Rais Magufuli: Maabara Kuu ya kupima sampuli za COVID-19 yaonyesha mafenesi, mapapai na mbuzi yana uambukizi

Rais Magufuli: Maabara Kuu ya kupima sampuli za COVID-19 yaonyesha mafenesi, mapapai na mbuzi yana uambukizi

Mmmh, huyu mzee ana uhakika lakini? Mbona hatujasikia sehemu nyingine

Sent using Jamii Forums mobile app
Inawezekana ni vipimo vyetu tulivyonavyo.
Lakini hii inatia wasi wasi kama hamna hatua zilizochukuliwa kuhakikisha tunapata majibu sahihi ya sampuli zinazopimwa. Maana fact ni kwamba ugonjwa upo hata kama vipimo wakati mwingine vimetoa majibu ya uongo ( haijulikani kama ni mtu au vipimo ndio vimetoa majibu hayo), tahadhari ni muhimu
 
Mkuu hii maabara ni ya pili kuwa accredited baada ya ile ya hospitali ya rufaa Mbeya.
Binafsi siwezi kusema chochote Kwa sasa, nasikilizia tu. Kuna shida kwenye maabara na wataalam wetu na shida kubwa ipo kwenye bajeti ya uendeshaji wa hizi maabara na kutowajibika ipasavyo kwa baadhi ya wataalam katika utendaji kazi kwa kutozingatia standard operating procedures zinavyotaka.
Umeongea professionally mkuu. Kudos.
 
Duuuh! sasa mananasi na mafenesi yana damu au hizo sampuli zake zilipenyezwa vipi ina maana hao waliokuwa wakipima walikuwa hawaoni na hawajui kuwa hizi sampuli siyo za binadamu jamani??

This dude seem to be so naive and ignorant!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Ila nahisi hapa imetumika lugha flani kuficha ukweli. Pengine hayo mapapai na mafenesi yanawakilisha kitu flani. Inaweza ikawa kweli sampuli za mtu mmoja zimepelekwa kwa majina tofauti na majibu yakawa positive na negative at the same time while it was from the same person. Ni mawazo yangu tuu.
 
Mkuu GUSSIE nashukuru kwa bandiko zuri. Naomba unitoe kidogo ujinga, hivi nini kinapelekwa kupimwa ili kubaini huyu MTU ameshambuliwa au hajaambuzwa Coronavirus? Naomba wataalam muliopo hapa JF mtutoe tongotongo.

Ahsante
Wanapima swab, siyo damu. Swab ni kama una unaingiza kitu kinachochukua majimaji kwenye sehemu ambayo unaamini kama mtu ana maambukizi ni lazima utakipata kisababishi.

Naona kwa suala la corona, wanaingiza kitu puani kinaitwa viral nose swab au wanaweza kuingiza kooni kitu kinachoitwa throat swab. Mchukuaji sample anakuwa kama anapangusa ndani ya pua yako au kwenye kooo ili kuweza kupata sample ya kupeleka maabara.

Lakini kuna taratibu za kuchukua. Siyo unakutana tu na mtu barabarani unaamua kumchukua sample. Samples hizi zinatakiwa kuchukuliwa kwenye chumba chenye ubaridi na negative pressure, na sample inabidi itunzwe kwenye vifaa maalum. Kosa katika uchukuaji, usafirishaji, vinaweza kuchangia kutoa majibu yasiyo sahihi.

Sample hizo za mbuzi zilichukuliwaje? Zilisafirishwaje, zilitunzwaje? Na vipi kuhusiana na reagents zinazotumika, zinaweza kutumika kwa wanyama kama mbuzi au tunda kama papai?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila nyie watu wakatili wa nafsi aiseee...
Kuangalia tuu TBC inahitaji roho ngumu,
Sasa kumwangalia Huyo jamaa TBC inahitaji uwe bandidu na nusu.

Nilienda ugenini, wanaangalia TBC mda wote, Maisha yangu ile jioni yalikua magumu sanaaa, nje kuna mvua, chumbn hakwendeki maana unasubr mwongozo wa wenyeji, kuvaa earphones utaonekana wa ajabu, kuchezea simu mda wote nako hakuleti picha nzuri,
Bahat nzuri mtoto akawa anakuja kuniongelesha kila mambo yakiwa magumu, mtoto wa mzee ambaye ndie mwenyeji wangu ndie alikua anamtuma dogo aje maana alijua.

Yaani yule Mzee mwenye nyumb anashangilia kila kitu asee, half anakuongelesha u comment...

Nilijitahd kuonesha unafk wa hali ya juu ile siku huku unajichekesha la sivyo naharibu hata kilichonipeleka,
Mpk nikahisi ana ni challenge kuona how deep i can handle pressure.
Baadae Mwanaye akanipa pole maana alijua ninavyoteseka.

Ila asikwambie mtu unafk wa nafsi yako unachoma moyoo aisee, naondoka huku najishangaa, hv kweli n mm wa kumshangilia yule jamaa... Nilitamani nikatubu.

Na huwezi ukanishangaa,
Maana haya sasa wewe umesikiliza, ulichoambulia ndio hicho, umefurahia?
Siku nyingine jipange fikia guest house kama una muda mchache huko kama bajeti inaruhusu otherwise kwenye miji ya watu utateseka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanapima swab, siyo damu. Swab ni kama una unaingiza kitu kinachochukua majimaji kwenye sehemu ambayo unaamini kama mtu ana maambukizi ni lazima utakipata kisababishi.

Naona kwa suala la corona, wanaingiza kitu puani kinaitwa viral nose swab au wanaweza kuingiza kooni kitu kinachoitwa throat swab. Mchukuaji sample anakuwa kama anapangusa ndani ya pua yako au kwenye kooo ili kuweza kupata sample ya kupeleka maabara.

Lakini kuna taratibu za kuchukua. Siyo unakutana tu na mtu barabarani unaamua kumchukua sample. Samples hizi zinatakiwa kuchukuliwa kwenye chumba chenye ubaridi na negative pressure, na sample inabidi itunzwe kwenye vifaa maalum. Kosa katika uchukuaji, usafirishaji, vinaweza kuchangia kutoa majibu yasiyo sahihi.

Sample hizo za mbuzi zilichukuliwaje? Zilisafirishwaje, zilitunzwahe? Na vipi kuhusiana na reagents zinazotumika, zinaweza kutumika kwa wanyama kama mbuzi au tunda kama papai?

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu Bams ubarikiwe kwa maelezo yako ya kitaalamu. Natumaini kupitia kwa maelezo uliyotoa tunaweza sasa ku argue critically katika mada iliyopo mbele yetu.

Ahsante
 
Hili la Mkuu wa nchi kupima Mbuzi na mapapai badala ya kupima watu, imetudhalilisha sisi Kama watanzania nimeona kule Kenya wameanza kutucheka na kutudhalilisha wakiandika kuwa kenya twapima binadamu Tanzania wao wapima mbuzi na mapapai, aiseee tumeanza kuchekwa Kama watoto wadogo, wakuuu hiii kitu imeshangaza Sana inamaana Mkuu wa nchi haaamini kuwa corona ipo?

Ninajiuliza kuwa tungekuwa na maaambukizi mengi Kama kenya Au Africa kusini Au zile nchi za ulaya ingekuaje? Ninasikitika Sana na kauli Kama hiii Ya mtu msomi kuhisi kuwa corona ni uongo huku anarudi kusema kuwa corona kweli ipo tuchukue hatua, sasa Mimi sielewi huku unasema kuwa corona kweli ipo huku unasema kuwa mabeberu wanatumika huku hao hao mabeberu unafaham kuwa ndio wenye idadi kubwa ya wagonjwa wa corona had majirani zako wako Juu kwa maaambukizi inamaaana wanakubeberu Halafu kwao wanaongeza Namba kwako wanakushusha?

Vipimo huviamini Wakati ndivyo vinavyopima kwao huko? Hivi ikitokea huyu akawa na maamabukizi Kama nchi zingne si ndio atatembea akiimba kuwa ameletewa corona? Haki ya MUNGU huyu Mkuu amedhalilisha nchi na kila Siku analete mambo ya hovyo

Sent using Jamii Forums mobile app
Alafu hayo ni mambo ya kitaalamu wala hakupaswa kuwavizia kama ni kweli kafanya hivyo. Naamini wataalamu wa wizara wanafanya kazi yao na kama kweli aligundua hilo angewasiliana na waziri ili warekebishe kasoro. Yote haya anayafanya lakini tayari mgeni Korona tunaye na inawezekana akatufanyizia sana siku si nyingi (siombei). Anafikiri anafunika kombe mwanaharamu apite lakini kuna tatizo kubwa kwake.
 
Magufuli baba lao, mabeberu na vibaraka wao wameze wembe. Hatutishiki, ng'o! Kinyago chao.
 
Mkuu GUSSIE nashukuru kwa bandiko zuri. Naomba unitoe kidogo ujinga, hivi nini kinapelekwa kupimwa ili kubaini huyu MTU ameshambuliwa au hajaambuzwa Coronavirus? Naomba wataalam muliopo hapa JF mtutoe tongotongo.

Ahsante
Kuna njia mbili So far za uchunguzi wa maambukizi haya ya Coronvirus Disease 2019 ( COVID-19) ... au ifanyike Chest CT scan

Njia ya kwanza ni kudetect antibodies ambazo mwili huzalisha kupambana na Adui , kwa case ya Corona tunaangalia IgG, IgM.. Kwa Bahati mbaya kabisa , hizi test kit za kudetect antibodies bado hazijakua confirmed na WHO ...nahii njia haijatumika sanaa.



Njia inayotumika kwa sasa ni kudetect uwepo wa Kirusi moja kwa moja ama kwakufanya rRT-PCR, au kudetect antigen wa COVID-19 yaan COVID-2019 n.k

Njia hii hutumia sample ambazo huchukuliwa kama swab ndani puani au kooni (kwa maambukizi yaliyo bado ktk eneo lajuu ya mfumo wa upumuaji).. Lkn punde maambukizi yanvyoshuka chini kuyafuata Mapafu, basi hapo lazima kufanyike aspiration ili kupata Aspirates kutoka katika Mapafu.

Kwa MTU aliyekufa, hufanyika Autopsy na kuchukua sehemu ya pafu na kwenda kuchunguza.


Kwa hapa bongo Nahiyo maabara , bila shaka wanafanya rRT-PCR test , ambapo wataalamu kwanza wana chukua sampo wanaitreat na Ku extract RNA pekeake , kisha wanaifanyia Reverse transcription kupata Viral DNA ndo sasa wanaingiza kwenye mashine kutengeneza copies zake kibao....

rRT-PCR ni nzuri kwa sababu hata kirusi kimoja kinaweza tumika kuzalisha copies kibao.


Turudi kwa JPM...


Kutokana na Mchakato mzima wa utendaji kazi wa Hii mashine., kwa kuzingatia hatua kwa hatua .

Na kwasababu amekiri kua Wataalamu Wetu sio kwamba hawana uelewa.




Basi niseme ivi, YEYE JIWE AACHE POROJO POROJO .


Kama hataki kusikia habari za maambukizi, asilazimishe mambo.


Aamue tu kuanzia Leo, Hamna kutangaza Idadi ya maambukizi.


Nasio kutisha tisha Watu nakufanya hawa wafanyakazi washindwe kutumia umahiri wa fani zao walizozisomea kwa miaka kadhaa ,badala yake waendelee kufanya Yale yanayompendeza yeye .



NASEMA IVI, HAMNA CHA PAPAI, WALA.OIL, WALA MBUZI ,WALA KWARE WALA BIBI YAKE MBUZI WALIOPIMWA.



JIWE NI MJANJA KTK KUZALISHA HOFU.














Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuanzia Leo Kwa kipindi kisicho julikana watanzania tujiepushile na vitu vifuatavyo sababu vinaweza kutumiwa na mabeberu muda wowote.

Oil ya gari Kwa jina la Jabir Hamza.

Fenesi Kwa jina la Sarah Samweli.

Papai Kwa jina la Elizabeth Anne.

Mbuzi Kwa jina la mtaki mtwale.

Pamoja na kondoo Kwa jina la Juma kifuko.

N:B
Adumu jiwe kutoka chato


IMG_20200503_162305.jpeg
IMG_20200503_162210.jpeg
IMG_20200503_162354.jpeg
IMG_20200503_161803.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom