Rais Magufuli alivyovuruga Uhusiano na Wadau wa Maendeleo

Rais Magufuli alivyovuruga Uhusiano na Wadau wa Maendeleo

Maoni mazuri ni kuboresha tuu hatuna haja ya kugombana na wahisani muhimu ni kukaa meza moja na kujadiliana lakini tatizo la wahisani kwakuwa wao wanapesa basi wanataka kila wanalojiskia wao nyie mufanye tuuu.
 
Watu hawajalipwa pesa za kustaafu mwaka ushapita
Tuna miradi mikubwa ambayo tunajenga kwa pesa zetu wenyewe, how come useme The GVT is broke.??

Utasukumwa ndani mkuu..

SGR, SG, Barabara 8 Morogoro road, Ubungo InterChange, Ununuzi wa ndege, Kuhamia Dodoma e.t.c.., miradi yote hii inatekelezwa kwa 'PESA ZETU WENYEWE' ,why saying serikali imefilisika.???

Sisi twatembea vifua mbele bhana ,hatutishwi na mabeberu..

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nadhani anajua anachokifanya si bure, tulipofikia panasikitisha, tumerudishwa nyuma miaka zaidi 30.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa kweli tuna safari ndeeefu sana! Kama mawazo ya wananchi wetu wasomi ni haya haya ya kufikiri kwamba misaada kutoka kwa wafadhili itatuondolea umaskini na kutuletea maendeleo makubwa basi safari ya maendeleo bado hatujaianza. Tumepata misaada mingi ya kutupumbaza tu toka tupate uhuru. Mpaka tukaitwa eti “darling of donors” ambao ni upuuzi tu wa kutufunga kitambaa cheusi machoni. Misaada yote tuliyokwishapata bado hatukuwa na vituo vya afya vya kutosha, shule za kutosha, umeme wa kutosha, barabara za kutosha, maji ya kutosha, reli na ndege za kutosha, nk, nk. Misaada hii inapokuja utaambiwa dola milioni mia lakini 55% ya pesa hizo inarudi kwao kwa njia ya uani..Inayobaki 45% inalifanya Taifa liwe tegemezi..Misaada hii ni aina ya “ukoloni” fulani ambao ni wa kijanja sana na ndiyo maana hakuna msaada ambao hauna masharti magumu maana ipo kumsaidia zaidi mtoa msaada kuliko mpokeaji. Sasa, awamu ya tano ya Serikali ya Tanzania imeliona hilo na kwa kweli kwa miaka 3 tu ya uongozi wa nchi imefanikiwa kuleta huduma nyingi sana kwa wananchi kuliko kipindi kingine chochote kwa miaka 30 iliyopita.
 
Mkuu kwanza napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwako kwa uelewa wako mkubwa katika namna ya uchangiaji wa hoja yako.

Kabla sija anza na section yako kubwa ya kukuthibitishia wewe kuwa watanzania hatuna budi kuwa wanyonge kila mara tunaposikia vitisho vya wazungu tuna ingia mteru na badala yake kutembea kifua mbele, nadhani kwanza ungefanya jitihada ya kutambua era za matukio ya maendeleo ya binadam badala ya kukazia mkazo kuwa wakati wa kutoa references zangu nizingatie kuwa North Africa was not Part of Africa.

Ndiyo maana nataka utambue kuwa ukisema maneno "North Africa was not a Part of Africa" ujue pia ni wakati gani au katika era ipi didn't North Africa belong to Africa. Ili uelewe haya yote vizuri inabidi usome vitabu vya zamani kutoka mataifa tofauti ya ulimwengu.

Lazima ukubali kitu kimoja kuwa sisi waafrika tulivamiwa na wazungu kinyume na matakwa yetu, hapo na maanisha mababu zetu. Kwa bahati moja au nyingine sisi wa East Afrika na hasa watanganyika hatukuathirika sana in terms of umwagaji wa damu kama mataifa mengine kama South Africa na mengineyo.

Wewe unajua kuwa sisi, I mean mimi na wewe, ni vizazi vilivyotokea kupata bahati mbaya au nzuri ya kuishi katika kipindi ambacho hatukuwa na jinsi nyingine ya kuishi zaidi ya kukubaliana na hali iliyo kuwepo, yaani ya kwenda shule na ku-participate kwenye madhehebu tofauti ya dini za watawala.

Utanisamehe kwa sasa. Nitarudi kukujibu! Ni maswali mazuri sana. Kuwa na subira kidogo.


Mheshimiwa, mbona unajichanganya katika maandiko yako? So boastful na arrogant,unajaribu kuchanganya mabwege, kisha premise zako zinaishia kwenye ubatili. Tell us, kitu unachojivunia wewe kama mtanzania, ambacho, hakina affiliation na wazungu, ambacho unaweza kutamba nacho, kituasaidie na kujitambua kuwa kweli sisi, baadaya kusoma elimu ya wazungu (kama walivofanya wajapani) sasa tuna haki ya kutowasikiliza na kufuata matakwa yao. Cite mifano miwili ya kitanzania,.miwili tu ili utuaminishe kuwa kweli TZ tumekua, tunaweza bila affiliation na wazungu.

Kisha utakapokuwa una fanya reference uifanye kwa ukweli, North Africa was part of Europe... enzi hizo. Wewe fikiria Africa South of Sahara, ndipo you belong. ..

Sent using Jamii Forums mobile app


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwanza napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwako kwa uelewa wako mkubwa katika namna ya uchangiaji wa hoja yako.

Kabla sija anza na section yako kubwa ya kukuthibitishia wewe kuwa watanzania hatuna budi kuwa wanyonge kila mara tunaposikia vitisho vya wazungu tuna ingia mteru na badala yake kutembea kifua mbele, nadhani kwanza ungefanya jitihada ya kutambua era za matukio ya maendeleo ya binadam badala ya kukazia mkazo kuwa wakati wa kutoa references zangu nizingatie kuwa North Africa was not Part of Africa.

Ndiyo maana nataka utambue kuwa ukisema maneno "North Africa was not a Part of Africa" ujue pia ni wakati gani au katika era ipi didn't North Africa belong to Africa. Ili uelewe haya yote vizuri inabidi usome vitabu vya zamani kutoka mataifa tofauti ya ulimwengu.

Lazima ukubali kitu kimoja kuwa sisi waafrika tulivamiwa na wazungu kinyume na matakwa yetu, hapo na maanisha mababu zetu. Kwa bahati moja au nyingine sisi wa East Afrika na hasa watanganyika hatukuathirika sana in terms of umwagaji wa damu kama mataifa mengine kama South Africa na mengineyo.

Wewe unajua kuwa sisi, I mean mimi na wewe, ni vizazi vilivyotokea kupata bahati mbaya au nzuri ya kuishi katika kipindi ambacho hatukuwa na jinsi nyingine ya kuishi zaidi ya kukubaliana na hali iliyo kuwepo, yaani ya kwenda shule na ku-participate kwenye madhehebu tofauti ya dini za watawala.

Utanisamehe kwa sasa. Nitarudi kukujibu! Ni maswali mazuri sana. Kuwa na subira kidogo.





Sent using Jamii Forums mobile app
Unaambaa ambaa, badala ya kujibu maswali, ndiyo sifa ya Utanzania. Kumbuka kuna nchi ambazo hazikuwahi kutawaliwa kabisa na hao wazungu. Ziko dunia ya ngapi? Kisha ujue kwamba wazungu hao walitawala Tanzania kwa takribani miaka 70 tu, na tangu tulipojitawala tuna zaidi ya miaka 57. Nipe bado mifano miwili tu ya kitu ambacho tunajivunia baada ya miaka 57, tangu tulipoachana na kunyanyaswa na hao wazungu. Something made in Tanzania, something a prestige of the country. Kwa mfano, wajapani ni watengezaji wa mameli makubwa duniani, watengezaji wa magari bora, wataalam katika electronics,camera nzsuri Japani, pikipiki nzuri Japan, genereta nzuri Japan, n.k.

Kitu gani tunacho?
 
Unaambaa ambaa, badala ya kujibu maswali, ndiyo sifa ya Utanzania. Kumbuka kuna nchi ambazo hazikuwahi kutawaliwa kabisa na hao wazungu. Ziko dunia ya ngapi? Kisha ujue kwamba wazungu hao walitawala Tanzania kwa takribani miaka 70 tu, na tangu tulipojitawala tuna zaidi ya miaka 57. Nipe bado mifano miwili tu ya kitu ambacho tunajivunia baada ya miaka 57, tangu tulipoachana na kunyanyaswa na hao wazungu. Something made in Tanzania, something a prestige of the country. Kwa mfano, wajapani ni watengezaji wa mameli makubwa duniani, watengezaji wa magari bora, wataalam katika electronics,camera nzsuri Japani, pikipiki nzuri Japan, genereta nzuri Japan, n.k.

Kitu gani tunacho?

Atakuambia tuna Rais bora duniani!
 
Mkuu umeongea kwa upole ila kiuwoga sana na inaonesha jinsi gani unavyowatukuza hiyo mibeberu eti economic partner tunao takriban 50 years hamn lolote zaidi ya misaad uchwara unayoambatan na sera didimizi wallah magu anajua anachofanya hawa jamaa hawajawahi kuwa wema kwa waafrika zaidi ya maslai makubwa kwao fatilia sera zao kwa afrika ndio utajua kutwa kutoa takwimu za kutufanya tujione wanyonge eti Tz ni Moj ya nchi masikini duniani na kunamisomi humu na elimu zao za kikoloni hata hayoni haya kwa nini wa sitoe takwimu za Tz ni nchi yenye utajiri mkubwa sana ila ni masikini ndio utaona ujinga wa hawa jamaa means wanajua tutashutka kwa sasa amekuja mtu binafsi anaongea ukweli kbs kama utaweka itikadi za chama pembeni au hii kitu mlolishwa eti demokrasia na hata hamtaki kujifunza kuona libya na maeneo mengine afrika kisa mlikaririshwa kuwa hy ni demokrasia nzuri na watesi wenu wa mangaribi na kweli mkasahau kuwa umoja ndio nguvu aloo tutasugua sana ndio maana lijitu linaanzisha uzi likitushawishi tuendele kuwa wanyonge kupiga magoti tu badala ya kutamani kujikomboa kiuchumi hlf unawez kuta jamaa lina phd asee au degrii[emoji848]
 
Mwitikio wa andiko langu wiki lililopita katika mtandao huu wa JF ulinipa hamasa kuendelea kuandika zaidi jinsi Rais Magufuli anavyoendelea kulipotezea mwelekeo taifa. Wiki hii naona nigusie kwa undani jinsi Magufuli anavyoharibu uhusiano mzuri sana uliokuwepo kati ya Tanzania na wadau mbalimbali wa maendeleo. Awali ya yote naomba mnisamehe, kiswahili changu si kizuri kama ambavyoningependa kiwe, ila anendela kujifunza;

Sio siri kwamba Tanzania ilijulikana kama kipenzi cha wadau wa maendeleo(darling of development partners); Ukiangalia twakimu za misaada iliyokuwa inaletwa na wahisani katika nchi za Africa, Tanzania ilikua haikosi katika 10 bora katika nchi za Africa. Umoja wa Ulaya, Benki ya Dunia, Marekani, China, Ufaransa, Uingereza, Ujerumani nchi zote hizi zilikua zinawekeza kwa nguvu kubwa katika maendeleo ya watanzania.

Magufuli alipoingia madarakani, mambo yakaanza kubadilika, mwanzoni walikua wanamvumilia sababu alionekana kama ni kiongozi mpya mwenye ‘zeal’ ya kupigana na rushwa ila siku zilivyokuwa zinazidi wakaona hali inazidi kuwa mbaya hususani katika utawala wa sheria, demokrasia na haki za binadamu.

Magufuli alipotangaza kuzuia wasichana wa kike kutoendelea na masomo yao kisa ya mimba alipiga msumari mkali katika mahusiano na hawa watu. Na hii ndio sababu husikii hawa development partners hawainvest kwenye sekta ya elimu, maana wakitoa msaada au wakiwakopa Tanzania, watanekana na wao wapo complicit kwenye hilo katazo. Athari zake tunaziona kwa jinsi hali ya elimu inavyozidi kuporomoka siku baada ya siku, madarasa hayatoshi, walimu hawashugulikiwi madai yao vizuri maana mzigo wa kuiinua hii sekta nyeti kwa Taifa limebaki tu kwa serikali.

Benki ya dunia

Katika wahisani ambao sikutegemea (hata Magufuli mwenyewe hakutegemea) wangeweza kuigomea serikali ni Benki ya dunia maana ndio ilikua taasisi iliyobaki ambayo ilikua inaipa serikali kiburi pamoja na kuwepo kwa ukiukwaji wa haki za kiraia.

Kwa msiofahamu wahisani wanachangia asilimia 40% ya bajeti ya Tanzania na Benki ya dunia inachakia takribani asilimia 10%(kubwa kuliko mdau yeyote) na hivyo kuifanya kuwa Tanzania’s biggest partner in development.

Benki ya dunia ilianza kuichoka serikali walipofanya marekebisho kwenye sheria ya twakimu ya mwaka 2018 ambayo inazuia taasisi yeyote kuto-desseminate statistics bila kupata verification kutoka NBS. Kazi kubwa za Benki ya Dunia ikiwemo repoti na miradi zinategema takwimu halisi, hii sheria mpya iliweka vikwazo vilivyoifanya WB kutofanya kazi zao freely and professionally

Tulisikia mwaka jana mwezi wa 11 jinsi benki ya dunia livyositisha mkopo wa $300million wa elimu (takribani billion 700tsh) kwa sababu ya sera ya serikali ya kutoruhusu hawa watoto kurudi shuleni. Magufuli anathamini na anajua mchango wa benki ya dunia katika maendeleo ya nchi na ndio maana alikubali kukutana na WB Regional Vice President wanegotiate kuhusu huu mkopo. Katika maongezi yao (japo hayajawekwa wazi) walikubaliana kuandaa program ambayo italipiwa na serikali itakayowawezesha watoto wa kike wenye mimba kupata elimu, kama mnakumbuka wakati ule nchi ilibujikwa katika sakata la ushoga lililoanzishwa na makonda, waliliongelea na Magufuli alimuhaidi kuwa amna mtu atakae kamatwa kwa ushoga na atamkataza Mkuu wa Mkoa kuongelea kuhusu swala hilo tena, tatu, alikubali kuendelea kuwa na maongezi juu ya ile sheria ya takwimu.

Cha kushangaza, siku chache tu baada ya kukubaliana nao, Magufuli wakati wa uzinduzi wa Library ya UDSM, akawakashifu kwa kuwapongeza waChina kwa kuwaambia kuwa, “misaada yenu hayana masharti, sio kama mashirika mengine”. Huyo makamu wa Rais alisikitiswa na kauli hii maana ilionyesha kuwa serikali haikuwa na commitment katika makubaliano hayo.

Ni kwa sababu hiyo mpaka leo hii mkopo haujatolewa na sidhani kama utaolewa. Sio hiyo tu, Benki ya Dunia imei-demote ofisi yake ya Tanzania. Benki ya Dunia inakuaga na Country Director- wa sasa ni ndugu Bella Bird lakini kuanzia June 2019, amabapo mda wake utaisha nchi itaanza kuwa na country manager.

Kuwa na country manager inamaanisha kuwa na portfolio ya nchi itapunguzwa. Miradi yote inayohusiana na P4R – Program for results, kwenye elimu, maji, umeme, yote inafutwa, maana huwezi kupata results without credible statistics.

Pamoja na balozi Mahiga na Prof Kabudi kwenda Brussels kuipigia magoti umoja wa ulaya bado wameendelea kusitisha msaada wao nchini.

Yamkini inabidi tutafute mbinu za kujitegemea lakini tupende tusipende bado tunawahitaji hawa wadau wa maendeleo. Hata Europe yenyewe iliendelea kwa kusaidiwa na Marekani through the Marshall Plan policy iliplay a big part in the reconstruction of Europe baada ya vita ya pili ya dunia.

Serikali ifanye nini

Kwanza wathibiti matamko ya Rais; Kuwaita mabeberu hadharani, kutangaza kwamba nchi ipo katika vita ya uchumi na kusema kwamba misaada yao inamasharti. Ushawahi kuona wapi jirani yako anakuja kukusaidia alafu unaanza kumtukana, unadhani ataendelea kukusaidia?? Sio lazima akubaliane nao ila awaheshimu, kiufuppi ajifunze lugha za kidiplomasia zaidi

Pili, na hii itakua ngumu kwake, aruhusu watoto wenye mimba waendelee na masomo yao, hii itabuild confidence kubwa sana kwa hawa wahisani. But we all know this is never going to happen maana Rais alishasema na ninanamnukuu, “katika utawala wangu watoto wenye mimba hawatarudi shuleni, siwezi somesha wazazi”. Kwa mtu mwenye ego kubwa kama Rais wetu, hawezi reverse such a statement, it will possibly be the biggest political miracle in our country’s history.

Tatu, Asisgn into law mswada wa vyama vya siasa. Hii itakua ushindi kwakwe in both the internal and external politics.. kwanini; 1. Itanesha kwamba kama Rais anaheshimu demokrasia ya vyama vingi, pili itabuild trust kwa wananchi kuwa rais kumbe anauwezo wa kutosign sheria mbaya hata iliyopitishwa na wabunge wa vyama vyake (hatausishwa na hii sheria kabisa), tatu, He will for once be on the positive side of the coverage of the international media. Tutaona makala mabali mbali za nje zitakavyomsifu jinsi kwa huo uwamuzi… But this is also never going to happen maana ukweli unajulika kuwa yeye ndio muasisi mkuu wa hiyo sheria.

Najua wengi mtasema kuwa “hatuitaji misaada yao” “serikali ina pesa” ila ukweli msioujua ni kuwa the government is sooooooooooo broke, na ndio maana unaona kuna msisitizo mkubwa hivi karibuni wa kulipa kodi na kufanya ulipaji kodi kuwa rahisi kwa watanzania.

Kama mnadhani tunaweza kuendelea bila ushirikiano na wadau wa maendeleo angalieni hali ya Zimbabwe wanaoenda nunua mkate na begi limejaa noti… Serikali ibadilishe mwelekeo, kabla mwelekeo haujatubadilisha… kuweni na siku njema
Akili mgando kabisa hii.Kitu hujui n kuwa hakuna free lunch katika dunia ya leo na hiyo misaada iliyomingi Ina masharti magumu lukuki

Kwa mtazamo uliowazi n kuwa misaada hiyo n maney trap au mitego ya wafadhili kwa nchi maskini kufanyiwa ukoloni mambo leo

Magufuli n Rais pekee aliyethubutu kuweka maslahi ya nchi mbele kwakuhakikisha misaana inakuwa ni ileyenye mashart nafuu na Kuna kuwa na maslah kwq nchi

Usifurahi hata kidogo nchi kuwa top ten ya nchi zinazopata misaada sana Bali furahi pale nchi inapoweza kupunguza utegemezi


Piga kazi changia pato la nchi hamasisha na Alie karibu na wewe afanye kazi tulipe Kodi.Wengi was waliokata misaada n wale ambao masharti yao tumeyakataa na magumu kwa maslahi mapana ya nchi.

Sikuzote watoa misaada wanapenda nchi yetu iendelee kuwa tegemezi ili waendeleee kufaidi kwa mlango wa nyuma.Ukilitazama hili juu juu utamlaumu Magufuli lakini ukijaribu kutumia sehemu ya akili yako vzr kuelewa namna misaada na mikopo inavyotolewa na siasa zake nyuma ya kapeti utakubaliana na mm kuwa n Bora kumuunga Mkono Magufuli kwa jitihada anazofanya.

Rais akimaliza muda wake tutamkumbuka sana ingawa kwasasa kwasababu ya mihemko ya kisiasa baadhi wanamuona Kama ameshindwa
 
Back
Top Bottom