Rais Magufuli, awashushua TAKUKURU na Watendaji wote wanajipendekeza kwake na kupeleka miradi ya Maendeleo Chato

Huyo boss was Takukuru kwa majibu hayo ya kutolewa nishai ili arudi kwenye chat, awafungulie haraka kesi CDM ya matumizi mabaya ya michango ya wabunge wake. Akifanya hilo atalinda nafasi yake. Kama alidhani kuwa jamaa hajui kuwa wanamsifia ili awape ulaji, basi kawaonyesha. Halafu huyo anayepewa hiyo kali ni mtu na manyota yake, na huwa anashinda na hilo kombati ili kutishia watu.
 
Huyu mzee kwa unafiki hana mfanowe!! Kuna Rais nchi hii aliyeendeleza kwao kama yeye?

Tumuulize yeye aliweka taa za barabarani chato kwa umuhimu gani?

Airport Chato na tawi la CRDB aliloshinikiza liwekwe Chato huku wafanyakazi wakishinda wamesinzia tu kwakukosa customers nani aloshinikiza yaende huko?

Huyu mzee sidhani kama yuko sawa upstairs maana hana aibu wala haya
 
Reactions: BAK
👊🏽👊🏽👊🏽👊🏽👊🏽

 
Jamaa MNAFIKI sana huyu. Anajua kweli kucheza na akili za majuha ili kuscore political points.
Huenda hata ile Eyapoti walipoijenga Chattle Rais wetu Kipenzi alichukia sana ila akashindwa tu kuwakemea..

"Rais wetu anaangushwa na wasaidizi wake" Kauli maarufu awamu hii..
 
mkuu hiyo Sanaa tu script ishandikwaga
 
Kuna mtu alienda kuchukua form akanyimwa?
 
Ulitaka akajenge kwenu?
 
ajitafakari sana, maana yawezekana hata hakujua kama Chato tayari kuna jengo la Takukuru.
hata kama Brigedia hakujua kuna ofisi tayari Chato, TAKUKURU walitumia vigezo gani kujenga Chato, off all the hundreds of districts in the country ambazo hazina ofisi, presumably including Chato, angeweza kujibu ??
 
Magufuli si wa mchezo mchezo utampelekaje Rais kufungua kajengo Kama kale tena Rais mwenyewe Kama magufuli lazima akutoenishai hii ni dharau kwa mkuu nchi
 
Walitakiwa wampangie Nyumba mtumishi wao na sio kubadili ofisi kuwa Nyumba ya kuishi labda Kama jengo lingekuwa na nafasi kubwa kuweka ofisi na makazi.
 
Mbona ilipokuwa inajengwa international airport hakufungua mdomo wake?
 
Tangu hii taasisi iwe na wakurugenzi toka jeshini ndo imekuwa ya hovyo zaidi
 
Naam huu ni ujumbe muruwa kabisa kwa wote wanaojipendekeza kwa Namba Moja.
Wenye Masikio na Wasikie...
 
Wakati unafungua Jengo la Tume ya uchaguzi jana, katika hotuba uliyotoa ulinifurahisha sana ulipowashushua watendaji wako, ambao wamepanga kwenda kujenga ofisi ya TAKUKURU huko Chato ambako tayari wanayo hiyo ofisi, ambapo kama ulivyoeleza Mheshimiwa Rais kuwa hao watendaji wako wanafanya hivyo kwa kujipendekeza kwako, jambo ulilolikemea vikali na kusema wazi kuwa halikufurahishi.

Imezoeleka kwa Watanzania wengi kuwa wanapenda mno tabia ya hiyo ya kujipendekeza kwa waheshimiwa wenye nafasi kubwa za kisiasa na wale matajiri na kuamini kuwa kwa kufanya hivyo ndiyo atakuwa amemfurahisha huyo mtu kwa kuamini kuwa siku moja atamkumbuka na kurudisha fadhila kwa kumkumbuka katika ufalme wake!

Hapo tunapata fundisho kubwa kuwa siyo vyema kwa wapangaji wa maendeleo kuendelea kupeleka maendeleo yale maeneo yasiyo na uhitaji ya "waheshimiwa" wakati maeneo mengi ya wanyonge yakiwa na uhitaji mkubwa yakisahauliwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…