Katibu wa bunge ametoa taarifa kwa bahasha kuletwa rasmi bungeni!.Mpambe ameileta bahasha kavukavu tuu bila briefcase kama spika alivyodai!, ila bahasha iko ndani ya bahasha na ndani ya bahasha tena! sasa inasomwa!.
Spika anasoma; '' Job Ndugai, Mh Spika, mimi mwenyewe kwa nafasi yangu kama Rais wa JMT nimemteua Mbunge wa Ruangwa mh. Kassim Majaliwa kuwa waziri mkuu wa JMT.''
Tusubiri kama ataendana na kauli mbiu ya #Hapakazi tu.
Hatimaye Waziri Mkuu Mh. Kasim Majaliwa apendekezwa na Rais kisha kupigiwa kura na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwenye Ukumbi wa Bunge Makao Makuu ya Tanzania, Dodoma, leo tarehe 19 November 2015.