Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

[emoji38][emoji38][emoji38]
FB_IMG_1546009134332.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekua nikishangaa ukimya wa viongozi wa vyama vya wafanyakazi hasa TUCTA pale wanapokua wanasifiwa na Rais Magufuri kua ndo aina ya viongozi anawaowataka nikashangaa kweli yani wewe uombe kura kwa kua utaenda kutetea maslahi ya watumishi na ulipwe vizuri kisha uufyate ukae kimya hadi wabunge waupinzani na watumishi wapaze sauti zao alafu Leo bila aibu Rais anatengua 25% Viongozi wa TUCTA,Cat,Tughe wanashangilia hadi wengine wakitikisa makalio yao kwamba wametetea watumishi je ni kweli wamekua wakitetea watumishi? Kwanza kabisa viongozi wanaopaswa kua ktk trade unions ni aina ya viongozi wenye ushawishi,uharakati na wengi kutopendwa na waajiri....Madai ya watumishi ni Zaidi ya Fao hili la 25%.... Labda niwakumbushe TUCTA wenzao wakina MGAYA na wengine walikua hawafanyi mazungumzo na serikali kwa kujificha zaidi walikua wakiomba wakutane mezani na serikali ilipokaidi walianzisha migogoro hadi serikali ilitii na tuluona mabadiriko....Lakini kwa Miaka hii mitatu ya JPM tumeona TUCTA wakikaa kimya baada ya kusifiwa na JPM kua ni viongozi bora uku serikali ikiwa haitimizi na zaidi kudumaza waajiriwa wake...Baadhi ya Mambo ambayo TuCTA ya sasa haijaweza na serikali kuendelea kukandamiza ni kama:-
1.Serikali kushindwa kuongeza mishaara tokea 2015
2.Serikali kuvurunda kwenye Madaraja ya watumishi yani serikali inaweza ikaamua kupandisha baadhi wengine ikaacha mfano mpaka sasa bado serikali inapandisha wa 2012 na kimsingi ilipaswa kua imemaliza 2016 na sasa ingekua inapandisha walioajiriwa 2014 au walipandishwa madaraja 2014....Lakini watumishi wamezulumiwa haki yao ya madaraja kwa miaka hii ya JPM na mbaya zaidi amedhulumu haki za msingi za madeni yatikanayo na madaraja....Aya ndo mambo ambayo ni ya msingi haingii akili watumishi wanaanza kazi mwaka mmoja,kada moja lakini mishahara yao tofauti na hivyo kupelekea ata mafao yao kua tofauti...Viongozi wa watumishi lazima mjue kua hakuna mahali popote Duniani viongozi wa wafanyakazi wakapendwa na serikali ukiona hivyo basi jueni hamtetei maslahi ya watumishi zaidi mnatetea unyonyaji wa serikali....Miaka 3 bila nyongeza mpo kimya,Miaka 3 madaraja yamekwama mpo kimya then mnaenda Ikulu mnatingisha mawezele kua mmeshinda! Poor You!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
UPDATES:



Viongozi wa Vyama vya wafanyakazi wametoa historia ya walikotoka hadi walikofika. Aidha, wamedokeza kuwa wapo waliozimia kwenye ofisi za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Rais Magufuli anawasikiliza na anataka kila mtu aongee na kutoa dukuduku ili aweze kuongea.

Viongozi wa vyama vya wafanyakazi (upande wa walimu) wanadai kikokotoo kimekuwa ni suala kubwa na Rais Magufuli kama mwalimu anatambua changamoto za walimu. Wanamwomba Rais aliangalie suala la kikokotoo kwa jinsi atakavyoweza kwakuwa wanajua anaweza na kwa wanavyomsaidia Mungu atamsaidia alitatue hili.

TUGHE: Tunakupongeza Mhe. Rais, lakini tunapenda ufahamu kuwa wastaafu wengi hawakuwa wameandaliwa na mabadiliko haya yametokea ghafla na kusababisha negative impact. Morali ya kazi imeshuka!

Waziri Mhagama
Hoja na kuunganisha mifuko ilikuwa ni hoja ya wafanyakazi.

Hapa tunazungumza tu kikokotoo, ili tupate kikokotoo lazima turudi kwenye contribution rate, tukitaka tuendelee na kikokotoo cha 50% contribution itabidi itoke kwenye 20% hadi 25%.

TUCTA: Tunafahamu kwa moyo wako na unavyowasaida wanyonge. Tunaamini utasaidia kutatua

Mwanzo Wastaafu walikuwa wanapata 50% kwa mkupuo na 50% kidogo kidogo kila mwaka

Tulipendekeza mkupuo uwe 40% na si 25%


CHAMA CHA WALIMU: Suala la kikokotoo ni shida, hakuna asiyejua shida za waalimu. Uzuri ni kwamba hata wewe Rais ni Mwalimu

Kwasasa hata mishahara ya mwisho wa mwezi haitoshi. Kwa namna unavyofanya mambo makubwa najua hata hili unaliweza


TUGHE: Wastaafu wengi hatukuwaandaa kisaikolojia. Mabadiliko haya ya kikokotoo cha mafao yametokea kwa ghafla sana.

Wafanyakazi wa umma waliowengi wanalalamika nakuomba mheshimiwa Rais uongee chochote ili Wafanyakazi warudi kwenye morali ya kazi

TUICO: Watu wa sekta binafsi kima chao cha chini ni 100,000. Ili kwenda vizuri kamati itakayoundwa ikachunguze hii mishahara

Pia kuna fao la kupoteza ajira hawalipwi na makampuni mengi yanaondoka bila ya kuwalipa


WAFANYAKAZI WA RELI: Tumepitia misukosuko sana ikiwemo mishahara kuwa kidogo na ulipwaji wake ni wa kusuasua sana

Tulitegemea mafao ya kustaafu yatusaidie kujenga nyumba ili hata tukifa tufe vizuri.

Ile 50% ya awali kama haiwezekani basi tunakubali iwe 40%


TAMICO: Kwenye suala la kikokotoo kuna shida hasa kwenye fao la kujitoa ambalo mbadala wake ni fao la kukosa ajira

Sekta binafsi tunapata shida kwasababu kazi zetu si za muendelezo. Tunaomba iwepo tofauti kwa watu wa sekta ya migodi na ujenzi kwenye fao la kukosa ajira


SERIKALI ZA MITAA: Tunapenda mifuko iwe imara lakini kwa mishahara yetu hii midogo kwa kweli inaumiza

Rais kelele ni nyingi sana, na kwa kikokotoo hiki mfanyakazi akistaafu atashindwa hata kujenga


CHAMA CHA WAAJIRI: Sheria hii ya mifuko ya jamii, ililenga kuiweka mifuko hii kuwa katika hali ya usawa

Baada ya mifuko kuunganishwa uchangiaji umekuwa ukitofautiana kutoka mfanyakazi mmoja hadi mwingine.

Kila mfuko una tafsiri yake ya mchango wa mwanachama


HOTUBA YA RAIS MAGUFULI

Nimeamua niwaite wote ili niwe referee na inawezekana nikawa refaree mbaya

Nisingeweza kuwaita Wafanyakazi wote na tatizo hili naona litafikia mwisho.

Rais Magufuli: Kwenye baraza la Mawaziri tulikubaliana kuinganisha mifuko ya jamii

Hatua hii ilitokana na maombi ya muda mrefu ya vyama vya Wafanyakazi kutaka mifuko iiunganishwe

Watu walijua inaelekea kufa na kweli ilikuwa inaelekea huko

Nimewasikiliza, hapa tunaweza kuongea ikafika jioni. Tunaweza kunaliza yakaletwa mengine na ndio maana nataka tu concentrate sehemu moja. Ndio maana nimeleta regulator ili watoe mawazo yaliyo academic.

Nilipokuwa mwalimu nilianza na mshahara wa 1045, ninapofanya kazi nikataka kustaafu nianze kupata usumbufu naomba sio vizuri ndio maana nimewaita hapa tuzungumze.

Mtakumbuka tarehe 20 Oktoba 2017 baraza la mawaziri tulipitisha kuunganisha mifuko ya kijamii iwe mmoja kwabajili ya watumishi wa umma na NSSF ifanyiwe marekebisho ili iwe kwa ajili ya wafanyakazi wa sekta binafsi.

Sababu ya kuunganisha mifuko hii ni kwamba watu walijua inakwenda kufa na kweli ilikuwa inakwenda kufa.

Kabla ya mifuko kuunganishwa kila mfuko ulikuwa na wanachama wake. Jumla ya wanachama wote ilikuwa milioni 1.2.

Awamu ya tano mifuko ilikuwa hali mbaya na walikuwa wanapigana vita na kugombania wanachama.

Hii mifuko pengine ilikuwa inaendesha kiajabu ajabu. Miradi mingi ikawa inaanzishwa hasa ya majengo. Nenda Dege Eco Village, Kigamboni uangalie majengo yale sasa mwekezaji alikuwa anategemea return gani?

Tulipoingia madarakan tulikuwa deni kubwa la trilioni 1.2, ikabidi tutafuta pesa Serikalini tukaanza kulipa madeni haya na tumelipa yote mpaka March 2017.

Rais Magufuli: Sheria inawataka wapewe kidogokidogo si bora unipe zote nikafe vizuri

Mtu anafanyakazi yake kwa muda wote, halafu anamaliza unamwambia apewe asilimia 25, haiingii akilini. utanipa kidogokidogo? hata Waziri akimaliza Ubunge wake ukimwambia utampa 25% kisha nyingine kidogo kidogo hawezi kukubali

Kuna challanges ambazo hatuwezi kuzikwepa kwenye mifuko hii na ninyi wenyewe mmesema kuwa matatizo yapo

Ni lazima kuzitatua changamoto hizi, mmesema watu wanapenda #Kikokotoo kitoe angalau 50% ya mafao kama ilivyokuwa hapo awali

Wakati wa kuunganisha mifuko wastaafu walikuwa wanadai bilioni 700 na zaidi ya bilioni 500 zimelipwa.

Hii fomula iliyotumiwa na PSPF na NSSF haipo duniani.

Walioiweka ni makatibu wakuu wa wakati ule, sio wakati wangu

Rais Magufuli: Niombe kwenye mifuko waboreshe daftari la wastaafu ili kuondoa wastaafu hewa

Kama tulikuwa na wanafunzi hewa, watumishi hewa, pembejeo hewa hatuwezi kukosa wastaafu hewa

Rais Magufuli: Hifadhi za Jamii zipunguze matumizi ya hovyo, zikiwa fedha za Wastaafu zinatakiwa kulipwa kwa mkupuo hata wa 60% haitawezekana kwasababu hakutakuwa na hizo fedha

Yawezekana tatizo halianzi kwenye kikokotoo bali hata uendeshwaji wa mashirika haya

Nafahamu shirika moja linalotumia bilioni 1.3 kuchapisha kaenda na matangazo. Wanachama hamuwezi kujua kama fedha zenu zinatumika hovyo

Limeajiri walinzi na kuwalipa bilioni 2 kwa mwaka, kama wangeajiri SUMA JKT wangelipa bilioni 1

Nitoe wito kwa watendaji wakuu, tupunguze gharama za uendeshaji wa mifuko. Sasa imebaki mifuko 2 hakuna sababu za kushindana

Wafanyakazi wa Serikali ambao ni wanachama wa NSSF wahamishiwe PSSSF na wale wa sekta binafsi vivyo hivyo

Mashirika yaanze kuangalia namna ya kuongeza wanachama sioni sababu ya NSSF kuwa na wanachama laki nne nchi nzima wakati sekta binafsi inakuwa kila siku

Wale wafanyakazi wa migodi na ujenzi kuna sababu gani ya wao kusubiri hadi miaka 60 wakati kazi zao ni za kipindi kifupi.

Tuongeze option za wanachama. Kustaafu sio dhambi, kustaafu ni heshima lazima mstaafu awe respected

Mwalimu aliyefundisha kwa uaminifu miaka 40 hadi chaki zimemharibia macho na aliowafundisha wamekuwa na mishahara mikubwa na wengine ndio wakurugenzi wa NSSF

Ukitaka kuchukua mafao yake unamwambia nitakupa kidogo ili ukaishi, aliyekwambia nani ataishi?

Nimeamua tuwe na kipindi cha mpito, nimeamua kikokotoo kilichokuwa kinatumika kabla ya mifuko kuunganishwa kiendelee katika kipindi cha miaka yote ya mpito

Kipindi cha mpito ni hadi mwaka 2023 ambapo wanachama wa mfuko 58,000 ndio watastaafu kipindi hicho.

Wanachama watakaokuwa wanastaafu wataendelea na kikokotoo cha 50%

Rais Magufuli: Mimi nitaichungulia hiyo mifuko na nina uhakika Waziri na Katibu Mkuu wa wizara zinazohusika wafuatilie mifuko isitumike hovyo

Katika kipindi hicho watawalipa watu mafao vizuri na kwasababu hali itakuwa imeimarika tutafanya mazungumzo ya mfumo bora

Niakubaliana kuwa si kweli lengo langu mifuko, ndani ya Serikali na vyama vya wafanyakazi mkae mjadili njia bora ya kukokotoa mafao

Mifuko itakuwa imeimarika na itaweza kulipa, hata mkikubaliana kupeana 70% mimi sina neno

Si kweli kwamba lengo langu mifuko ife, ndani ya Serikali na vyama vya wafanyakazi mkae pamoja mjadili njia bora ya kukokotoa mafao

Mifuko itakuwa imeimarika na itaweza kulipa, hata mkikubaliana kupeana 70% mimi sina neno

Viongozi wa wafanyakazi muache kutumiwa na wanasiasa, watakaotumiwa na wanasiasa wataondoka

Mafao yakiwa bora hata wizi na ufisadi utapungua, kwasababu kila mmoja atakuwa anajua kuwa akistaafu atapata fungu lake

Huyu Jamaa ana watu na taasisi fulani ambazo huwa anawatuma wafanye kituko fulani ili yeye mwishoni aje aonekane anawasikiliza wanyonge. Alianza Mwakyembe na kanuni ngumu za kuoa akaja yeye kubadilisha. Ni mchezo wa siasa wa kutuchezea tu huu. Maana kama ni uamuzi wa serikali huwa na mchakato mrefu kweli kweli. Iweje awe hajui haya mambo hadi tulalamike? Amesikia Lissu atagombea urais ikabidi ajiongeze. Bado la Katiba Mpya. Atanyooka tu.
 
Kwa mujibu wa ITV, wafanyakazi hao wameandamana chini ya uratibu was vyama vya wafanyakazi. Swali ni lini waliandaa mabango na kibali cha maandamano waliomba lini na hata RC alijulishwa saa ngapi?...inafanana na maigizo!
 
Jiji la Mwanza lilisimama baada ya maelfu ya wafanyakazi kuandamana hadi ofisi ya Mkuu wa mkoa kumpongeza Rais Magufuli kwa kuwaondolea kikokotoo cha 25%.
Waandamanaji hao walipokelewa na RC Mongella na wamemuahidi Rais Magufuli ategemee ushindi wa kishindo.

Source ITV habari!
 
Yaaani unavoandika utadhani haupo Bongo hii ya bahati mbaya!!!!! Wahuni washajua huyu mshamba anataka nini, so wanampa bila ajiziiii
 
hayo ni mapandikizi sawa na yale yaliyokuwa yanaimba tuna imani.. na ... oya oya oya!
 
habari wadau..

mifuko imeunganishwa imebaki miwili tu..

kuna haja gani ssra kuwepo.

watu wanaiba na kujenga ma eco village na elephant project kwa hela za wanachama ssra kimya tu.

watu wanaweka vikokotoo vya kinyonyaji ssra kimya..


najiuliza ssra wanafanya kazi gani

nazani ssra ingefutwa tu kama ile taasisi ya dodoma ya viwanja janja janja ilivyofutwa
Hiyo sheria 13.7.018,hao ulio wataja ndio waliitia sahihi?acheni kuwapa lawama watu,mtu alitengeneza tatizo mwenyewe kisha asome upepo unavyovuma eti aje na soln aonekane shujaaa!!!???
 
Kumbe maandamano ya kumuunga mkono Rais ruksa??

Mbona wakitaka kuandamana wanaChadema wanapambana na kipigo cha mbwakoko cha Polisi??

Hivi hao Polisi wanajua kwamba wajibu wao ni kulinda maandamano yoyote ya wananchi kwa mujibu wa Katiba ya nchi na wala siyo kuyazuia??
 
Back
Top Bottom