Rais Magufuli amteua Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania

Hongera zake,Naona Walimu wako vizuri kwa sasa,by Professional PM mwalimu,President nae Mwalimu,,,,,Hongera saana Walimu,na mimi naanza mipango ya kuwa Mwalimu.
 
Hapa Kazi Tu ni "Majaliwa"...!

Nadhani "wenzetu" wamefurahishwa sana na uteuzi huu...

A kind of "remote-controlled" governance...!
 
Rais akisafiri/ akifariki ni nani atafanya shughuli za serikali bungeni ma shughuli zingine za waziri mkuu?
Kama rais hajawahi kufariki ni kwa nini unabet afariki!? Kwani CJ, Mkuu wa majeshi na spika hawapo!?
Hivi vyeo vyote tumeiga kutoka kwa mababa wa demokrasia na utawala, ndio maana Waingereza wana PM lakini hawana rais, Amerika wana rais na VP lakini hawana PM, vivyo hivyo na kwingineko. Sasa sisi kwa vile shida yetu ni kugawa vyeo tumecombine vyote mradi kila mtu apate cheo! Ni gharama kwa nchi changa na masikini.

 
Ni mda sahihi sasa kwa watanzania kupigania katibu mpya, hiki cheo cha waziri mkuu kina maana gani kama kuna makamu wa rais?? Kwanini makamu wa rais asifanye kazi za waziri mkuu au awepo waziri mkuu tuu?? Hizi nchi ndogo ndo zina vyeo vya ajabu sana.

Waziri mkuu ni rais wa Tanganyika. Hawezi kuwa mzanzibar mkuu
 
Raisi Kanda ya ziwa, waziri mkuu kusini safi sana.
 
Tetesi zinasema Makamba ndio waziri mkuu. Pathetic sana, kama atamteua Makamba nitajua kuwa kuna remote control.
kama Makamba angekuwa waziri mkuu mitandao yote ingedhibitiwa uhuru wa habari kuminywa kisawasawa, kama angemteua mwigulu, uonevu dhidi ya wananchi wasio na hatia hasa wapinzani wangeumia, kama angemteua Lukuvi basi misifa ingekuwa kibao, mwakyembe hapo kiu ya wananchi ingekamilika lakini swala dini likawa kikwazo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…