Rais Magufuli: Huduma za NIDA ziwe kila Wilaya au NIDA watoe hela ya 'guest' kwa Wananchi. Ukiona bei ya mahindi iko juu, kalime yako

Rais Magufuli: Huduma za NIDA ziwe kila Wilaya au NIDA watoe hela ya 'guest' kwa Wananchi. Ukiona bei ya mahindi iko juu, kalime yako

Sasa mkurugenzi akienda Morogoro ndio itakuwa nini? Matatizo ya NIDA yanajulikana, rasilimali walizonazo haziendani na mahitaji halisi,kimsingi wamezidiwa.

Wanahitaji, fedha, ofisi,rasilimali watu na vifaa vya kutosha sio mkurugenzi wao kwenda Morogoro! Wanasiasa waache kutafuta cheap popularity. Tufanye kazi,sifa zitakuja tu kama kweli ni za muhimu.

Naona hapo juu kuna watu wanasifia hiyo amri ya kwenda Morogoro,wananchi tujitahidi kupunguza ujinga, upumbavu na ushamba. Tujifunze kuwa critical thinkers, tuache ushabiki wa kitoto na ulimbukeni.
 
1574244554007.png

Kiongozi!!! habari iongezee nyama, Mh Rais John Pombe Magufuli yupo Ikulu?

 
Nimesikia Muheshimiwa anasema hawezi kupanga bei ya mahindi, yakipanda yapande huu ni mwaka wa wakulima na wafanyabiashara.

Okay thats well and good free market in the workings, swali linakuja ni wapi soko huria linaishia, mbona kwenye korosho hatukufuata market inavyosema?

Sioni ubaya wa kuchagua njia hii au ile, ila we need consistency.
 
Ndio ubaya wa maamuzi ya mtu mmoja, anachosema yeye ndio hicho kifuatwe.
 
Eti mkirugenzi akae Guest. Huyu akija tu. Kila siku posho yake na malazi sio chini ya laki 6.
 
Rais kavaa kijeshi naona nchi inaenda kijeshi jeshi safi sana
 

Rais Magufuli amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Arnold M. Kihaule kufika Mkoani Morogoro leo na ikiwezekana akae Mkoani humo hata siku tatu ili kushughulikia tatizo la Watu wengi kukosa Vitambulisho vya Taifa huku Mkoa mzima ukiwa na ofisi moja pekee ya NIDA.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo pamoja na kuzungumzia masuala mengine mbalimbali wakati akiongea na wananchi wa Msamvu, Morogoro akiwa njiani akielekea mkoani Dodoma.

Kuhusu usajili wa NIDA, Rais amesema:

"Mkurugenzi ondoka sasa hivi Dar es Salaam uje hapa Morogoro kushughulikia hili tatizo la NIDA, Nimemtaka Mkurugenzi Mkuu NIDA aje ashughulikie changamoto ya vitambulisho na nataka huduma hii iende kila Wilaya, haiwezekani watu wasafiri kutoka Wilayani kuja Mjini au muwape nauli na hela ya ‘Guest’,na hili litazamwe nchi nzima watu wapewe vitambulisho”

''Leo uje hapa ukae na mkuu wa mkoa na wilaya muangalie namna ya kuseti namna ya kutoa huduma hizi kwa wananchi hawa. Na hili liwe pia kwa Tanzania nzima. Inawezekana matatizo haya hayapo hapa Morogoro tu''

''Hatuwezi kucheleweshwa na watu fulani fulani kwa kushindwa kufanya majukumu yao na kuharibu majukumu ya wananchi kushindwa kufanya kazi zao huko''

“Watu wanataka kusajili laini zao za simu na mambo mengine lakini zoezi la vitambulisho linacheleweshwa na watu wachache; suala la NIDA linaenda polepole sana. Mkurugenzi Mkuu wa NIDA nitahitaji unipe na tathmini ya zoezi lote Nchi nzima"

Kuhusu wakulima na wafanyabiashara, Rais amesema:

“Wanaofanya biashara ndogondogo nilishasema wasionewe ndiyo maana nilitoa vitambulisho. Nilisema mfanye biashara mahali popote lakini sikusema wapiga debe na wazuluraji waendelee kuzulura tu, kuna sheria na mimi nimeapa kulinda sheria"

“Nataka wakulima washangilie kama bei ya mahindi imepanda, biashara hii lazima iwe huru, bei ya mahindi itajipanga yenyewe, wakati wa kuwapangia bei wakulima kwenye mazao yao umekwisha”

‘’Morogoro Ilikuwa ni mmoja kati ya mikoa muhumu sana katika uzalishaji. Viongozi wa Morogoro mukawahamasishe watu kufanya kazi ili mkoa uendelee na sifa yake ya siku zote’’

"Ukiona wengine wachache wanalalamika bei ya mahindi iko juu, najua wakulima wanashangilia, na nataka wakulima washangilie zaidi,tulizungumze hili wazi kwa watanzania wote,ukiona mahindi yako juu nenda kalime yako ya bei ya chini biashara hii lazima iwe huru"

“Wana Morogoro JPMMorogoro “Wana Morogoro nataka mtunze amani, navipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuendelea kulinda amani yetu, kila mtu atimize wajibu wake katika eneo lake la kazi”

Kuhusu kamatakamata ya wazururaji, Rais amesema:

''Wapo wanaokamatwa kwa kosa la uzururaji na wanapopelekwa mahakamani wanashindwa. Kwanini wasishinde kule mahakamani kwamba siyo wazururaji? Wapo waliojitetea mahakamani wakashinda, sasa hao waliofungwa kwa uzururaji munataka niwarudishe?''

''Wale wanaofanya biashara ndogondogo wala wasionewe ndiyo maana nikatoa vitambulisho. Sikusema wapiga debe, wazururaji waendelee kuzurura tu – kuna sheria na mimi nimeapa kulinda sheria.''

''Niviombe vyombo vya usalama vinavyo-deal na wazururaji, wasiwaonee watu kwa kuwashitaki kama wazururaji wakati wana kazi zao. Haya ya uonevu yasiwepo.''

‘’Wale ambao siyo wazururaji musiwaonee, muwaache wafanye kazi zao.''

AKIWA WILAYANI GAIRO

Akiwa Gairo, Rais Magufuli amechangia shilingi milioni 5 kwa ajili ya kujenga maabara ya Shlue ya Sekondari Sekwawa baada ya kaka Mkuu wa shule hiyo Athumani Saidi Omari kufikisha ombi la kuongeza ukubwa wa maabara hiyo ambayo amesema haitoshi.

‘’Changamoto kubwa inayaotu-cost wanafunzi wako ni maabara haitoshi’’, alisema Kaka Mkuu huyo

Rais Magufuli: ‘’Nitachangia milioni tano kama mchango wa kujenga maabara; nakabidhi milioni tano kwa ajili ya ujenzi, ikiliwa na nyie mujiandae kuliwa’’

Mkuu wa Wilaya Gairo: ‘’Hakuna mahakama ya wilaya, wanaenda Kilosa, zaidi ya kilomita 100. Hakuna ofisi ya Mkuu wa Wilaya, nimejishikiza katika ofisi za Mji Mdogo. DAS ana-share ofisi na Afisa Tarafa.''
We are really in big trouble.

Tatizo la NIDA si Morogoro peke yake, ni nchi nzima. Huyo Mkurugenzi maskini sijui atajigawa vipi. Kila wilaya ina ofisi siku hizi. Kwa nini isitumike hiyo? Hilo la kwanza, la pili, hizo ofisi za NIDA zinapewa fedha za kutosha kufanya kazi hiyo? Jibu ni dhahiri, bajeti yao ni ndogo sana.

Kuhusu biashara ya mazao, naona kuna mkanaganyiko mkubwa zaidi. Ni soko huria au serikali itaendelea kupanga bei kama kwenye korosho na pamba? Itaacha kuwazuia wakulima kuuza nje ya nchi ili wapate bei nzuri?
 

Rais Magufuli amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dkt. Arnold M. Kihaule kufika Mkoani Morogoro leo na ikiwezekana akae Mkoani humo hata siku tatu ili kushughulikia tatizo la Watu wengi kukosa Vitambulisho vya Taifa huku Mkoa mzima ukiwa na ofisi moja pekee ya NIDA.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo pamoja na kuzungumzia masuala mengine mbalimbali wakati akiongea na wananchi wa Msamvu, Morogoro akiwa njiani akielekea mkoani Dodoma.

Kuhusu usajili wa NIDA, Rais amesema:

"Mkurugenzi ondoka sasa hivi Dar es Salaam uje hapa Morogoro kushughulikia hili tatizo la NIDA, Nimemtaka Mkurugenzi Mkuu NIDA aje ashughulikie changamoto ya vitambulisho na nataka huduma hii iende kila Wilaya, haiwezekani watu wasafiri kutoka Wilayani kuja Mjini au muwape nauli na hela ya ‘Guest’,na hili litazamwe nchi nzima watu wapewe vitambulisho”

''Leo uje hapa ukae na mkuu wa mkoa na wilaya muangalie namna ya kuseti namna ya kutoa huduma hizi kwa wananchi hawa. Na hili liwe pia kwa Tanzania nzima. Inawezekana matatizo haya hayapo hapa Morogoro tu''

''Hatuwezi kucheleweshwa na watu fulani fulani kwa kushindwa kufanya majukumu yao na kuharibu majukumu ya wananchi kushindwa kufanya kazi zao huko''

“Watu wanataka kusajili laini zao za simu na mambo mengine lakini zoezi la vitambulisho linacheleweshwa na watu wachache; suala la NIDA linaenda polepole sana. Mkurugenzi Mkuu wa NIDA nitahitaji unipe na tathmini ya zoezi lote Nchi nzima"

Kuhusu wakulima na wafanyabiashara, Rais amesema:

“Wanaofanya biashara ndogondogo nilishasema wasionewe ndiyo maana nilitoa vitambulisho. Nilisema mfanye biashara mahali popote lakini sikusema wapiga debe na wazuluraji waendelee kuzulura tu, kuna sheria na mimi nimeapa kulinda sheria"

“Nataka wakulima washangilie kama bei ya mahindi imepanda, biashara hii lazima iwe huru, bei ya mahindi itajipanga yenyewe, wakati wa kuwapangia bei wakulima kwenye mazao yao umekwisha”

‘’Morogoro Ilikuwa ni mmoja kati ya mikoa muhumu sana katika uzalishaji. Viongozi wa Morogoro mukawahamasishe watu kufanya kazi ili mkoa uendelee na sifa yake ya siku zote’’

"Ukiona wengine wachache wanalalamika bei ya mahindi iko juu, najua wakulima wanashangilia, na nataka wakulima washangilie zaidi,tulizungumze hili wazi kwa watanzania wote,ukiona mahindi yako juu nenda kalime yako ya bei ya chini biashara hii lazima iwe huru"

“Wana Morogoro JPMMorogoro “Wana Morogoro nataka mtunze amani, navipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuendelea kulinda amani yetu, kila mtu atimize wajibu wake katika eneo lake la kazi”

Kuhusu kamatakamata ya wazururaji, Rais amesema:

''Wapo wanaokamatwa kwa kosa la uzururaji na wanapopelekwa mahakamani wanashindwa. Kwanini wasishinde kule mahakamani kwamba siyo wazururaji? Wapo waliojitetea mahakamani wakashinda, sasa hao waliofungwa kwa uzururaji munataka niwarudishe?''

''Wale wanaofanya biashara ndogondogo wala wasionewe ndiyo maana nikatoa vitambulisho. Sikusema wapiga debe, wazururaji waendelee kuzurura tu – kuna sheria na mimi nimeapa kulinda sheria.''

''Niviombe vyombo vya usalama vinavyo-deal na wazururaji, wasiwaonee watu kwa kuwashitaki kama wazururaji wakati wana kazi zao. Haya ya uonevu yasiwepo.''

‘’Wale ambao siyo wazururaji musiwaonee, muwaache wafanye kazi zao.''

AKIWA WILAYANI GAIRO

Akiwa Gairo, Rais Magufuli amechangia shilingi milioni 5 kwa ajili ya kujenga maabara ya Shlue ya Sekondari Sekwawa baada ya kaka Mkuu wa shule hiyo Athumani Saidi Omari kufikisha ombi la kuongeza ukubwa wa maabara hiyo ambayo amesema haitoshi.

‘’Changamoto kubwa inayaotu-cost wanafunzi wako ni maabara haitoshi’’, alisema Kaka Mkuu huyo

Rais Magufuli: ‘’Nitachangia milioni tano kama mchango wa kujenga maabara; nakabidhi milioni tano kwa ajili ya ujenzi, ikiliwa na nyie mujiandae kuliwa’’

Mkuu wa Wilaya Gairo: ‘’Hakuna mahakama ya wilaya, wanaenda Kilosa, zaidi ya kilomita 100. Hakuna ofisi ya Mkuu wa Wilaya, nimejishikiza katika ofisi za Mji Mdogo. DAS ana-share ofisi na Afisa Tarafa.''
Mheshimiwa Rais napenda kukutaarifu kuwa wanaolalamika ni hao hao wakulima!! Mahindi toka kwa wakulima yalinunuliwa na wafanyabiashara na nafco.Rais wenye kipato cha chini wanaumia sana na bei!
Nchi yangu Tanzania Rais,waziri mkuu,waziri wa kilimo,naibuwaziri.............................
 
Rais Magufuli amesema serikali haiwezi kuwapangia wakulima wa mahindi bei ya kuuza mazao yao kwa sababu haikuwasaidia wakati wanalima.

Rais Magufuli amesisitiza kuwa wakati wa serikali kuwapangia wakulima bei za mazao yao umepita na hizi ni zama za soko kuamua.

Source Eatv habari!
 
Back
Top Bottom