Rais Kikwete atangaza nia ya kuanza kwa Ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR)

Bongo wepesi wa kusahau
 
SGR,JNHPP,BRT phase 2 kwenda mbele,flyovers etc,Tanzanite bridge,busisi bridge,wami bridge,gvt city,magufuli,bridge etc zote JPM
Acheni hizo, hiyo inakuwa kwenye mpango wa taifa wa miaka mitano na huwa hizo mega projects zinaainishwa then zinatengewa bajeti yake. Sio eti kila raisi anakuja na mradi wake. Tukumbuke hela ni zetu kwa hiyo serikali ikiongozwa na raisi ndio hutekeleza. Pia miradi ina michakato mingi, kwa hiyo inawezekana kabisa ilianza hata kipindi cha mkapa.
 
Wabongo hua tunasahau upesi sana. Na pia ni wakurupukaji, Tena wepesi kudanganywa...hii miradi ilikuwa ni mipango ya serikali, mingine ilikwishatengewa fedha na mingine iloshaomnewa fedha na serikali ya awamu ya tatu na nne... JPM alikuwa waziri wa ujenzi na anayajua haya..alipokuwa Rais alitekeleza miradi iloyoleishapangwa na WENZAKE...ni vile tu serikali Ile ilianzaga mambo ya kusifu sana..nasema Ally Mwinyi, Mkapa na Kikwete walifanya makubwa sana ya maendeleo nchi hii
 
Ila mipango ya kuiba hela za nchi huwa inapitia michakato gani? Mbona kila mwaka CAG anatoa ripoti za madudu?

Huyo mzee wala hana relevance sababu hakuna alichokifanya zaidi ya kutia nia ila hakutekeleza aliyemfuata ndiye katekeleza.

Hilo la relevance ni maoni yako tu haiondoi ukweli kuwa alijenga UDOM, Mloganzila, Mabarabara mengi tu, Mieadi ya umeme Kinyerezi 1 na 2, Mwendokasi, Uwanja wa Ndege wa JKN, Daraja la Kigamboni, Malagarasi na mamiradi mengi tu ambayo mwendazake alijilimikisha baada ya kuingia madarakani.
 
Sawa ila kwenye SGR msimpe sifa ambazo hastahili
 
JK hakujenga uwanja wa Ndege wa JKNI, aliongeza Terminal 3 tu ambayo nayo haikuimaliza hadi anaondoka.
 
Kuahidi ni Rahis lakini bingwa ni yule anayetafuta fedha na kusimamia.Harafu hapa kikwete alikuwa na akili ya SGR kama Ile ya Kenya inayotumia mafuta
 
Asante Intaneti na google, historia inawekwa sawa. Miradi mikubwa mtu mmoja hawezi kukamilisha.
Rais Samia Suluhu Hassan naye atamuachia mwingine kumaliza

 
Kiko wapi?
 
Alikuwa mzee wa michakato tupu, nchi ilipata hasara sana kuwa na huyu uongozini

..hakuna awamu ambayo hajafanya maamu

..waliowezesha nchi kuwa na access na matrilion ni Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa.

..Mwinyi na Mkapa walikuta serikali ina matatizo makubwa ya kifedha na ina wakati mgumu sana kupata misaada au mikopo.

..Mzee Kikwete, Magufuli, na Mama Samia, wao wamekuta nchi inaweza kukopeshwa, na kupata misaada toka nje.

..hakuna Raisi ambaye hakujenga mradi wa umeme, daraja la kimkakati, au kuendeleza bandari.

..kwa mfano, daraja la mto Rufiji, ujenzi wake ulianza wakati wa Mzee Mwinyi ukakamilika wakati wa Mzee Mkapa. Wananchi wa mikoa ya kusini walikuwa na shida kubwa ya usafiri wa barabara wakati wa Rais Nyerere, na Mwinyi, wamepata nafuu wakati wa Mkapa.

..Mkapa ndio alikamilisha ujenzi wa daraja la Mto Rufiji lakini hawezi kubeza jitihada za Nyerere na Mwinyi kupeleka barabara kusini.

NB:

..Wazo la kujenga bwawa la umeme Stieglers lilikuwepo toka wakati wa Mwalimu Nyerere.

..pia kulikuwa na wazo barabara ya kwenda mikoa ya kusini ipite ktk mradi wa Stieglers.

..Mradi wa ujenzi wa reli toka Tanga kwenda Musoma uko kwenye mipango ya serikali toka wakati wa Mwalimu Nyerere. Na una kikwazo kikubwa kwamba unaepuka vipi kupita ktk mbuga ya Serengeti.
 
Alikuwa mzee wa michakato tupu, nchi ilipata hasara sana kuwa na huyu uongozini

..barabara zilizojengwa wakati wa Kikwete thamani yake ni trillion ngapi?

..kitu kingine Kikwete hakujitangaza sana kama Magufuli matokeo yake hapaswi sifa za kujenga miundombinu.

..kwa upande mwingine Kikwete alikuwa na nafasi ya kufanya vizuri zaidi ya pale alipofika.

..SGR ilipaswa kuanza wakati wa JK ila alikuwa na tabia ya uzembe na upigaji.
 
Very true maguguli alikuwa na mission na vision ndo maana tukafika
 
Kikwete amejenga barabara kibao kipindi chake sema kipindi chake hakuwa mtu wa kuchukua sifa za kila kitu ndio maana magufuli naye alipata sifa za kujenga barabara kama waziri kwa sababu kikwete hakuwa mtu wa kubeba credit za mawaziri.
 
Watu ukiwauliza shule za Kata wanasema ni Lowasa huyo teh teh teh

Hivyo ndivyo jinsi JK anavyochukiwa
Yote kwa sababu ya chuki tu,waziri mkuu hana ubavu wa kuamua kitu bali Rais ndiye mwenye mamlaka hata barabara utasikia Magufuli lakini wakati wa Magufuli kila kitu alikuwa akisifiwa Rais husikii PM wala waziri wa ujenzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…