Rais Magufuli kuvunja Jiji la Dar es Salaam

Rais Magufuli kuvunja Jiji la Dar es Salaam

pakaywatek

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
4,660
Reaction score
6,282
Akiwa katika uzinduzi wa daraja la juu Ubungo amesema atalivunja jiji na kuipa Ilala hadhi ya jiji na wilaya zingine zibaki kuwa Manispaa.
----




Rais Magufuli ameyasema haya

Nategemea Jiji la Dar es Salaam kulivunja na hii nawaambia hapa ili tutengeneze jiji la eneo fulani, tunaweza tukaifanya Ilala ndio ikawa jiji, ita-depend na mambo yatakavyoenda lakini kuwa na madiwani ambao wanakaa hapa juu, wanachangiwa hela, hawana miradi ya maendeleo, wanakula posho na hawakuchaguliwa na watu, hili nitalikataza.

Kwa hiyo ninalizungumza hapa, wale wanaojiandaa kuwa Mameya wa jiji la Dar es Salaam na wanakaa hawana maeneo wajue hicho kimekwisha. Tunataka Manispaa moja katika jiji la Dar es Salaam ndio ipandishwe hadhi iwe jiji halafu nyingine ziwe manispaa, ni kama ilivyo katika majiji mengine.

Kwahiyo mjiandae kisaikolojia wale waliokuwa wanataka umeya wajiji la Dar es Salaam, meya atapatikana kutoka Ilala au kutoka manispaa mojawapo ya hapa, huu ndio ukweli na ukweli utabaki kuwa ukweli na draft nimeshaletewa na mheshimiwa Jafo, nafikiri nikitoka huku nitakwenda kuisaini.

Ili turahisishe mambo, bajeti ya jiji ambayo haipo, fedha zilikuwa zinapotea ndugu zangu waheshimiwa wabunge, jiji la Dar es Salaam litaendelea kuwepo lakini tutachukua eneo fulani nafikiri Ilala inafaa kuwa jiji, ndio katikati ya jiji la Dar es Salaam, wewe Ubungo utasubiri kwanza kwasababu hata barabara bado hazijatengenezwa tengenezwa lakini nafanya haya ndugu zangu kwa kuangalia matumizi mazuri ya fedha zetu.
Mwiso wa Nukuu
 
... yale yale ya matokeo ya mitihani sekondari kuacha kutolewa ilivyozoeleka A, B, C, D, F badala yake yakatolewa kwa mtindo wa GPA halafu akaja mtawala mwingine akarudisha A, B, C, D, F! Bila kuwa na proper instruments and mechanisms to control, regulate and balance powers za viongozi na mihimili tutapata tabu sana.
 
Akiwa katika uzinduzi wa daraja la juu ubungo amesema atalivunja jiji na kuipa ilala hadhi ya jiji na wilaya zingine zibaki kuwa manispaa.

Kama kuna madiwani walikua wanajiandaa kuwania umeya wa jiji na wasahau 'kwanza hawakuchaguliwa na wananchi' alafu wanagombania umeya wa jiji.
Kwahiyo madiwani walichaguliwa na nani? (Anathibitisha wizi wa kura kufanyika?)

Kwahiyo jiji la Dar Es Salaam linaenda kuwa historia? (Dar inakuwa ya "mikoani")

Ikiwa Jiji la Dar linaenda kufa, jiji kubwa kuliko yote Tz linaenda kuwa Mwanza.... (ok ok ok inaeleweka)

Ukienda kutafuta majiji makubwa East Africa, Nairobi anakosa mpinzani rasmi.
 
Akiwa katika uzinduzi wa daraja la juu ubungo amesema atalivunja jiji na kuipa ilala hadhi ya jiji na wilaya zingine zibaki kuwa manispaa.

Kama kuna madiwani walikua wanajiandaa kuwania umeya wa jiji na wasahau 'kwanza hawakuchaguliwa na wananchi' alafu wanagombania umeya wa jiji.
He! Kwahiyo kinondoni, temeke, kigamboni ziwe manispaa alafu Ilala ndio jiji?

So jina la Dar Es Salaam ndio litakuwa kwishney?
 
Akiwa katika uzinduzi wa daraja la juu ubungo amesema atalivunja jiji na kuipa ilala hadhi ya jiji na wilaya zingine zibaki kuwa manispaa.

Kama kuna madiwani walikua wanajiandaa kuwania umeya wa jiji na wasahau 'kwanza hawakuchaguliwa na wananchi' alafu wanagombania umeya wa jiji.
Ukitaka kula hela peke yako hasa katika kipindi chako cha mwisho cha madaraka , dhibiti jiji la DSM lenye mapato mengi , hivi ndivyo alivyofanya Mkapa , alivunja halmashauri ya Jiji na kumweka rafiki yake Keenja kuwa Mkurugenzi , baada ya muda mfupi wote wakawa matajiri wa kutupwa .
 
Akiwa katika uzinduzi wa daraja la juu ubungo amesema atalivunja jiji na kuipa ilala hadhi ya jiji na wilaya zingine zibaki kuwa manispaa.

Kama kuna madiwani walikua wanajiandaa kuwania umeya wa jiji na wasahau 'kwanza hawakuchaguliwa na wananchi' alafu wanagombania umeya wa jiji.nimemnukuu
Hawakuchaguliwa na wananchi ?Hapo sijaelewa. Au kwenye udiwani kuna viti maalum ?Pia Ilala kuwa Jiji sababu ni nini?
 
Walichaguliwa na madiwani wa Manispaa za Kinondoni, Ilala, Ubungo, Kigamboni, Temeke! Hawakuchaguliwa na wananchi ndiyo maana walikuwa wana-hang tu bila kuwa na Manispaa. Hata Meya wa Jiji alikuwa ana-hang tu, hakuwa na Manispaa maana kila Manispaa ina Meya wake.
 
Back
Top Bottom