Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

Sijui wewe ni Malay wa aina gani. Wapinzani ndo walistukia hiki kikokotoo kibovu na wakakipinga kwa nguvu leo hii mmetatua tatizo mlilotengeneza wenyewe then unakuja hapa unashangilia Kama zuzu


Mkuu punguza hasira hahaha.
 
Siku za mbele litaibuka kundi linataka kuandamana kumpongeza kwa uamuzi alioufanya leo
wakati mwingine huwa nashangaa sana kwakweli.... nakumbuka watu walivyoshangilia kuhusu korosho kilichofuatia hakuamini.
Raisi magufuli ni katili hana huruma na mtu yule
 
Pascal mayalla nahitaji utie neno hapa nisaidie kumtag huyu mtu jamani nisikie hekima yake hapa
 
Watu kama wewe ndio wapumbavu wa kwanza, ambao hamna tofauti na viongozi wa vyama vya wafanyakazi Rais anaosema wanatumika kisiasa.
Kila kukicha ni kusifia tu jembe lako hata kama kafanya upuuzi, walipo leta 25% ulisifia wenye akili wakakosoa leo rais kusema 25% iwe suspended baada ya kuwaelewa wenye akili unasifia tena.
Bora ungekuwa nyama uwe kitoweo


Sent using Jamii Forums mobile app



Kuna watu kazi yao kusifia kila kitu.
 
Bwanamkubwa kapata la kufungia mwaka. anamaliza mwaka akiwa shujaa anasifiwa. makofi na vigeregere kwake. kama ilivyo kawaida yake anatengeneza tatizo kisha analaumu watangulizi . anatufanya fyatu hatuna akili. kwakuwa tumezoea kusifia tutasifia .... haijawahi kutokea? .... ni raisi wa pekee... hamnazo.
kama nilimsikia vizuri bwana haambiliki alisema kikotoo kimeahirishwa hadi 2020 nasi twashangilia kama kumeza panadol kupunguza maumivu mnashangilia nini?
Mwaka wa tatu baada ya raisi kuingia madarakani 2015 hakuna nyongeza ya mishahara wala maslahi mengine huku hali na gharama za maisha zikiwa zimepanda sana kuanzia kodi ya pango mpaka nauli za kwenda kazini. watumishi wananyanyaswa wanaitwa majina mabaya kila uchao.
swali langu kwa viongozi wa vyama MLIKUWA MNASHANGILIA NINI PALE IKULU?
watumishi wa umma wa Tanzania amkeni hakuna viongozi wanaowajali ni waigizaji tuu
Hakuna mtu anayejali maslahi ya watumishi hapo.
Watumishi lazima mjue namna mtakavyo compansate mjiandalie maisha yenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watumishi ndio wakati wenu huu! Tembeeni kifua mbele
 
halafu mpaka waliotunga hii sheria ya ovyo nao walikuwa wanashangilia na kumpongeza rais kwa kuwatetea watumishi.
 
hiki kinachofanyika ikulu leo ni kulivua bunge nguo,kwa utaratibu wa kawaida ili mswada wa (usio wa dharula)kuingia bungeni ni lazima hatua ya kwanza kuwashilikisha wadau husika...sasa hawa wote walioko ikulu ni wadau wa mifuko ya jamii iweje leo kila mtu analalamika inamaana maoni yao hayakutiliwa maanani au labda kanuni hazikufuatwa!
Mkuu ukimsikia Rais kwa Umakini Inaonesha Wazi Mifupo haina pesa sasa kikotoo cha 25% ilikuwa ni njia yakutokea, all in all Aibu kwa wabunge Wa CCM.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Asalaaam,wapendwa!!!!
  • Namshukuru mheshimiwa Rais Dr John Magufuli kwa kazi kubwa anayofanya kwa Taifa letu pendwa la Tanzania.Lakini sikubaliani na namna watendaji wetu wanavyoacha majukumu yao ama kwa kuharibu,kukosea,kuchanganya mambo na kuleta sintofahamu kwa wananchi hivyo kumuachia mzigo wa lawama Mh Rais.
  • Hivi karibuni kulijitokeza suala la kikokoto kwa watumishi wa umma,ni jambo ambalo kiukweli lilifanywa bila weledi wa kutosha watumishi walio wengi walilalamikia sana hili lakini watendaji(wahusika)walikaa kimya hadi leo hii ambapo Rais amejitokeza kuliongelea na kufuta mpango ule.
  • Sio hivyo tu kuliibuka suala la wimbo wa Taifa,bendera wahusika(wizara &co)wananchi walitoa maoni yao lakini hola hadi pale tena alipojitokeza mh Rais na kulitolea ufafanuzi na kufuta mpango huo.
  • Suala la korosho nalo wahusika walishindwa vibaya kutafuta ufumbuzi mpaka pale alipojitokeza Mh Magufuli na kulitatua kwa uharaka.
  • Ni mengi sana hadi yanayopaswa kufanywa na watendaji wa vijiji,kata hadi yamsubiri Mh Rais ajitokeze kutatua?????shame!!!!!ifikie mahala tumsaidia Kiongozi huyu kuyafanya masuala mengine ili na yeye afanye ya kimataifa zaidi,tusimzeeshe kwa vijimambo vidogo vidogo tumpe changamoto zile kubwa.
  • Wabunge,mawaziri,wakuu wa mikoa,wilaya na makatibu tawala wote,tarafa na watendaji wa kata,vijiji,wasomi wetu msaidieni dr Magufuli aweze kudumu na kumaliza kipindi chake akiwa timamu na sio dhaifu.
  • Kama yote haya anayafanya yeye na tunamtegemea kwa kila jambo basi tumpeni nafasi kubwa ya kutawala hadi siku akichoka mwenyewe.
  • Masinki,serengeti
 
Wabunge wa ccm na mawaziri pamoja na mwenyekiti wao wanakaa wanashauriana ujinga na kuupitisha..
Halafu wanakuja tena kukaa na kushangaa ujinga wao.
TUNAEANDA AU TUNARUDI NYUMA?
 
nimeanzisha uzi huu kabisa kumpongeza rais wetu kwa maamuzi yake ya leo.
tunahitaji Rais msikivu na anayejali maslahi ya Taifa na ustawi wa wananchi wake. Hili rais wangu umelionyesha bila kusita.

pia umegusia hata fao muda maalum kama wafanyakazi wa migodi au kazi za muda

niseme ukweli kabisa napenda upinzani sutawi lakini utendaji wako hauna shaka kabisa.
sisemi hatuhitaji upinzani ila tunahitaji upinzani wa mawazo mbadala na kuboresha zaidi

pi a natumia nafasi hii kumpongeza mbunge wa chadema aliyesimamia swala la kanuni ya kikokotoo kuingia kwenye sheria.

Tanzania yetu ni moja na sisi sote ni wamoja. hongera wapinzani na hongera Rais wetu

pia hongera wa elimu bur watoto wa masikini kule kijiji umefanya difference kubwa sana, pia hongera kwa mradi wa kimara to kibaha na pia hongera kwa stand ya ubungo.

maamuzi ya leo umegusa wengi na umeonyesha namna gani unaelewa haki


kama umeguswa na maamuzi ya leo ema kitu hapa
 
Kwe
Wabunge wa ccm na mawaziri pamoja na mwenyekiti wao wanakaa wanashauriana ujinga na kuupitisha..
Halafu wanakuja tena kukaa na kushangaa ujinga wao.
TUNAEANDA AU TUNARUDI NYUMA?
aliyekwambia kikokotoo ni cha ccm nani?, bunge halitengenezi kikokotooo ndugu
 
Back
Top Bottom