Uchaguzi 2020 Rais Magufuli ndiyo anaibuka kuwa atawaongezea mishahara wafanyakazi. Tunamwambia kuwa hatudanganyiki ng'oo

Uchaguzi 2020 Rais Magufuli ndiyo anaibuka kuwa atawaongezea mishahara wafanyakazi. Tunamwambia kuwa hatudanganyiki ng'oo

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Nilimsikia Rais Magufuli, katika mkutano wake wa kampeni hapo Jana, huko Bagamoyo mkoani Pwani, akiwaahidi wafanyakazi kuwa atawaongeza mishahara yao wafanyakazi hao, iwapo watamchagua tena katika uchaguzi mkuu ujao!

Hivi si ndiyo huyu huyu Rais Magufuli amekuwa akigoma katakata kuongeza mishahara ya wafanyakazi, kila amapoonbwa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi kutokana na kupanda kwa hali ya maisha kwa wafanyakazi hao, katika kila sherehe za Mei Mosi, kila mwaka tokea aiingie madarakani mwaka 2015, akidai kuwa hawezi kuongeza mishahara wafanyakazi, kwa kuwa katika kipindi hiki anajenga miundo mbinu mikubwa ya reli ya SGR na bwawa la umeme la Stieglers Gorge?

Wakati Rais Magufuli amekuwa akigoma katakata kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa sababu hizo zisizokuwa na mashiko hata kidogo, marais wenzake wote waliomtangulia walikuwa wakiwaongeza mishahara yao wafanyakazi, pamoja na marais hao pia walikuwa wakiendelea kujenga miundo mbalimbali hapa nchini

Hivi Rais Magufuli kutoa ahadi hiyo wakati huu wa kampeni, anatugeuza sisi wafanyakazi wa nchi hii ni wajinga mno na tunaoweza kudanganyika kirahisi hivyo?

Sisi wafanyakazi wa nchi hii, hatudanganyiki tena na Rais Magufuli na tuna jambo letu ambalo tutalitimiza ifikapo Oktoba 28 mwaka huu kwenye sanduku la kura kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
 
Tundu Lissu ongeza kupiga spana, kwakuwa huyo Jiwe ameanza kutepeta.

Hadi hivi sasa anaanza kuwaahidi wananchi, vitu ambavyo siku za nyuma alikuwa akijibu kwa jeuri kubwa kuwa hataongeza hiyo mishahara ng'ooo
 
Tundu Lissu ongeza kupiga spana, kwakuwa huyo Jiwe ameanza kutepeta.

Hadi hivi sasa anaanza kuwaahidi wananchi, vitu ambavyo siku za nyuma alikuwa akijibu kwa jeuri kubwa kuwa hataongeza hiyo mishahara ng'ooo
Kwakweli apige zaidi spana had Maji ayaite Mmaa. Sasa hivi tayari yupo desperate kila ahadi nzuri za Lissu naye adandia na kuahidi kama vile hakuwahi kuziahidi.

Wale wawasha mitambo wake wote Jamii imewapuuza wamebaki Kufokea watu Tu.
 
Maskini huwa hana kumbukumbu huyu mzee!
Screenshot_20201020-060657.jpg
 
Uzalendo ni pamoja na kusema ukweli na kuacha unafiki pamoja na ubinafsi , JPM tunampenda wote ilaa kwa hili na mishahara amabalo lipo kikatiba na kikanuni mkuu amebugi sana.

Kumtetea na kumsifia nikutomtendea haki yeye na hivyo hatumkosei Mungu tu bali pia yeye. Ndio, amefanya mengi ilaa hili la kutoongeza mishahara na kupandisha makato ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu kwa wanufaika ni kutokosa utu na kutowajali wafanyakazi.

Sema ukweli na ukweli utakuweka huru, saidia nchi yako kwa kuwa muwazi na kuacha ubinafsi. Shauri vizuri na kwa upendo, huu ndio uzalendo.
 
Back
Top Bottom