ahamie malawi ila ardhi ni yetu watakaa watanzania.
Huyo ni hayawani Tu. Malawi nchi masikin kweli kweli na imejaa walevi
 
Zamani Wakazi wengi wa Mbeya walikuwa wa kabila la Kingoni, ambalo pia linapatikana Malawi. Viongozi wengi wa Malawi wakiongozwa na Banda Waliona uhusiano wa karibu na Malawi kuliko Tanzania, na walitaka baadhi ya mikoa ya Tanzania iliyokaribu na Malawi kujiunga na nchi hiyo. JW wapo makini na mipaka yetu
 
They are stupid najua hata wakati wa uongozi wa yule mama ndio alianzisha hii chokochoko, aisee pale panalindwa kuliko wanavyodhani na hatutaachia hata hatua moja mipaka ilishakuwa settled zamani so wasitutafute ubaya sababu wanajua vema uwezo tulionao.

Africa iligawanywa na wazungu ikawekwa mipaka kila nchi ikapigania uhuru wake na kulinda mipaka yake. Haya yanayokuja kuibuka baada ya miaka zaidi ya 60 ya uhuru ni uhuni tu na hakika hakuna ardhi wataipata kama ni ziwa Nyasa tulishakubaliana miaka kibao ligawanywe katikati na hiyo imekuwa hivyo miaka yote sasa haya wanayoleta kuna kitu wanakitafuta na watakipata watanzania sio wapole kiasi hicho mbona tunawaacha tunwanakaa kwetu hatuwapi shida hata kuwasumbua kuhusu permits zao? Si tunaishi nao tu ? Hakika kwa hili diplomasia ikishindwa naamini kila mtanzania atakuwa tayari kuvaa konbati na kuingia front uzuri watanzania halisi tunajijua when it comes to national interests.
Ingia mwenyewe front mimi naenda zangu ulaya kama mkumbizi wa vita mambo ya kuyapigania ma ccm siwezi mimi
 
Back
Top Bottom