Rais Magufuli: Lukuvi hawezi kuwa Mgombea urais wa CCM 2025 kwa sababu ana umri mkubwa. Ni fursa ya Vijana

Rais Magufuli: Lukuvi hawezi kuwa Mgombea urais wa CCM 2025 kwa sababu ana umri mkubwa. Ni fursa ya Vijana

Ina maana mzee baba hatobadilisha katiba ili aendelee kubaki madarakani? Sisi wapiga ramli kwamba ataendelea kubakia madarakani tutaambia nini watu?
 
Kitendo cha Mh Rais kutamka hadharani kuwa mtu yeyote aliyemzidi umri asijidanganye kuomba nafasi hiyo ni kwenda kinyume kabisa na katiba ya Nchi.

Hakuna sehemu katika katiba ya Nchi yetu inayomkataza mtu yeyote kugombea nafasi ya Urais kwa kigezo cha umri mkubwa.

Washauri wa Rais jaribuni kumshauri Bwana Mkubwa kuna kauli akizisema ninaleta mtafaruku mkubwa sana katika jamii.
Huo ndo ukweli hata kama ni mchungu. Watanzania ni wabishi sana. Wanamhitaji Rais mwenye nguvu kimwili na kiakili. Huwezi kumweka mtu mwenye miaka 80. Nchi hii inahitaji mtu mwenye nguvu na mbabe kidogo. Hili hata Mbowe na Mnyika wanalielewa. Waliomba sana kipindi cha Kikwete nchi ije impate mbabe kiaina.
 
Kabudi kashaambiwa hawezi kuwa Rais...macho yamemmchomoka yakagonga kwenye lensi...yakarudi kwenye soketi

Kama sio miwani kuzuia saa hii tungeshasema mengine

Ila JPM sio poa kuwananga wanaomzidi umri, mbona Joe Biden kawa Rais na miaka 78.!

Au dhambi ya ubaguzi inaendelea.?
Wewe ni mtu mbadi sana
 
Hadi ifike 2025 tutaona na kusikia mengi kutoka chama cha wakwapuaji kura na hapa ndio kwanza movie imeanza.
 
Lissu alishasemaga "hakuna aliye salama, wakitumaliza upinzani watafata wao kwa wao kufarakana
 
Sifa zote anazo, muadilifu, mzalendo, mchapakazi, nk lakini sasa shida kazaliwa kabla ya Magufuli!. Hafai kuwa Rais huyo [emoji2][emoji2]
 
Lukuvi alimkodi Harmonize akampa milioni 60 aende akaimbe Isimani wakati wapiga kura wake hata uhakika wa maji hawana.

Ikumbukwe Lukuvi ni mbunge wa Isimani kwa miaka 20 mfululizo.
Kama kweli alitoa huu mlungula, basi naapa kwa mizimu ya Yericko asipewe hata unaibu waziri!!!
 
Tough times ahead, kama unaweza kupata hata kikazi cha kuosha vikongwe Ulaya sepa.

Mpaka wabongo waje kujitambua na kuanza kupigania nchi yao, siyo leo wala kesho na hilo genge litakuwa limeshakita Mizizi mizito.

Maana Mbongo mpe Chakula akishiba mpe Pombe, ukiweza kumpa na demu umemaliza, unamfanya Mateka akiwa hajielewi anakuabudu kuliko Mungu
Umesema kweli kabisa. Kama tumeshindwa kukombolewa na Lissu, basi kwisha habari yetu.
Kama ulivyosema Mtanzania akipata mihogo ya watoto, jioni akapata kahawa na mwanamke, basi inatosha ...... tumefikishwa hapo. Majitu mazima yanamuita Jiwe Yesu...
 
Katiba haina ukomo wa juu wa umri kwa mgombea, labda wabadirishe katiba.
Anaongelea CCM huyu. Vyama vingine nadhani hata Babu wa 82 years inaweza kuwa sawa, as per Katiba zao

Halafu kwanini kawasingle out Lukuvi na Kabudi? Vita ya Urais wa 2025 imeanza mapema
 
Kitendo cha Mh Rais kutamka hadharani kuwa mtu yeyote aliyemzidi umri asijidanganye kuomba nafasi hiyo ni kwenda kinyume kabisa na katiba ya Nchi.

Hakuna sehemu katika katiba ya Nchi yetu inayomkataza mtu yeyote kugombea nafasi ya Urais kwa kigezo cha umri mkubwa.

Washauri wa Rais jaribuni kumshauri Bwana Mkubwa kuna kauli akizisema ninaleta mtafaruku mkubwa sana katika jamii.
Marehemu Komba alipotunga wimbo wa kuisoma namba wengi, akiwemo yeye mwenyewe, walidhani namba itasomwa kwa wapinzani peke yao. Huko waliko wanajuutaaa nakuambia.... [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Back
Top Bottom