Rais Magufuli: Hakuna lockdown Tanzania! Mwanangu amepona COVID-19 kwa kujifukiza (Mei 17, 2020)

Rais Magufuli: Hakuna lockdown Tanzania! Mwanangu amepona COVID-19 kwa kujifukiza (Mei 17, 2020)

"chocheeni kuni mbichi moto ukolee,ugali uivee,mnachotaka kitokee........"
 
Muuamini mkuu kwani nilikulazimisha uamini nianachokiami.

Ila kwa upande wangu namuona mtu ambaye si mkweli kweli kwenye mambo mengi na isitoshe nimemuweka kwenye kundi la wanafiki.

Usimuamini muongo hata kama akiongea ukweli huo ndio msimamo wangu ninaouamini whether you like or not.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mm sina tatizo na msimamo wako wa kuchagua kutomuamini "because as u said is non of my business and I respect that" tatizo lilikuwa pale tu unataka na wengine tusimuamini kwa sababu tu ww humuamini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Lakini pia tukumbuke mwisho wa mwanadamu yeyote ni kifo" mwisho wa kunukuu
Na ukumbuke pia hakuna anaependa kutangulia kufa,na ndio maana watu wanaambiwa wachape kazi wkt wao wako MBOCHI.
 
Hivi Rais huyu hawezi hutubia bila vijembe na kufoka?!
 
Je wagonjwa wamepungua sababu Corona imeisha au sababu tumesimamisha upimaji wiki ya tatu hii sasa??
 
Mkuu usishawishike hata siku moja kumuamini huyu mzee,hana ukweli hata mmoja.

Anatupeleka sipo kabisa mkuu,yaani kauli zake tu ni utata mtu alafu sijui hana kumbukumbu ya kile alichokinena hapo awali.

Tumeangamia kama taifa,dereva wenyewe ndo huyu basi tupo hatarini kutumbukia mto wami.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nikikumbuka uongo wake kwenye sakata la korosho, siwezi kumuamini huyu jamaa, labda baada ya kuvuta bangi ya lumumba inayolimwa na chakubanga.
Yeye yuko vichakani, halafu anatuambia sisi tuchape kazi.
 
Huyo Anna Mgwira alijitangaza ana Corona then juzi kasema kuna majani ameyatumia sasa akipimwa anaonekana ni Negative,hayo ndio maajabu tuliyobarikiwa.
Hata angesema alikula mchicha akapona tusingemlaumu kuliko huyu anayetafuta Kiki nyepesi. Ina maana yeye alikuwa na mgonjwa ndani halafu akawa anatoka nje kuonana na wakuu wa vyombo vya usalama na mawaziri wake huku akijua ndani kwake kuna mgonjwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mhe. Rais Magufuli anatarajiwa kutuma salaam kwa Taifa leo Mei 17, 2020.

Hotuba yake inaaminika itajaa mambo mazito.

Kaa standby kwenye media zote na mitandao ya kijamii muda si mrefu ujao.

Inatarajiwa kuanzia mida ya saa sita na nusu mchana (12:30PM) ndipo atakuwa mubashara.

======




View attachment 1452519

‪RAIS AMETOA SALAAM BAADA YA KUSHIRIKI KATIKA IBADA YA KANISA LA KKKT USHARIKA WA CHATO‬

Raisi Magufuli akiwa katika kanisa la KKKT Chato amepata nafasi ya kuzungumza mbapo ameongea mambo mbalimbali,

Katika hotuba hiyo Raisi ameanza kwa kumshukuru Mungu na viongozi wa dini wote nchini. Raisi magufuli amesema “Waimbaji wameimba hapa kwamba bila mungu huwezi kuongoza, bila kumtanguliza mungu huwezi ukafanya chochote. Kwahiyo napenda niwashukuru Watanzania wote, Viongozi wa dini mbalimbali ambao wameshiriki kuliombea taifa hili"

"Na ndio maana siku za nyuma wakati ugonjwa huu umeingia niliwaomba ndugu zangu watanzania angalau tutumie siku tatu za kuomba kwelikweli. Ninawashukuru sana kwa sababu wote tuliomba tulifunga na Mungu amejibu na Mungu ametusikia”

“Ndugu zangu mifano mingi imetolewa, hata katika mahubili yako leo Baba Mchungaji katika injili na katika matendo ya mitume umeeleza ni namna gani watu walivyoweza kumtegemea Mungu walivyoweza kufanikiwa”

“Yule kipofu alimlilia yesu, Mwana wa Daudi nirehemu, Yesu ambaye ni mtoto wa Mungu ambaye naye pia ni Mungu alimponya. Wakati wa dhoruba kula baharini wanafunzi walivyokuwa wamelala wakaona mtumbwi unataka kuzama walipiga kelele” Katika maandiko pia sehemu zingine Yesu aliwakemea kwanza mitume kwa kuwa na Imani ndogo na baadaye akaikemea pepo na mambo yakawa shwari kwahiyo sisi katika kipindi chochote kigumu cha aina yoyote tukimtanguliza Mungu tutafanikiwa”

“Kwahiyo ninawashukuru sana ndugu zangu, ninawashukuru sana Wachungaji, Masheikh, Mapadri, Maaskofu kila mmoja katika eneo lake ambao tulimtanguliza Mungu na Mungu ametusaidia sana”.

“Ndugu zangu katika mapambano ya aina yoyote ni vita. Ugonjwa huu wa Corona hauna tofauti na vita nyingine. Nilikwisha eleza na wataalamu pia wameahaeleza ni namna gani nzuri ya kuweza kupambana na ugonjwa huu hata Baba Mchungaji umezieleza mbinu zote”.

“Ni kweli sikutoa amri ya lockdown ya kuwafungia watu majumbani, ulikuwa ni utumwa wa ajabu. Imagine wewe Lyabange ufungiwe saa nyingine hata usionane na Mme wako Iseme au na watoto wako. Sisi hapa huwa tunaondoka asubuhi kwenda kuchukua chakula, ukachume viazi, maharage yako, uende ziwani ukavue hivyo vyote vingekuwa vimezuiliwa tungekuwa tuko wapi sisi Watanzania miliono 60?"

Huruhusiwi kwenda sokoni, na saa nyingine unaruhusiwa kutoka kidogo tu, halafu usiku usitoke kana kwamba Corona inatembea usiku tu. Hebu tujiulize sisi Watanzania tuna miradi mingi tumeweka katika nchi yetu, Hiyo miradi yote ingekuwa imesimama.

"Tunajenga reli kwa mabilioni ya fedha, Makandarasi kutoka Nje wale wote tungewazuia vijana wasipate kazi tungekuwa wapi?"

"Tunajenga Mradi wa umeme, thamani yake ni Zaidi ya Trilioni saba zimechukuliwa na Watanzania kwenda kuinvest pale kusudi tuwe na umeme, leo wale wote tungekuwa tumewasimamisha, vijana wale wote tungekuwa tumewasimamisha; tunajenga barabara zote zingekuwa zimesimama."

"Hapo tunajenga meli kwenye ziwa Viktoria na juzi mmeona Injini zimekuja kutoka Korea, zote zile zingekuwa tumesimamisha na injini zisingekuja."

“Kila mmoja afikirie katika maeneo yake tungekuwa wapi? Ndio maana nilimuomba sana Mungu na nawashukuru sana viongozi wa dini zote nikasema hapana, hakuna kujifungia ndani kwa sababu huu utakuwa ugonjwa mkubwa Zaidi kuliko Corona”

Lakini watu ukishawafungia ndani utawalisha chakula? Watafanyaje? Sitaki kueleza matatizo wanayoyapata katika maeneo mengine nyinyi wenyewe mnajua lakini sisi tumeamua kwenda hivi.

Tuliamua tumtangulize Mungu, tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu. Na katika hali halisi Mungu amesikia sala zenu kwa taarifa za leo nilizoletewa na naomba niwaeleze kidogo nilizoandika hapa.

Wagonjwa wamepungua san ahata katika hospitali zetu; Mfano Hospitali ya Amana ya Dar es Salaam ilikuwa inalaza watu 198, leo walikuwepo watu 12 tu.

- Hospitali ya Mloganzila ilikuwa inalaza watu 30 leo wamebaki 6

- Pale kibaha palikuwa pana kituo kinaitwa Rulanzi huwa wanalazwa pale Zaidi ya watu 50 leo walikuwa wamebaki 22 na hawa 22 sio kwamba wamezidiwa wako kama sisi ila tu ado wanaonesha positive.

- Kwenye hospitali ya Agha Khani nako wamepungua wamebaki watu 31,
- Hindu Mandal wamebaki 16,
- Ragent Hospital wamebaki 17,
- TMJ wamebaki 7,
- Labinisia kule Tegeta wamebaki watu 14

"kwahiyo, unaweza kuona trend ya majibu ya Bwana Mungu wetu yalivyofanya kazi".

"Lakini pia hata katika mikoa, Arusha wana vituo vitatu.
- Mshono kina wagonjwa 11,
- Longido jina la kituo linaitwa Nyorendeke hakuna mgonjwa hata mmoja.
- Karatu kuna kituo kinaitwa Dofu hakina mgonjwa.

"Mwanza hapa wana vituo jumla kumi, vinane ni kutoka Halmashauri zifuatazo;

- Busweru wana wagonjwa wawili
- Misungwi wana wagonjw wawili wote wana hali nzuri
- Ukerewe kuna kituo kinaitwa Nyakatunguru hakuna hata mgonjwa mmoja
- Nagu kuna kituo kinaitwa John Mongela hakuna mgonjwa
- Jiji la Mwanza kituo cha Mkuyuni hakuna mgonjwa
- Buchosa kituo cha Nyamunge hakuna mgonjwa
- Sengerema hakuna mgonjwa
- Kwimba hakuna Mgonjwa
- Hospitali mbili za Bugando na seketule Wagonjwa ni wawili hao wana uhitaji wa kuangaliwa kwa sababu pia wana magonjwa mengine.

Lakini Dodoma kuna vituo vinne mjini viko viwili vina wagonjwa wawili kwa vyote wanahitaji uangalizi na karibu na pia wanamagonjwa mengine, wawili walikuwa wagonjwa Zaidi ya arobaini na kitu wengine wote wamerudi nyumbani.

- Kongwa hakuna mgonjwa
- Kondoa tuna kituo kinaitwa Baleko hakuna mgonjwa. Na kadhalika na kadhalika


.

Haombewi yeyote hapa.Kila mtu apambane na kushinda mechi yake. Na maabara ipi mtoto wako ulimpima kama ya taifa uliipiga kwara? Atakayekuamini ni kwa hasara zake mwenyewe.
 


Magufuli amesema ni ujinga wa kupitiliza kwa nchi ambazo zimeizunguka Tanzania kujaribu kufunga mipaka yao na Tanzania kwasababu nchi hizo zinaitegemea sana Tanzania.

Ametolea mfano kwa nchi moja(Kenya) ambayo inaitegemea Tanzania kwa mahindi, mchele na hata mifugo(nyama), kutangaza kufunga mipaka wakati ikijua kwamba hawana chakula cha kutosha.

Magufuli anategemea kufungua shule na vyuo vya elimu na kuruhusu ndege kuanzia safari zake za kawaida ndani ya wiki mbili zijazo kutokana na hali ya ugonjwa wa Corona kutengemaa nchini.
 
Rais ni muongo, hakuna aliyesema awafungie wakulima, kwanza lockdown ya Dar ndiyo ingewaepusha wakulima na maambukizi. Halafu watu hata hawaelewi. Dah!
 
Back
Top Bottom