Nimemsikiliza Rais Magufuli katika hotuba yake ya jana kwa makini sana, ambayo alimmwagia sifa kem kem kiongozi wa ACT Wazalendo kwa kukubali kujiunga katika serikali ya umoja kitaifa huko Zanzibar.
Aliendelea kueleza kuwa Maalim Seif ni kiongozi shukaa na wa kipekee, kwa kuwa ameamua kuweka maslahi mapana ya visiwa hivyo na kuacha maslahi yake binafsi na kujiunga na serikali aliyoiunda Dr Mwinyi.
Swali langu ninalojiuliza iwapo Rais Magufuli ameona umuhimu wa maridhiano huko Zanzibar, ni kwanini naye haundi serikali ya umoja wa kitaifa na viongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema?
Umetolewa mwito na viongozi wa Chadema kwa Rais Magufuli kwa muda mrefu, kuwa aangalie uwezekano wa kuwaalika wao viongozi wa Chadema ili wajadili mustakabali wa kitaifa, lakini kwa bahati mbaya ni yeye Rais Magufuli ambaye amewafungia mlango viongozi hao wa Chadema kwa kukataa kufanya maridhiano hayo.
Kama alivyoongea Rais Magufuli kuwa ni muhimu kuwa na mwafaka wa kitaifa na viongozi wa upinzani kwa maendeleo ya Taifa.
Sasa ni kwanini yeye Rais Magufuli amesifu serikali hiyo ya umoja wa kitaifa huko Zanzibar wakati yeye anaukataa umoja huo wa kitaifa kwa serikali ya Muungano?
Ninachojua ni kuwa yeye Rais Magufuli siyo muumini wa serikali ya umoja wa kitaifa na anachotaka yeye ni kuwaona viongozi hao wa Chadema "wakisalimu amri" kwa kujiunga na CCM ndipo awaingize kwenye serikali yake, lakini kwa viongozi hao kubaki Chadema, hakubali kabisa kuwajumuisha kwenye serikali yake!
Mbona Rais Mwinyi amekubali kumwingiza kwenye serikali ya umoja wa kitaifa huko Zanzibar akiwa kiongozi wa ACT Wazslendo, ni kitu gani kinachomshinda yeye Rais Magufuli kuwajumuisha akina Mbowe katika serikali ya umoja wa kitaifa katika serikali ya umoja wa kitaifa katika serikali ya Muungano?
Ni lazima Rais Magufuli ajue kuwa viongozi wa Chadema wana makovu mengi sana yaliyotokana na uchaguzi mkuu uliopita, kwa hivyo namna pekee ya kuyaondoa makovu hayo ni kukubali kuwajumuisha viongozi hao wa Chadema katika serikali yake na siyo "kuwanunua" viongozi hao ili wajiunge na CCM!
Kama asemavyo Mara kwa Mara Rais Magufuli kuwa maendeleo hayana chama, tujenge Taifa letu kwa umoja wetu, kwa kuheshimiana na kuondoa uhasama kwa vyama vyetu.