Rais Magufuli ajibu hoja za Marekani, Asijifiche kwenye hoja za uzalendo, Kwanza sio Mzalendo

Rais Magufuli ajibu hoja za Marekani, Asijifiche kwenye hoja za uzalendo, Kwanza sio Mzalendo

Swali dogo tu plz naomba jibu hivi Magu anawajibika kwa marekani hadi ajibu hoja zao?

Yes! Marekani wanampa mikopo na misaada yenye masharti nafuu...!
Masharti hayo ni pamoja na kuendesha na kusimamia UTAWALA BORA....!
Wamerekani hawataki kuona Fedha yao inatumika ndivo sivo hivo wana haki ya kuhoji.,.!!
 
Marekani ndo nani?

Yeye anaweza akajibu hoja zetu?

Yaani Marekani ndo kawa Mungu wenu?
Yeye ana utakatifu gani?

Hivi ukiongea masuala ya ukiukaji Haki za Binadamu, huyo Marekani anaweza hata kusogeza pua yake?

Anaweza hata kujilinganisha na Tanzania?
Akili za kitumwa hizo kamanda!

Mnajipendekeza hadi mnatia kichefuchefu.
Wewe nae una hoja au vihoja?
 
Unayoyasema hatuna uhakika nayo lakini tuna uhakika Marekani hawawateki wala kumpoteza mtu yeyote anayemkosoa Trump. Trump anajibizana na wakosoaji wake kwenye tweeter kama wanadamu wenzake. Hawapotezi watu.

Hapa kwetu JF imekuwa maarufu kutokana na hofu ya watu kuwa huwezi kuwakosoa watawala wala serikali kwa uwazi, na ukajulikana, na ukawa na uhakika wa 100% utakuwa salama.
Mkuu uyasemayo yawezekana ikawa kweli ama lah! kwan hakuna ushahidi wa moja kwa moja kulielezea ama kulionyesha hilo though tunatumia utashi binafsi + hisia kuelezea ktk hali hiyo uisemayo.

Hakuna asiyejua ya kuwa wanasiasa & watu maarufu + matajiri ni watu wenye maadui wengi sasa ya nini kumnyooshea kidole fulani ya kuwa ndio mhusika? huoni ya kuwa huo ni mtazamo wa ki-hisia zaidi kuliko uhalisia?
 
Utawala wa Marekani nao hiwa wanateka wananchi wao wanaomkosoa Rais? Mbona Trump anasema kila siku lakini hatusikii waliotekwa?
Hivi mkuu unaweza thibitisha hizi tuhuma hizi nzito kwa taifa letu?
 
Marekani haijamtuma mtu kuua watu kufunga watu na kuteka watu hapana, Marekani haijatuma mtu kuwashambulia watu kwa risasi hapana, Marekani haijamtuma kuzima vyombo vya habari na kuzuia siasa kwa wapinzani kwa miaka 5 hapana,

Kama serikali haijawatuma hao watu kwanini hafanyi upelelezi kuleta mlejesho? kwanini hawakamatwi watekaji? wauaji na wanaopiga risasi?

Eti hoja ni kwa vile kadhibiti madini yasiibiwe hoja ya kipumbavu kweli nawapa somo tu wafuasi mnaoamini izi propaganda kutoka Ikulu ya Magufuli, hakuna nchi iliyodhibiti rasilimali zake kama Botswana lakini huwezi sikia wanapambana na upinzani.

Na huwezi sikia Marekani ikiwanyoshea kidole halafu eti unasema umedhibiti madini yapi yale ya twiga 84/16 upo serious kweli? unachekesha kweli ! jibu hoja za Marekani.

Umeyakoroga mwenyewe yanywe mwenyewe hakuna atakayekubeba uvune ulichopanda nakuhakikishia uchomoki uchaguzi mwaka huu.


JPM hana sababu yoyote ya kuwajibu USA, wao ni kina nani? Nyie mnaowaabudu USA hameni nchi.
 
Mbona a
Marekani haijamtuma mtu kuua watu kufunga watu na kuteka watu hapana, Marekani haijatuma mtu kuwashambulia watu kwa risasi hapana, Marekani haijamtuma kuzima vyombo vya habari na kuzuia siasa kwa wapinzani kwa miaka 5 hapana,

Kama serikali haijawatuma hao watu kwanini hafanyi upelelezi kuleta mlejesho? kwanini hawakamatwi watekaji? wauaji na wanaopiga risasi?

Eti hoja ni kwa vile kadhibiti madini yasiibiwe hoja ya kipumbavu kweli nawapa somo tu wafuasi mnaoamini izi propaganda kutoka Ikulu ya Magufuli, hakuna nchi iliyodhibiti rasilimali zake kama Botswana lakini huwezi sikia wanapambana na upinzani.

Na huwezi sikia Marekani ikiwanyoshea kidole halafu eti unasema umedhibiti madini yapi yale ya twiga 84/16 upo serious kweli? unachekesha kweli ! jibu hoja za Marekani.

Umeyakoroga mwenyewe yanywe mwenyewe hakuna atakayekubeba uvune ulichopanda nakuhakikishia uchomoki uchaguzi mwaka huu.
Mbona amesha waijibu???? Some times being silenc the best reply.
'Silence is Golden'
 
Si vyema kujipiga kifua wkt upo hoi taabani. Kuongoza nchi ni maarifa na hekima.
 
Dikteta hawezi kua mzalendo anakuwepo madarakani kwa ajili ya maslahi ya kundi dogo sn linalotawala nchi.....
 
Marekani haijamtuma mtu kuua watu kufunga watu na kuteka watu hapana, Marekani haijatuma mtu kuwashambulia watu kwa risasi hapana, Marekani haijamtuma kuzima vyombo vya habari na kuzuia siasa kwa wapinzani kwa miaka 5 hapana,

Kama serikali haijawatuma hao watu kwanini hafanyi upelelezi kuleta mlejesho? kwanini hawakamatwi watekaji? wauaji na wanaopiga risasi?

Eti hoja ni kwa vile kadhibiti madini yasiibiwe hoja ya kipumbavu kweli nawapa somo tu wafuasi mnaoamini izi propaganda kutoka Ikulu ya Magufuli, hakuna nchi iliyodhibiti rasilimali zake kama Botswana lakini huwezi sikia wanapambana na upinzani.

Na huwezi sikia Marekani ikiwanyoshea kidole halafu eti unasema umedhibiti madini yapi yale ya twiga 84/16 upo serious kweli? unachekesha kweli ! jibu hoja za Marekani.

Umeyakoroga mwenyewe yanywe mwenyewe hakuna atakayekubeba uvune ulichopanda nakuhakikishia uchomoki uchaguzi mwaka huu.
You write like a diva. Man up and write like a man. "unachekesha kweli !"
 
Jibu hoja, Marekani kavunja haki gani za binadamu?
Marekani ndo nani?

Yeye anaweza akajibu hoja zetu?

Yaani Marekani ndo kawa Mungu wenu?
Yeye ana utakatifu gani?

Hivi ukiongea masuala ya ukiukaji Haki za Binadamu, huyo Marekani anaweza hata kusogeza pua yake?

Anaweza hata kujilinganisha na Tanzania?
Akili za kitumwa hizo kamanda!

Mnajipendekeza hadi mnatia kichefuchefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali dogo tu plz naomba jibu hivi Magu anawajibika kwa marekani hadi ajibu hoja zao?
Kama hoja zao zinamhusu yeye au Tanzania, ajibu mwenyewe au kupitia kwa Msigwa wa Ikulu au Hassan msemaji wa Serkali. Kukaa kimya ni kushindwa kujibu kwa sababu hoja ni za kweli. Marekani wanajua nchi hii, yaliyomo na yanayotendeka humo kila siku kuliko huyo anaeshauriwa ajibu hoja zao. Ndani ya Ubalozi wa Marekani Dar kuna mfanyakazi wa kila Idara muhimu ya Serkali yao na teknolojia ya hali ya juu ya mawasiliano na kwao. Maili 25 tu juu ya anga ya Tanzania wana mitambo inaangalia kinachoendelea hapa chini kama were unavyoangalia wapita njia ukiwa ghorofa ya kwanza nyumbani kwako. Msaidie kujibu!
 
Hivi siku zile alipokuwa akipokea taarifa ya madini/almasi alipotamka yale maneno hadharani tena mbele ya vyombo vya habari alitegemea nini?? Eti tuko kwenye vita vya uchumi na anapotokea mtu mmoja akatusaliti basi askari wanaofahamu wajibu wao dhidi ya msaliti dawa yake huwa ni nini?? Nini kilimpata Mh Lissu baadae?? Sote tunajua. Sasa hapo atajitetea kwa lipi Mkuu??

Sas hivi kaongeza kaongeza maadui ndani ya chama chake mwenyewe. Hivyo asitegemee hoja za Wapinzani pekee bali mashambulizi makali na mabaya zaidi dhidi ya Serikali yake yatatoka ndani ya chama chake mwenyewe.

Yeye aendelee kupambana na kina Mh Halima Mdee na Ester Matiko na siyo Wamarekani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hiyo Tindu lisu ndio msaliti? Alitisaliti kwa hao walokuwa wanachimba madini?

Kama ni kweli msaliti na yaliyosemwa na Magufuli yalimuhusu basi kwa kinyakyusa tunasema mbombo ngafu.. I wish isiwe kweli hana usaliti wowote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si vyema kujipiga kifua wkt upo hoi taabani. Kuongoza nchi ni maarifa na hekima.
Haiwezekani watu wote kwenye taifa kuwa watawala ama kutawala, ni lazima watawale wachache. Ila suala la wachache hao kutawala kwa maslahi yao hilo ni jambo jingine
 
Kuna mijitu mipuuzi hapa Tanzania hasa hii mitu ya CCM inafikri hii nji ni kisiwa au iko dunia ingine...!
Kama Magufuli na CCM hawamjui Marekani waulize Iraq, Iran,Libya na DRC Congo...!
Wapi Saadam Hussein, wapi Qhaddafy, wapi Jeneral Casseimu na wapi Patrice Lumumba..??!!
Marekani ikitaka kumung'oa Mtu yeyote awe sijui Rais au Mkuu wa Majeshi maarufu duniani atang'oka tu....! Seuze mtu mfupi toka Chato??
We kweli pompimpo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marekani ndio Mungu wetu, kama nyie vyombo vya dola vilivyo Mungu wenu. Tunataka Marekani ashikilie hapo hapo mpaka madhalimu hapa nchini wanyooshe maelezo. Na iwapo Marekani ataamua kuja hapa nchini tutampa msaada wowote autakao. Hatuko radhi kurejeshwa kwenye mfumo wa chama kimoja na dhalimu yoyote.
Wewe naona ushapelekewa moto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani we ndio kichefuchefu full. Mtunyanyase kisa ulimbukeni wa madaraka kisha mtuambie Marekani hana rekodi ya haki za binadamu? Hata kama hana sifa nzuri za haki za binadamu, ili mradi anaingilia sisi kurudishwa kwenye mfumo bwana chama kimoja kimabavu, tunamuunga mkono.
Inaonekana ww ulikuwa kwenyemkumbo wa veti fake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom