kiraremapojoni
JF-Expert Member
- Nov 30, 2018
- 391
- 512
sidhani kama linahitaji tochi jambo hilo kwa Bwana Muheshimiwa January?January ni mchapakazi?!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
sidhani kama linahitaji tochi jambo hilo kwa Bwana Muheshimiwa January?January ni mchapakazi?!
Wakati wapinzani wanateswa, kuuawa, kupigwa risasi huyo makamba alikuwa wapiMsema ukweli.sio kweli kwamba anamtetea makamba ,ila anaongea uhalisia namna vitu makamba kafanya
Huyo makamba anayemtetea hatujawahi kumsikia hata siku moja angalao kulaani tu kitendo cha Lissu kupigwa risasi sasa ndiyo amekuwa wa maanaNi haki yake ya kikatiba kutoa maoni na anaelezakwa uchungu wake toka moyoni anavyoumizwa na hali halisi ya nchi kwa wakati huu na ndo wabunge wachache wa upinzani wanaokemea kila jambo baya ndani ya bunge kwa wakati huu
Sawa na hii pia useme hujaionaSijamsikia popote Rais Magufuli akitaja sababu za kumtumbua January......ni kama vile unamlisha maneno!
Huyo ni CCM-tetea tetea asikupe shida, hata kama amesikia atajifanya kutafuta tafsiri yake. Tunawajua wapuuzi wa aina yake. Hata mume wao aliposema fyatueni watoto walikuja na utetezi wa kitoto eti ni utani, lakini baada ya siku chache alipofuta matangazo ya mpango wa uzazi wakaabika.Ulikuwa husikilizi au hukuelewa
Kasema kulikua na miradi hewa ya kupanda mikoko, matumizi mabaya ta fedha za wafadhili, na marufuku ya mifuko ya plastiki aliichelewesha kwa miaka 4 na hata lilipotekelezwa juzi ni yeye alimlazimisha
Sijui kama ni kweli au ni kumpaka matope jamaa, Makamba nae katia ngumu, kagima kwenda Ikulu leo kama watumbuliwa wengine wanavyohudhuria
Mchukueni awasaidie kwenye chama chenu,usimpangie rais cha kufanya ,yapo maovu mengi nyuma ya pazia aliofanya January ,na sasa kalipwa,Rais Magufuli kwenye sababu za kumuondoa January Makamba bora jikalie zako kimya.
Nimekusikia Rais leo ukijaribu kuelezea sababu za kumuondoa Uwaziri Bwana January Makamba. Kwa kweli hukuwa umejiandaa na maelezo ya kuridhisha.
Rais, kwenye suala la mifuko ya plastiki tunajua ukweli kwamba wewe ndiye ulizuia lisiendelee ulipoambiwa kwamba litaua viwanda. Tunajua kwamba January ndiye ametumia miaka mitatu kuwaandaa wenye viwanda vya mifuko ili wabadilishe teknolojia na wasipate hasara. Tunajua kwamba January alifanya vikao vya umma (public hearings) kuanzia Karimjee mwaka 2017 hadi Mwanza mwaka 2018 na kwingineko kushirikisha wananchi kwenye jambo hili. Tunajua kwamba hatukusikia kauli yako kwenye mifuko ya plastiki hadi baada ya suala hili kufanikiwa. Hii sio kawaida yako maana wewe ni very predictable.
Tunajua kwamba mlimtegea Makamba ili afeli halafu mumtimue. Hakufeli. Sasa mnamtimua kwa kukamilisha kazi kwa weledi mkubwa! Mhe Rais wewe ni mkali maelekezo yako yasipotekelezwa. Umemuachaje Waziri miaka minne kwa kutotii maelekezo halafu unamtoa baada ya utekelezaji? Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kukubali hoja yako hii dhaifu sana.
Bwana Rais ulikutana na wafanyabiashara kote nchini kutwa nzima. Walitaja kero zao zote, nami nikaziorodhesha. Sikusikia hata mmoja akilalamikia NEMC. Kwasababu gani? Kwasababu January ameibadilisha NEMC. Alitaka kuibadilisha huko nyuma na akavunja bodi na kuondoa menejimenti lakini kwakuwa inasemekana kulikuwa na ndugu zako walioguswa ukaagiza uamuzi ule ubatilishwe. Unadhani Watanzania wamesahau?
Bwana Rais fedha zinazotolewa na wahisani kwenye miradi ya mazingira zinakaguliwa na CAG na hakuna popote palipoonyesha ubadhirifu au upotevu. Kama upo uweke hadharani kama sisi tulivyoweka hadharani ubadhirifu wa TZS 1.5 Trilioni. Wacha wahisani, Serikali yako haijaweka hata senti tano kwenye miradi ya mazingira nchini. Mimi ni Mbunge na ninapitia kila Bajeti ya Serikali na Taarifa za CAG. Hujawahi kutenga fedha za Mazingira. Kwa kifupi, tunajua wewe binafsi sio mpenzi wa mazingira na umesema hivyo mara kadhaa. Hata huyo January mwenyewe “ulimtupa” kwenye mazingira ili apotee lakini ghafla kila Mtanzania leo anaongea mazingira. Hata wewe nawe leo unayaongea.
Bwana Rais hulazimiki kutoa sababu unapomuondoa Waziri. Kwa kutafuta kutoa sababu zisizoshiba leo, umeonyesha kwamba umesikia hisia za Watanzania kuhusu kuondolewa January Makamba. Umeondoa Waziri kipenzi cha Watanzania na Waziri weledi. Tunajua umemfukuza kwasababu nyingine, sio uchapakazi. Watanzania wote tunajua kwamba siku zote alikuwa anatafutiwa sababu tu ya kuondolewa. Ukisema uchapakazi ndio sababu Watanzania tunakushangaa kwasababu hawa mawaziri umewateua wewe lakini tathmini tunafanya sisi Watanzania. Na January Makamba ndiye alikuwa Waziri mbunifu na bora kabisa. Na ataendelea kuwa maarufu miongoni mwa Watanzania. Hakika ana nafasi kwenye uongozi siku sio nyingi sana zijazo. Mabadiliko ni lazima na January naamini atakuwa sehemu ya mabadiliko ili kujenga Tanzania inayojali watu wake na yenye Demokrasia iliyokomaa
Zitto ZR Kabwe
Mbunge Kigoma Mjini
Hapana mkuu, kwenye issue ya Zitto kumchalenji JPM katika asemayo kuhusu January ni kweli kabisa.Naona sasa umegeuka na kuwa mtetezi wa CCM, tumeshakudharau
Mkuu tuseme ukweli tu, umewahi kumsikia hata siku moja makamba analaani kupigwa risasi Lissu, kuteswa wapinzani, kutekwa wapinzani, kuuawa wapinzani n.k. eti leo kichwa cha panzi kasahau kila kitu anawatetea maccm😂 😂 😂 sawa boss
Wapi kasema anamtumbua kwa sababu hiyo?!Sawa na hii pia useme hujaiona View attachment 1159370
wazungu wanasema No research No Right to speak tusiwe tunapenda kuzungumza ili kupata public sympath na kumbuka m atukio ni mengi na kama majeraha yako kwa watu wengi tu na wala sio Lissu peke yako kama unavyosema, na hata kama Januar ana changamoto zake lakini ni mchapakazi asiye na makekena anapopanga jambo basi utekelezaji wake unakuwa ni rahisi na matokeo hasi yanaonekana( Angalio katazo la mifuko ya Plastic). Unadhani kama sio busara na akili yake huo mshike mshike wake barabarani na sokoni ingekuwaje. Mnyonge mnyngeni ila haki yake mpeniHuyo makamba anayemtetea hatujawahi kumsikia hata siku moja angalao kulaani tu kitendo cha Lissu kupigwa risasi sasa ndiyo amekuwa wa maana
Watu walitegemea JPM leo angeongea mengi sana,bahati nzuri naona washauuri wake walikuwa smart sana ktk hili tangu aingie madarakani,Ameongea short and clear hajaongea wengi walivyotarajia maana hata radio za mbao zilijiunga ikulu leo.Rais Magufuli kwenye sababu za kumuondoa January Makamba bora jikalie zako kimya.
Nimekusikia Rais leo ukijaribu kuelezea sababu za kumuondoa Uwaziri Bwana January Makamba. Kwa kweli hukuwa umejiandaa na maelezo ya kuridhisha.
Rais, kwenye suala la mifuko ya plastiki tunajua ukweli kwamba wewe ndiye ulizuia lisiendelee ulipoambiwa kwamba litaua viwanda. Tunajua kwamba January ndiye ametumia miaka mitatu kuwaandaa wenye viwanda vya mifuko ili wabadilishe teknolojia na wasipate hasara. Tunajua kwamba January alifanya vikao vya umma (public hearings) kuanzia Karimjee mwaka 2017 hadi Mwanza mwaka 2018 na kwingineko kushirikisha wananchi kwenye jambo hili. Tunajua kwamba hatukusikia kauli yako kwenye mifuko ya plastiki hadi baada ya suala hili kufanikiwa. Hii sio kawaida yako maana wewe ni very predictable.
Tunajua kwamba mlimtegea Makamba ili afeli halafu mumtimue. Hakufeli. Sasa mnamtimua kwa kukamilisha kazi kwa weledi mkubwa! Mhe Rais wewe ni mkali maelekezo yako yasipotekelezwa. Umemuachaje Waziri miaka minne kwa kutotii maelekezo halafu unamtoa baada ya utekelezaji? Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kukubali hoja yako hii dhaifu sana.
Bwana Rais ulikutana na wafanyabiashara kote nchini kutwa nzima. Walitaja kero zao zote, nami nikaziorodhesha. Sikusikia hata mmoja akilalamikia NEMC. Kwasababu gani? Kwasababu January ameibadilisha NEMC. Alitaka kuibadilisha huko nyuma na akavunja bodi na kuondoa menejimenti lakini kwakuwa inasemekana kulikuwa na ndugu zako walioguswa ukaagiza uamuzi ule ubatilishwe. Unadhani Watanzania wamesahau?
Bwana Rais fedha zinazotolewa na wahisani kwenye miradi ya mazingira zinakaguliwa na CAG na hakuna popote palipoonyesha ubadhirifu au upotevu. Kama upo uweke hadharani kama sisi tulivyoweka hadharani ubadhirifu wa TZS 1.5 Trilioni. Wacha wahisani, Serikali yako haijaweka hata senti tano kwenye miradi ya mazingira nchini. Mimi ni Mbunge na ninapitia kila Bajeti ya Serikali na Taarifa za CAG. Hujawahi kutenga fedha za Mazingira. Kwa kifupi, tunajua wewe binafsi sio mpenzi wa mazingira na umesema hivyo mara kadhaa. Hata huyo January mwenyewe “ulimtupa” kwenye mazingira ili apotee lakini ghafla kila Mtanzania leo anaongea mazingira. Hata wewe nawe leo unayaongea.
Bwana Rais hulazimiki kutoa sababu unapomuondoa Waziri. Kwa kutafuta kutoa sababu zisizoshiba leo, umeonyesha kwamba umesikia hisia za Watanzania kuhusu kuondolewa January Makamba. Umeondoa Waziri kipenzi cha Watanzania na Waziri weledi. Tunajua umemfukuza kwasababu nyingine, sio uchapakazi. Watanzania wote tunajua kwamba siku zote alikuwa anatafutiwa sababu tu ya kuondolewa. Ukisema uchapakazi ndio sababu Watanzania tunakushangaa kwasababu hawa mawaziri umewateua wewe lakini tathmini tunafanya sisi Watanzania. Na January Makamba ndiye alikuwa Waziri mbunifu na bora kabisa. Na ataendelea kuwa maarufu miongoni mwa Watanzania. Hakika ana nafasi kwenye uongozi siku sio nyingi sana zijazo. Mabadiliko ni lazima na January naamini atakuwa sehemu ya mabadiliko ili kujenga Tanzania inayojali watu wake na yenye Demokrasia iliyokomaa
Zitto ZR Kabwe
Mbunge Kigoma Mjini
Usitujumlishe na wengine...Naona sasa umegeuka na kuwa mtetezi wa CCM, tumeshakudharau