Rais Magufuli atokwa na Chozi la huzuni: Mzee Mkapa alinilea kama mtoto wake, alikuwa ni shujaa wangu, alinionyesha upendo

Rais Magufuli atokwa na Chozi la huzuni: Mzee Mkapa alinilea kama mtoto wake, alikuwa ni shujaa wangu, alinionyesha upendo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760


RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli, amejikuta akitokwa machozi hadharani baada ya shindwa kujizuia wakati akielezea mazungumzo yake ya mwisho na Rais mstaafu awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam

Hilo limejitokeza leo Jumanne tarehe 28 Julai 2020 katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kulipokuwa kunafanyika shughuli ya kuaga Kitaifa mwili wa Mkapa aliyefariki dunia Alhamisi tarehe 23 Julai 2020 saa 3:30 usiku kwa mshituko wa moyo.

Akihutubia taifa katika shughuli hiyo iliyohudhuriwa na maelfu ya waombolezaji uwanjani hapo, Rais Magufuli amesema “hakuna mtu anayeweza kumwelezea vizuri Mzee Mkapa zaidi alivyojieleza mwenyewe vizuri kwenye kitabu chake cha My Life, My Purpose.” (Maisha Yangu, Kusudio Langu).

Katika hotuba yake, Rais Magufuli ambaye alikuwa mara kadhaa anatulia, akilengwa lengwa na machozi akisema kifo cha Mkapa ni pigo kwani ilizoeleka katika matukio makubwa anaungana na marais wenzake wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Jakaya Mrisho Kikwete ‘lakini leo hapa hayupo.”

“Mzee Mkapa alinilea kama mtoto wake, alikuwa ni shujaa wangu, alinionyesha upendo,

“Hata kwenye shida Mzee Mkapa hakuniacha kamwe, hakutaka nianguke, alinilea kama mtoto wake. Wakati wote alikuwa ananionyesha upendo, hivyo basi kuondoka kwake ni pigo kubwa kwangu, nimepoteza mtu muhimu kwangu.”

“Saa nyingine machozi yanakuja tu msinishangae sana, hata Mzee Kikwete nilimuona juzi anadondosha machozi tena Kikwete ni Kanali ila alitoa chozi kwahiyo msinishangae mimi,” amesema Rais Magufuli

“Nilipata fursa ya kuongea na Mzee Mkapa kwa simu akiwa hospitalini saa chache kabla hajafariki, nakumbuka aliniambia John usiwe na wasiwasi naendelea vizuri sikujua kwamba maneno yale yalikuwa ya kuniaga. kazi ameikamilisha,” amesema Rais Magufuli huku akitulia na kutoa kitambaa kufuta machozi.
 
Swali zuri sana. Nimesikia kuwa kulikuwa na kodi ya kichwa, baiskeli na mifugo wakati huo! Lakini usishangae wanasiasa wakampamba Mwinyi kuliko Mkapa. Tuombe tu uzima.

Kwa mujibu wa sifa zilizotolewa katika kipindi hiki ni wazi kuwa Mkapa alipokea taifa toka kwa Mzee Mwinyi likiwa KOPO TUPU. Sasa sijui Mzee Mwinyi sifa zake zitakuwa zipi akifa.
 
Haya maneno alitakiwa ayaongee wakati Mkapa yuko hai. Maana mzee Mkapa angeona fahari kwamba kuna fadhila ana rudishiwa.

Lakini kumsifu marehemu haileti faida zaidi ya kuongea.

Tulizowea kusikia Mh JPM akituambia watangulizi wake hawakufanya kitu. Na nchi imeliwa sana. Kumbe sio kweli? Leo ana tuambia Mzee Mkapa ndie royal model wake. Ndie mwanzilishi wa karibu vitu vyote anavyo endeleza. Tushike lipi? /RIP BABA Mkapa.
 
Wakuu naomba niwaulize kitu.
Wakati nasikiliza hiki kipande machozi yamenitoka. Ni kila mmoja wetu yamemtokaaa au ni mimi tu na watu wachache. Nikimaanisha kweli kunaambae ataangalia hiki kipande asitokwe na machozi kabisa?

Je yule ambaye hayajatoka machozi kwamba yuko stronger than sisi tuliotokwa machozi??!!
Hem naombeni michango yenu ktk hili maana dah basi binadam tutakua tunatofautiana sana tena.
 
Kwa mujibu wa sifa zilizotolewa katika kipindi hiki ni wazi kuwa Mkapa alipokea taifa toka kwa Mzee Mwinyi likiwa KOPO TUPU. Sasa sijui Mzee Mwinyi sifa zake zitakuwa zipi akifa.
Sifa hutengenezwa chap, wabongo tu nao madizaina na makonstrakta wa sifa subiri utakujashangaa.
 
Wakuu naomba niwaulize kitu.
Wakati nasikiliza hiki kipande machozi yamenitoka. Ni kila mmoja wetu yamemtokaaa au ni mimi tu na watu wachache. Nikimaanisha kweli kunaambae ataangalia hiki kipande asitokwe na machozi kabisa?

Je yule ambaye hayajatoka machozi kwamba yuko stronger than sisi tuliotokwa machozi??!!
Hem naombeni michango yenu ktk hili maana dah basi binadam tutakua tunatofautiana sana tena.
mwenzako kalia sababu marehemu ndio alimfikisha hapo alipo. wewe umelia sababu gani?
 
Back
Top Bottom