Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Hii yote Ni Lissu Impact, watu mpaka wanaharibu Sasa yote kutafuta Kiki, Hakika kweli siku ya kufa nyani miti huteleza.
 
Ndio ni raisi wa nchi hivyo ana nafasi nyingi za kutafuta mahari muafaka wa kuchangia huo msikiti. Ninacho ona ana nia nzuri lakini hakuusoma mchezo vizuri au hakupata ushauri muafaka hasa wakati huu wa uchaguzi.
Mahari ndio nini?
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] duh!!
 
Ila hapa tuchutame. Taasisi imekosea tena mm ninavyojuwa Kwa Sheria za waislam lile Jambo laweza Kuwa haram. Jaman
 
Acheni unafki wenu,kwani huku mitaani na stendi za mabasi hii michango ya ujenzi wa misikiti mbona hamjaweka icho kipengele cha wanaotakiwa kuchangia hiyo michango.

Mwandishi chunga hiyo kalamu yako na usikute wewe wala sio muislamu ila unataka kuchonganisha wenye dini yao na serikali.
 
Nimesoma hadi mwisho sijaruka kipengele chochote, japo sikujua kinachoendelea lakini umeelezea vizuri nikapata mwanga,

Binafsi nakazia kwa msumari yote uliyoyaandika, Dini isichanganywe na Siasa.
Si kwa ubaya lakini ukweli ni kwamba pale ilikwa inafanyika siasa dhaifu za ccm na serikali yake, ccm hii imeshindwa kuendesha mambo kistaarabu na kujiheshimu
 
Kafiri ni mtu asie Muislam

Pera,Embe, Nanasi ukiita kwa Pamoja ni matunda si kashfa wala tusi

Kama hutaki kuitwa Kafiri tupe jina moja la kuwaita wasio waislam
Na mpagani ni mtu asiye mkristo. ngoma droo.
 
Asant kwa darasa hili pia nimejifunza kitu
 
Yeye si anawaombea Waislamu sadaka kanisani ili wajenge msikiti wao, ni lini atawaombea waislamu mahakama ya kadhi huko kanisani ili wakiristo waikubali wasiipinge?

Maana hoja za "kodi za wote zisitumike kwa ajili ya ibada ya dini fulani" zitakuwa hazina mashiko tena kwa kuwa kwa mujibu wa Magufuli wakiristo kumbe ni wema sana kuchangia mambo ya ibada za waislamu!!
 
Mkuu,

With all due respect, you won't be able to see it because that how you have been PROGRAMMED.

Nenda msome mtu anaitwa SULEIMAN TAKADIR.

Au nikikwambia tu kamsome mzee Mohamed Said na maandiko yake utasema hupendi because huyo ni mdini
Mohamed Said nimemsoma mara kadhaa humu jamnvini. Ni kweli amekuwa akituhumu sana kuwa Tanzania kuna mfumo kristo. Suleiman Takadir nimemgoogle sasa hivi na kwa kweli historia yake imenihuzunisha sana.
Lakini sijaona chochote hapo kinachohusu wakatoliki kuwachukia waislam na waislam kuwachukia wakatoliki/wakristo.
Katika jamii outliers huwa hawakosekani. Lakini outliers hawafanyi jamii nzima ya waislam kuwachukia wakatoliki au jamii nzima ya wakrtisto kuwachukia waislam.
Tukiwa objective unaweza kukuta kuna waislam wengi saaana wanamapenzi makubwa sana kwa wakristo na wakristo wengi sana wana mapenzi makubwa sana kwa waislam.
 
Moja ya misikiti bora kabisa Jijini mwanza Pale kilimahewa ulijengwa na Lowasa kama kumbukumbu zangu ziko vizuri ...maendeleo hayana vyama wala dini
 

Ungekuwa humpingi JPM kila siku. Pengine ningesoma. Naomba kuuliza kabla ya kuandika. Ulifikiria Kama. Mwislamu au kama mpinzani wa JPM. Fuatilia miaka 5 hii ya JPM na waislamu. Una akili ndogo sana. Duniani Kuna watu wana nia njema. Usiasa wa kijinga unakufanya upoteze hata akili yako. Unakuwa mtumwa wa chuki Zako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…