Uchaguzi 2020 Rais Magufuli, ile Tanzania ya Viwanda uliyotuahidi ndiyo hii?

Kilichosemwa ni kwamba ifikapo mwaka 2025 Tanzania itakuwa nchi ya viwanda na uchumi wa kati. iweje uanze kuhoji hivi sasa: kwani tayari tuko kwenye mwaka 2025? Kuhusu uchumi wa kati, World Bank (siyo Magufuli) walitangaza tumefikia hatua hiyo miaka mitano kabla ya tarehe iliyopangwa. Kwa nini sasa kumsema Magufuli? Tuwe wakweli hata kama ni wapinzani.
 

Na wewe ulivyosema wananchi kama wataiondoa serikali ya CCM madarakani itakuwa ni kwasababu ya kile ulichokiita “kunyimwa maisha ya ujanja ujanja” uliaminishwa na nani? Au kuna document yoyote umesoma ukafahamu hilo, Hahahhaa!
 
Reactions: BAK
Na wewe ulivyosema wananchi kama wataiondoa serikali ya CCM madarakani itakuwa ni kwasababu ya kile ulichokiita “kunyimwa maisha ya ujanja ujanja” uliaminishwa na nani? Au kuna document yoyote umesoma ukafahamu hilo, Hahahhaa!
Mhu!! Pumba!

Mimi nimepitia maisha ya ujamaa, maisha ya ruksa, maisha ya ukapa, na maisha yakibaba kutoka safarini. Sasa kama wewe ulikulia maisha ya kibaba, hutaweza kujadiliana nami hata siku moja kwani hatuwezi kuelewana.
 
Mhu!! Pumba!

Mimi nimepitia maisha ya ujamaa, maisha ya ruksa, maisha ya ukapa, na maisha yakibaba kutoka safarini. Sasa kama wewe ulikulia maisha ya kibaba, hutaweza kujadiliana nami hata siku moja kwani hatuwezi kuelewana.

PUMBA na wewe. Kama Wewe kupitia maisha yote hayo na bado haijakuondolea “upumbavu” basi kuna tatizo kubwa.

Uache kufikiria kuwa wananchi wataitoa CCM madarakani ni kwasababu wamenyimwa maisha ya ujanja ujanja tuna sababu zaidi ya 26 za kuiondoa serikali iliyopo madarakani.
 
Reactions: BAK
Yeye alichokuwa anafanya au anachofanya ni kuweka mazingira mazuri na umeme ili wewe na Mimi tuweke hivyo viwanda, kama wewe hutaki au huwezi subiri kukuta hizo nyama chini.
Kwani aliahidi kuweka mazingira mazuri ya umeme au Tanzania ya viwanda?
 
Naona mnaendeleza propaganda za babu yenu tu!
 
Tunaoteseka ni sisi watumishi wa umma
 
Sasa hiyo picha inahusiana vipi na viwanda au haujapenda huyo mama kuonganishiwa umeme kwenye kijumba chake cha nyasi? Maana miaka ya nyuma, nyumba za nyasi zilikuwa haziwekewi umeme.
 
Ni ujinga tu anaweza kuamini Agadirza za kichaa
 
Sasa hiyo picha inahusiana vipi na viwanda au haujapenda huyo mama kuonganishiwa umeme kwenye kijumba chake cha nyasi? Maana miaka ya nyuma, nyumba za nyasi zilikuwa haziwekewi umeme.
Ila mzee katuwekea piacha ya REA ndo anathaminisha na viwanda . . . Tupe picha nyingine mzee tuone uhalisia
 
Sasa hiyo picha inahusiana vipi na viwanda au haujapenda huyo mama kuonganishiwa umeme kwenye kijumba chake cha nyasi? Maana miaka ya nyuma, nyumba za nyasi zilikuwa haziwekewi umeme.
Huyo ni mtanzania wa uchumi wa kati ulioletwa na viwanda.
 
Hivi yule Mwijage aliyetuambia kuna viwanda 3000 vipya toka 2015 yuko wapi [emoji23][emoji23][emoji23]
Viwanda vipya 3,000 ? Vimetoka wa pi ? Na ni vya aina gani ? Mi nilidhani tunaingia kwenye heavy industries kumbe nothing ? Na sasa mnaambiwa Tanzania kuwa kama Ulaya hahahahaaaa . . . Ile Ulaya ninayoijua mimi au ? Mfano pale Elland Road ninapopita kwenye lile jiji la Leeds lilioanza ujenzi tngu miaka ya 1700 ? Au pale Hamburg palipoanza ujenzi tangu 1800 tupalinganishe na Dar es Salaam hii ambayo hata miaka 150 haina ?

Tanzania kama Ulaya ? Come on . . .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…