Sayansi ipi kwenye CORONA? Sayansi ambayo haikufaa Marekani, Spain, UK, Italy, France, German, Canada ingevaa nini Tanzania?
Endeleeni tu kujitoa akili!!!
TUtarudia tena na tena! Hizo nchi ulizotaja zote zilianza kwa mizaha kama mizaha inayofanywa na Magufuli!!
Kila mmoja anakumbuka porojo za Trump, mara aite Chinavirus, mara aite Wuhan virus, siku anahojiwa kuhusu uwezo wa US kukabili janga, Trump akajibu kwa mbwembwe wana professionals wa kutosha!!
Na hili la kuwa na professionals akawakejeli hadi Iran kwamba wakitaka msaada wa US, watawasaidia, kama ambavyo Tanzania tulivyowahi kuwaambia China tunaweza kuwapelekea madaktari wetu!!
Trump kaendelea na mizaha yake, hadi anakuja kushituka, kirusi kimeenea kila mahali! Na coronavirus akishaingia tu mtaani, kudhibiti kwake sio jambo dogo!!
Kuhusu Spain, Google mwenyewe jina la Dr. Fernando Simon uone alisema nini wakati Italy inateketea!! In short, hakudhani kabisa kwamba coronavirus ingeingia Spain, na ndio maana kama ulifuatilia, La Liga ilichelewa sana kusimamishwa!
Wakati Italy inateketea, ndo kwanza Wahispania wakawa wanaendelea kujazana kwenye viwanja vya soka, kuja kushituka.... TOO LATE!
Iran wenyewe wakati Uchina mambo si mambo, ndo kwanza wakatangaza kwamba wao hawatafunga mpaka kwa sababu nchi yao inalindwa na Mungu! Na wenyewe hadi wanakuja kushituka, ilishakuwa too late!
Mifano ipo mingi, itoshe tu kusema kote huko walichelewa kuchukua hatua!!
Kinyume na wenzetu, nchi kama Tanzania international flights ni chache, kwahiyo tulikuwa na uwezo wa kujifunza kutokana na kile kilichokuwa kinaendelea kwingine kwa sababu tulichelewa kupata maambukizi!!
Lakini wakati watu tunashauri international flights zipigwe ban ndo kwanza wenye mamlaka wakatangaza hawawezi kufanya hivyo kwa sababu itaathiri utalii!!
Matokoe yake, na sisi tukaendelea kufanya mizaha ile ile ingawaje tulikuwa na pa kujifunza!! Mizaha ikazidi, kirusi kimeshaenea hadi mtaani, na bado tunaambiwa tunaweza kuua coronavirus kwa kujifukisha mvuke!