Nikukumbushe tu kwamba aina ya quotation uliyofanya inapendeza zaidi kwa kujibu hoja badala ya kujibu hoja na kuchomekea maswali kwavile inakuwa headache kujibu kila kipengele hasa kv ukishafanya quotation; maelezo zile individual quotation huwa zinachanganyika. Hata hivyo, acha nijibu machache.
...niwie radhi.
Mimi nilisema hivi:
Ninachosema ni kwamba huwezi kujenga uchumi kwa njia za kufikirika...kwamba kwavile (say) Air Tanzania haina ndege wakati hata Rwanda wana ndege ndo basi tena nasi tununue ndege bila kufanya prioritization...huo utakuwa ni uchumi wa ajabu! Ninachosema ni kwamba we've already messed up for the past 50 years kwahiyo katika mazingira kama hayo ni lazima ufahamu uanze na nini kisha ufuate nini!
Kisha wewe unahoji:
..tuliposema tunafufua shirika na tukaweka mkuu "mpya", kumbe haikuwa priority? what are you trying to say? we are jokers? or am i missing the point here.
Ngoja nikuulize; yaani unaamini hoja yako inafanana na nilichosema mimi? Mimi nimezungumzia suala la ku-prioritize…kwamba kwavile kunakuwa na multiple objectives wakati resources haziwezi kukidhi mahitaji yote, basi busara zakiuchumi ni ku-choose among multiple objectives! Na ndio maana nikasema, huwezi kununua ndege kwavile tu umeona Rwanda nchi ndogo wana ndege. Inawezekana wao ndege ndiyo kipaumbele!
...ndugu, ulipoweka mfano wa shirika la ndege tu, uliupeleka mjadala huko! sasa, labda tujadili au pengine tujiulize, nia ya kufufua shirika -ambapo kulikuwa na mpango wa kununua ndege- ilikuwa ni nini? je, hii haikuwa kipaumbele katika sekta husika?
...kwani, tuliposema tunafufua shirika la ndege, na tutanunua ndege, tulikuwa tunashindana na mtu? si tulikuwa tunatekeleza vipaumbele kwenye sekta hii.
...je, katika miaka ile, vipaumbele katika sekta ya usafirishaji vilikuwa ni vipi? sidhani kama ilikuwa ni barabara pekee. ila, unaweza argue kwamba, ukiangalia resource allocation, ilikuwa ni barabara pekee. but that is misleading, as far as mipango ya taifa inahusika.
Baadae uka-quote kipengele kidogo tu katika hoja mzima. Ulicho-quote ni:
Umechukulia mfano wa umeme....kuna watu wanadai zamani hapakuwa na matatizo ya umeme huku wakisahau kwamba enzi hizo hatukuwa na demand kubwa ya umeme!!
Ulichohoji ni:
..umeme unatolewa bure? kama unatolewa bure -kwa watu kutolipa bill zao- tunafanyaje? tunaacha ku fulfill mahitaji yaliyopo na yajayo?
...kwa mtindo huo, tutavutia wawekezaji wa aina gani?
Lazima niseme wazi wala
sijaipata hoja yako hasa nikizingatia kwamba hakuna uhusiano kati ya nilichosema na ulichohoji.
JokaKuu alihoji nchi kuwa na uhaba wa umeme kwa muda mrefu sasa nami nikaeleza demand ya umeme before economic liberalization kwamba ingawaje tulikuwa hatuzalishi umeme mwingi kabla ya mageuzi ya kiuchumi lakini bado umeme huo huo kidogo ulionekana kutosha na hivyo nchi kutokuwa na mgao. Umeme ulikuwa unatosha kv hapakuwa na demand ya umeme even at household level; na ndio maana nikatoa mfano wa pasi ya umeme, kwamba ungeweza kuzunguka mtaa mzima (tena mahali kama Dar) lakini bado usikute nyumba yenye pasi ya umeme! Kwa bahati mbaya au mzuri, tuka-liberalize our economy; demand ya umeme ika-shoot ghafla not only at commercial level bali hata kwenye household level! Matokeo yake wakati zamani ungeweza kuzunguka mtaa mzima usikute nyumba yenye pasi ya umeme, leo kwa mji kama Dar unaweza kukuta nyumba yenye familia tano nayo ina pasi tano za umeme, mafriji matano, majiko matano ya umeme and so on!! Haya yalitokea kabla hatujajiandaa na matokeo yake umeme nao ukawa ni among of multiple objectives! Huku tunahitaji umeme, kule tunahitaji barabara! Huku tunahitaji hospitali na madawa kule hakuna shule. Hizo ndizo multiple objectives. Sasa basi, katika mazingira kama hayo ni lazima uangalie uanze na kipi na kwa kiasi gani kisha kifuate kipi na kwa level gani. Unatakiwa kuangalia uanze na kipi na kwa level gani kwavile huna resources za kutosha ku-cover yote kwa pamoja! Wewe wa mjini unaweza kuona kipaumbele chako ni umeme wakati wa kijijini kipaumbele chake ni angalau zahanati!
...maana yangu, kwa ufupi, ni, kama kuna soko la kitu, halafu ni cha muhimu katika maendeleo, yeyote, nasisitiza!, yeyote ya nchi, hiyo huwa kipaumbele namba uno!
...infact, si kipaumbele, ni zaidi ya kipaumbele. ni msingi wa vipaumbele vyote!
...hatuwezi kujitetea tukatoka salama hapo. tukubali tu. tumefeli huo mtihani, ili, tuurudie vyema.
Kisha uka-quote hii:
Baada ya economic liberalization, demand ya umeme ikaongezeka maradufu ndani ya kipindi kifupi wakati uzalishaji ulikuwa ni uleule! Demand ikaendelea ku-shoot year after year na hivi sasa umeme ni moja ya zile multiple objectives ambazo nimezisema awali! Sasa unapokuwa katika mazingira kama hayo ni lazima u-choose among the best alternatives! Huku hakuna umeme, kule hakuna barabara, upande wa pili hakuna maji; mtaa wa tatu, shule na idadi ya wanafunzi vimeongezeka maradufu; ukigeuka upande mwingine unakuta unalazimika kuongeza vituo vya afya...and so on!! Katika mazingira kama hayo, lazima uchague, uanze na kipi na kwa ukubwa gani unless kama kuna sehemu ambako unaweza kwenda kuchota fedha na kumaliza yote hayo kwa pamoja!
Kisha na wewe unahoji:
...kama movie ati eeh! and unafikiri hivi vyote vilitokea kwa overnight?
...kwa ufupi, unasema there is none we can do about it.
Hiyo hoja yako ya kwamba "kwa ufupi, unasema there's none we can do it about!" Are serious? Kwanini unasoma vitu nusunusu? Ni kweli unasoma nusunusu au unaamua tu kupotosha? Ina maana hujasoma kipengele cha chini nilichosema: "Katika mazingira kama hayo, lazima uchague, uanze na kipi." Kwahiyo according to you, ku-prioritize mambo ni sawa na nothing we can do?!
...sikuamua kupotosha, si hulka yangu.
...nadhani, hili nimeshalijibu hapo juu.
Kisha ukaja hoji tena kwa kusema:
..NasDaz, umekuwa humu kipindi sasa, unataka kusema hujawahi ona mjadala unaoongelea nini kifanyike kuhusiana na suala fulani?
...suluhisho la maana ni lipi?
...nadhani, uzembe mwingi ni ule wa kutumia akili.
Kama umenisoma vizuri nimesema kwamba watu tunajadili mambo yale yale tena kijumla jumla. BInafsi niliweka tatizo kubwa la msingi kwamba ubongo wetu ume-stuck na tumeshindwa kuwa na vyanzo vikubwa vya mapato. Sijaona mjadala wa kina unaozungumzia vyanzo vikubwa vya mapato. Kama upo, nipe link.
...wengi hujadili hivyo, ndio. ila, wapo wanaojadili to the word.
...vyanzo vya mapato vilivyopo havitumiki vizuri, or rather, mapato yenyewe. sidhani kama ubongo umekwama.
...hizo threads zipo, sina link zake.
Kisha tena ukaja na hoja hii:
...vyanzo (vya umasikini) vinafahamika! angalia ubora na ufaulu katika elimu, ubora na upana wa huduma za msingi za afya. angalia vikwazo katika umiliki mali, na uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.
Tunaambiwa kwamba zamani tulikuwa na ubora mkubwa sana wa elimu; je tulikuwa katika hali gani kiuchumi kwa kulinganisha na ubora wa elimu ambao tulikuwa nao? Unapozungumzia vikwazo ktk umiliki mali unamaanisha nini hasa? Unataka kuniambia kwamba unakatazwa kumiliki mali au unazungumzia wale wanaotaka kuwa madalali wa vitalu vya gesi?
...ni kiasi gani iko rahisi kwa mwananchi wa kawaida kabisa aka masikini, kupimiwa ardhi na kuthaminishwa, kisha kupewa cheti cha umiliki na cha uthibitisho wa thamani yake? je, nyumba ya Abdallah pale kwa Mnyamani, haina thamani? au anawezaje kuithaminisha katika namna iliyo rahisi?
...MKURABITA uko wapi?
Kisha ukahoji:
...nigusie zao moja tu, korosho. tunajua jinsi gani mkulima wa zao hili huko nyuma alifaidika na hivi sasa hali ikoje? hapa ndipo kilipo chanzo cha umasikini katika eneo hili.
Hiyo neema ya zao la korosho ilidumu kwa muda gani? Mimi natokea Lindi, moja ya mkoa ambao unazalisha korosho lakini hiyo neema ya korosho inayozungumzwa wala sikuikuta! Which means, hata kama neema hiyo ilikuwepo lakini haiku-exist kwa muda mrefu.
...swali ni kwanini? je, utekelezaji wa zoezi la vijiji vya ujamaa ulichangia?
...hali hivi sasa ikoje? unapomkopa mkulima masikini unategemea nini?
Hoja yako nyingine:
...matumizi ndugu, matumizi! hata kama tukipata fedha wanayopata Saudia, haitasaidia kama matumizi yatakuwa ya hovyo hovyo na yasiyo na ufuatiliaji wala kuwajibishana. unasoma ripoti za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali? unajua ni kiasi gani cha fedha kinapotea katika halmashauri zetu? hebu tuanzie hapo!
Hilo la ufisadi nimeshalisema sana hadi nikatoa thread zaidi ya tatu humu jamvini nikishauri tuachane na na what's so called Good Governance na badala yake tuwe na Approved Dictatorship Governance. Nilitoa hoja kama hiyo kwavile mimi naamini Tanzania kuna tatizo kubwa sana la ufisadi…jamii yote imeoza bila kujali dini wala itikadi za kisiasa; wengi wetu ni watu wa hovyo sana! Tanzania ni jamii ya watu tusiokuwa na maadili; in short wengi ni wezi! Kwa bahati mbaya wezi hawa wanalindwa na Mfumo wa Utawala Bora! Moja ya misingi mikuu ya Utawala Bora ni Utawala wa Sheria! Katika Utawala wa Sheria mtu ataonekana ana hatia provided imekuwa proved beyond reasonable doubt in the court of law kwamba muhusika ametenda kosa! Ni nani basi anaweza ku-prove beyond reasonable doubt kwamba mtuhumiwa ametenda kosa wakati jamii yenyewe imeoza kwa ukosefu wa maadili?
...swali muhimu kabisa. nakubaliana nawe.
Lakini kwa upande mwingine, leo hii hata kama haitaibwa hata senti tano, lakini bado changamoto za umaskini hazitaisha kwavile bado mapato yetu ni madogo sana. TRA kwa mwaka wanakusanya kiasi cha Sh. Trillion 7 tu (and am afraid kama wanafika). Tuseme wamekwiba nusu, wameleta nusu na sasa tuseme wanakusanya Trillion 14 na kisha Bajeti yetu ipande kutoka kutoka Trillio 18 hadi Trillion 30! Hata hivyo, ni bado sana katika kuwa na uchumi bora.
...mapato yetu si madogo. na bado kuna uwanja wa kuyaongeza.
...kuna tatizo kwenye matumizi. don't ask me for details, zinaonekana wazi. nilikutolea mfano wa halmashauri zetu.