Rais kateleza kutumia lugha za vijiweni kutetea Katiba - Matamko Kurugenzi Ikulu yafanana

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,925

Kikwete hajaonyesha ukomavu wa kisiasa na kushindwa kujibu hoja badala yake kumshambulia Tundu Lissu kwa lugha za vijiwe kitu kisichokubalika kwa nafasi na heshima yake kama Rais. Lugha hii aliyotumia hapa chini katika nukuru pengine amehamasika na labda kuelekezwa namna ya kujibu kwa vile amezoea ya kuambiwa bila kufanyia utafiti kujiridhisha na kile anachoambiwa.

Kwa namna nyingine lugha aliyotumia si ya kiwango chake na kwa nafasi yake na kabisa anapolihutubia taifa, amejiruhusu kushuka chini mno kiasi cha kutoa lugha isiyostahiki kwa jamii na pengine si kile kilichotazamiwa na watanzania walio wengi kusikia live toka kwake mwenyewe.

Kwenye kumbukumbu zangu zimetokea lugha za vijiweni toka Kurugenzi ya Habari Ikulu inapotoa matamko ya utetezi mara kadhaa, na lugha hizo zilizotumika hazitofautiani sana na hii ambayo Kikwete ameitoa safari hii kwenye hotuba yake ya Mwisho wa Mwezi alipoamua kumtolea uvivu Mbunge na Mnazimu Bungeni Tundu Lissu.

Kama nilivyoainisha mara moja kuhusu Dr Slaa katika mada mojawapo hapa juu kuhusu kupima lugha ambayo inatakiwa kama kiongozi mwenye nafasi kubwa kitaifa kutuliza kichwa na kutoa kitu ambacho kinaonekana hekima, busara na uvumilivu kuwepo.

Hivyo basi Kikwete naye kama rais wa nchi hii kauli aliyotoa hailingani na nafasi, wajibu, hekima na busara kwa nafasi aliyo nayo na wakati alipoitoa. Kwa nchi zilizopaa kidemokrasia hiyo lugha ingekuwa gumzo kubwa na pengine kuwa ni kashfa kitaifa, lakini kwa kuwa tumezoea basi tunaendelea na mazoea.

Sehemu ya majibu ya Tundu Lissu kwa kauli ya Kikwete:
 
Kuna mambo mengine Marais wa Nchi huongea kwa kuwa wanajua hakuna mtu yoyote wa kuwafanya kitu chochote...
 
Umeeleweka kiongozi. Jk hajijui kama yeye ndo Mkuu.............ananjihisi hisi na kuwa na inferiority compl............
 
Mi sishangai kwa sanabu Kikwete ni mwimba taarabu kama mzee nani yule.... Huyu wa jahazi. Tena JK ana mp3 kabisa inaitwa neno.
 
Inawezekana utotoni alikuwa mtu kukaa sana vijiweni!!

Kauli yake hiyo ilishatokea mara kadhaa Kurugenzi ya Habari Ikulu kwa lugha za mitaani za uzandiki nk, pengine naweza kufikiria na kushawishika kwamba iliandikwa hivyo kwa maelekezo yake, vinginevyo hicho alichokisema kwenye hotuba yake angepima kwanza, lakini Mmmmmm, ukubwa nao kazi ndio maana unatakiwa kuwa na washauri mahiri.
 
Kuna some incidences watoto hudondoka kutoka kwenye mizani ya clinic na kuanguka chini kwa kuanza na kichwa.....pale lazima cartiledge ya lugha kwenye ubongo i shake.....!!!!!
 

kulikuwa na hoja gani ya kujibiwa na Rais Kikwete?
 
kwa kweli he has stooped so low, ila ninawonder na ni maswali haya; hivi hotuba zake zinaandikwaga? na kama zinakua zimeandikwa/kutayarishwa zinakua na hayo maneno au anakua anayatoa kichwani?
 

Si mlikuwa mnajipa matumaini jana kuwa amewapuuza CCM? sasa mnajing'ata nini?
 
Kuna mambo mengine Marais wa Nchi huongea kwa kuwa wanajua hakuna mtu yoyote wa kuwafanya kitu chochote...

Ukweli mtupu, nchi za Kiafrika Marais wanajiona miungu mtu hivyo hakuwa wa kumwajibisha, wakumnyooshea kidole, wa kumrudi, wa kumshikisha adabu nk. Hali hii ndiyo inayowapa sana kiburi hawa viongozi wa mataifa yetu. Wanatalii sana lakini hawajifunzi huko waendako.
 
kwa kweli he has stooped so low, ila ninawonder na ni maswali haya; hivi hotuba zake zinaandikwaga? na kama zinakua zimeandikwa/kutayarishwa zinakua na hayo maneno au anakua anayatoa kichwani?

na hotuba nzuri ni inayotoka kichwani, mbona mnamtetea sana LISSU.
 
Hajitambui kwamba yeye ni rais wa nchi... anadhani yuko kijiweni.
Na hili linatokana na kuwa na washauri kama rweyemamu... rejea press release za ikulu zilivyojaa mipasho ya taarabu !
Siku hizi viongozi woote wa ccm hawawezi kujenga na kujibu hoja.... wamejikita zaidi kwenye mipasho na personal attacks; Ni aibu kwamba hata raisi amefikia huko. But it is not surprising... rejea hotuba yake miaka kadhaa iliyopita alivyomshambulia Mgaya wa TUCTA.
 
Mkuu umeeleza jambo ambalo binafsi lilinichanganya kichwa kwani ukiona Rais wa nchi anaongea vile ni wazi watendaji wengine wameoza zaidi. Sio mara ya kwanza kuongea lugha kama hiyo nakumbuka wakati wa Mgomo wa waalimu alimwongelea Mgaya ktk lugha isiyomkidhi Rais wa nchi. Na mengine mengi yaliyokuwa yanaonyesha kwamba amegadhifika. Lazima tuwe makini sana tunapozungumzia mustakabadhi wa taifa letu kiuongozi kwani tunakoelekea ni pabaya zaidi. Mimi ningependekeza vyama vya siasa vitumie utaratibu wa nchi kama Marekani kupata Wagombea wa Urais ili mwisho wa siku tupate cream ya wagombea urais. Kipimo tunachotumia cha kikundi cha watu 10 au 50 kuchagua Rais wa wananchi mil 40 ndio matokeo yake haya.
 
kwa kweli he has stooped so low, ila ninawonder na ni maswali haya; hivi hotuba zake zinaandikwaga? na kama zinakua zimeandikwa/kutayarishwa zinakua na hayo maneno au anakua anayatoa kichwani?

Inawezekana waandaaji wa hotuba ni kumpa habari za anayotakiwa ayaseme, vinginevyo angekuwa ameiandaa na kupitia kisha kupima lugha iliyotumiwa hayo maneno yangeshtukiwa na kufanyiwa uhariri kabla hajatokea jukwaani. Pengine amezoea ya kichwani mwake tu.
 
Wewe ulitaka mtu mnafiki amwambiaje zaidi ya kumwambia ukweli wake jk kafanya haki mnafikinlazima lazima ambiwe ukweli lisu kazidi unafiki na umbea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…