Rais Magufuli awachana Kilwa kwa kumchagua mpinzani Bwege. Awataka kutofanya makosa tena uchaguzi ujao

Rais Magufuli awachana Kilwa kwa kumchagua mpinzani Bwege. Awataka kutofanya makosa tena uchaguzi ujao

Mimi huwa najuliza hivi anapopita kwenye majimbo yanayoongozwa na wabunge wa CCM na kukuta wananchi wana matatizo kama hayo au pengine makubwa zaidi huwa anawaambia kuwa walikosea kuchagua...??!!
Huyu dingi ni sheedah
 
ILANI ya ccm inatekelezwa na wana CCM,,, ukimchagua mbunge wa chama cha Jahazi Asilia au Tadea basi atatekeleza ILANI ya chama chake

Kwa hiyo ilani inaposema kuinua uchumi wanainua uchumi wana ccm tu? Ilani ikisema kujenga uchumi wa viwanda wanaccm ndio wanaolipa kodi za kujenga viwanda? Au ndio ma engineer? Au ndio wanaozalisha malighafi za viwandani? Au ndio wanaotafuta masoko au kununua bidhaa? Maboresho ya huduma za Afya wanaccm wanaboreshaje? Wanatoa fedha za kujenga hosptailini ama kununua madawa ama kutengeneza madawa? Unajua nguvu kazi ya kiwango gani ambayo haitumiki ipasavyo kwa maendeleo ya taifa kutokana na ukiritimba wa watu wenye mitazamo na uelewa kama zako? Kwa kuwazuilia maendeleo wananchi waliochagua upinzani unaelewa kumeathiri maendeleo ya taifa zima kwa kiwango gani?

Fedha zote za maendeleo ni za wananchi wote bila kuajli vyama, kabila wala rangi. Mikopo ya nje inalipwa kwa kodi za Watanzania ambazo hawalipi wanachama wa chama kilichoko madarakani tu. Niambie mradi wowote wa maendeleo ya wananchi unaojengwa kwa fedha za ccm.

Kama kuna ubadhilifu katika halmashauri ama matumizi mabaya ya raslimali viko vyombo vya dola ambavyo vinawajibu wa kulinda maslahi ya kila mtu na kuwajibisha kila mtu anayevunja sheria. Kama ndivyo kwa nini hivyo vyombo havijaichukulia hatua halmashauri hiyo kama ni badhirifu?a

Mbona vyama vya upinzania wanapotuhumiwa kwa makosa wanakamatwa na kupelekwa katika vyombo husika bila kujali kwamba si wanachama wa ccm? Halmashauri zote zinafanyiw aukaguzi wa mahesabu na hakuna sheria inayozuia mamlaka kuchukua hatua muhimu kwa halmashauri za vyama visivyo madarakani.

Kama kuna matatizo ya kiwango na uwezo wa mbunge, ninadhani ilikuwa sahihi kuwatahadharisha wananchi kwamba wachague viongozi wenye uwezo wa kuelewa na kufuata kanuni kitu ambacho hakina uhusiano wowote na uanachama wa chama cha siasa cha mtu. Na hili linatakiwa kwenda kwenye maboreshoya sifa za mtu kugombea nafasi za uongozi badala ya mtu kujua kusoma na kuandika tu kana kwamba elimu ya nchi haikui.

Watu wanashuhuda za kutosha tu kwamba maeneo ya upinzani zimekuwa zikikwamishwa katika mipango ya maendeleo makusudi ili wananchi waendelee kuishi katika ujima tofauti na zile za ccm. Hii ni hila ya kutaka kuwaaminisha kwamba wasipochagua ccm wataadhibiwa kwa kunyimwa maendeleo bila kujali kwamba maendeleo ni haki yao ya kikatiba.

SASA MUNGU AMETUPONYA COVID 19, TUNAPASHWA KUMSHUKURU KWA TOBA. TOBA YA KWELI NI KUJUTIA DHAMBI NA KUZIACHA. TUKIENDELEA KUJIFANYA WAJANJA KANA KWAMBA MUNGU HANA HAONI AMA HATA ANAPOONA HANA UWEZO TWAJIDANGANYA. TUWENI WA KWELI.
 



Wakuu, MAENDELEO HAYANA CHAMA

Rais Magufuli akiwa safarini kutoka Mtwara, ameombwa na mwanakijiji Jimbo la Kilwa kwamba hawana Stendi ya Magari hivyo anaomba wajengewe. Rais Magufuli amejibu kwamba siku nyingine waangalie wawakilishi wanaowachagua ili waweze kufanya vile yeye anavyowaagiza. Mbunge wa jimbo hili aliyemaliza muda wake ni Seleman Bungara aka Bwege Mzee wa ''Umesikia Wapi'' ambaye alikuwa anatokea chama cha wananchi CUF Habari

Rais amezidi kusema kwamba miradi kama hiyo ni ya wabunge na Madiwani ndiyo wanapaswa kuisimamia hivyo kuwataka wabaki na Bwege wao


Rais Magufuli amesema haya...

Nilikuja hapa nikasema nichagulieni watu nitakaokuwa nawaagiza wanafanya ninayoyataka mkasema hapana, Mkamchagua Bwege basi shauri yenu na bwege wenu mwambie awatengenezee stendi

Kazi ya Stendi ni ya madiwani, wabunge. Ukikosea kuchagua, nafuu ukosee kuoa au kuolewa. Ukikosea kuchagua ni tatizo kubwa.


Na hili ndugu zangu niwaombe, muwe waangalifu katika kuchagua. Mchague watu ambao watakuwa kwa ajili ya watu masikini.

Tunatuma hapa fedha za road fund, tunatuma fedha hapa za halmashauri, zimeshindwa kweli kujenga stendi?

Lakini kwa sababu mnanichagulia, wao wenyewe mastendi unategemea mimi mwenyewe nifanyeje? Huo ndiyo ukweli sitaki kuwaficha mlikosea kuchagua.


Sasa katika uchaguzi wa mwaka huu mjipange vizuri, mchague mtu ambaye mtakuwa mmempa stendi akikataa nitamfukuza hata kwenye chama. Lakini leo nitamfukuza huyo aliyeko kwenye chama sijui hata yuko kwenye chama gani, nitamchukulia hatua gani?


Chama cha ACT Wazalendo kimelaani vikali na kuwahamasisha wananchi kukemea vikali kauli hizi za kibaguzi. Wamedai kuwa kitendo cha kuhamasisha ubaguzi na kuingilia mamlaka ya wananchi katika kuchagua mtu wamtakaye kinakiuka misingi ya Katiba yetu.

Jimbo la Kongwa, kuna mbunge sijui katokea chama gani yule. Na kama katoka ccm mbona hakuna la maana pale. Wananchi shida ya maji ni ya
Amesema wachaguliwe watu ambao anaweza kuwawajibisha wakifanya ndivyo sivyo hata kuwafukuza kwenye Chama
Jimbo la Kongwa sijue walichagua wa chama gani maana shida ya maji haijawahi kutatuliwa na wananchi wana shida kweli kweli. Nadhani angetoka chama cha kijani angefukuzwa.
 
Ndo maana nasema kama Jpm amekuwa rais hakuna asiyeweza kuwa rais nchi hii.Sijawahi on a rais mbaguzi mkubwa tangu nchi yetu ipate Uhuru kama huyu.
bora tungeongozwa na pierre au amber rutty kuliko huyu mhutu wa chattle mwenye roho mbaya, chuki na mbaguzi! raiss wa ajabu hajawahi kutokea!

sijui kwann hachambui hachambui kauli zake kabla ya kuzitamka, ni aibu!
 
Kwa hiyo ilani inaposema kuinua uchumi wanainua uchumi wana ccm tu? Ilani ikisema kujenga uchumi wa viwanda wanaccm ndio wanaolipa kodi za kujenga viwanda? Au ndio ma engineer? Au ndio wanaozalisha malighafi za viwandani? Au ndio wanaotafuta masoko au kununua bidhaa? Maboresho ya huduma za Afya wanaccm wanaboreshaje? Wanatoa fedha za kujenga hosptailini ama kununua madawa ama kutengeneza madawa? Unajua nguvu kazi ya kiwango gani ambayo haitumiki ipasavyo kwa maendeleo ya taifa kutokana na ukiritimba wa watu wenye mitazamo na uelewa kama zako? Kwa kuwazuilia maendeleo wananchi waliochagua upinzani unaelewa kumeathiri maendeleo ya taifa zima kwa kiwango gani?

Fedha zote za maendeleo ni za wananchi wote bila kuajli vyama, kabila wala rangi. Mikopo ya nje inalipwa kwa kodi za Watanzania ambazo hawalipi wanachama wa chama kilichoko madarakani tu. Niambie mradi wowote wa maendeleo ya wananchi unaojengwa kwa fedha za ccm.

Kama kuna ubadhilifu katika halmashauri ama matumizi mabaya ya raslimali viko vyombo vya dola ambavyo vinawajibu wa kulinda maslahi ya kila mtu na kuwajibisha kila mtu anayevunja sheria. Kama ndivyo kwa nini hivyo vyombo havijaichukulia hatua halmashauri hiyo kama ni badhirifu?a

Mbona vyama vya upinzania wanapotuhumiwa kwa makosa wanakamatwa na kupelekwa katika vyombo husika bila kujali kwamba si wanachama wa ccm? Halmashauri zote zinafanyiw aukaguzi wa mahesabu na hakuna sheria inayozuia mamlaka kuchukua hatua muhimu kwa halmashauri za vyama visivyo madarakani.

Kama kuna matatizo ya kiwango na uwezo wa mbunge, ninadhani ilikuwa sahihi kuwatahadharisha wananchi kwamba wachague viongozi wenye uwezo wa kuelewa na kufuata kanuni kitu ambacho hakina uhusiano wowote na uanachama wa chama cha siasa cha mtu. Na hili linatakiwa kwenda kwenye maboreshoya sifa za mtu kugombea nafasi za uongozi badala ya mtu kujua kusoma na kuandika tu kana kwamba elimu ya nchi haikui.

Watu wanashuhuda za kutosha tu kwamba maeneo ya upinzani zimekuwa zikikwamishwa katika mipango ya maendeleo makusudi ili wananchi waendelee kuishi katika ujima tofauti na zile za ccm. Hii ni hila ya kutaka kuwaaminisha kwamba wasipochagua ccm wataadhibiwa kwa kunyimwa maendeleo bila kujali kwamba maendeleo ni haki yao ya kikatiba.

SASA MUNGU AMETUPONYA COVID 19, TUNAPASHWA KUMSHUKURU KWA TOBA. TOBA YA KWELI NI KUJUTIA DHAMBI NA KUZIACHA. TUKIENDELEA KUJIFANYA WAJANJA KANA KWAMBA MUNGU HANA HAONI AMA HATA ANAPOONA HANA UWEZO TWAJIDANGANYA. TUWENI WA KWELI.
Deep sana hii mpaka machozi yamenijia kwa hisia
 
Anaposemaga maendeleo hayana chama huwa anamaanisha nini?
 



Wakuu, MAENDELEO HAYANA CHAMA

Rais Magufuli akiwa safarini kutoka Mtwara, ameombwa na mwanakijiji Jimbo la Kilwa kwamba hawana Stendi ya Magari hivyo anaomba wajengewe. Rais Magufuli amejibu kwamba siku nyingine waangalie wawakilishi wanaowachagua ili waweze kufanya vile yeye anavyowaagiza. Mbunge wa jimbo hili aliyemaliza muda wake ni Seleman Bungara aka Bwege Mzee wa ''Umesikia Wapi'' ambaye alikuwa anatokea chama cha wananchi CUF Habari

Rais amezidi kusema kwamba miradi kama hiyo ni ya wabunge na Madiwani ndiyo wanapaswa kuisimamia hivyo kuwataka wabaki na Bwege wao


Rais Magufuli amesema haya...

Nilikuja hapa nikasema nichagulieni watu nitakaokuwa nawaagiza wanafanya ninayoyataka mkasema hapana, Mkamchagua Bwege basi shauri yenu na bwege wenu mwambie awatengenezee stendi

Kazi ya Stendi ni ya madiwani, wabunge. Ukikosea kuchagua, nafuu ukosee kuoa au kuolewa. Ukikosea kuchagua ni tatizo kubwa.


Na hili ndugu zangu niwaombe, muwe waangalifu katika kuchagua. Mchague watu ambao watakuwa kwa ajili ya watu masikini.

Tunatuma hapa fedha za road fund, tunatuma fedha hapa za halmashauri, zimeshindwa kweli kujenga stendi?

Lakini kwa sababu mnanichagulia, wao wenyewe mastendi unategemea mimi mwenyewe nifanyeje? Huo ndiyo ukweli sitaki kuwaficha mlikosea kuchagua.


Sasa katika uchaguzi wa mwaka huu mjipange vizuri, mchague mtu ambaye mtakuwa mmempa stendi akikataa nitamfukuza hata kwenye chama. Lakini leo nitamfukuza huyo aliyeko kwenye chama sijui hata yuko kwenye chama gani, nitamchukulia hatua gani?


Chama cha ACT Wazalendo kimelaani vikali na kuwahamasisha wananchi kukemea vikali kauli hizi za kibaguzi. Wamedai kuwa kitendo cha kuhamasisha ubaguzi na kuingilia mamlaka ya wananchi katika kuchagua mtu wamtakaye kinakiuka misingi ya Katiba yetu.
Kama hoja ndio hiyo, kuna uhalali gani wa kuwa na mfumo wa vyama vingi? Vifutwe tu ijulikane wazi tuna mfumo wa chama kimoja kuliko kuudanyanya ulimwengu.
 
Back
Top Bottom