Rais Magufuli huhitaji kujieleza unapomtoa Waziri. Kwa January Makamba jikalie kimya

Rais Magufuli huhitaji kujieleza unapomtoa Waziri. Kwa January Makamba jikalie kimya

Ila sio fair kabisa ,jamaa ana character zote za mwalimu wa vidudu
 
Huyo makamba anayemtetea hatujawahi kumsikia hata siku moja angalao kulaani tu kitendo cha Lissu kupigwa risasi sasa ndiyo amekuwa wa maana

Kwenye hili la Makamba kutolewa ni kwa ajili ya ule waraka, hizo nyingine ni sababu za kulazimisha. Ila mtu kama Makamba sio wa kutetea kwani ni mtu anayekalia kimya uovu ili kulinda madaraka yake. Kilichomkuta Makamba ni vita dhidi ya shetani aliye madarakani dhidi ya genge la maibilisi walio nje ya madaraka. Hapo Zitto anamtetea tu mshikaji wake lakini Makamba ni useless kwa upinzani.
 
Truth be said January was a megalomaniac who took environment issues so serious that he became an obstacle in some areas of development.

Inawezekana talents zake zingefaa wizara nyingine lakini hapo kwenye mazingira alihitajika mtu ambae yupo flexible na mwenye mtazamo mpana wa kitaifa zaidi ya kila kitu kujifanya anataka kuona environmental analysis kwanza.

Hata hizo credit mnazompa za process alizozifuata baada ya ku postpone ban ya kwanza kaziokota humu humu JF.
 
Tunachozungumza hapa Zitto kama mpinzani aliwahi kumuona makamba anapinga kutekwa wananchi, kulaani kitendo cha kupigwa risasi Lissu, kulaani mateso kwa wapinzani, n.k. mbona yeye anajifanya kimbelembele kuwatetea maccm

Nimekuelewa mkuu
 
Rais Magufuli kwenye sababu za kumuondoa January Makamba bora jikalie zako kimya.

Nimekusikia Rais leo ukijaribu kuelezea sababu za kumuondoa Uwaziri Bwana January Makamba. Kwa kweli hukuwa umejiandaa na maelezo ya kuridhisha.

Rais, kwenye suala la mifuko ya plastiki tunajua ukweli kwamba wewe ndiye ulizuia lisiendelee ulipoambiwa kwamba litaua viwanda. Tunajua kwamba January ndiye ametumia miaka mitatu kuwaandaa wenye viwanda vya mifuko ili wabadilishe teknolojia na wasipate hasara. Tunajua kwamba January alifanya vikao vya umma (public hearings) kuanzia Karimjee mwaka 2017 hadi Mwanza mwaka 2018 na kwingineko kushirikisha wananchi kwenye jambo hili. Tunajua kwamba hatukusikia kauli yako kwenye mifuko ya plastiki hadi baada ya suala hili kufanikiwa. Hii sio kawaida yako maana wewe ni very predictable.

Tunajua kwamba mlimtegea Makamba ili afeli halafu mumtimue. Hakufeli. Sasa mnamtimua kwa kukamilisha kazi kwa weledi mkubwa! Mhe Rais wewe ni mkali maelekezo yako yasipotekelezwa. Umemuachaje Waziri miaka minne kwa kutotii maelekezo halafu unamtoa baada ya utekelezaji? Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kukubali hoja yako hii dhaifu sana.

Bwana Rais ulikutana na wafanyabiashara kote nchini kutwa nzima. Walitaja kero zao zote, nami nikaziorodhesha. Sikusikia hata mmoja akilalamikia NEMC. Kwasababu gani? Kwasababu January ameibadilisha NEMC. Alitaka kuibadilisha huko nyuma na akavunja bodi na kuondoa menejimenti lakini kwakuwa inasemekana kulikuwa na ndugu zako walioguswa ukaagiza uamuzi ule ubatilishwe. Unadhani Watanzania wamesahau?

Bwana Rais fedha zinazotolewa na wahisani kwenye miradi ya mazingira zinakaguliwa na CAG na hakuna popote palipoonyesha ubadhirifu au upotevu. Kama upo uweke hadharani kama sisi tulivyoweka hadharani ubadhirifu wa TZS 1.5 Trilioni. Wacha wahisani, Serikali yako haijaweka hata senti tano kwenye miradi ya mazingira nchini. Mimi ni Mbunge na ninapitia kila Bajeti ya Serikali na Taarifa za CAG. Hujawahi kutenga fedha za Mazingira. Kwa kifupi, tunajua wewe binafsi sio mpenzi wa mazingira na umesema hivyo mara kadhaa. Hata huyo January mwenyewe “ulimtupa” kwenye mazingira ili apotee lakini ghafla kila Mtanzania leo anaongea mazingira. Hata wewe nawe leo unayaongea.

Bwana Rais hulazimiki kutoa sababu unapomuondoa Waziri. Kwa kutafuta kutoa sababu zisizoshiba leo, umeonyesha kwamba umesikia hisia za Watanzania kuhusu kuondolewa January Makamba. Umeondoa Waziri kipenzi cha Watanzania na Waziri weledi. Tunajua umemfukuza kwasababu nyingine, sio uchapakazi. Watanzania wote tunajua kwamba siku zote alikuwa anatafutiwa sababu tu ya kuondolewa. Ukisema uchapakazi ndio sababu Watanzania tunakushangaa kwasababu hawa mawaziri umewateua wewe lakini tathmini tunafanya sisi Watanzania. Na January Makamba ndiye alikuwa Waziri mbunifu na bora kabisa. Na ataendelea kuwa maarufu miongoni mwa Watanzania. Hakika ana nafasi kwenye uongozi siku sio nyingi sana zijazo. Mabadiliko ni lazima na January naamini atakuwa sehemu ya mabadiliko ili kujenga Tanzania inayojali watu wake na yenye Demokrasia iliyokomaa

Zitto ZR Kabwe
Mbunge Kigoma Mjini
mh Zitto, January kaondolewa ili kumkomoa baba yake, mzee Yusuph.
kweli jiwe hapendi mazingira, ndo maana kaamua kuharibu uoto wa asili selou game reservre kwa kilomita mia tatu za mraba na kufanya bwawa la maji,, lakini pia ETI MTU AJENGE KIWANDA NDIO AOMBE KIBALI, najua anachotaka yeye ni kuzindua hata kama hakitafanya kazi, mradi tu azindue, , ugonjwa wa "media-phobia" yeye tu ndio ae mubashara kenye TBC ambayo Ryoba ameiua kabisa.

Mtu amejenga kiwanda cha kuchenjua maiti eneo la kariakoo, sokoni, alafu baadae umwambie aombe kibali., inaingia akilini kweli, yaani haya kimeharibu afya, watu wamepata kansa, likiwanda lishazinguliwa the EIA wakasema kiondolewe, kwanza huyo afisa na timu yake na mkurugenzi wote wanatumbuliwa, sasa hivi kila mtu anafanya kazi kwa hofu kumfurahisha mfalme, nakwambieni tuendelee kumuomba Mungu amlete kiongozi wetu
 
Dah aisee sishangai haya maana sio mara ya kwanza Magufuli kusema uongo ....Alishasema alikuta sukari kilo ni 5000 wakati yeye ndiye aliyesababisha sukari kupanda bei.
ushawahi kumwamini Jiwe, u esahau ule ujinga wa dhahabu za mwanza na wale askari?
 
Hapana mkuu, kwenye issue ya Zitto kumchalenji JPM katika asemayo kuhusu January ni kweli kabisa.
Ni jambo baya sana mkuu wa nchi kusingizia mtu kwa vile anajuwa hawezi kubishana naye.
Kwenye mifuko ya plastiki Jpm anataka kujifanya alihusika wakati sio yeye maana imefanikiwa bila usumbufu kwa raia tofauti na operashini zake anazisema zina hitaji MTU kichaa kuzitekeleza.
Kwa hiyo wewe ndio mpanga mipango ya selikali?

Mbona mnatia aibu sana? Alafu kwanini Zitto kachukia sana kuondoka kwa Makamba?
 
Membe baki CCM.
January baki CCM.
Nape baki CCM.
Kinana baki CCM.
Makamba Sr baki CCM.

Mkiwa na vinyongo vyenu endeleeni kubaki huko huko mkichochea kuni mpaka 2020.

LISSU rudi haraka Tanzania wakati ni huu, Mbowe kaa chini na ACT mkubaliane pamoja na Seif na akina Jussa na wazanzibar wote, bara asimame LISSU na visiwani kama kawa Maalim na ACT.. CCM kwa hali waliyonayo kuni zikichochewa wanaanguka mapema sana 2020..
 
Uongo ni upi na ukweli ni upi?
Sii yawekwe wazi! Mbona tumaneno maneno kama kitchen party?
Kwani angemtengua na akanyamaza angeulizwa na nani?
Au angesema namtengua kwa sababu wa waraka wa baba yake kuuliza kuhusu mwanangu Musiba kuna mtu angelalama?
Kisichofaa ni UONGO UONGO maana ni kudhalilisha kiti
 
Kwa hiyo wewe ndio mpanga mipango ya selikali?

Mbona mnatia aibu sana? Alafu kwanini Zitto kachukia sana kuondoka kwa Makamba?
Lioneni hili nalo! Kanywe supu kwanza uondoe hangover ndio utaelewa.
 
Sijafurahishwa na ukosefu wa staha kwa Rais wa nchi yetu Tanzania. Nakushauri uwe na staha kwa Rais wetu hata kama amefanya yasiyopendeza utashi wako wewe binafsi. Nakuzungumzia wewe mleta mada.
===
Vitu vidogo vidogo hivi vinasababisha baadhi ya vinaja kukosa kuaminiwa kupewa madaraka makubwa. Tuulinde ujana wetu na kuaminiwa kwetu kwanza kwa kuwa na staha kwa wakubwa na mamlaka zilizopo.
Tatizo huyo mkubwa mwenyewe unayemtetea hana staha,anadanganyaje vijana mchana kweupe?aseme ukweli isitoshe hata angekaa kimya hakuna ambaye angemuuliza kuliko kuelezea sababu ambazo ni mwendawazimu pekee ndiye atakubaliana nazo.
 

Attachments

  • IMG-20190722-WA0031.jpg
    IMG-20190722-WA0031.jpg
    80.1 KB · Views: 19
Back
Top Bottom