Rais Kikwete amteua Biswalo Mganga kuwa Mkurugenzi mpya wa mashtaka (DPP)

Rais Kikwete amteua Biswalo Mganga kuwa Mkurugenzi mpya wa mashtaka (DPP)

Rais Kikwete amemteua Biswalo Mganga kuwa Mkurugenzi Mpya wa Mashtaka nchini (DPP). Kabla ya uteuzi wake, Biswalo alikuwa Mkurugenzi msaidizi katika ofisi hiyo ya mashtaka. Uteuzi umeanza rasmi ijumaa iliyopita.

Dr Eliezer Feleshi ndie alikuwa akishikilia wadhifa wa DPP kabla ya uteuzi huu wa DPP mpya kufanyika.

==============


Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Biswalo Mganga kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) nchini.

Taarifa iliyotolewa Ikulu, Dar Es Salaam, leo, Jumatatu, Oktoba 6, 2014, na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi (KMK), Bwana Peter Ilomo imesema kuwa uteuzi huo umeanza Ijumaa iliyopita, Oktoba 3, mwaka huu, 2014.

Kabla ya uteuzi wake, Bwana Mganga alikuwa Mkurugenzi Msaidizi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka na Wakili wa Serikali Mfawidhi.

Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu – Dar es Salaam.

6 Oktoba, 2014


Mkiambiwa kuna mtu ameshika remote control na kutuonesha channel anazotaka yeye mnabisha sasa mnaona ushahidi
 
Mkiambiwa kuna mtu ameshika remote control na kutuonesha channel anazotaka yeye mnabisha sasa mnaona ushahidi
kuna kitu jiwe alikuwa anajaribu ku prove!

watu wake hao hao walipitia mikono ya huyu jamaa!

haya na kazi iendelee!
 
kuna kitu jiwe alikuwa anajaribu ku prove!

watu wake hao hao walipitia mikono ya huyu jamaa!

haya na kazi iendelee!
1620757941726.png
 
Back
Top Bottom