Rais Magufuli ameamua nchi ifungue sura mpya ya kimaendeleo kuelekea 2025

Rais Magufuli ameamua nchi ifungue sura mpya ya kimaendeleo kuelekea 2025

Safari 2020

2020 kuna safari gani, hiyo ya kutegemea kufanya ukatili kwa uratibu wa vyombo dola? Hamuwezi ushindani na hamtakaa muweze, sana sana mnategemea madaraka ya rais yafanye hujuma ili mfanikiwe kutangazwa washindi. Hakuna mtu mwenye akili timamu atasimama kwenye mstari wa kura ashiriki huo ushenzi unaoitwa uchaguzi. Kama mlipanga kuua watu hizo mbinu elekezeni kwenye mambo mengine.
 
Comrade umegusia masuala mengi lkn muhimu kujua Rais aliyeko madarakani amepokea kijiti kutoka kwa mtangulizi wake ipo miradi iliyokuwa kwenye hatua ya upembuzi yakinifu kwenda utekelezwaji wake katika Awamu ya Tano ya Rais wetu John pombe Magufuli..

Pili miradi mikubwa ya SGR na wa Umeme MTO Rufiji ni maamuzi Magumu ya Rais wetu John pombe Magufuli dunia inajua kutumia malighafi za chuma ya linganga na mchuchuma zipo sababu za msingi zilizopelekea hilo kushindikana jua hivyo.

Kila ukienda wilaya yoyote hapa nchini kuna mradi mkubwa unaendelea unatoa wapi ujasiri wa kutoona juhudi za Rais wetu katika mapinduzi ya maendeleo nchini

Umeme wa Rea miradi mipya ya maji next time nitakuja na detail za mradi umesainiwa lini na unakamilika lini

Wajasiriamali wamepunguziwa kodi za kero kwa kupewa vitamburisho vya ujasiriamali

Demokrasia ya aina gani unataka ya wanasiasa kufanya mikutano jangwani au Wamachinga kufanya biashara zao popote bila bugudha ya polisi Uhuru wa kufanya kazi au Uhuru wa kutukana Uhuru wa aina gani unataka kila bajeti zinarekebishwa sheria za kodi ili kuchochea sekta binafsi kuwekeza nchini

Mfano bajeti yetu ya 2019/20 kodi 54 zimefutwa kwa lengo la kuchochea sekta binafsi kuwekeza nchini na kuzalisha zaidi Mhe Rais wetu John pombe Magufuli kakutana na wafanyabiasha 5 kutoka kila wilaya lengo kusika kero zao na akachukua hatua palepale

Mnataka nini afanye mbona nia na utashi wake kwa Taifa letu upo wazi Rais wetu John pombe Magufuli kuiona Tanzania inasonga Mbele Kimaendeleo

Mleta mada seriously unaamini kuwa REA ni mradi ulionza na JPM?.
Nenda kaangalie risiti zako za kununua Luku kuanzia 2014 kurudi nyuma utaona kuwa ulikuwa ukikatwa kodi kwa ajili ya REA, na vijiji vingi sana vimepatiwa umeme wa REA kabla ya 2015

Na seriously unaamini kuwa SGR ni maamuzi magumu ya JPM?

Ngoja nikueleze sasa kuhusu SGR, SGR ni mradi uliobuniwa, na serikali ya JK, na hata Memoraundum of understanding ya awali kabisa kati yetu na EXIM bank ya China ya mkopo nafuu wa miaka 20 ulishasainiwa na serikali ya JK. Huyu wa sasa alipoingia madarakani alifanya kubadiri mkataba tu, badala ya wachina akawapa Waturuki

Angalia hapa Chini JK anahangaikia SGR kabla hata JPM hajawahi kudhani kuwa anaweza kuwa rais

1565106218131.png
 
Rais wetu John pombe Magufuli ameamua Nchi iende Mbele... hii ndio kusema Chagua Magufuli Kazi iendelee

1. Ujenzi wa barabara Nchi Nzima kwa gharama Sh. Trilioni 5.3 ili kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ya biashara kutoka sehemu moja kwenda nyingine.....

2. Ununuzi Ndege Mpya Sh. Trillioni 1.3 ili kuchochea sekta ya Utalii na Biashara ya ndani ya nchi yetu....

3.Ujenzi wa Hospital za wilaya 67 Wakati tangu tupate Uhuru hadi Leo tulikuwa na hospital 77 za wilaya, vituo vya Afya Sh.Bilioni 321

4.Kufufua Mradi wa kuzalisha Umeme MTO Rufiji Sh.Trilioni 6.5 utakaozalisha MW 2100 Wakati tangu tupate Uhuru hadi Leo hii tunazalisha MW 1500 za Umeme tu......

5. Ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) Sh. Trillioni 7 baada ya kukaa na reli ya mkoloni tuliyorithi zaidi ya miaka 200 iliyopita.....

6. Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya juu 2015-2019 Sh. Trilioni 1.6

7. Elimu Msingi bila malipo (Elimu Bure) kwa Shule za Msingi hadi kidato cha nne sh. Bilioni 945.9

8.Ukarabati Shule kongwe 62, Ujenzi wa Maabara, nyumba za Walimu kwa Sh. Bilioni 308

9.Ukarabati Viwanja vya Ndege Nchi Nzima Sh. Trilioni 1.8

10. Ujenzi wa meli Mpya na ukarabati za Mv Victoria na Mv Butiama katika Ziwa Victoria Sh. Bilioni 152,

Ujenzi wa meli Mbili Ziwa Tanganyika meli ya mizigo na Abiria MV Liemba, Ujenzi wa meli Mbili za Abiria na Mizigo Ziwa Nyasa MV Ruvuma na MV Njombe Umekamilika.....

11. Miradi ya Usambazaji Umeme vijijini kupitia Rea Umeme unaendelea kuchomoza vijijini....

12. Upanuzi wa Bandari ya Mtwara kwa kiwango kikubwa, Bandari ya Tanga, Bandari ya Dar es salaam

13 Ununuzi wa vivuko vya Majini maeneo mbalimbali ili kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ya biashara......

14. Ujenzi wa madaraja mfano Mfugale, Ubungo interchange, Surrender bridge n.k

15. Miradi ya Maji inayoendelea Kujengwa Maeneo Mbalimbali ya Nchi yetu ni mapinduzi kwenye sekta ya Maji......

N.K N.K N.K

We are proud of you, our president Honorable John Pombe Magufuli.....

Naungana na Mwenyekiti wangu wa Vijana Taifa Comrade kheri James kuwa yoyote anaempinga Rais wetu kwa haya anayofanya kwa Mustakbari wa Taifa letu kuna mambo mawili kwa mtu huyu either ni Chizi au Mkimbizi nchini kwetu........

Fahami Matsawili
Mjumbe wa baraza kuu Uvccm Taifa..
Nadhani hata RAISI WETU MPENDWA AMEKWISHA SEMA WATANZANIA SIO WAJINGA. hivyo wanaonao yanafanyika na hawana Sababu ya kusoma andiko lako ili wajue.
 
Huyo ni 'mshamba' tu hana jipya , hayo yote uliyo orodhesha ulikuwa ni mipango ya serikali EXCEPT hilo la kununua ndege, and it is something which is not important for Tanzanians right now,
Watanzania wanahitaji maji safi na sio mindege.....ulikinganisha na uhitaji wa maji.

Jk amefanya makubwa mno katika mabarabara na huyo ' mshamba ' ndio alikuwa msimamizi wa miradi hiyo na anajua kuwa nini serikali ili plan.

Yeye hana pesa ya kufanya lolote kwa sababu kazi zote zinafanywa kwa kodi ya Watanzania ikiwepo kumnunulia suti anayovaa, chakula anachokula n.k

Therefore, huyo ni ' mshamba tu' hana jipya.
Kama huwezi kujenga hoja bila kutukana huo ni uwezo mdogo sana wa kufikiri.
 
Duh naona umeathirika sana as policies za JPM vumilia sindano imeingia hadi kwenye mfupa huyo unaye muita mshamba ndo kakufanya wewe mtoto wa mjini kulialia na mambo mpaka 2025
2025 hafiki....kama sio Mungu,wananchi au "mabeberu"
 
Rais wetu John pombe Magufuli ameamua Nchi iende Mbele... hii ndio kusema Chagua Magufuli Kazi iendelee

1. Ujenzi wa barabara Nchi Nzima kwa gharama Sh. Trilioni 5.3 ili kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ya biashara kutoka sehemu moja kwenda nyingine.....

2. Ununuzi Ndege Mpya Sh. Trillioni 1.3 ili kuchochea sekta ya Utalii na Biashara ya ndani ya nchi yetu....

3.Ujenzi wa Hospital za wilaya 67 Wakati tangu tupate Uhuru hadi Leo tulikuwa na hospital 77 za wilaya, vituo vya Afya Sh.Bilioni 321

4.Kufufua Mradi wa kuzalisha Umeme MTO Rufiji Sh.Trilioni 6.5 utakaozalisha MW 2100 Wakati tangu tupate Uhuru hadi Leo hii tunazalisha MW 1500 za Umeme tu......

5. Ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) Sh. Trillioni 7 baada ya kukaa na reli ya mkoloni tuliyorithi zaidi ya miaka 200 iliyopita.....

6. Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya juu 2015-2019 Sh. Trilioni 1.6

7. Elimu Msingi bila malipo (Elimu Bure) kwa Shule za Msingi hadi kidato cha nne sh. Bilioni 945.9

8.Ukarabati Shule kongwe 62, Ujenzi wa Maabara, nyumba za Walimu kwa Sh. Bilioni 308

9.Ukarabati Viwanja vya Ndege Nchi Nzima Sh. Trilioni 1.8

10. Ujenzi wa meli Mpya na ukarabati za Mv Victoria na Mv Butiama katika Ziwa Victoria Sh. Bilioni 152,

Ujenzi wa meli Mbili Ziwa Tanganyika meli ya mizigo na Abiria MV Liemba, Ujenzi wa meli Mbili za Abiria na Mizigo Ziwa Nyasa MV Ruvuma na MV Njombe Umekamilika.....

11. Miradi ya Usambazaji Umeme vijijini kupitia Rea Umeme unaendelea kuchomoza vijijini....

12. Upanuzi wa Bandari ya Mtwara kwa kiwango kikubwa, Bandari ya Tanga, Bandari ya Dar es salaam

13 Ununuzi wa vivuko vya Majini maeneo mbalimbali ili kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ya biashara......

14. Ujenzi wa madaraja mfano Mfugale, Ubungo interchange, Surrender bridge n.k

15. Miradi ya Maji inayoendelea Kujengwa Maeneo Mbalimbali ya Nchi yetu ni mapinduzi kwenye sekta ya Maji......

N.K N.K N.K

We are proud of you, our president Honorable John Pombe Magufuli.....

Naungana na Mwenyekiti wangu wa Vijana Taifa Comrade kheri James kuwa yoyote anaempinga Rais wetu kwa haya anayofanya kwa Mustakbari wa Taifa letu kuna mambo mawili kwa mtu huyu either ni Chizi au Mkimbizi nchini kwetu........

Fahami Matsawili
Mjumbe wa baraza kuu Uvccm Taifa..
Umesahau ujenzi wa Kiwanja kipya cha ndege Chato na uzinduzi wa hifadhi mpya ya wanyama Burigi
 
Yaani point zako no.1,3,4,5,8,910,11,12,14,15 zote ni ujenzi,ujenzi,ujenzi it’s boring.

Hivi hakuna mambo mengine ya kufanya kama vile kuboresha maslahi ya wafanyakazi,utatuzi wa changamoto ya wanafunzi wanaomaliza vyuo vikuu kila siku lkn hawana ajira,etc.

Huko kwny miradi mnaishia kusema tu ooh miradi ya ujenzi inaleta ajira kwa wananchi,ajira zipi hizo?labda za kua vibarua huko site.

I bet huko kwny ujenzi kuna ‘wazalendo’ wanapiga pesa nyingi sana kwny hio miradi ndio maana kila wakiamka wana create projects nyingi nyingi za ujenzi ili waendelee kupiga ‘mtonyo’.

‘Wazalendo’ bana.
 
MLETA MADA UNASEMA

HOJA: 1. Ujenzi wa barabara Nchi Nzima kwa gharama Sh. Trilioni 5.3 ili kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ya biashara kutoka sehemu moja kwenda nyingine.....

JIBU: Acha kutamka tu, sema ni barabara zipi hizo zinazokusudiwa kujenga, Tunachojua ni Kwamba Barabara zilijengwa za kuunganisha Kila mkoa na almost kila wilaya wakati wa JK , Na huyu JPM ndiye aliyekuwa msiamazi mkuu wa ujenzi huu!. Siku nyingine badala ya KULETA FIGURE pekee ili kuibua hisia leta mifano halisi.

HOJA: 2. Ununuzi Ndege Mpya Sh. Trillioni 1.3 ili kuchochea sekta ya Utalii na Biashara ya ndani ya nchi yetu...

JIBU: Ni utafiti gani umeufanya kuwa Ununuzi wa ndegu Unaongeza utalii?, maana kudhani kuwa na ndege ndo kuinua utalii ni dhana potofu, kwa mfano takwimu ziko wapi kuonyesha kuwa ununzi wa ndege umechochea utalii?. Takwimu ziko wapi zinazoonyesha namna Ndege tulizonunua zimestimulate utalii?. Operation cost za kuendesha hizo ndege ukilinganisha pesa zinazoingiza ni kiasi gani?, lete takwimu ndugu, usiorodheshe vitu kama listi ya wachezaji wa pira oyesha impact ya kitu. Tunachojua ni kwamba biashara ya ndege ni baishara pasua kichwa, na Taarifa za PAC na ripoti za CAG zimeonyesha miongoni mwa mashirika yanayopata hasara mpaka sasa ni ATCL, hizo ndege zimetusaidia vipi?. Lakini pia hizo ndege zimenunuliwa bila pesa kuidhinishwa na bunge, ndege zimenunuliwa kwa utashi tu bila kufuata sheria, hatujui tumepigwa au la, inabidi kamati maalum ya bunge au CAG achunguze hili.

HOJA: 5. Ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) Sh. Trillioni 7 baada ya kukaa na reli ya mkoloni tuliyorithi zaidi ya miaka 200 iliyopita....
JIBU: Mleta mada, seriously unaamini hatujawahihi kuwa na reli nyingine isipokuwa iliyoaachwa na mkoloni?. Reli ya TAZARA unaijua?

HOJA: 9.Ukarabati Viwanja vya Ndege Nchi Nzima Sh. Trilioni 1.8
JIBU: Ukarabati wa viwanja vya ndege nchi nzima ulifanywa kwa asilimia kubwa na serikali iliyopita ya JK, labda utuambie kuwa huyu anamaliziamalizia kazi na pia gharama kubwa hapo imetumika kwenye ujenzi wa Uwanja mpya wa Chato usio na faida yoyote ya maana kiuchumi kwa nchi

HOJA: 11. Miradi ya Usambazaji Umeme vijijini kupitia Rea Umeme unaendelea kuchomoza vijijini...
JIBU: Usitutanie kuhusu REA, Sema JPM anaendeleza REA, lakini REA ilikuwepo toka awamu iliyopita, watu wamekatwa kodi wakati wakinunua umeme wa LUKU kwa ajili ya REA kwa muda mrefu kabla JPM hajawa raisi, na kukuonyesha kuwa REA ipo toka awamu iliyopita mimi kwa mfano umeme wa REA ulifika kijijini kwetu toka mwaka 2013 wakati wa JK

HOJA: 13 Ununuzi wa vivuko vya Majini maeneo mbalimbali ili kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ya biashara.....
JIBU: Hujaeleza kivuko gani?, Maana huyuhuyu JPM alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ujenzi alikuwa akisifu kila wakati kuwa JK kanunua vivuko vingi sana hapa nchini, Msidhani watanzania hatuna kumbukumbu vizuri na msitake kusafiria nyota za wenzenu , tengenezeni Legacy zenu lakini msiibe legacy za watu

HOJA : 14. Ujenzi wa madaraja mfano Mfugale, Ubungo interchange, Surrender bridge n.k
JIBU: Daraja La baharini la Surrender siyo necessity ya Mtanzania ni la show off zaidi kuliko haja na umuhimu wake, Daraja la Mfugale, pesa ilitafutwa na utawala uliopita na mikataba ilisainiwa na utawala uliopita. Hebu Linganisha Significance ya madaraja hayo na daraja kama la Mkapa lilojengwa na BWM, Malagarasi, Kilombero, Kigamboni yaliyojengwa na JK . Hayo ndiyo madaraja ya Legacy na kujivunia kwa mtu mwenye hadhi ya Raisi siyo daraja la Flyover ya Mfugale

HOJA: 15. Miradi ya Maji inayoendelea Kujengwa Maeneo Mbalimbali ya Nchi yetu ni mapinduzi kwenye sekta ya Maji.....
JIBU: Mkapa alileta maji kutoka ziwa Victoria mpaka Shinyanga, Kikwete akatutengenezea mradi mpya kutoka Ruvu chini kupitia bunju kuja mpaka Dar, Visima kibao vilijengwa nchi nzima!. Upo wapi mradi wa scale ya ule wa BWM au JK katika serikali hii?

Baada ya kukujibu hoja zako nikueleze sasa mambo ya msingi sana ambayo yanatugusa wananchi serikali hii haijafanya
1. Haiheshimu katiba iliyoapa kuilinda, kuna uonevu uliokithiri nchini kwa watu na taasisi mbalimbali kama vile wanasiasa wa upinzani, waandishi wa habari, vyama vya siasa etc

2. Wakulima wameendelea kutendewa visivyo haki, wakulima wa korosho walichukuliwa korosho zao kinguvu, zao la mbaazi limevurugwa, Zao la kahawa limeveurugwa

3. Wafanyakazi hawapewi stahiki zao kwa mujibu wa sheria za kazi, nyongeza ya kila mwaka iliyopo kwa mujibu wa sheria haipo

4. Wastaafu wanahangaika, wanapigwa danadana nenda rudi, wengine wanakaa miaka kibao bila mafao

5. Hali ya usalama wa wananchi iko matatani, watu wanatekwa, wengine wanapotea katika hali ya kutatanisha, watu wanaogopa hawajui fate yao itakuwa nini

6. Biashara zinaporomoka, Juzi hapa wafanyabiashara wamekiri jinsi TRA ilivyokuwa ikiwanyanyasa, biashara nyingi zimefungwa, maisha yamezidi kuwa magumu

7. Kilimo kiko arijojo, bajeti ya kilimo imezidi kupungua mwaka after mwaka, Pesa zinazopelekwa kwenye kilimo wakati mwingine haifiki hata asilimia 30 ya bajeti iliyotengwa, katika hali kama hii utainuaje hali za watanzania wakati zaidi ya asilimia 70 ya watu wetu wantegemea kilimo?

8. Ajira zimeendelea kuwa bomu linalosubiri kupasuka, mwaka wa 4 huu serikali inasuasua kwenye ajira, hata sekta binafsi ambayo ingebidi iisaide serikali kuajiri inasuffer, Sekta binafsi imekuwa paralysed, sasa katika hali kama hii Ujenzi wa uwanja wa ndege Chato au daraja la Surrender unawasaidia vipi vijana?. hata pesa ambazo inabidi zitengwe na Wakurugenzi kwa mujibu wa sheria hazitengwi, wewe mwenyewe unalifahamu hili vizuri

HITIMISHO:
Mleta mada umeleta habari za utendaji wa awamu hii lakini ambacho hujakisema ni kwamba miradi mingi inayofanyika kwenye awamu hii ni miradi iliyoanzishwa kutafutiwa fedha na serikali zilizopita, kwa hiyo awamu hii inamaliziamalizia na kuongezea hapa na pale palipopungua

Pili, Miradi mikubwa kama SGR inatoa pesa nje badala ya kuingiza pesa ndani, Chuma tunatoa nje, kabla ya kuanza ujenzi pale tungehakikisha tumewekeza Liganga na mchuchuma ili tutumie chuma chetu cha humuhumu nchini ili pesa nyingi zaidi ibaki ndani etc, Lakini pia miradi mingine siyo Miradi PRIMARY kwa uchumi ni miradi SECONDARY kiuchumi kwa mfano mradi wa uwanja wa ndege Chato au Daraja la kupitia "Baharini" la Surrender

Tatu miradi hii inafanyika wakati maisha na mahitaji ya watu hayaguswi ipasavyo, Mkulima kama vile wa korosho, kahawa,etc ameendelea kutopewa umuhimu wa maana, Ajira za wananchi ziko chini, Private sector imesuffer mno ndani ya miaka hii minne.

Hali ya Kidemokrasia na kuheshimu viapo vya uongozi kama vile NAAPA NITALINDA NA KUTETEA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOWEKWA KWA MUJIBU WA SHERIA, NA KWAMBA KATIKA KUTIMIZA MAJUKUMU YANGU SITAPENDELEA WALA KUONEA MTU.....haviheshimiwi ipasavyo viapo hivi

NAWASILISHA

Ni mimi:
Missile of the Nation (Komboro hatari la Ulinzi wa Taifa)
Umetisha sana your real a GT
 
Kama huwezi kujenga hoja bila kutukana huo ni uwezo mdogo sana wa kufikiri.
Na wewe pia kama ni walewale wa kule chatle city....nawe ni 'mshamba tu' tatizo lenu mnamsapoti huyu mshamba kwa mambo ya kipuuzi kabisaaa eti kisa tu ni mtu wa huko kwenu....kweli nimeamini ushamba ni mzigo aiseee
 
Huyo ni 'mshamba' tu hana jipya , hayo yote uliyo orodhesha ulikuwa ni mipango ya serikali EXCEPT hilo la kununua ndege, and it is something which is not important for Tanzanians right now,
Watanzania wanahitaji maji safi na sio mindege.....ulikinganisha na uhitaji wa maji.

Jk amefanya makubwa mno katika mabarabara na huyo ' mshamba ' ndio alikuwa msimamizi wa miradi hiyo na anajua kuwa nini serikali ili plan.

Yeye hana pesa ya kufanya lolote kwa sababu kazi zote zinafanywa kwa kodi ya Watanzania ikiwepo kumnunulia suti anayovaa, chakula anachokula n.k

Therefore, huyo ni ' mshamba tu' hana jipya.
Mkuu huyu mshamba atakuongoza wewe mjanja hadi 2025 upo hapo?Huyu mshamba anakufanya ujifiche kwenye ID fake humu, upo hapo?Kwa haya mawili tu Wewe na yeye nani MSHAMBA?
 
Nimeshindwa nijibu nini yeye ni msimamizi wa matumizi wa kodi zetu kwa kuna Rais yoyote duniani anaendesha nchi kwa pesa yake ya mfukoni???

Hayo matusi sio utamaduni wetu watanzania badirika ndugu yangu jenga hoja
Na wewe pia mshamba tu, ni wale wale tu nyie
 
MLETA MADA UNASEMA

HOJA: 1. Ujenzi wa barabara Nchi Nzima kwa gharama Sh. Trilioni 5.3 ili kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ya biashara kutoka sehemu moja kwenda nyingine.....

JIBU: Acha kutamka tu, sema ni barabara zipi hizo zinazokusudiwa kujenga, Tunachojua ni Kwamba Barabara zilijengwa za kuunganisha Kila mkoa na almost kila wilaya wakati wa JK , Na huyu JPM ndiye aliyekuwa msiamazi mkuu wa ujenzi huu!. Siku nyingine badala ya KULETA FIGURE pekee ili kuibua hisia leta mifano halisi.

HOJA: 2. Ununuzi Ndege Mpya Sh. Trillioni 1.3 ili kuchochea sekta ya Utalii na Biashara ya ndani ya nchi yetu...

JIBU: Ni utafiti gani umeufanya kuwa Ununuzi wa ndegu Unaongeza utalii?, maana kudhani kuwa na ndege ndo kuinua utalii ni dhana potofu, kwa mfano takwimu ziko wapi kuonyesha kuwa ununzi wa ndege umechochea utalii?. Takwimu ziko wapi zinazoonyesha namna Ndege tulizonunua zimestimulate utalii?. Operation cost za kuendesha hizo ndege ukilinganisha pesa zinazoingiza ni kiasi gani?, lete takwimu ndugu, usiorodheshe vitu kama listi ya wachezaji wa pira oyesha impact ya kitu. Tunachojua ni kwamba biashara ya ndege ni baishara pasua kichwa, na Taarifa za PAC na ripoti za CAG zimeonyesha miongoni mwa mashirika yanayopata hasara mpaka sasa ni ATCL, hizo ndege zimetusaidia vipi?. Lakini pia hizo ndege zimenunuliwa bila pesa kuidhinishwa na bunge, ndege zimenunuliwa kwa utashi tu bila kufuata sheria, hatujui tumepigwa au la, inabidi kamati maalum ya bunge au CAG achunguze hili.

HOJA: 5. Ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) Sh. Trillioni 7 baada ya kukaa na reli ya mkoloni tuliyorithi zaidi ya miaka 200 iliyopita....
JIBU: Mleta mada, seriously unaamini hatujawahihi kuwa na reli nyingine isipokuwa iliyoaachwa na mkoloni?. Reli ya TAZARA unaijua?

HOJA: 9.Ukarabati Viwanja vya Ndege Nchi Nzima Sh. Trilioni 1.8
JIBU: Ukarabati wa viwanja vya ndege nchi nzima ulifanywa kwa asilimia kubwa na serikali iliyopita ya JK, labda utuambie kuwa huyu anamaliziamalizia kazi na pia gharama kubwa hapo imetumika kwenye ujenzi wa Uwanja mpya wa Chato usio na faida yoyote ya maana kiuchumi kwa nchi

HOJA: 11. Miradi ya Usambazaji Umeme vijijini kupitia Rea Umeme unaendelea kuchomoza vijijini...
JIBU: Usitutanie kuhusu REA, Sema JPM anaendeleza REA, lakini REA ilikuwepo toka awamu iliyopita, watu wamekatwa kodi wakati wakinunua umeme wa LUKU kwa ajili ya REA kwa muda mrefu kabla JPM hajawa raisi, na kukuonyesha kuwa REA ipo toka awamu iliyopita mimi kwa mfano umeme wa REA ulifika kijijini kwetu toka mwaka 2013 wakati wa JK

HOJA: 13 Ununuzi wa vivuko vya Majini maeneo mbalimbali ili kurahisisha usafiri wa watu na mizigo ya biashara.....
JIBU: Hujaeleza kivuko gani?, Maana huyuhuyu JPM alipokuwa Waziri wa Mambo ya Ujenzi alikuwa akisifu kila wakati kuwa JK kanunua vivuko vingi sana hapa nchini, Msidhani watanzania hatuna kumbukumbu vizuri na msitake kusafiria nyota za wenzenu , tengenezeni Legacy zenu lakini msiibe legacy za watu

HOJA : 14. Ujenzi wa madaraja mfano Mfugale, Ubungo interchange, Surrender bridge n.k
JIBU: Daraja La baharini la Surrender siyo necessity ya Mtanzania ni la show off zaidi kuliko haja na umuhimu wake, Daraja la Mfugale, pesa ilitafutwa na utawala uliopita na mikataba ilisainiwa na utawala uliopita. Hebu Linganisha Significance ya madaraja hayo na daraja kama la Mkapa lilojengwa na BWM, Malagarasi, Kilombero, Kigamboni yaliyojengwa na JK . Hayo ndiyo madaraja ya Legacy na kujivunia kwa mtu mwenye hadhi ya Raisi siyo daraja la Flyover ya Mfugale

HOJA: 15. Miradi ya Maji inayoendelea Kujengwa Maeneo Mbalimbali ya Nchi yetu ni mapinduzi kwenye sekta ya Maji.....
JIBU: Mkapa alileta maji kutoka ziwa Victoria mpaka Shinyanga, Kikwete akatutengenezea mradi mpya kutoka Ruvu chini kupitia bunju kuja mpaka Dar, Visima kibao vilijengwa nchi nzima!. Upo wapi mradi wa scale ya ule wa BWM au JK katika serikali hii?

Baada ya kukujibu hoja zako nikueleze sasa mambo ya msingi sana ambayo yanatugusa wananchi serikali hii haijafanya
1. Haiheshimu katiba iliyoapa kuilinda, kuna uonevu uliokithiri nchini kwa watu na taasisi mbalimbali kama vile wanasiasa wa upinzani, waandishi wa habari, vyama vya siasa etc

2. Wakulima wameendelea kutendewa visivyo haki, wakulima wa korosho walichukuliwa korosho zao kinguvu, zao la mbaazi limevurugwa, Zao la kahawa limeveurugwa

3. Wafanyakazi hawapewi stahiki zao kwa mujibu wa sheria za kazi, nyongeza ya kila mwaka iliyopo kwa mujibu wa sheria haipo

4. Wastaafu wanahangaika, wanapigwa danadana nenda rudi, wengine wanakaa miaka kibao bila mafao

5. Hali ya usalama wa wananchi iko matatani, watu wanatekwa, wengine wanapotea katika hali ya kutatanisha, watu wanaogopa hawajui fate yao itakuwa nini

6. Biashara zinaporomoka, Juzi hapa wafanyabiashara wamekiri jinsi TRA ilivyokuwa ikiwanyanyasa, biashara nyingi zimefungwa, maisha yamezidi kuwa magumu

7. Kilimo kiko arijojo, bajeti ya kilimo imezidi kupungua mwaka after mwaka, Pesa zinazopelekwa kwenye kilimo wakati mwingine haifiki hata asilimia 30 ya bajeti iliyotengwa, katika hali kama hii utainuaje hali za watanzania wakati zaidi ya asilimia 70 ya watu wetu wantegemea kilimo?

8. Ajira zimeendelea kuwa bomu linalosubiri kupasuka, mwaka wa 4 huu serikali inasuasua kwenye ajira, hata sekta binafsi ambayo ingebidi iisaide serikali kuajiri inasuffer, Sekta binafsi imekuwa paralysed, sasa katika hali kama hii Ujenzi wa uwanja wa ndege Chato au daraja la Surrender unawasaidia vipi vijana?. hata pesa ambazo inabidi zitengwe na Wakurugenzi kwa mujibu wa sheria hazitengwi, wewe mwenyewe unalifahamu hili vizuri

HITIMISHO:
Mleta mada umeleta habari za utendaji wa awamu hii lakini ambacho hujakisema ni kwamba miradi mingi inayofanyika kwenye awamu hii ni miradi iliyoanzishwa kutafutiwa fedha na serikali zilizopita, kwa hiyo awamu hii inamaliziamalizia na kuongezea hapa na pale palipopungua

Pili, Miradi mikubwa kama SGR inatoa pesa nje badala ya kuingiza pesa ndani, Chuma tunatoa nje, kabla ya kuanza ujenzi pale tungehakikisha tumewekeza Liganga na mchuchuma ili tutumie chuma chetu cha humuhumu nchini ili pesa nyingi zaidi ibaki ndani etc, Lakini pia miradi mingine siyo Miradi PRIMARY kwa uchumi ni miradi SECONDARY kiuchumi kwa mfano mradi wa uwanja wa ndege Chato au Daraja la kupitia "Baharini" la Surrender

Tatu miradi hii inafanyika wakati maisha na mahitaji ya watu hayaguswi ipasavyo, Mkulima kama vile wa korosho, kahawa,etc ameendelea kutopewa umuhimu wa maana, Ajira za wananchi ziko chini, Private sector imesuffer mno ndani ya miaka hii minne.

Hali ya Kidemokrasia na kuheshimu viapo vya uongozi kama vile NAAPA NITALINDA NA KUTETEA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOWEKWA KWA MUJIBU WA SHERIA, NA KWAMBA KATIKA KUTIMIZA MAJUKUMU YANGU SITAPENDELEA WALA KUONEA MTU.....haviheshimiwi ipasavyo viapo hivi

NAWASILISHA

Ni mimi:
Missile of the Nation (Komboro hatari la Ulinzi wa Taifa)
Swali dogo tu kwenye viwanja vya ndege kuwa ye anamalizia malizia tu.Uwanja wa ndege Dar terminal 3 umeanza mwaka gani?Hadi unazinduliwa juzi ni miaka 4 toka utawala wa JPM uanze, Je ni kweli hicho kiwanja JPM kamalizia malizia tu kwa maana ya kazi kubwa ilifanywa na JK?
 
Swali dogo tu kwenye viwanja vya ndege kuwa ye anamalizia malizia tu.Uwanja wa ndege Dar terminal 3 umeanza mwaka gani?Hadi unazinduliwa juzi ni miaka 4 toka utawala wa JPM uanze, Je ni kweli hicho kiwanja JPM kamalizia malizia tu kwa maana ya kazi kubwa ilifanywa na JK?

Suala la miradi huwa tunaangalia haswa ni nani aliyeplan kisha akatafuta fedha. anayeplan na kutafuta fedha ni kama ARCHITECT wa NYUMBA yaani , Anayesiamamia ujenzi mpaka ikaisha ni msimamizi tu wa kuwasiamamia mafundi, kuwakaripia hapa na pale wafanye kazi vizuri etc, Sasa huwezi kumlinganisha Architect na msimamia ujenzi aliyepewa ramani na fedha za kuimplement ramani hiyo mpaka jengo likamilike
 
Mleta mada seriously unaamini kuwa REA ni mradi ulionza na JPM?.
Nenda kaangalie risiti zako za kununua Luku kuanzia 2014 kurudi nyuma utaona kuwa ulikuwa ukikatwa kodi kwa ajili ya REA, na vijiji vingi sana vimepatiwa umeme wa REA kabla ya 2015

Na seriously unaamini kuwa SGR ni maamuzi magumu ya JPM?

Ngoja nikueleze sasa kuhusu SGR, SGR ni mradi uliobuniwa, na serikali ya JK, na hata Memoraundum of understanding ya awali kabisa kati yetu na EXIM bank ya China ya mkopo nafuu wa miaka 20 ulishasainiwa na serikali ya JK. Huyu wa sasa alipoingia madarakani alifanya kubadiri mkataba tu, badala ya wachina akawapa Waturuki

Angalia hapa Chini JK anahangaikia SGR kabla hata JPM hajawahi kudhani kuwa anaweza kuwa rais

View attachment 1173856
Shida mnashindwa kujua Yote unayoyaona saizi yanatoka kwenye BAJETI YA AWAMU YA TANO. Ukisoma Ilani ya CCM 2015/20 iko wazi kabisa. Kuna miradi inatakiwa kumaliziwa, Kuendelezwa na kuanzishwa.

Sasa wewe ukisema REA kafanya JK sijui kama unataka kusema Jk alipotoka madarakan aliacha hela za kuhakikisha vijiji vyote vinapata umeme hata kama ni hadi 2050.JK kaacha Ujenzi wa Kinyerezi 1 na Jpm kaja kaendeleza kinyerezi 2,wewe ukija na hoja za kinyerezi ni mradi wa JK na JPM hana alichofanya sijui kama unakua na logic. JK kaacha mipango ya SGR,hajaacha hata sent na ilikua iwe mchina lkn JPM kampa mturuki, Reli inajengwa unakuja kusema ni kazi ya Jk na JPM hakuna anachotaka. Hivi huyo Jk toka alipoondoka 2015,haya yote yanayofanyika yeye ndio director?

Mradi wa Bagamoyo ulianzishwa na JK lkn JPM kaja kaupiga chini,kwanini hatuoni kuwa ktk miradi iliyoasisiwa na JK,JPM ananguvu nayo?Nilifuatilia uzinduzi wa hospital ya mloganzila Jk aliacha hatua ndogo sana pamoja na pesa ya mradi, lkn JPM kama Ilani ilivyosema kuwa anatakiwa akamilishe huo mradi tunaona fungu la kukamilisha hiyo hospital lilitoka kwenye bajeti yake.Leo unakuja unasema Jpm hospital ya mloganzila haimuhusu, ni Jk. Uko serious au unafanya SIASA UCHWARA?

Unajua mradi wa REA ulikua ukwame baada ya msaada wa 900B kupigwa chini 2016?Lkn je umekwama?Leo unaendelea kama kawaida, unasema mradi ni wa JK na JPM hana lolote. Are u serious?Miradi mingapi huwa inaishia kwenye makaratasi?Miradi mingapi huwa inakwama na mingine kwenda mwendo wa konokono?Kwamba mlitaka JPM aje apige chini terminal 3,apige chini mloganzila, barabara ambazo hazijaisha aachane nazo naye aanze zake, SGR apige chini au REA apige chini?Nini maana ya mipango ya serikali Kama kila kiongoz ili aonekane kafanya kazi lzm aje na mipango mipya?
 
Hoja namba 2 ndege wakati mmezikimbizia ofisi ya raisi na hamruhusu hata CAG akague we bwege sana,Ajira karibu awamu 4 zimelala mtaani we unajipendekeza ati upate cheo.
 
Mkuu huyu mshamba atakuongoza wewe mjanja hadi 2025 upo hapo?Huyu mshamba anakufanya ujifiche kwenye ID fake humu, upo hapo?Kwa haya mawili tu Wewe na yeye nani MSHAMBA?

Mkuu fake ID zilianza enzi za awamu ya tano!?
 
Back
Top Bottom